Utawala wa Awamu ya 5 kulikuwa na kampeni ya wazi ya kutaka aliyekuwepo aongoze milele, Sababu hasa ya kampeni hii ilikuwa nini?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,779
218,404
Tunaendelea na nyuzi zetu za mwezi wa 3, ambao ni mwezi wa Mungu.

Ni wazi kila mwananchi anafahamu kuhusu kampeni za wazi kabisa za kutaka Rais wa awamu ya 5 Dkt John Magufuli aongezewe muda wa utawala wake kinyume kabisa cha Katiba ya Tanzania, yaani baada ya kumaliza utawala wake wa miaka 10, bado aongezewe miaka mingine isiyo na idadi.

Kampeni hii kabambe iliongozwa na kundi lisilo rasmi lililopachichwa jina la "Sukuma gang" na baadaye kuanza kuungwa Mkono hadharani na baadhi ya watu , na hatimaye likatua bungeni likiletwa na mbunge wa ccm Jimbo la Nkasi (zipo taarifa kwamba nyuma yake kulikuwa na kundi kubwa), Huku hoja yake ikiungwa mkono na Spika wa Bunge hilo Job Ndugai , na kwamba inasubiriwa muda ufike lipelekwe bungeni ili lijadiliwe na Katiba ya Nchi ibadilishwe.

Screenshot_2024-03-18-15-22-08-1.png


Hata baada ya Jambo hilo kupoa kidogo likaibuliwa tena na Mbunge wa Bahi Juma Nkamia , akisisitiza umuhimu wa kumuongezea John Magufuli muda wa uongozi , huku akisisitiza kwamba muhula wa Urais uwe miaka 7 badala ya mitano iliyowekwa kwenye Katiba ya Nchi .

Wale wote waliopinga jambo hili walionekana Wasaliti na walishughulikiwa chini kwa chini na Wateule wa Rais kuanzia kwenye chama hadi serikalini , huku Wateuliwa wengi wakichekelea na kuvimba kwa kiburi wakijua watakuwa wateule milele (Hapa ndipo ilipoanzia sumu aliyolishwa Mangula)

Ushahidi wa wapinga milele kushughulikiwa ulikuja kuthibitishwa na Juma Nkamia mwenyewe , alipokiri hadharani kwamba Alilazimika kutamka kwamba Magufuli aongezewe muda ili kunusuru uanachama wake ndani ya ccm , kwamba kulikuwa na mpango wa kumvua uanachama , na kwa vile mkubwa alifurahishwa na kauli ya Nkamia ya kumuongezea muda , Nkamia hakutimuliwa tena .

Screenshot_2024-03-18-13-20-07-1.png


Wakati haya yakiendelea , Viongozi karibu wote wastaafu walikuwepo huku wakinyamaza kimya as if hakuna uchafu unaopangwa , Wakuu wa vyombo vya dola wakiwa kimya ikiwa ni ishara ya kuunga mkono uharamia huo .

Sasa Swali letu ni hili , Waliokuwa wanafanya Kampeni hiyo haramu walichagizwa na nini hasa , Je ni Utendaji bora wa Magufuli na kwamba hakuna Mwanaccm mwingine angeweza kutenda kama Yeye , ama walichagizwa na Uroho wa madaraka ili waendelee kula miaka yote baada ya Rafiki yao kuwa madarakani milele ?

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
 
Kwa kauli yake mwenyewe alisema hataongeza hata dakika moja siku akimaliza uongozi wake,

Point to note moja ya watu ambao walitoa kauli ya suala la kuongezewa muda ni aliyekuwa Mbunge wa kule Rukwa ambae alisema atapeleka hilo jambo rasmi Bungeni ili lijadiliwe

Mwaka 2020 alivyoanguka kwenye uchaguzi (akiangushwa na Mbunge wa Chadema) mbona Mwendazake hakumrudisha Bungeni wakati ana nafasi 10 za uteuzi na wengi ambao walikuwa na hizo nafasi wameingia jimboni na wamepata ushindi?? Mf. Dkt. Mpango??

