Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Punguza kupenda bure na rahisi mkuu m’ spoil uyo binti, ameshakujua na wewe ndo wale wa “njoo ghetto uchukue hiyo hela” ndo anakuja kuifata tu apo, narudia tena punguza kupenda vya bure m’spoil uyo binti....
 
Unapokuwa unazungumza swala la uovu wa wanaume, sijajua ni kwann unafanya kuwa ni ajenda ambayo kuna mtu anaitetea au kuipendekeza.....

Umeshasema ni uovu why sasa nipende uendelee......?!
Kwa sababu sijawahi kuona maovu ya wanaume yakikemewa kama yanavyokemewa ya wanawake! Zaidi sana utapewa sababu zile zile kuwa oh wanawake ndiyo wanaumia zaidi ilihali wanaume hawana cha kupoteza mara oh sijui wanawake wakianza wanaume ndiyo watafuata!

Hii inafanya jamii ione kama wanaume kufanya maovu ni sawa tu kwa sababu hayakemewi na ati hawana cha kupoteza! Haya tangu muanze kutoa hizo sababu zisizo na kichwa wala miguu zimesaidia nini kwenye jamii je kuna matokeo yoyote chanya!

Hivi kwanini tusiache tu kuwa biased na tuwe tunakemea maovu ya jinsia zote bila kuangalia nani anaumia zaidi au sijui nani hana cha kupoteza! Kwa sababu unaposema eti mwanamke ajitunze halafu hapo hapo hukemei tabia ya wanaume kurubuni au kubaka wanawake huoni kama utakuwa unafanya kazi ya kumtawaza mbuzi!

Hiyo jamii mnayoitaka ya kwamba eti mwanamke ndiyo aanze kubadilika halafu mwanaume atafuata haipo na haitakaa itokee zaidi sana ndiyo mnazidi kuharibu tu! Na hata tukitrace back kwenye history utagundua wanaume ndiyo walioanza maovu kwenye mapenzi hata pale ambapo wanawake wengi walikuwa innocent (naomba usiniletee story za Adam na Evah hapa naongelea ancient na medieval times)!

Kwahiyo mtu atakushangaa utakapoanza kumuambia eti wanawake ndiyo waanze kubadilika halafu wanaume ndiyo watafuata kana kwamba wanawake ndiyo walianza hayo maovu! Lazima atakuuliza kama ninyi ndiyo mlianzisha na mkashindwa kubadilika hata pale wanawake walipokuwa innocent ndiyo mnataka mbadilike sasa hivi!

Ni wazi kwamba wanaume wengi wanataka jamii ambayo ni wanaume tu ndiyo watakaoruhusiwa kufanya maovu na ionekane ni sawa (kama ilivyokuwa zamani) ila wanawake wanatakiwa kuwa wakamilifu tu siku zote! Mnashindwa tu kusema directly mnakaa mnazunguka lakini mtu akisoma between the lines ya mnavyoviandika atagundua hiki ndicho mnachokitaka!

Na mbaya zaidi ni kwamba hiki kitu hakiwezekani na hakitakaa kiwezekane! Wanaume wa zamani walipokuwa wanafanya maovu hawakujali mambo ya kubadilika walijiona wako sawa tu na walitegemea wanawake wangeendelea kuvumilia maovu yao milele!

Sasa tuko kwenye modern times wanawake wameamua kujibu mapigo baada ya kuchoka kuvumilia ujinga ndiyo wanaume wanaanza kuongelea habari za kubadilika! Hii ni baada ya kuona na wao wanaanza kuumia sasa kutokana na wanawake kuamua kujibu mapigo ndiyo wanajifanya wamekuwa wahubiri wa mabadiliko!

Tena na bado kwenye hayo mahubiri wanaanza kuleta siasa sasa eti wanawake ndiyo waanze kubadilika halafu wanaume watafuata! Wakati ukweli ni kwamba wanataka turudi kwenye jamii za zamani zile ambazo mwanaume alikuwa anafanya makosa na mke anavumilia tu kwa sababu mwanaume kufanya makosa ilikuwa kawaida na mke kukosea ilikuwa ni jinai!

