Video: Tathmini ya Tundu Lissu ya Uchaguzi mkuu Kenya Agost 9, 2022; Ausifu na kueleza aliyoyaona na ambayo hakuyaona yakifanywa na tume - IEBC

The Palm Beach

JF-Expert Member
Dec 30, 2015
804
1,646

Niseme nini hasa? Tundu Lissu ni miongoni mwa wanaharakati, wanasheria na wanasiasa brilliant wanaojua kuelezea jambo kwa lugha rahisi, iliyonyooka na kueleweka na yeyote...

Ni wazi kuwa huyu jamaa kasoma kweli na ameelimika pia na anajua mambo mengi sana...

Hapa anaeleza maoni na mtazamo wake akirejea uchaguzi mkuu wa Kenya juzi kati na namna ulivyofanyika akilinganisha na mfumo wa uchaguzi wa Tanzania...

Fuatiilia kwa kumsikiliza mwenyewe. Utampenda.....
======================

===Point highlights ya alichosema===

MABAYA AMBAYO HAKUYAONA KTK UCHAGUZI MKUU WA KENYA:

1. Mgombea/wagombea wa vyama na binafsi wa nafasi mbalimbali za ubunge & Urais kuenguliwa au kuzuiliwa na hivyo kuwa disqualified kwa sababu yoyote ile..

2. Mgombea akiingiliwa katika misafara au ktk kampeni zake na vyombo vya dola i.e KenPolice, JWK au usalama wa taifa...

3. Hakuona wala kusikia mawakala wa wagombea wa vyama vyote kutoapishwa, kunyimwa IDs, kuzuiwa kuingia kwenye vituo vya kupiga kura, kufukuzwa kwenye vituo vya kupigia kura na kunyimwa matokeo ya vituo...

4. Vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa completely neutral. Havikuingilia mwenendo wa process yoyote ya uchaguzi...

5. Hakuna election observers wa ndani ama wa nje, NGOs za ndani ama nje walionyimwa vibali (accreditation)...

6. Hakuona incumbent president Uhuru Kenyatta japo alikuwa na mgombea aliyemtaka ashinde, lakini hakutokea hata mara akipanda jukwaani kumfanyia kampeni....

Wala hakupata nafasi kabisa kutumia mamlaka yake kuamuru vyombo vya ulinzi vifanye fujo ili mradi mtu wake ashinde...

MAZURI ALIYOYAONA;

1. Kulikuwa na complete transparency ktk hatua zote za uchaguzi wa Kenya kuanzia uteuzi wa wagombea, kampeni, usimamizi, upigaji kura na utoaji matokeo hatua kwa hatua kuanzia vituoni hadi kwenye kutangaza rasmi...

2. Matokeo yalikuwa wazi mno kwa kila mtu kuona kila kitu mwanzo hadi mwisho. Ndiyo maana mpaka sasa kuna utulivu mkuu nchi ni Kenya kulinganisha na chaguzi zilizopita zilikuwa zikiishia kwa kunyukana kwa sbb ya kutokuwepo na uwazi ktk mchakato mzima...

3. Tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya haina impunity kama ikifanya uharamia wowote na ndiyo maana matokeo ya ushindi wa William Rutto yanapinga mahakamani...
 
Ahsante kwa kutujuza

IEBC iliwaengua baadhi ya Wagombea uRais

IEBC ilichanganya mabox ya kura Mombasa na Kakamega hali iliyopelekea Chaguzi za Magavana na Maseneta kuahirishwa

IEBC wameshindwa kujumlisha kura kwa Haki na sasa Kesi iko mahakamani
 
IMG-20220823-WA0020.jpg
 
View attachment 2337725
Niseme nini hasa? Tundu Lissu ni miongoni mwa wanaharakati, wanasheria na wanasiasa brilliant wanaojua kuelezea jambo kwa lugha rahisi, iliyonyooka na kueleweka na yeyote...

Ni wazi kuwa huyu jamaa kasoma kweli na ameelimika pia na anajua mambo mengi sana...

Hapa anaeleza maoni na mtazamo wake akirejea uchaguzi mkuu wa Kenya juzi kati na namna ulivyofanyika akilinganisha na mfumo wa uchaguzi wa Tanzania...

Fuatiilia kwa kumsikiliza mwenyewe. Utampenda.....
======================

===Point highlights ya alichosema===

MABAYA AMBAYO HAKUYAONA KTK UCHAGUZI MKUU WA KENYA:

1. Mgombea/wagombea wa vyama na binafsi wa nafasi mbalimbali za ubunge & Urais kuenguliwa au kuzuiliwa na hivyo kuwa disqualified kwa sababu yoyote ile..

2. Mgombea akiingiliwa katika misafara au ktk kampeni zake na vyombo vya dola i.e KenPolice, JWK au usalama wa taifa...

3. Hakuona wala kusikia mawakala wa wagombea wa vyama vyote kutoapishwa, kunyimwa IDs, kuzuiwa kuingia kwenye vituo vya kupiga kura, kufukuzwa kwenye vituo vya kupigia kura na kunyimwa matokeo ya vituo...