Hii inaonesha wazi hakuwa na mpango huo na kama angekuwa nao angekuwa wa kwanza kumrejesha yule ambae alionesha hadharani kutaka kulipeleka hilo suala bungeni
 
Kwa kauli yake mwenyewe alisema hataongeza hata dakika moja siku akimaliza uongozi wake,

Point to note moja ya watu ambao walitoa kauli ya suala la kuongezewa muda ni aliyekuwa Mbunge wa kule Rukwa ambae alisema atapeleka hilo jambo rasmi Bungeni ili lijadiliwe

Mwaka 2020 alivyoanguka kwenye uchaguzi (akiangushwa na Mbunge wa Chadema) mbona Mwendazake hakumrudisha Bungeni wakati ana nafasi 10 za uteuzi na wengi ambao walikuwa na hizo nafasi wameingia jimboni na wamepata ushindi?? Mf. Dkt. Mpango??

Hii inaonesha wazi hakuwa na mpango huo na kama angekuwa nao angekuwa wa kwanza kumrejesha yule ambae alionesha hadharani kutaka kulipeleka hilo suala bungeni
Ngoja wadau wajadili
 
Hizo zilikuwa ni hearsays tu

Sidhani kama mlengwa aliwahi kutamka hayo hadharani juu ya jambo hilo

Isije kuwa zilikuwa mbinu za Wapambe tu kutaka kuharakisha safari ya Mwamba

Maana sote tunajua jinsi "Wapambe walivyo na nguvu kuliko mwenye Mali" 🙌
 
Tunaendelea na nyuzi zetu za mwezi wa 3, ambao ni mwezi wa Mungu.

Ni wazi kila mwananchi anafahamu kuhusu kampeni za wazi kabisa za kutaka Rais wa awamu ya 5 Dkt John Magufuli aongezewe muda wa utawala wake kinyume kabisa cha Katiba ya Tanzania, yaani baada ya kumaliza utawala wake wa miaka 10, bado aongezewe miaka mingine isiyo na idadi.

Kampeni hii kabambe iliongozwa na kundi lisilo rasmi lililopachichwa jina la "Sukuma gang" na baadaye kuanza kuungwa Mkono hadharani na baadhi ya watu , na hatimaye likatua bungeni likiletwa na mbunge wa ccm Jimbo la Nkasi (zipo taarifa kwamba nyuma yake kulikuwa na kundi kubwa), Huku hoja yake ikiungwa mkono na Spika wa Bunge hilo Job Ndugai , na kwamba inasubiriwa muda ufike lipelekwe bungeni ili lijadiliwe na Katiba ya Nchi ibadilishwe.

View attachment 2938286

Hata baada ya Jambo hilo kupoa kidogo likaibuliwa tena na Mbunge wa Bahi Juma Nkamia , akisisitiza umuhimu wa kumuongezea John Magufuli muda wa uongozi , huku akisisitiza kwamba muhula wa Urais uwe miaka 7 badala ya mitano iliyowekwa kwenye Katiba ya Nchi .

Wale wote waliopinga jambo hili walionekana Wasaliti na walishughulikiwa chini kwa chini na Wateule wa Rais kuanzia kwenye chama hadi serikalini , huku Wateuliwa wengi wakichekelea na kuvimba kwa kiburi wakijua watakuwa wateule milele .

Ushahidi wa wapinga milele kushughulikiwa ulikuja kuthibitishwa na Juma Nkamia mwenyewe , alipokiri hadharani kwamba Alilazimika kutamka kwamba Magufuli aongezewe muda ili kunusuru uanachama wake ndani ya ccm , kwamba kulikuwa na mpango wa kumvua uanachama , na kwa vile mkubwa alifurahishwa na kauli ya Nkamia ya kumuongezea muda , Nkamia hakutimuliwa tena .

View attachment 2938287


Wakati haya yakiendelea , Viongozi karibu wote wastaafu walikuwepo huku wakinyamaza kimya as if hakuna uchafu unaopangwa , Wakuu wa vyombo vya dola wakiwa kimya ikiwa ni ishara ya kuunga mkono uharamia huo .

Sasa Swali letu ni hili , Waliokuwa wanafanya Kampeni hiyo haramu walichagizwa na nini hasa , Je ni Utendaji bora wa Magufuli na kwamba hakuna Mwanaccm mwingine angeweza kutenda kama Yeye , ama walichagizwa na Uroho wa madaraka ili waendelee kula miaka yote baada ya Rafiki yao kuwa madarakani milele ?

NITASEMA KWELI DAIMA FITINA KWANGU MWIKO
Lengo hasa mafisadi waendelee kama wanavyotaka
 
Back
Top Bottom