Kama kila jinsia imeshindwa kubadilika kwa nafasi yake mimi naona tuendelee tu hivi hivi huu mchezo wa kuviziana na kupimiana! Hata kama wanawake ndiyo wanaumia zaidi lakini trust me sidhani kama siku hizi wanaumia kama walivyokuwa wanaumia zamani!

Maana imagine zamani mwanamke alikuwa anaumia huku hafaidiki na chochote ilihali mwanaume alikuwa hana cha kupoteza kabisa! Siku hizi mwanamke anaumia lakini atleast wana pa kujipoozea ambapo ni kwenye pesa za wanaume na hiki kinawaumiza wanaume wengi ndiyo maana wanalalamika kingekuwa hakiwaumizi wasingekuwa wanalalamika!

Fact is mwanaume huwa hapendi kupoteza chochote mbele ya mwanamke yaani siku zote anapendaga atoke mshindi kwenye hii vita ya mapenzi (ofcourse siku hizi mapenzi yamekuwa vita)! Sasa inapotokea wanaona kuna vitu wameanza kupoteza hasa pesa lazima tu waanze kujifanya wahubiri wakati wasingekuwa wanapoteza hata hizo pesa wasingekuwa wanaongea chochote narudia tena wanaume hamjawahi kusimamia kidete suala lolote ambalo haliwanufaishi ninyi binafsi!
 
Tusipokua makini huko mbele tutakua na kizazi cha Ovyo...mno
Hata kizazi cha sasa kimevurugika sana. Jaribu kutazama tu enzi za zile wakati unakua, na kipindi cha hawa wadogo zetu now, utaona watoto wanajua mambo mengi kabla akili hazijakomaa vya kutosha.
 
Kama utakumbuka maneno ya baba wa taifa, Hayati Julius Kambarage Nyerere, kuwa miongoni mwa maadui wa kuwapiga vita usiku na mchana na kuhakikisha wametokomea basi UMASIKINI ni nambari one.

Sababu umasikini ukitapakaa kwenye jamii utatengeneza njia kwa mambo mengi sana mbaya kuingia, mfano tamaa, njaa, maradhi, uhasama, chuki, usaliti, rushwa, na kadhalika.

Hili la watoto wa kike kupenda sana pesa lina uhusiano na insecurities zitokanazo na umasikini wa hali na akili huko walipotoka yaani makwao na familia zao.

Binti aliyelelewa kwa maadili ya utu hawezi kuwa na tamaa za mali au pesa ya mwanaume ambaye si mume wake. Mabinti wa sasa wanatoka familia zenye mentality za kimasikini sana yaani baba na mama wanataka kupata maisha kupitia mtoto wao, haijalishi anatoa wapi.

Kuna vitu vingi vinawaponza watoto wa kike, mfano, kutaka kuonekana mrembo kwa mavazi ya kisasa, kumiliki simu za bei, kuhang maeneo ya bata ya gharama ili kuweza kupiga picha za kupost kwenye social networks na social media. Pesa za kumudu haya yote unadhani wanatoa wapi na wanatoka familia za kipato cha chini kabisa.....

Lakini mbaya zaidi ni pressure ya familia wanazotoka hawa mabinti kuwaambia kuwa mwanaume ambaye hana pesa hana cha kukupa katika maisha, nyuma ya pazia, ni hii familia ya binti kutafuta mfadhili kupitia binti yao awatatulie matatizo yao ya ndani ya kifamilia.

Tukirejea miaka ya nyuma kidogo, si kwamba watu walikuwa na pesa sana, lahasha, bali utu ulishika nafasi yake na umasikini haukuwa na nafasi katika jamii.

Kukosa pesa sio umasikini bali ni hali ya kiuchumi ya kutokuwa na kipato. Ila umasikini ni tamaa ya kutaka kuwa na miliki isiyo stahiki yako ukilinganisha na jitihada zako wewe binafsi. Na ndio maana hata watu wezi, mafisadi, wadangaji, mbele ya safari huishia kufilisika sababu ndani ya nafsi zao ni masikini.

