Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Utatu wenye utata: Umri, Pesa na Mapenzi

Hapo kwenye upendo hauna macho wala masikio hebu fafanua kidogo

Valentina unapopenda au unapopendwa hakuna atakae kuambia kitu ukamsikia na wala hakuna utakachoona ukakikubali.
Jinsi ulivyomkubali mpenzi wako ndivyo itakavyo kuwa hata kama awe bubu,kipofu au kiwete,ndo ushapenda hivyo hakuna wa kukuzuia wala kukwambia mpenzi wako mbaya au hafai ukamuelewa.
Hata waswahili walishasema kipenda roho,hula nyama mbichi ,kwanini basi ?
Kwa kuwa uono wa macho yako na usikivu wa masikio yako ni tofauti na wengine.
 
Last edited by a moderator:
Valentina unapopenda au unapopendwa hakuna atakae kuambia kitu ukamsikia na wala hakuna utakachoona ukakikubali.
Jinsi ulivyomkubali mpenzi wako ndivyo itakavyo kuwa hata kama awe bubu,kipofu au kiwete,ndo ushapenda hivyo hakuna wa kukuzuia wala kukwambia mpenzi wako mbaya au hafai ukamuelewa.
Hata waswahili walishasema kipenda roho,hula nyama mbichi ,kwanini basi ?
Kwa kuwa uono wa macho yako na usikivu wa masikio yako ni tofauti na wengine.

Ooh kumbe ndio hivo!
 
Last edited by a moderator:
kayaman rudi ktk uzi wangu nimeshaeleza kuwa pesa itanunua mapenzi lakini haitonunua mapenzi ya kweli,subiri pesa ikuishie ndo utajua kama ulipendwa wewe au ilipendwa pesa yako.
 
Last edited by a moderator:
Ndio Valentina usimshangae siku ukimuona rafiki yako,ndugu yako au jamaa yako kampenda bubu au kiziwi au kipofu ukasingizia nini,ni mapenzi hayo.
Rejea hata Dk Remy aliwahi kuimba na kama unafahamu historia yake,rejea kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Kila mmoja anahitaji kitu ambacho hakijui na kama hakijui sijui atakipata namna gani...
 
Kaboom ,inawezekana hilo ulisemalo lakini ni kwa njia ya tofauti na fikra za wengi.
Na kama ingekuwa ni njia ya moja kwa moja basi wala wafanyao biashara ya ukahaba wangekuwa ni namba moja ktk kuyafahamu mapenzi ya kweli kwa kuwa wao wanafanya "sx" kama sehemu ya kazi yao ila wanatambua fika kuwa hakuna mapenzi hapo.
SX Inaleta mapenzi ya kweli pale mnapokuwa sasa mnaupendo wa kweli na kila mmoja anaweza kumfikisha mwenzake sehemu husika.
Akili ya binadamu inapokubaliana na matendo fulani ndipo tendo lenyewe hufanyika.
 
Last edited by a moderator:
Kaboom ,inawezekana hilo ulisemalo lakini ni kwa njia ya tofauti na fikra za wengi.
Na kama ingekuwa ni njia ya moja kwa moja basi wala wafanyao biashara ya ukahaba wangekuwa ni namba moja ktk kuyafahamu mapenzi ya kweli kwa kuwa wao wanafanya "sx" kama sehemu ya kazi yao ila wanatambua fika kuwa hakuna mapenzi hapo.
SX Inaleta mapenzi ya kweli pale mnapokuwa sasa mnaupendo wa kweli na kila mmoja anaweza kumfikisha mwenzake sehemu husika.
Akili ya binadamu inapokubaliana na matendo fulani ndipo tendo lenyewe hufanyika.

Falsafa ngumu sana hii.
 
Last edited by a moderator:
Ukita nchi kuwa na uchumi imara na makini lazima iwe imepita ktk changamoto ya umasikini ukitaka jeshi liwe na nguvu imara,lazima liwe liliwahi kushindwa vita.Ukitaka kufaulu maisha,lazima upitie changamoto.

Na ukitaka kupata mapenzi ya kweli lazima ufuate kanuni na taratibu za mapenzi ambazo ndio dira ya kukuongoza na kukufikisha kwenye ndoto.
Ni wengi waloumizwa na mapenzi,ni wengi waloteseka na mapenzi,ni wengi wenye majeraha yasipona maumivu.

Maumivu ya mapenzi hayaelezeki,hayasimuli,ni siri kati ya mgonjwa na maumivu yenyewe.Ni uongo na kujidanganya kuwa utaweza kununua mapenzi ya kweli kama ununuavyo gari au nyumba au nguo au chochote kile.

