Uteuzi: Rais Samia amteua Humphrey Polepole kuwa Balozi Malawi, Mchechu arudishwa NHC

kuna kakikundi kamoja kanajifanya kanataka kujimilikisha nchi yetu ya Tanzania na kuifanya mali yao ya kifamilia yao "ya ukoo wao". Hii nchi kuna siku tutaidai mikononi mwao, wanajaribu kutuchezea chezea kama midori. Siku moja watatafuta kwa kuficha sura zao mbaya....:(:(:(. Watanzania sio wapole, sio wote wazungumzaji..ukiwaficha wazungumzaji ambao wanawakilisha upande wa sisi ujue unazidisha chuki upande wako
Utakuwa mfuasi mfia jiwe wewe si bure
 
Inasemekana kuna njaa Malawi na ushauri ni Polepole achukuwe nafaka Tanzania hasa mahindi na maharage.

4F495FA5-2BBE-4AF7-9DD1-AD224F0544AD.jpeg
 
Kwa anaejua, ernest mangu bado ni polisi? Anavaa sare za polisi. Na kama kastaafu ni lini?
 
Hiki kibibi bwana, mwalimu wake alifeli na yy anawlwkea huko huko.
 
Kijana mfupa hauwezi bora aende zake Malawi akale mema ya nchi, baada ya hapo apelekwe Afghanistan, Bulgaria na Mongolia....

Vita na hao wazee wa SAIGON bwana mdogo Polepole haiwezi, Hiyo vita kaipigana Lowasa kashindwa kutimiza ndoto zake na wamemtuliza, nk nk...Polepole bado sana..sema tu ndio vile tu wazee wa saigoni hawapendi kelele....vyeo vipo vingi...wangeweza kumuweka benchi na bado asingewafanya kitu...

Mkuu ukizungumzia SAIGON ninaamini wanaokuelewa hawajai hata kiganja cha mjukuu wangu hivyo simplify kwa kuwaita wahuni tu na kadamnasi itakuelewa zaidi
 
Kuteuliwa na Mkuu Wa Nchi kumuwakilisha kama Balozi ni heshima kubwa, inawezekana isiwe nafasi kubwa kwako lakini inaonyesha imani kubwa aliyo nayo Rais kwako.

Wapo wanaosema kelele zako zimemuwasi usingizi lakini yote kwa yote nenda katuwakilishe vyema.

Binafsi nilitamani ubaki ndani na kelele zako ili uwaseme vizuri wahuni lakini siyo mbaya

Ulitembea na uongozi uliopita yapo mazuri mliyofanya na yapo ya hovyo pia, nilidhani ukibaki ndani unaweza kuisaidia zaidi CCM na kumshauri zaidi Rais kundi litakalokuja sasa hivi kwenye uchaguzi Wa chama linaweza kubwa na sura mpya nyingi watu wamejifuta tongotongo,
lakini wewe nenda tu.

Kwa sababu unakuja hapa pembeni ya Tunduma tu wengine tutakutembelea kijana wetu.

Hapa ni karibu utaendelea kupata habari za wahuni

Wengine wangetamani ungeteuliwa kwenda ubarozi ukraine, washindwe na walegee. Ningejua mapema ningemuomba hiyo nafasi uliyoachia ya ubunge lakini bahati mbaya imeshagawiwa kwa Mtz mwingine.

Uishi milele Samia Suluhu Hasani pigs kazi Dada yetu.
 
Uchanjwe uwe balozi, au ushikilie msimamo utoke kabisa kwenye mfumo?...Nimempigia muda huu namuuliza hill swali anashindwa kujibu, analia tu. Namuuliza nini kinakuliza bro?! Anasema huu mwezi ndio aliondoka mzee, namkumbuka sana. Namuuliza, mzee yupi? Anajibu, dogo kataa wahuni.🤣🤣
 
Simpi hongera maana ni kama anaenda fichwa utulivu upatikane. Huo ni mtego hatari sana kwa Polepole maana lazima achome kinga ya COVID-19. Pili yuko chini ya mamlaka ya rais na si spika, anaweza fukuzwa anytime bila kuchelewa. Ajiandae na yajayo maana si mepesi.....ataonyeshwa mamlaka aliyonayo Rais wa nchi.
 
Back
Top Bottom