Ahsante,
Mimi nawaambia wana JF hapa, kama mnasimamia priciple za kupinga uovu, basi pingeni uovu bila kujali kwamba aliyefanya ni Slaa au Kikwete, CCM au CHADEMA.
Tatizo watu wanataka kuvaa miwani ya mbao kama matatizo ni ya CHADEMA.
Kuna mkuu alitukumbusha huko juu, kipendacho roho, chongo huita kengeza. Hata Malcolm X alipokuwa katika Nation of Islam alipoanza kupata habari za ubaradhuli wa Elijah Muhammad kuwaingilia vimwana wadogo waumini wake na kuwapa mimba alitaka kumu excuse kwa kila jinsi aliyoweza, hakuweza kuamini ati. Mpaka baadaye alivyoenda Hajj na kurudi Marekani ndipo alipofunguka macho na kuona hila za Elijah Muhammad.
Najua baadhi yetu tuna shock kuona mtu kama Slaa ambaye tulimuwekea matumaini makubwa sana anakuja kutu dissapoint vibaya hivi.Lakini ukweli - so far- unaonekana kwamba Slaa is just a man na ana matatizo yetu yale yale ya kila siku, na ana matatizo ya integrity kama uongozi wetu wa sasa.
Kwa hiyo hata kama mnaenda kumchagua Slaa, mumchague huku mnajua hili.Kwamba msitegemee muujiza, na mambo yanaweza kabisa kuwa mabaya zaidi ya CCM.
I am not a CCM fan, but I am just asking myself, kama mtu ana guts za kupiga campaign ya urais huku amemuweka kinyumba mke wa mtu, je akipata urais atakuwa na guts za kufanya nini ?