KERO Vibaka wamekithiri katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja

KERO Vibaka wamekithiri katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi ni mdau wa JamiiForums, naishi Zanzibar mkoa wa Mjini Magharibi, Shehia ya Kwahani.

Kero yangu kwa mamlaka za Usalama na hasa Jeshi la Polisi Zanzibar - mbona lipo kimya sana huku kukiwa na matukio ya baadhi ya wananchi mitaa hiyo wakitembea usiku na mchana Kuna vibaka wanawapora Mali walizokuwa zao?

Zinaweza kuwa Aidha ni simu au Pesa na kisha wanawashambulia kwa silaha za ncha kali na kuwaacha na majeraha mwilini.

Zilisharipotiwa kesi kadhaa katika vituo vya Polisi lakini bado Jeshi la Polisi mkoa wa Mjini Magharibi lipo kimya na hakuna hatua zilizochukuliwa huku hali ya hofu ikiwa kubwa katika baadhi ya mitaa ya mkoa wa Mjini Magharibi
 
Vibaka watoke wapi kwenye nchi ya kidini kama ile, ina maana dini haifundishwi tena?
 
Nilitaka kuja huko kupumzika baada ya hekaheka nyingi kumbe huko kwa moto.

Hivi Mtambuzi where you ?
 
BAADA YA MUDA SI MREFU UTASIKIA VIBAKA WAMETOKA BARA
 
Vibaka watoke wapi kwenye nchi ya kidini kama ile, ina maana dini haifundishwi tena?
Tuliza mshono dogo siyo lazima uchangie hoja,masuala ya dini yanatafuta nini sasa?Au ndiyo unatafuta basha kinguvu?
 
Back
Top Bottom