Uamasikini unaambukiza (contagious), umasikini ni hali ya akili kuamini mafanikio ni muujiza na sio uhalisia wa matokeo ya jitihada.

Umasikini unapigwa vita kwa kutafuta namna tofauti tofauti za kujitafutia kipato bila kudharau ni kiasi gani unaingiza bali muhimu ni malengo ya leo, kesho na kesho kutwa kipato kinakupeleka wapi kukutoa hapo ulipo.

Tunaposema umasikini ni adui wa taifa haya ndo matokeo ya kudharau hiyo kauli. Unakutana na binti anatumia mwili kama qualifications ya kufanya maisha na wewe ila ukikaa nae ndani hana mchango katika swala la kupigana na umasikini cha zaidi atavuta familia yake waje karibu yenu wamsaidie kukuambukiza umasikini.

Ukiona mwanamke hana elements za productivity kwa namna yoyote basi jua unaandaa kizazi au familia ya watu masikini. Mwanamke mwenye maradhi ya umasikini hatokei familia ya watu wa kipato cha chini, anatokea familia ya watu wasio na utu na wenye uchu na tamaa, hao ni masikini pure, aidha wawe na pesa au mafukara umasikini utaugundua kwao kupitia tabia zao za tamaa na uchu na husuda za kukurudisha nyuma wewe ili wao kupata.

Nilishawahi ona familia ya mzee ambae hana uwezo sana, ni mkulima tu wa kipato cha chini, binti yake ameolewa na kijana ana uwezo wa kipato cha kati. Ila yule mzee kila mwezi alikuwa anafunga kiroba cha mahindi, unga, na gallon kubwa ya mafuta ya alizeti kumtumia binti yake na mumewe kutoka kwenye ghala yake. Na akifanya mauzo ya mazao yake ya kilimo anatoa sehemu ya pesa anamtumia kijana na binti yake.

Imagine huyu mzee utamwita ni masikini?! Au huyu binti anatoka familia ya kimasikini?! Umasikini ni akili au fikra ya kuendekeza tabia ya kuelemea wengine ile hali unaweza kupambana kujitafutia na ukasaidia wengine.

Sasa leo, kupitia elimu, tumezalisha kundi kubwa la vijana makabwela na mafukara wa hiyari wasio na mawazo ya maendeleo hata kidogo. Hebu wazia ni kwa namna hii tutafikia malengo ya taifa kweli ya kuwa uchumi wa kisasa na kuwa na idadi ndogo sana ya watu wa kipato cha chini.....?!

So ndugu, kumalizia tu niseme, ukiona binti analeta mazoea ya kuomba pesa usipepese macho wala kuona aibu, mwambie ukweli, mwambie aache tamaa na kuendekeza akili za kimasikini, kama anataka kupata mahitaji kwako kwanza ajue wajibu wake kwako katika vita na umasikini miili ya ngono hii isikuponze ukatumia pesa yako uliyoipata kwa shida sana kirahisi rahisi kisa unafuata maneno ya mjini kuwa sijui mwanaume wa kweli sio bahiri kwa mwanamke.

Mtawalaumu hawa mabinti wanaodanga ila ukweli ni kuwa sisi wanaume baadhi yetu ndio tunachangia huu utomvu wa maadili na nidhamu kukua. Imagine kama wanaume wote tukaweka azimio la kutotoa pesa za matumizi katika maswala ya ngono nje ya kusaidia, utaona kama hawa wadangaji watakuwapo.

Kwanza familia zitaimarika, ndoa zitaheshimika, na wanawake watajua umuhimu wa ndoa. Hivi viburi vyao vinakuja sababu wahongaji na mabwege wa kutoa hela mpo wengi, na mimi nasema nikikuta mwanaume ambaye hajaoa mwanamke ila alikuwa ana muhudumia kama mke kisha huyo mwanamke akapata mtu mwingine akapita hivi, mimi nitatetea huyo mwanamke, sababu yupo sahihi hawezi olewa na mwanaume mpuuzi anayetoa pesa nje ya familia au nje ya ndoa.

