VIDEO: Mkalimani aliyeingiza watu "Chemba"

VIDEO: Mkalimani aliyeingiza watu "Chemba"

Ujue kutafsiri papo kwa papo ina hitaji kufikiri kwa haraka waongeaji wana sound tofauti ..
 
"I am honoured that president Magufuli was not a great traveler, he likes to stay with his people here home'" " Ninafurahishwa kwamba Rais Magufuli hakupenda safari za nje, alipenda kukaa na watu wake hapa nyumbani/Tanzania".

Sasa, yule mkalimani alichokitafsiri ni tofauti na alichokisema Cyril Ramaphosa (SA President) kwamba "anafurahishwa kuwa Rais Magufuli hakuwa mtu wa safari za nje ya nchi bali alipendelea kukaa na watu wake hapa nyumbani/Tanzania".
 
Watu hamna dogo.

Tz sihami,
IMG-20210322-WA0040.jpg
 
Mkalimani katuvua nguo wakati wa majonzi, ndugu zetu watatusema hadi tukome.

Mkuu, Kenya ina-trend! Wanasema sisi ni wabishi. Wanasisitiza hata waalimu wa shule alizosema Ramaphosa kuwa zinafundisha kiswahili, walimu sio WaTanzania kwa sababu ili ufindishe kiswahili inakupata kujua kiingereza kwa ufasaha!!

Tumevuliwa nguo na jamaa yetu. Utetezi wa kiingereza hakina maana haupo tena!! Kumbe hatukitaki kwa sababu hatukiwezi!
 
Mi nimpongezee mkalimani huyu ni mtu smart sana sana anastahili zawadi na yupo makini na kazi yake, kiukweli katwist maneno ndio ila ameyaweka vyema sana. Marehemu si kwwli hakupenda kusafiri marehemu alikua ni great traveller mzuri tu.

Uyo alieongea kiingereza hajamsema vyema pengine hajanyoosha vyema alikua na nia njema ila hakunyoosha maelezo rahisi alikua ni mtembeaji wa ndani anasafir safar za ndani zaid ya km500 kila wiki

Angeasema was not a great traveller Abroad basi angeondoa ile generelized. I ivoo pia jamaa ni lecture na anajua lugha zaid ya 50
 
Na hasa kwenye kutafsiri alipokuwa anaongea rais wa South...
Kuna kiongozi sijui wa wapi, kasema na kumaanisha jina la Marehemu liwe katika miji mikuu ya Afrika (all African capitals), jamaa yeye kasema jina liwe katika makabati yote ya Afrika!
 
yawezekana jamaa alijua akisema jamaa hakupenda safiri na alipenda kaa home tu watu watasema alikuwa anaogopa english basi akaamua akaushe tu
Na baada ya pale, rais wa Afrika kusini aliendelea aje, pengine ilikuwa yeye alibahatika kutembelewa na Marehemu. Sasa sijui mkalimani alisema nini?
 
Mkalimani katuvua nguo wakati wa majonzi, ndugu zetu watatusema hadi tukome.
Sijui ni nguo gani tulizo nazo mwilini bado, maana marehemu alishatuvua kabla ya mkalimani.
 
Kuna kiongozi sijui wa wapi, kasema na kumaanisha jina la Marehemu liwe katika miji mikuu ya Afrika (all African capitals), jamaa yeye kasema jina liwe katika makabati yote ya Afrika!
Hakuna cha protocol wala nini. Jamaa kazingua. Ukiondoa wakenya wengine waliobaki hawajui kiswahili. So hatujaaibika sana.
 
Back
Top Bottom