4. Vyombo vya ulinzi na usalama vilikuwa completely neutral. Havikuingilia mwenendo wa process yoyote ya uchaguzi...

5. Hakuna election observers wa ndani ama wa nje, NGOs za ndani ama nje walionyimwa vibali (accreditation)...

6. Hakuona incumbent president Uhuru Kenyatta japo alikuwa na mgombea aliyemtaka ashinde, lakini hakutokea hata mara akipanda jukwaani kumfanyia kampeni....

Wala hakupata nafasi kabisa kutumia mamlaka yake kuamuru vyombo vya ulinzi vifanye fujo ili mradi mtu wake ashinde...

MAZURI ALIYOYAONA;

1. Kulikuwa na complete transparency ktk hatua zote za uchaguzi wa Kenya kuanzia uteuzi wa wagombea, kampeni, usimamizi, upigaji kura na utoaji matokeo hatua kwa hatua kuanzia vituoni hadi kwenye kutangaza rasmi...

2. Matokeo yalikuwa wazi mno kwa kila mtu kuona kila kitu mwanzo hadi mwisho. Ndiyo maana mpaka sasa kuna utulivu mkuu nchi ni Kenya kulinganisha na chaguzi zilizopita zilikuwa zikiishia kwa kunyukana kwa sbb ya kutokuwepo na uwazi ktk mchakato mzima...

3. Tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya haina impunity kama ikifanya uharamia wowote na ndiyo maana matokeo ya ushindi wa William Rutto yanapinga mahakamani...
Asante mwamna kwa ufafanuzi mzuri
 
Ahsante kwa kutujuza

IEBC iliwaengua baadhi ya Wagombea uRais

IEBC ilichanganya mabox ya kura Mombasa na Kakamega hali iliyopelekea Chaguzi za Magavana na Maseneta kuahirishwa

IEBC wameshindwa kujumlisha kura kwa Haki na sasa Kesi iko mahakamani
Hivi wewe kada wa Sisiem, johnthebaptist ukilinganisha hayo uliyoyaita mapungufu ya IEBC na Tume yetu, huoni hata aibu kulinganisha Tume hiyo na hii yetu ya makamishna watupu wa wa Sisiem, ambao wanaonyesha upendeleo wa 100% kwa chama tawala?🥺
 
Ahsante kwa kutujuza

IEBC iliwaengua baadhi ya Wagombea uRais

IEBC ilichanganya mabox ya kura Mombasa na Kakamega hali iliyopelekea Chaguzi za Magavana na Maseneta kuahirishwa

IEBC wameshindwa kujumlisha kura kwa Haki na sasa Kesi iko mahakamani..
Ungemsikiliza mpaka mwisho, ungeelewa na usingeandika hiki....

La basi, huna MB za kutosha kusikiliza hiyo video voice clip, ungesoma kwa makini muhtasari wa alichosema hapo juu...

Point No. 3 kwa mazuri ya tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya - IEBC ni kuwa, hailindwi na sheria kwa ujinga wowote inaoweza kuufanya..

That's why mgombea u - Rais wa upande wa pili aliyeshindwa, na kuonyesha kutoridhika kwake, yuko mahakamani kujiridhisha ushindi wa mwenzake...

Hilo ni nzuri. Hapa Tanzania lipo hilo? Unadhani tungekuwa na mfumo bora wa uchaguzi wa viongozi wa kuongoza serikali/nchi hii chini ya tume huru kwelikweli kama ilivyo Kenya sasa, tangu uchaguzi mkuu wa 1995 chini ya mfumo wa vyama vingi, tungekuwa na upuuzi unaoitwa CCM leo hii unadhani..?

Hakuna..!!!

Tungeshaizika CCM tangu 1995 na siyo uchaguzi mkuu wa mwaka 2000 au 2005 au 2010 au 2015 au 2020. Na taifa hili lisingeangukiaga pua kwa kujipatia the most hopeless president in the history of Tanganyika wa sampuli ya hayati John Pombe Magufuli na sasa huyu mrithi wake bibie mwimba taarabu, Bi Samia Suluhu Hassan...!

Nakuambia, CCM ingeshakuwa historia 27yrs ago...!!
 
When it comes to election in Tanzania, (the incumbent president and his/her appointees, ccm, Tiss, police, Tume ya Uchaguzi); all this bunch turns a laughing stock
They don't turn to be a laughing stock, rather they turn to be monsters killing whoever stands on their way just to avoid losing the power and authority they have...
 
Tanzania is lucky to have Tundu
Absolutely...

This guy is really a good teacher..

Jamaa anasoma vitabu sana huyu. Ndiyo maana ana ufahamu na uelewa mkubwa sana wa mambo ..

Laiti ungefuatilia mjadala huu in full length, ungeona jinsi ambavyo Steven Wasira alivyoaibika..

Ungeweza kuona jinsi ambavyo watu hawa wanatofautiana kiufahamu kama ambavyo kaskazini na kusini zilivyo mbali na ambavyo haziwezi kuja kukutana hata siku moja....
 
Back
Top Bottom