Nimejiweka Zantel ni burudani kabisa raha mustarehe.
1500=1.5 gb-160 mnts-500 sms per 7 dys.
1000=1 gd 7 dys.
10,000=10 gb 30 dys.
Sipendi kuweka mambo yangu humu kwahiyo sitatoa ushahidi tofauti na maelezo (japo ninao ushahidi wa kutosha)
Tangu nisajili laini nimekuwa nikiunga bando kwa easypesa tu, ni mara chache sana (nadhani mbili au tatu tu) kuweka vocha kutokana na kutokuwepo kwa vocha za Zantel huku nilipo na hata zikiwepo bei inakuwa juu maradufu
Februari mwaka huu tarehe fulani nikaweka vocha na kuunga kifurushi kisha salio likabakia, baada ya muda fulani walipoona situmii ile vocha mara pap napata notifications kucheki nakuta sms mbili dabo ya kwanza hongera kwa kujiunga na *¥$&?(natajiwa lihuduma hata silijui) na ya pili umefanikiwa kujitoa kwenye *¥$&?
Muda huo nilikuwa nahangaika kuunga kifurushi kingine maana niliona kile nilichonacho kimebakia kidogo, basi kila nikiunga naambiwa sina salio la kutosha kucheki salio kweli halitoshi aisee nikalipuka kwa hasira nikawapigia na hapo ndipo nilipoamini ile kauli ya mitandao ni wezi wanatuibia halafu wana majibu ya kukaririsha, kama mtu asiyependa bugdha ndo kwanza anaachilia mbali kufuatilia
Eti kajidai kucheki anasema hakuna tatizo hakuna hela iliyokatwa mara nilipombananisha anasema umejiunga na huduma flani kumbana zaidi ndo akanifanya nicheke badala ya kukasirika. Ananambia eti hiyo huduma ulijiungaga tangu mwezi wa 10 mwaka uliopita ila kwakuwa leo ndo umeweka vocha basi ndomana umekatwa leo gharama za huduma
Nikazidi kumthibitishia kuwa sijajiunga akasema eti huenda mtu ameniunga nikamkazia zaidi kwamba simu yangu haijawahi kutumiwa na mtu jamaa akawa amekomalia tu hapohapo eti huenda tu kuna siku labda nilibonyeza hata kwa bahati mbaya wakati wa kuongea au hata ikiwa mfukoni. Nikamuuliza vipi na swala la kujitoa nalo maana sms yapili inaonesha nimejitoa jamaa akakosa la kujibu
Habari hiyo ndefu sana ngoja tuikate tu maana hata hapo ilipoanzia siyo mwanzo
Hiyo part one na tuiache sasa twende kwenye part two
Juzi nimeunga bando halafu sikulitumia kutokana na maswala ya chaji sasa Leo hii naingia jamiiforums data haifanyi kazi kila nikiingia kwenye app yoyote ya kuhitaji internet mambo hayaendi nikasema ngoja niangalie salio nakuta sms hakuna data hakuna hata zile dakika tano tano za Zantel hakuna (huku sina mtu wa Zantel wa kumpigia) na wakati huo mimi naunga mara kwa mara vifurushi vya 'bao bila kikomo' sms100 dk5Z-Z na gb1. Basi nikaunga kifurushi kingine kisha nikawatwangia tena huduma kwa wateja
Eti anasema hapa nikiangalia una dk za Zantel na sms kadha wa kadha na data unazo mb za kutosha kabisa (anataja mb zile nilizounga muda huo). Nikamkomalia akasema subiri nicheki zaidi. Mara kurudi anasema sasa kifurushi chako inaonesha kimeshaisha kwakuwa aina ya kifurushi hicho kinadumu ndani ya siku tatu tu nikamuuliza haya ndo mabadiliko mliyotuahidi sasa mbona hayapo wazi akajibu eti niwe mvumilivu kwa muda huu maana kuna mabadiliko mengi yanajitokeza
Nilipombana zaidi kwamba kama ni hivyo mbona dakika umenitajia hapo inaonesha mpaka za juzi bado zipo na sms inakuwaje data pekee ndo imeexpire halafu kwanini wewe uone vingine huko na mimi nikiangalia salio niletewe vingine? Hakuwa na cha kujibu cha maana
Mpaka hapo nikagundua kuwa
1. Tumepigwa changa kuhusu vifurushi kurejeshwa kama zamani. Either TCRA au Mitandao kuna anayerudisha gharama za hasara alizokula
2. Mitandao wanajivunia kwamba hatuwezi kuwafanya lolote/ kuwashtaki kwakuwa hela wanayokata au kuiba ni ndogo kwa mtu mmoja mmoja
3. Huduma kwa wateja imewekwa options nyingi na za kuzunguka sana ili kuepuka au kuepusha wao kupatikana kiurahisi (mfano chagua 1 kwa Kiingereza- ila ukiingia unakuta huduma ni vilevile kwa Kiswahili)
4. Jamaa wanakuibia halafu ukiwapigia mbinu zao ni tatu
-upigwe kalenda, ngoja kidogo mpaka ukate tamaa na mara nyingine simu isipokelewe au ikatwe kabisa
-ubambikiziwe (kwamba umejiunga) lihuduma ambalo hata hulijui ilimradi tu ionekane umekatwa kihalali
-haiwezi wala haitaweza kutokea ukarudishiwa hela uliyoibiwa (sijawahi kusikia mtu amerudishiwa pesa zaidi ya kuombwa radhi tu) ukiwabananisha maswali au ukija juu kidogo mara nyingine wanakata simu