Huwa tunawaona wanawake ni wakatili kwa kuwakimbia watu waliowahudumia ile hali hawakuwa wanaume wao wa ndoa. Ila ngoja nikwambie wanawake wenye akili huwa wakiona mwanaume ni bahiri wanajua huyu sasa ni mwanaume wa ndoa maana pesa zake hazitachezewa na wadangaji.

Sasa nyie mnaojiita laki si pesa endeleeni kupoteza pesa kwa mshahara wa ngono na maradhi, wenzenu wanajenga siku hizi, akipata maboya yake kama sita akijisikia usiku anayapigia kuwa anafukuzwa kodi yanatoa laki tatu kila boya moja anajipatia 1.8 ya fasta. Wewe unajikuta mwanaume kumbe fala tu, ndio maana siku hizi watoto wa kike maisha kwao ni utelezi tu akiwa na mwili wa kudatisha.... Sasa wewe endelea kusema laki si pesa honga, watoto wako kwenye mipumbu yako unawadhurumu urithi wao sababu ya kutaka kuonekana mwamba fala m'moja wewe......

Hayo ni maneno tu ila ukweli ni kuwa mwanamke ambaye sio mkeo kumpatia fedha ni hisani tu, ila sio jambo la lazima au msingi kutoa pesa kwake hata kama ni buku ya vocha. Wacha wakuite bahiri sijui mkono mfupi, but usiwe under pressure kutoa pesa ambayo haupo tayari kutoa kwasababu unataka kuonekana mwanaume, but kama ni mkeo mnaishi nyumba moja then atajua matumizi na kipato chako so hawezi omba hovyo........
This is in Too Deep!
Ujaacha hata kipengele, safi sana! Wakuelewa wataelewa...Hii mambo lazma iende iishe.
 
Siku hizi maisha yanebadilika sana. Mahitaji yameongezeka sana na yanazidi kadri muda unavyokwenda.
Hapo zamani, hakukuwa na smartphone, hakukuwa na accesories za urembo kama sasa hivi, hakukuwa na social networks. Hivyo basi kutokana na utandawazi wanawake wanalazimika kuconform na kile kinachotazamiwa na wengi kuwa ni muhimu. Siku hizi mwanamke atatamani awe na mikoba 10, pair za viatu 20, magauni ya kubadili kila siku. Hivyo vyote vinampa mwanamke pressure kwa sababu anataka awe wa kisasa aendane na muda. Kutokana na mahitani hayo na mwanamke hana uwezo analazimika kulazimisha maisha yaliyo nje ya uwezo wake. Atakuomba hela ya vocha, hela ya kusuka, hela ya kodi, hela ya gari kama umejaaliwa fedha, na vingine vingi anavyotazamia ni mahitaji yake.
Mwanamke hata kama ana upendo wa dhati na wewe kama huna pesa na akatokea mwanaume mwenye uwezo kukushinda wewe, basi mwanamke atalazimika kuwa na mahusiano na huyo mtu ili aweze kupata mahitaji yake.
But doesn't that feel kind of Odd! Huoni kama kuna elements za ubinafsi hapo?
Kwamba ukiwana na hela anakuwa wako akitokea aliyekuzidi hela anakuhama. Hii ndio mentality ya kimaskini sasa aliyoizungumzia mwanangu Samcezar zer
 
Huyo mwanamke anaetaka uingize TU...umpe hela yake...Atakuwa anafanya biashara..
Mimi...napenda maandalizi mujarab
Mapenzi ya kibongo sikuhizi ni biashara tu za kuuziana papuchi in real sense. Mnafanya barter trade bila kujua. You give money you get pussy
 
Anaegandamizwa ni yule ambaye anaambiwa ukweli ama una maana gani kusema mtu anagandamizwa?
Ukweli? Ukweli upi huo?

