Inadaiwa huyu askari alimkodi huyo boda boda kwenye video na baada ya kumzungusha kwa saa moja kagoma kumlipa, kwa mujibu wa maelezo ya boda kulitokea ugomvi ambao ulisababisha huyo polisi kumng'ata kidole huyo boda hali iliyomfanya yeye ampige ngumi ndipo alipomuachia.
Hizi aibu kwa jeshi hili zimepita kiasi, Ila kadiri wananchi tunavyoondoa hofu ndivyo ambavyo wao wanapoteza nguvu yao.
Kauli ya Wizara ya Mambo ya Ndani ~ Patrobas Katambi: Tutachunguza clip ya Bodaboda kuvutana na Askari Polisi, haki itatendeka