Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #301
SEHEMU YA 94
Waliwaulizia lakini madaktari hawakutaka kuzungumza kitu chochote kile, kila walipokuwa wakiulizwa, waliruka na kuliacha swali hilo kitu kilichowafanya kuwa na hofu kwamba inawezekana walikuwa wamefariki dunia ila madaktari hawakutaka kuwaambia ukweli.
Waliendelea kubaki hospitalini hapo, mtu aliyekuwa akiwajulia hali zaidi alikuwa msichana Catherine ambaye hakukuwa na siku iliyokuwa ikipita pasipo kufika katika chumba walichokuwa wamelazwa na kuzungumza nao.
Hakuwaambia ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea, alijua kwamba ni Edmund ndiye ambaye alisababisha hayo yote, alihofia kuwaambia ukweli kwa kuwa alihisi kwamba wangemchukia kwa kuwa mwanaume huyo alikuwa karibu naye.
Kila siku walikuwa wakiwaulizia wazazi wao, walitaka kujua ukweli kama walikuwa wamekufa au walikuwa hai, na kama walikuwa hai walikuwa mahali gani.
Hakukuwa na mtu aliyewaeleza ukweli mpaka pale ambapo walipopewa taarifa kwamba wazazi wao nao hawakuwa katika hali nzuri, walikuwa hapo hospitalini kwani sumu iliyokuwa imewapata, ilikuwa mbaya sana.
“Sumu?” aliuliza Walker huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo! Mliwekewa sumu!” alijibu Dk. John.
“Nani alifanya hivyo?”
Hakukuwa na mtu aliyejibu hilo, kila mtu alihofia kwamba kama wangejibu basi wangewafanya mapacha hao wamchukie Catherine ambaye alionekana kuwa karibu na mwanaume aliyekuwa amesababisha hayo yote.
Siku ziliendelea kukatika mpaka pale walipoanza kupata nafuu. Kila mmoja alionekana kuwa na furaha na baada ya siku mbili, wazazi wao ambao hawakujua mahali walipokuwa kipindi cha nyuma, wakakutana nao hospitalini hapo na kuanza kuzungumza nao.
Sumu ile haikuwapata sana kama ilivyowapata wao, katika kipindi chote hicho hata nao walikuwa wakifichwa juu ya hali waliyokuwa wakiendelea nao watoto wao.
Walipokutana, wakashindwa kuvumilia, wakakumbatiana kwa furaha, kila mmoja hakuamini kwamba hatimaye familia hiyo iliungana kwa mara nyingine.
Watu wakapewa taarifa kwamba hatimaye mapacha hao walikuwa wameinuka kitandani, kila mtu aliyeziangalia picha zao alibaki na furaha tele kwani kwa kipindi hicho hakukuwa na watu waliokuwa wakipendwa kama ilivyokuwa kwa Walter na Walker.
Waliwaulizia lakini madaktari hawakutaka kuzungumza kitu chochote kile, kila walipokuwa wakiulizwa, waliruka na kuliacha swali hilo kitu kilichowafanya kuwa na hofu kwamba inawezekana walikuwa wamefariki dunia ila madaktari hawakutaka kuwaambia ukweli.
Waliendelea kubaki hospitalini hapo, mtu aliyekuwa akiwajulia hali zaidi alikuwa msichana Catherine ambaye hakukuwa na siku iliyokuwa ikipita pasipo kufika katika chumba walichokuwa wamelazwa na kuzungumza nao.
Hakuwaambia ukweli juu ya kile kilichokuwa kimetokea, alijua kwamba ni Edmund ndiye ambaye alisababisha hayo yote, alihofia kuwaambia ukweli kwa kuwa alihisi kwamba wangemchukia kwa kuwa mwanaume huyo alikuwa karibu naye.
Kila siku walikuwa wakiwaulizia wazazi wao, walitaka kujua ukweli kama walikuwa wamekufa au walikuwa hai, na kama walikuwa hai walikuwa mahali gani.
Hakukuwa na mtu aliyewaeleza ukweli mpaka pale ambapo walipopewa taarifa kwamba wazazi wao nao hawakuwa katika hali nzuri, walikuwa hapo hospitalini kwani sumu iliyokuwa imewapata, ilikuwa mbaya sana.
“Sumu?” aliuliza Walker huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo! Mliwekewa sumu!” alijibu Dk. John.
“Nani alifanya hivyo?”
Hakukuwa na mtu aliyejibu hilo, kila mtu alihofia kwamba kama wangejibu basi wangewafanya mapacha hao wamchukie Catherine ambaye alionekana kuwa karibu na mwanaume aliyekuwa amesababisha hayo yote.
Siku ziliendelea kukatika mpaka pale walipoanza kupata nafuu. Kila mmoja alionekana kuwa na furaha na baada ya siku mbili, wazazi wao ambao hawakujua mahali walipokuwa kipindi cha nyuma, wakakutana nao hospitalini hapo na kuanza kuzungumza nao.
Sumu ile haikuwapata sana kama ilivyowapata wao, katika kipindi chote hicho hata nao walikuwa wakifichwa juu ya hali waliyokuwa wakiendelea nao watoto wao.
Walipokutana, wakashindwa kuvumilia, wakakumbatiana kwa furaha, kila mmoja hakuamini kwamba hatimaye familia hiyo iliungana kwa mara nyingine.
Watu wakapewa taarifa kwamba hatimaye mapacha hao walikuwa wameinuka kitandani, kila mtu aliyeziangalia picha zao alibaki na furaha tele kwani kwa kipindi hicho hakukuwa na watu waliokuwa wakipendwa kama ilivyokuwa kwa Walter na Walker.