Wakuu habarini!
Katika utafiti wangu nilioufanya kwa muda mrefu nimeweza kugundua 99% kuwa pesa ndio kila kitu katika mapenzi.
Wanawake wengi siku hizi wametanguliza pesa mbele kuliko upendo wa dhati,pia pesa imeingia zaidi katika ndoa za watu( mke na Mme) ili uweze kuheshimika katika familia kuwa na pesa .
Mwanamke yeyote ukishakutana nae siku moja tayari ashaanza kuonyesha dalili za kuomba pesa hasa vibinti ambavyo havijazaa.
Ukiwa na pesa hata kama ukimuuliza mwanamke kuwa wewe una mtu wako? jibu utakalopewa sina mpenzi kwa sasa.
Kwakweli wanaume wenzangu kama hautoi pesa utaendelea kusota na hautopata mwanamke mzuri katika jamii hii labda tu itokee mwanamke kakupenda hasa mijimama.
Wakuu tutafuteni pesa ,nishaachwa na wanawake wengi kisa pesa.