Na kama mnasema ukweli kwanini huo ukweli muuseme kwa wanawake tu ila kwa wanaume hamsemi! Huo ni ukweli au unafiki maana hata biblia imemuita mnafiki mtu ambaye anatoa boriti kwenye jicho la mwenzie ilihali yeye hajatoa kibanzi kilichopo kwenye jicho lake mwenyewe!
 
Suala hapa siyo fikira wala msitafute wa kuwatupia lawama! Siku hizi kila jinsia inajifanya imevurugwa na mapenzi kila mtu anaingia kwenye mahusiano akiwa na maslahi yake!

Huyu anataka ngono huyu anataka fedha hakuna mwenye muda na mwenzie! Wanaume msitake kujifanya mko innocent sana kwenye mahusiano na kwamba ati wanawake tu ndiyo wako guilty kila siku!

Wanaume na wanawake wenye mapenzi ya dhati bado wapo! Lakini wengi sasa hivi hawana mapenzi siyo wanaume siyo wanawake!

Hivi wanaume kwanini huwa hampendi kukubali makosa yenu? Kwanini kila kitu lazima msingizie wanawake ndiyo chanzo kwamba ninyi hamnaga makosa kabisa au?
Sisi hatuna mapenzi sababu huwezi ku dedicate your mind and soul kwa mtu ambaye mwisho wa siku hatakuwa na shukrani. Wanawake hamfadhiliki ndio shida.
 
Ukweli? Ukweli upi huo?

Na kama mnasema ukweli kwanini huo ukweli muuseme kwa wanawake tu ila kwa wanaume hamsemi! Huo ni ukweli au unafiki maana hata biblia imemuita mnafiki mtu ambaye anatoa boriti kwenye jicho la mwenzie ilihali yeye hajatoa kibanzi kilichoûpo kwenye jicho lake mwenyewe!
Kumpenda mwanamke ni kama kucheza kamari. Huwa mna endeless demands ambapo mtu akishafikia mahali amekwama then you take him for granted kisha anakukimbia.
 
Extrovert kwani ninyi huwa hamna demands? Mkiingia kwenye mahusiano huwa hakuna vitu mnavyovitaka kutoka kwa hao wanawake mnaoingia nao kwenye mahusiano?
Utaratibu unaotakiwa ni kupeana mapenzi na kuwa loyal to each other. Ila hivyo vipengele havizingatiwi wala.

Mapenzi yamekuwa conditional sikuhizi. Yanategemea sana financial status ya ME na wenyewe mnajipaishaga kuwa huwezi kumiliki pisikali bila kutoa hela. Huna hela ya kunimiliki wewe!

Ni utamaduni ambao KE mmeujenga ili kutufanya kuona kumiliki mpenzi kuna uspesho flani lazma uwe nao esp. kipato kizuri. Maslahi makubwa kwenye uhusiano sio utu na mapenzi tena bali uwezo wa kifedha ndio mnachozingatia zaidi. Hata humu jukwaani ukimwambia mwanamke ukweli unaomuuma lazma akimbilie kusema tafta hela. Utaona kwa hali ilipofikia mapenzi yamekuwa ni kama biashara sasa.
 
Extrovert kwani ninyi huwa hamna demands? Mkiingia kwenye mahusiano huwa hakuna vitu mnavyovitaka kutoka kwa hao wanawake mnaoingia nao kwenye mahusiano?
Vitu ambavyo tunavitaka na kuvitarajia ni upendo na loyalty. Ila tunavyokutana navyo ni mizinga na bill zisizo na ukomo. Yani wanawake wa sikuhizi mnatia sana aibu sana!

Mtu hata kama ulikuwa na nia njema na mtoto wa mtu unabadili gia angani. Unachapa unasepa maana hamna ushawishi wa ku push further!
 
Kama utakumbuka maneno ya baba wa taifa, Hayati Julius Kambarage Nyerere, kuwa miongoni mwa maadui wa kuwapiga vita usiku na mchana na kuhakikisha wametokomea basi UMASIKINI ni nambari one.

