Vibanda vilivyowekwa kando ya barabara Jijini Dar es Salaam kuondolewa

Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es Salaam.

--- UPDATE MAY 11, 2021--

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri amewataka wafanyabiashara waliojenga vibanda katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuviondoa kabla ya Mei 18, 2021.

Wakati Shauri akieleza hayo, gari lenye spika za matangazo linapita katikati la mitaa ya Jiji hilo likitangaza kuhusu mchakato huo kwamba vibanda havitakiwi kuonekana kando ya barabara.

Akizungumza na Mwananchi Digitial leo Jumanne Mei 11, 2021 Shauri amesema hawajazuia wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao, wanachotakiwa kufanya ni kutojenga vibanda na kuwataka wauze bidhaa zao kwenye meza ili wakimaliza iwe rahisi kuziondoa na kuacha maeneo wazi.

Amebainisha kuwa sheria ya mipango miji hairuhusu kujenga vibanda, kuwataka wafanyabiashara hao kutii agizo hilo.

“Mwisho Mei 18 kama ambavyo gari la matangazo linavyotangaza waviondoe vibanda vyao kwa sababu vingine vinajengwa hadi kwenye njia za watembea kwa miguu na barabarani na kuleta adha kwa watumiaji. Wanatakiwa watii sheria bila shuruti waviondoe wenyewe,” amesema Shauri.

MWANANCHI

Wasiwasi wangu ni baadae hata hizo meza kusema waondoe
 
Huyo mkuu kajichanga kutoa maamuzi, hakuna sheria inayoruhusu kuweka meza ya biashara kando ya barabara, hivyo alipaswa kusema vibanda, meza ni marufuku.

Hawa wenye mamlaka sijui wanakwama wapi?
No, Sheria ni sawa hakuna ata kuweka izo meza lakini kuna ile kwamba Serikali inawasaidia hawa wafanyabiashara wadogo wadogo ili maisha yaende, kule Zanzibar Dr Shein aliondoa vibanda vyote maeneo ya darajani ambapo ndio eneo mashuhuri la biashara Zanzibar lakini Mwinyi kasema HAPANA watu wamerudi kiasili biashara kirindanda, jambo hili linatoa motisha kwa kiongozi aliye madarakani angalau kupunguza chuki kwa wananchi
 
No, Sheria ni sawa hakuna ata kuweka izo meza lakini kuna ile kwamba Serikali inawasaidia hawa wafanyabiashara wadogo wadogo ili maisha yaende, kule Zanzibar Dr Shein aliondoa vibanda vyote maeneo ya darajani ambapo ndio eneo mashuhuri la biashara Zanzibar lakini Mwinyi kasema HAPANA watu wamerudi kiasili biashara kirindanda, jambo hili linatoa motisha kwa kiongozi aliye madarakani angalau kupunguza chuki kwa wananchi
Kwa hiyo sheria inarusu wananchi hasa wanyonge wazibe njia za waendao kwa miguu, waweke biashara popote watakapo?

Walianza kama mzaha tu pale kariakoo ('soko la kimataifa' ) leo hii hapapitiki kuna meza zisizo hamishika yaani panakeraa sana.

Mimi naamini wanao haribu majiji yetu (hasa Dar) ni viongozi wenye dhamana
 
Kwa hiyo sheria inarusu wananchi hasa wanyonge wazibe njia za waendao kwa miguu, waweke biashara popote watakapo?

Walianza kama mzaha tu pale kariakoo ('soko la kimataifa' ) leo hii hapapitiki kuna meza zisizo hamishika yaani panakeraa sana.