Mapenzi ya kweli huzaliwa katika upendo wa kweli na hauihitaji pesa,utajiri,dini,rangi wala kabila.Pesa inaweza kununua mapenzi lakini pesa haiwezi kununua upendo ambao ndio mapenzi ya kweli.

Ashakum si matusi,utakapo toa pesa na kuhonga mapenzi utapata kitu kiitwacho " sex'' lakini ule upendo unaozaa mapenzi ya kweli yanayopelekea ndoa ya kudumu hautokuwepo kwani ni sawa na kuuwekea kumpa kuku aatamie yai la mbuni.

Mapenzi yamejengwa katika ukubwa ambao haulingani na thamani ya pesa.Ni masikini wangapi wameoana au kuolewa na matajiri,ni wenye elimu wangapi wameona na wasio na elimu ?Huo ndio ukubwa wa mapenzi,usiofanana na chochote kile.

Kweli wengi tunafanya kazi kwa juhudi zote ili tupate pesa za kupatia mapenzi lakini ni kweli tunapata mapenzi ya kweli au tunaishia kufanya mapenzi na mwisho wa siku kusalitiana,na kuachana vibaya.Hakuna soko la mapenzi duniani ambalo utafika na kuyanunua.

Mapenzi ya kweli hujengwa ktk mfumo wa mwili wa binadamu ambao upo ktk sehemu iitwayo upendo,upendo unatokea ktk roho au moyo wa binadamu.
Kwa kawaida upendo hauna macho wala masikio.

Upendo una akili na ufahamu peke yake.Hivyo basi,yule utakae muona mbaya,wenzako watamuona mzuri na yule utakae muona mzuri wenzako watamuona mbaya,hapo mapenzi hayana macho.Yule mchafu kwako,kwa wenzako ni msafi.

Mapenzi siyo sawa na bidhaa sokoni eti utoe hela uipate,laa.Mapenzi ni sawa na upofu,lakini upofu wenye maono.Hata ufanye nini,kwa wenye mapenzi ya kweli huwezi kuwatenganisha kwani hawakuyanunua sokoni wala dukani,wanatambua thamani ya mapenzi yao.

Muda mwema wote.
Ni kweli tena kwelii kabisaa, asiyeelewa hili au linampa ugumu kulipambanua bdo ajapendaa au kukutan na mtu akamuingia moyoni, UPENDO wa kweli ni mtamuu sana unaenjoy mpaka unasahau yote ya dunia....
 
Kata mpunga kama Kyela ili upate usajiri. Watu wanataka goto weweee
 
"Love ana money are two sides of the same coin"
"pesa haileti furaha ila inaongeza furaha"
tafakari chukua hatua....

Kweli kabisa mkuu. Jamani bila hela yaani kumpenda mwanamume ni kazi. Hahaa. Mnaweza msielewe ila ndo ukweli. Pesa inachochea sana mtu kukupenda. Kinakaka tafuteni tu hela. Wengi tu mmekataliwa kisa mfuko umesinyaaa.
 
Teh teh..Bro wapo watu kibao tu ambao SEX(gud sex) ndo imeimarisha mahusiano yao..Utakuta demu hana feelings na ww..anakuchuna tu..Ila siku anakutunuku ile kitu anakutana na mziki wa hatari..Kidogokidogo feelings zake zinaanza kuchange

Hahaha. Hizi mambo huwa mi nazisikia tu. So, you hit it with the rage of Pau Gasol against the French(all round perfomance), au sio? Binafsi huwa siamini katika kumshawishi Manzi. Ananikubali mwenyewe toka mwanzo, ndio tunaendelea.
 
Hahaha. Hizi mambo huwa mi nazisikia tu. So, you hit it with the rage of Pau Gasol against the French(all round perfomance), au sio? Binafsi huwa siamini katika kumshawishi Manzi. Ananikubali mwenyewe toka mwanzo, ndio tunaendelea.

Teh teh..That's it bro..Ndo pale unakuta manzi anahudumiwa kila kitu na mtu wake ila anakuwa na side-dude kisa sex tu..Na feelings zote anazielekeza huko..

Talking bout the last line..u never make the first move???
 
Teh teh..That's it bro..Ndo pale unakuta manzi anahudumiwa kila kitu na mtu wake ila anakuwa na side-dude kisa sex tu..Na feelings zote anazielekeza huko..

Talking bout the last line..u never make the first move???

Damn those hoz.

You can say that. I prefer tiki taka(keeping the ball and let scoring chances open-up automatically). I never shoot, til I'm 100% sure it's a stunner. Other than that, I'm happy to keep possession. I never chase.
 
Back
Top Bottom