Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,101
- 2,344
This video is Courtesy of SK Media Online TV.
=====================================================
KWA UFUPI;
1. Paul Makonda ni Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi ndani ya CCM. Yupo barabarani anatembea nchi mzima hata sasa kwa kinachoitwa "ziara ya kuimarisha uhai wa chama..."
2. Ukifuatilia hotuba zake ktk mikutano yake, utaona kwa uwazi kabisa nyuma ya pazia sura ya Mtendaji mkuu wa serikali (Rais Samia Suluhu Hassan) na sio sura ya kiongozi wa idara ndogo tu ndani ya Chama Cha Mapinduzi - CCM yaani Idara ya Itikadi na Uenezi.
Mtu anaweza jiuliza, huyu mtu anafanya hivi kwa makusudi, kwa bahati ya kutojua au ana baraka za boss wake M/kiti CCM taifa na Rais wa JMT?
Ni Kwa sababu maagizo yake ni maigizo tu. Hakuna Mtendaji makini wa serikali atayatilia maanani na kuyatekeleza. Ni kwa sababu hayatoki kwa mtu sahihi kwa mtiririko wa utendaji wa kiserikali..
Mtu anajiuliza Yuko wapi Rais mwenyewe? Yuko wapi VP, Dr Phillip Mpango? Yuko wapi PM, Mwl Kassimu Majaliwa? Wako wapi mawaziri wa kisekta ili kushughulika na matatizo na changamoto za nchi? Je, ya Paul Makonda ni kiashiria cha nchi na taifa kukosa uongozi makini na thabiti? Bila shaka hili la mwisho laweza kuwa jibu..!!
3. Kwa hili kila mtu anajiuiza kuikoni huko CCM kwa maigizo haya? Mifumo sahihi haitendi kazi tena au ndio kuchoka kwenyewe huku? Na kwanini Rais Samia Suluhu Hassan, VP Dr Phillip Mpango na PM Mwl Kassimu Majaliwa wanamtanguliza huyu mtu kupiga kelele ambazo kiuhalisia hazitakuwa na matokeo yoyote kwa wananchi?
4. Fuatilia uchambuzi wa jambo hili toka Kwa mwandishi wa habari mkongwe na nguli Ansbert Ngurumo ktk video ili ujue uongo, hadaa, hila na maigizo ya serikali ya CCM kupitia watu wake wa ajabu ajabu..