Mimi naamini wanao haribu majiji yetu (hasa Dar) ni viongozi wenye dhamana
Ukiona hivyo serikali yenyewe imeshindwa kutoa ajira sasa wananchi lazima watafute namna na wakijaribu kulazimisha ndio yale madhara ambayo ni mabaya zaidi yatatokea wizi, watu kufa njaa, umasikini uliokithiri na kama hayo

Wewe unakereka kupita njia lakini wenzako wanateseka kimaisha mtu ata mlo 1 kwa siku inabidi akazungushe zungushe hapo kariakoo akale na watoto., jambo hili kwa nchi masikini huwezi kuliepuka. Na shida kubwa kwamba 'Aliyeshiba hamjuwi mwenye njaa'

Nchi zilizoendelea huwezi kukuta hizo interference kwenye miji kama huko kwenu sababu tayari ambaye hana kiajira kwenye kampuni au government basi angalau anapata bonus mwisho wa mwezi kutoka Serikalini, kuna njia nyingi za kutafuta kipato
 
Ukiona hivyo serikali yenyewe imeshindwa kutoa ajira sasa wananchi lazima watafute namna na wakijaribu kulazimisha ndio yale madhara ambayo ni mabaya zaidi yatatokea wizi, watu kufa njaa, umasikini uliokithiri na kama hayo

Wewe unakereka kupita njia lakini wenzako wanateseka kimaisha mtu ata mlo 1 kwa siku inabidi akazungushe zungushe hapo kariakoo akale na watoto., jambo hili kwa nchi masikini huwezi kuliepuka. Na shida kubwa kwamba 'Aliyeshiba hamjuwi mwenye njaa'

Nchi zilizoendelea huwezi kukuta hizo interference kwenye miji kama huko kwenu sababu tayari ambaye hana kiajira kwenye kampuni au government basi angalau anapata bonus mwisho wa mwezi kutoka Serikalini, kuna njia nyingi za kutafuta kipato
Kama serikali imeshindwa kurekebisha hilo tatizo la wanyonge kushindia mlo mmoja ama kukosa kabisa basi haina budi kuachia ngazi
 
Gari la tangazo linapita kutangaza ya kuwa ifikapo tarehe 18 mwezi huu hakitakiwi kibanda chochote kuonekana kando kando ya barabara katika jiji la Dar es Salaam.

--- UPDATE MAY 11, 2021--

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Jumanne Shauri amewataka wafanyabiashara waliojenga vibanda katikati ya Jiji la Dar es Salaam kuviondoa kabla ya Mei 18, 2021.

Wakati Shauri akieleza hayo, gari lenye spika za matangazo linapita katikati la mitaa ya Jiji hilo likitangaza kuhusu mchakato huo kwamba vibanda havitakiwi kuonekana kando ya barabara.

Akizungumza na Mwananchi Digitial leo Jumanne Mei 11, 2021 Shauri amesema hawajazuia wafanyabiashara kuendelea na shughuli zao, wanachotakiwa kufanya ni kutojenga vibanda na kuwataka wauze bidhaa zao kwenye meza ili wakimaliza iwe rahisi kuziondoa na kuacha maeneo wazi.

Amebainisha kuwa sheria ya mipango miji hairuhusu kujenga vibanda, kuwataka wafanyabiashara hao kutii agizo hilo.

“Mwisho Mei 18 kama ambavyo gari la matangazo linavyotangaza waviondoe vibanda vyao kwa sababu vingine vinajengwa hadi kwenye njia za watembea kwa miguu na barabarani na kuleta adha kwa watumiaji. Wanatakiwa watii sheria bila shuruti waviondoe wenyewe,” amesema Shauri.

MWANANCHI

I hail the decision. They are a high environmental pollutant.
 
Rahisi. Watengewe maeneo "special" na siyo hovyohovyo ilivyo kwa sasa.
Tatizo lipo kwetu wanunuzi. Wakitengewa eneo hatuendi kununua huko tunabaki kununua barabarani, ndio maana wanaacha maeneo waliyotengewa wanarudi barabarani. Imeshatokea machinga complex na sehemu nyingine nyingi tu
Tuache kununua barabarani tuone kama watabaki.
 
IMG_0583.jpg

IMG_0582.jpg

IMG_0581.jpg
 
Back
Top Bottom