Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #281
Sehemu ya 85
Katika kila njia alizopita kulionekana kuwa na nafuu kwake, na kwa sababu ilikuwa ni siku ya Jumamosi, siku ambayo mashabiki wa timu za mipira, raga na kriketi walikuwa wakienda viwanjani, njiani alikuwa akipishana na watu wengi kiasi kwamba kwa mhalifu kama yeye ilikuwa rahisi sana kwenda bila kukamatwa.
Aliendesha gari mpaka katika kituo cha mafuta cha Shell ambapo haraka sana akateremka na kuchukua kadi yake, akaiingiza katika kitundu kidogo, akaandika lita alizotaka na kuweka mpitra katika mdomo wa gari lake, akajaza, akaichukua gari lake na kuondoka mahali hapo.
Wakati hayo yote yakiendelea, hakujua kama alikuwa akitafutwa na polisi. Wakati akikaribia Bristol ndipo alipoamua kufungua redio kusikiliza kilichokuwa kikiendelea. Katika kila redio taarifa ambayo ilikuwa ikitangazwa sana ilikuwa ni kuhusu tukio lile lililotokea hospitalini.
Alisikiliza kwa makini, alitaka kujua kama mapacha hao walikufa au la. Kila aliposikiliza, alisikia kwamba walikuwa kwenye hali mbaya m,no ambapo muda wowote ule wangefariki dunia.
Hakuhuzunika, ndiyo kwanza akafurahia kwa kuona kwamba alimkomoa na kama kukosa basi wakose wote. Wakati akiendelea kusikiliza ndipo akapokea taarifa kwamba tayari mtu aliyefanya tukio hilo alijulikana, na mpaka jina lake likatajwa.
Hakushangaa kwani hata alipoondoka nyumbani aliwaacha polisi wakiingia hapo. Aliendelea mbele mpaka kufika Bristol huku akiwa amechoka.
Wazo lake kwa kipindi hicho lilikuwa ni kuendelea na safari kwa gari lake mpaka katika kituo cha treni cha Bristol Packway.
Katika kila njia alizopita kulionekana kuwa na nafuu kwake, na kwa sababu ilikuwa ni siku ya Jumamosi, siku ambayo mashabiki wa timu za mipira, raga na kriketi walikuwa wakienda viwanjani, njiani alikuwa akipishana na watu wengi kiasi kwamba kwa mhalifu kama yeye ilikuwa rahisi sana kwenda bila kukamatwa.
Aliendesha gari mpaka katika kituo cha mafuta cha Shell ambapo haraka sana akateremka na kuchukua kadi yake, akaiingiza katika kitundu kidogo, akaandika lita alizotaka na kuweka mpitra katika mdomo wa gari lake, akajaza, akaichukua gari lake na kuondoka mahali hapo.
Wakati hayo yote yakiendelea, hakujua kama alikuwa akitafutwa na polisi. Wakati akikaribia Bristol ndipo alipoamua kufungua redio kusikiliza kilichokuwa kikiendelea. Katika kila redio taarifa ambayo ilikuwa ikitangazwa sana ilikuwa ni kuhusu tukio lile lililotokea hospitalini.
Alisikiliza kwa makini, alitaka kujua kama mapacha hao walikufa au la. Kila aliposikiliza, alisikia kwamba walikuwa kwenye hali mbaya m,no ambapo muda wowote ule wangefariki dunia.
Hakuhuzunika, ndiyo kwanza akafurahia kwa kuona kwamba alimkomoa na kama kukosa basi wakose wote. Wakati akiendelea kusikiliza ndipo akapokea taarifa kwamba tayari mtu aliyefanya tukio hilo alijulikana, na mpaka jina lake likatajwa.
Hakushangaa kwani hata alipoondoka nyumbani aliwaacha polisi wakiingia hapo. Aliendelea mbele mpaka kufika Bristol huku akiwa amechoka.
Wazo lake kwa kipindi hicho lilikuwa ni kuendelea na safari kwa gari lake mpaka katika kituo cha treni cha Bristol Packway.