Sababu umasikini ukitapakaa kwenye jamii utatengeneza njia kwa mambo mengi sana mbaya kuingia, mfano tamaa, njaa, maradhi, uhasama, chuki, usaliti, rushwa, na kadhalika.

Hili la watoto wa kike kupenda sana pesa lina uhusiano na insecurities zitokanazo na umasikini wa hali na akili huko walipotoka yaani makwao na familia zao.

Binti aliyelelewa kwa maadili ya utu hawezi kuwa na tamaa za mali au pesa ya mwanaume ambaye si mume wake. Mabinti wa sasa wanatoka familia zenye mentality za kimasikini sana yaani baba na mama wanataka kupata maisha kupitia mtoto wao, haijalishi anatoa wapi.

Kuna vitu vingi vinawaponza watoto wa kike, mfano, kutaka kuonekana mrembo kwa mavazi ya kisasa, kumiliki simu za bei, kuhang maeneo ya bata ya gharama ili kuweza kupiga picha za kupost kwenye social networks na social media. Pesa za kumudu haya yote unadhani wanatoa wapi na wanatoka familia za kipato cha chini kabisa.....

Lakini mbaya zaidi ni pressure ya familia wanazotoka hawa mabinti kuwaambia kuwa mwanaume ambaye hana pesa hana cha kukupa katika maisha, nyuma ya pazia, ni hii familia ya binti kutafuta mfadhili kupitia binti yao awatatulie matatizo yao ya ndani ya kifamilia.

Tukirejea miaka ya nyuma kidogo, si kwamba watu walikuwa na pesa sana, lahasha, bali utu ulishika nafasi yake na umasikini haukuwa na nafasi katika jamii.

Kukosa pesa sio umasikini bali ni hali ya kiuchumi ya kutokuwa na kipato. Ila umasikini ni tamaa ya kutaka kuwa na miliki isiyo stahiki yako ukilinganisha na jitihada zako wewe binafsi. Na ndio maana hata watu wezi, mafisadi, wadangaji, mbele ya safari huishia kufilisika sababu ndani ya nafsi zao ni masikini.

Uamasikini unaambukiza (contagious), umasikini ni hali ya akili kuamini mafanikio ni muujiza na sio uhalisia wa matokeo ya jitihada.

Umasikini unapigwa vita kwa kutafuta namna tofauti tofauti za kujitafutia kipato bila kudharau ni kiasi gani unaingiza bali muhimu ni malengo ya leo, kesho na kesho kutwa kipato kinakupeleka wapi kukutoa hapo ulipo.

Tunaposema umasikini ni adui wa taifa haya ndo matokeo ya kudharau hiyo kauli. Unakutana na binti anatumia mwili kama qualifications ya kufanya maisha na wewe ila ukikaa nae ndani hana mchango katika swala la kupigana na umasikini cha zaidi atavuta familia yake waje karibu yenu wamsaidie kukuambukiza umasikini.

Ukiona mwanamke hana elements za productivity kwa namna yoyote basi jua unaandaa kizazi au familia ya watu masikini. Mwanamke mwenye maradhi ya umasikini hatokei familia ya watu wa kipato cha chini, anatokea familia ya watu wasio na utu na wenye uchu na tamaa, hao ni masikini pure, aidha wawe na pesa au mafukara umasikini utaugundua kwao kupitia tabia zao za tamaa na uchu na husuda za kukurudisha nyuma wewe ili wao kupata.

Nilishawahi ona familia ya mzee ambae hana uwezo sana, ni mkulima tu wa kipato cha chini, binti yake ameolewa na kijana ana uwezo wa kipato cha kati. Ila yule mzee kila mwezi alikuwa anafunga kiroba cha mahindi, unga, na gallon kubwa ya mafuta ya alizeti kumtumia binti yake na mumewe kutoka kwenye ghala yake. Na akifanya mauzo ya mazao yake ya kilimo anatoa sehemu ya pesa anamtumia kijana na binti yake.

