UTEUZI: Rais Samia amteua Jenerali Venance Mabeyo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro

Naomba kujua jambo hili kwanza namkubali mama na sina nongwa na mabeyo ila!? Naomba mwenye kumjua mtu huyu. Elisifa Ngowi alikuwa RSO MOROGORO akaletwa dsm kama drso wa dar baadae akapelekwa ikulu na alipostahafu tiss inasemekana CIA walimpa contract na baadae akaibukia kwenye tanapa na ile operation iliyolalamikiwa sana wakati wa jpm alikuwa master mind beyond the curtain!!!
Yaani ufanye kazi CIA kirahisi rahisi afu ubaki salama
 
Hapo wamasai kazi tunayo.

Lakini kwakua Mabeyo ni mfugaji mwenzetu labda atatuelewa.
Tatizo pekee lililopo ninaloliona mimi hapa ni pale mtakapomwambia kuwa ng'ombe alizonazo huko kwao usukumani ni za kwenu wamasai! Atakachofanya baada ya hapo ni kujiuzulu uenyekiti wa Bodi na kukimbia kabisa Ngorongoro, na hatarudi tena huko. Mkitaka Mabeyo awaelewe vizuri wamasai, wakusanyeni ng'ombe wote mlionao huko umasaini muwapeleke usukumani!
 
In less than 24 tokea amestaafu kashapewa ajira nyingine, kwa style hii vijana watasubiri sana, chifu kaamua kutumia mjeshi kuzima sakata la loliondo
Sasa mda mwingine mlalamike muwe na logic bas hv kijana aliemaliza chuo Cha wanyamapori pasiansi au sijui udom nk Leo mnataka ateuliwe kua mwenyekiti wa bodi kweli embu tuwen serious kidogo
 
Kitendo cha mabeyo kuteuliwa na mh rais kuwa Mwenyekiti wa bosi ya uhifadhi wa Ngorongoro je ni mtego kwake au ni njia ya kunyamazisha Makele ya wanaharakati dhidi ya hamisha hamisha ya wenyeji kwenda handeni?
 
Kitendo cha mabeyo kuteuliwa na mh rais kuwa Mwenyekiti wa bosi ya uhifadhi wa Ngorongoro je ni mtego kwake au ni njia ya kunyamazisha Makele ya wanaharakati dhidi ya hamisha hamisha ya wenyeji kwenda handeni?
Njia ya rais kuendelea kutisha watu, kama Magufuli!
 
Ni Uteuzi wa Kupongezwa, Yaliyomo kwenye Hifadhi Ngorongoro sio kuhamisha watu tu,
Kuna lililo kuu ambalo ni Kuhifadhi Hifadhi yenyewe.
Hapo ameonekana bado anahitajika kwenye utumishi nchini.
 
Back
Top Bottom