Uchaguzi 2020 VIDEO: Wachambuzi wa siasa Kenya washangazwa na muundo wa uchaguzi wa Tanzania, wasema walitoka huko kitambo sana

Hawa ni wachambuzi wa kisasa nchini Kenya wakishangazwa na namna Tanzania ilipo bado kwenye ukoloni japo ni wa watu weusi.
View attachment 1590849
Tufikiri kwa ndani zaidi. Kweli tunadhani kuwa tume ya uchaguzi iliyoteuliwa na mmoja wa mgombea inaweza kuwa huru? Inaweza kumtangaza mgombea mwingine kuwa mshindi hata kama kashinda kihalali? Inaweza isimbebe kweli anayewalipa mshara?

Kama chadema na Lissu wanafikiri kutendewa haki na tume, wanastahili Pole. Inabidi wajiandae kisaikolojia kushinda na kunyanganywa ushindi. Ni vema kuandaa mazingira ya hilo. Sina sababu yoyote kuiamini tume hata chembe. Bila nguvu ya umma hakuna jawabu.
 
Kiukweli wakenya wana haki ya kutucheka! Katiba yao na jinsi wanavyoheshimu haki za makundi ya kiraia ni darasa tosha kwa Tanzania! Yote hayo ni matokeo ya kukitupa nje chama kikongwe cha KANU!

Sisi huku bado tunaendeleza sisasa za kikoloni kwasababu bado tunatawaliwa na chama kikongwe kilichong'ang'ania hadi sheria za kikoloni na ulaghai wa kila aina! Mkiongeza pressure ya kudai katiba mpya, wakija kwenye kampeni wanawambia chagua flani ataleta katiba mpya, mkshamchagua mnaambiwa katiba mpya sio kipaumbele!
 
Siasa za Kenya ni za ubaguzi wa kikabila.
Kenya wapambane kwanza waondoe hili kabla ya wao kukosoa wengine.

Kenya kuna ukabila kwa sababu kuna makabila makubwa yenye watu wengi. Tz hatuna ukabila siyo kwasababu tuna akili sana au maarifa sana, hapa Tz makabila makubwa matatu yakisema yawe na mgombea wao wampe kura hazitatosha kushinda, mwanasiasa hawezi kutegemea ukabila kushinda uchaguzi Tz.

Kenya makabila makubwa Wakikiyu, Wajaluo na Wakalenjin wana wapiga kura wa kutosha kuweza kumweka Rais madarakani ila Tz idadi ya makabila makubwa matatu hayawezi kuweka Rais madarakani tuna makabila not less than 120 , huwezi ukategemea kura za kabila moja au mawili.kushinda urais
 
Pale Kenya sasa hivi ni kama hamna mkubwa! Kila mtu ni kambare! Wamejaa ukabila, hayo ndio waliyoendelea hakuna kingine.

Fikiria uchaguzi bado miaka 2 lakini ofisi ya rais Kenyata ina mgogoro wa kugombea madaraka ya 2022
Rudi kwenye mada mkuu.
 
Ni kweli ukabila ni tatizo Kenya . Lakini pia ukabila ni tatizo hapa Tanzania . Labda kidogo mijini watu hawajali ukabila. Lakini nje ya miji mikubwa ukabila ni tatizo .

Tukirudi kwenye hoja yao, ni ya msingi . Ukiwapinga ni mpungufu wa akili. Katiba yetu ina mapungufu sana na uelekeo wake ni wa ki communist. Wa kumsifu na kumuabudu kiongozi hata pale anapotenda majukumu yake ya kikatiba. Na kama si kiongozi basi ukitukuze chama tawala hata kama sera zao haziwezi kuisaidia nchi . Mfano ni Korea kaskazini.

Huwezi kuwa na tume ya aina hii karne hii labda Tanzania tu.
 
Back
Top Bottom