Imagine huyu mzee utamwita ni masikini?! Au huyu binti anatoka familia ya kimasikini?! Umasikini ni akili au fikra ya kuendekeza tabia ya kuelemea wengine ile hali unaweza kupambana kujitafutia na ukasaidia wengine.

Sasa leo, kupitia elimu, tumezalisha kundi kubwa la vijana makabwela na mafukara wa hiyari wasio na mawazo ya maendeleo hata kidogo. Hebu wazia ni kwa namna hii tutafikia malengo ya taifa kweli ya kuwa uchumi wa kisasa na kuwa na idadi ndogo sana ya watu wa kipato cha chini.....?!

So ndugu, kumalizia tu niseme, ukiona binti analeta mazoea ya kuomba pesa usipepese macho wala kuona aibu, mwambie ukweli, mwambie aache tamaa na kuendekeza akili za kimasikini, kama anataka kupata mahitaji kwako kwanza ajue wajibu wake kwako katika vita na umasikini miili ya ngono hii isikuponze ukatumia pesa yako uliyoipata kwa shida sana kirahisi rahisi kisa unafuata maneno ya mjini kuwa sijui mwanaume wa kweli sio bahiri kwa mwanamke.

Mtawalaumu hawa mabinti wanaodanga ila ukweli ni kuwa sisi wanaume baadhi yetu ndio tunachangia huu utomvu wa maadili na nidhamu kukua. Imagine kama wanaume wote tukaweka azimio la kutotoa pesa za matumizi katika maswala ya ngono nje ya kusaidia, utaona kama hawa wadangaji watakuwapo.

Kwanza familia zitaimarika, ndoa zitaheshimika, na wanawake watajua umuhimu wa ndoa. Hivi viburi vyao vinakuja sababu wahongaji na mabwege wa kutoa hela mpo wengi, na mimi nasema nikikuta mwanaume ambaye hajaoa mwanamke ila alikuwa ana muhudumia kama mke kisha huyo mwanamke akapata mtu mwingine akapita hivi, mimi nitatetea huyo mwanamke, sababu yupo sahihi hawezi olewa na mwanaume mpuuzi anayetoa pesa nje ya familia au nje ya ndoa.

Huwa tunawaona wanawake ni wakatili kwa kuwakimbia watu waliowahudumia ile hali hawakuwa wanaume wao wa ndoa. Ila ngoja nikwambie wanawake wenye akili huwa wakiona mwanaume ni bahiri wanajua huyu sasa ni mwanaume wa ndoa maana pesa zake hazitachezewa na wadangaji.

Sasa nyie mnaojiita laki si pesa endeleeni kupoteza pesa kwa mshahara wa ngono na maradhi, wenzenu wanajenga siku hizi, akipata maboya yake kama sita akijisikia usiku anayapigia kuwa anafukuzwa kodi yanatoa laki tatu kila boya moja anajipatia 1.8 ya fasta. Wewe unajikuta mwanaume kumbe fala tu, ndio maana siku hizi watoto wa kike maisha kwao ni utelezi tu akiwa na mwili wa kudatisha.... Sasa wewe endelea kusema laki si pesa honga, watoto wako kwenye mipumbu yako unawadhurumu urithi wao sababu ya kutaka kuonekana mwamba fala m'moja wewe......

Hayo ni maneno tu ila ukweli ni kuwa mwanamke ambaye sio mkeo kumpatia fedha ni hisani tu, ila sio jambo la lazima au msingi kutoa pesa kwake hata kama ni buku ya vocha. Wacha wakuite bahiri sijui mkono mfupi, but usiwe under pressure kutoa pesa ambayo haupo tayari kutoa kwasababu unataka kuonekana mwanaume, but kama ni mkeo mnaishi nyumba moja then atajua matumizi na kipato chako so hawezi omba hovyo........
Am proud to read you mind thank you for sharing you thought am blessed with your thinking ability i wish you could be my mentor/coach

Btw kwa nn usimuoe Karma mtatengeneza combination nzuri sana [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom