Video: Dkt. Mpango arejea ofisini, apokelewa kwa bashasha

Video: Dkt. Mpango arejea ofisini, apokelewa kwa bashasha

Wakati na bahati hupata kila mmoja, ila neema ya Mungu hutupitisha mahali tusipo dhani tunapita!

Sifa na utukufu ni vyake yeye, sio kwamba mh anasali sana, sio kwamba anamjua Mungu sana, ni neema yake Mungu yeye kuwa mzima na kusudi la Mungu litimie!
Mkuu wangu:
Maneno yako yananitia kizunguzungu. Sijui nianzie wapi na niishie wapi!
 
Nitajie hatua sitahiki ya kuzuia kolona ilituwapelekee na wazungu huko wasije wakaisha kabisaaa.
 
Mungu amsaidie 🙏 🙏 🙏 🙏 ❣️


😷😷😷😷😷😷😷😷😷😷😷😷
 
Sidhani kama umeelewa kilichoandikwa hapo , watu wanaongelea Mask kukaa na kufunika vizuri pua na mdomo wewe umekuja na habari nyingine kabisa
Ni nini kimekufanya udhani sijaelewa.
 
Waziri wa Fedha Dkt Philip Mpango amerejea kazini baada ya kulazwa kwa wiki kadhaa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma.

Amerejea na kuanza kufanya kazi ndogondogo huku akimshukuru Mungu kumponya na maradhi
 
Waziri wa Fedha Dkt Philip Mpango amerejea kazini baada ya kulazwa kwa wiki kadhaa
Kaacha kukohoa na kulia/kutoa machozi??

Kama ni ndio basi Mungu ashukuriwe kama ni Hapana basi namuombea apate nafuu,ni bora aendelee kupumzika kuliko kujilazimisha kuja kazini akiwa hayuko fiti bado. Nilimsikitikia sana alipoongea na Waandishi wa habari akingali mgonjwa
 
Waziri wa Fedha Dkt Philip Mpango amerejea kazini baada ya kulazwa kwa wiki kadhaa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma.

Amerejea na kuanza kufanya kazi ndogondogo huku akimshukuru Mungu kumponya na maradhi
Angalizo tu Ambulance isikae mbali nae.
 
Hiyo mbona irrelevant!
Humo CDC wana insist, lakini Politicians ndiyo wanaotangaza to put to an end with the aim of reopening and and getting back to normal.
Sasa sijui ulilenga ku prove nini hapo.!
CDC unfortunately iko compromised na wanasiasa. Hili gonjwa la Covid lina ugonjwa, siasa na biashara ndani yake. Bahati mbaya watu mnaangalia ugonjwa tu na hamuoni sehemu mbili zilizobakia. Na hapo ndio wengi wataumia.

Nikupe mfano hai, kama una lengo la kuelewa. California ni moja kati ya majimbo Marekani yalikuwa strict kwenye Covid. Baada ya wananchi kuchoka udikteta wakaamua kujusanya sahihi kulazimisha uchaguzi. Ghafla baada ya kuona kibarua kinaelekea kuota nyasi akaanza kulegeza masharti kipindi ambacho alidai ni hatari siku chache nyuma. Na sasa anatafuta fedha ili afungue mashule yote.

Covid imeondoka ghafla? Jibu ni hapana. Mengi ya maamuzi yalikuwa ya kisiasa na ndio maana alikuwa akiyavunja mara nyingi tu.

Issue ya barakoa wengi huongea bila ufahamu. Barakoa zinazozuia virusi ni ghali na wengi, hasa nchi za kwetu hatuzitumii. Hizi tunazozitumia hazikutengenezwa kuzuia virusi na nyingi zinakuwa sub standard. Kwa hiyo kuvaa barakoa kunampa psychological confidence mvaaji ila kiafya hazizuii virusi (isipokuwa kama unevaa zile zilizoundwa kuzuia virus)

Pili kwenye barakoa wengi hukosea kuvaa. Wakiwa wanaongea wanashusha kidevuni. Which means kama kuna virusi walikuwa kidevuni ukiipandisha unawaingiza kwenye njia ya hewa. Kwa hiyo wengi wanaovaa barakoa wana risk kubwa kutokana na misuse.

Tatu, kuvaa barakoa muda mrefu kunaweza kukusababishia infections kwenye mfumo wa hewa. Rejea utafiti wa Dr. Fauci et al juu ya spanish flu.

Kuna mengi ila hiwa nawashauri Watanzania haswa wanaoamini barakoa ni kinga, wasigeuke Gestapo kwa wale wasioamini. Kila mtu afuate anachoamini. Kama hutaki kukutana na wasiovaa barakoa, kaa zako home, maisha yaendelee. Vinginevyo wanaweza jikuta ni madikteta wasio na madaraka.

Anyway, nimeandika zaidi ya nilivyokusudia, naamini kuna mtu atasaidika.
 
Back
Top Bottom