Mr Dudumizi
JF-Expert Member
- Sep 9, 2020
- 6,885
- 12,325
Habari zenu wana JF wenzangu, ama baada ya salam ningependa sasa nijielekeze kwenye mada husika.
Kwa muda wa miaka mingi kumekuwa na tuhuma nyingi zinazomuhusu huyu jamaa. Wengi wakidai kwamba mwanachama huyu ni jasusi maalum ambae yuko katika kiti kile kwa sababu maalum.
Moja kati ya sababu kadhaa zinazofanya watu wawe na uhakika kuwa jamaa ni jasusi maalum ni lile picha alilolicheza mwaka 2015, ambalo baadae lilikuja kuleta matokeo chanya kwa chama tawala.
Sababu nyingine ambayo imenifanya niandike hivi ni kitendo cha mwanachama huyo kutoa kauli tata katika mazingira ambayo watu wengi hawakuyategemea, na kujiuliza inakuaje jasusi huyo aanze kutoa siri mapema kiasi kile na kuleta mtafaruku mkubwa kwa wanaomuamini.
Je, kulikuwa na sababu gani ya kujitapa mbele ya watu kwamba yeye ni mwanachama wa CCM? Inamaana ameshajiona ana nguvu kiasi kwamba anaweza kuongea lolote, wakati wowote na asifanywe chochote!!
Ama kweli dunia hadaa na walimwengu ndio mashujaa.
Kwa muda wa miaka mingi kumekuwa na tuhuma nyingi zinazomuhusu huyu jamaa. Wengi wakidai kwamba mwanachama huyu ni jasusi maalum ambae yuko katika kiti kile kwa sababu maalum.
Moja kati ya sababu kadhaa zinazofanya watu wawe na uhakika kuwa jamaa ni jasusi maalum ni lile picha alilolicheza mwaka 2015, ambalo baadae lilikuja kuleta matokeo chanya kwa chama tawala.
Sababu nyingine ambayo imenifanya niandike hivi ni kitendo cha mwanachama huyo kutoa kauli tata katika mazingira ambayo watu wengi hawakuyategemea, na kujiuliza inakuaje jasusi huyo aanze kutoa siri mapema kiasi kile na kuleta mtafaruku mkubwa kwa wanaomuamini.
Je, kulikuwa na sababu gani ya kujitapa mbele ya watu kwamba yeye ni mwanachama wa CCM? Inamaana ameshajiona ana nguvu kiasi kwamba anaweza kuongea lolote, wakati wowote na asifanywe chochote!!
Ama kweli dunia hadaa na walimwengu ndio mashujaa.