Utapeli mpya kwa mafundi, kuweni makini

Utapeli mpya kwa mafundi, kuweni makini

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
23,877
Reaction score
31,632
Huu uzi unawahusu mafundi aina zote haswa mafundi ujenzi.

Usione watu wana miliki nyumba zaidi ya 10 ukadhani zote wamejenga kihalali kumbe nyuma ya pazia kuna uchafu umefanyika kukamilisha ujenzi huo.

Mchezo upo hivi, tajiri atakuita vizuri atakupa kazi na mtaanza vizuri tu mwanzoni , ila sasa kazi ukishakamilisha ataanza kukutafutia kesi yoyote ili kusudi pesa yako asikulipe , fidia utamlipa na jera usioangalia utaenda.

Utapewa kesi ya upotevu wa mali /wizi. Unaweza ukapewa kesi hata ya ubakaji au kesi aina yoyote ile ili mtokomee na pesa juu mlipe.

Unaweza kukuta kazi ambayo wewe ungeenda kulipwa hata milioni 5 ,ubao unageuzwa unalipishwa mara mbili yake ,ukijifanya mjuaji zaidi unaenda kuozea jela.
 
Kabla hujaenda jela vizia na kufanya jambo lililotukuka

1773882567074.png
 
Huu uzi unawahusu mafundi aina zote haswa mafundi ujenzi.

Usione watu wana miliki nyumba zaidi ya 10 ukadhani zote wamejenga kihalali kumbe nyuma ya pazia kuna uchafu umefanyika kukamilisha ujenzi huo.

Mchezo upo hivi, tajiri atakuita vizuri atakupa kazi na mtaanza vizuri tu mwanzoni , ila sasa kazi ukishakamilisha ataanza kukutafutia kesi yoyote ili kusudi pesa yako asikulipe , fidia utamlipa na jera usioangalia utaenda.

Utapewa kesi ya upotevu wa mali /wizi. Unaweza ukapewa kesi hata ya ubakaji au kesi aina yoyote ile ili mtokomee na pesa juu mlipe.

Unaweza kukuta kazi ambayo wewe ungeenda kulipwa hata milioni 5 ,ubao unageuzwa unalipishwa mara mbili yake ,ukijifanya mjuaji zaidi unaenda kuozea jela.
Chai

Cc marehemu T.O Elias Kihombo.
 
Kazi za ujenzi ni ngumu sana na inabidi kuwa na uangalifu sana. Migogoro mingi inahusu malipo na ubora wa kazi. Kuna hatua kadhaa inabidi kuzichukua.

1. Kabla ya kazi kuwa na mkataba ulioandikwa.
2. Kuwe na hesabu ya kazi iliyoandikwa ikielezea kazi zinazotakiwa kufanyika na gharama zake.
3. Malipo yafanyike kupitia benki au miamala ya simu, Malipo yafuatiwe na risiti.
4. Hakikisha kuna mtu wa kati, ambaye ataangalia kazi anaweza kuwa Architect au Engineer. Huyu ana ueleewa kuhusu kazi na anasaidia kutatua migogoro baina ya mjenzi na mwenye nyumba.
5. Kama mwenye nyumba ananunu vifaa, hakikisha usalama wa vifaa na ulinzi uwe juu yake.
6. Mabadiliko yoyote yasifanyike mpaka kwanza bei yake imejulikana kwa pande zote
7. Kata bima
8. Hakikisha unatumia pesa kwa ajili ya kazi na kwa mujibu wa makubaliano
 
Unatengenezewa kesi kulingana na mazingira ili usilipwe

Mfano unaweza ukatenenezewa kesi ya kuiba nondo, simenti nk.
Hii inaweza kuwa ni isolated incidence na siyo tatizo kubwa. Matatizo mengi ya ujenzi hutokea kwa mafundi kuwa wakorofi na siyo wenye nyumba kama unavyotaka watu waamini. Na possibly huyo fundi ni kweli aliiba au kiwango cha kazi kilikuwa duni, na sheria zilichukuliwa kwa uhalali. Mafundi wa Bongo ni nani asiyejua matatizo yao? Hapa ni kama umekuja na tahadhari eti abiria wanaibia wapiga debe wa stendi
 
Sitaki kuhalalisha ila kuna kibwana mdogo kimoja ,kilikuja kufunga camera kwenye ofisi na biashara za mnene mmoja .Kufikia wakati wa malipo mnene akaanza kuleta gozigozi .Kibwana mdogo wakakitupa ngome wakadai pia kimekwiba na kimetapeli.Ilibidi tukichangie mpaka nauli ya kurudi Dar.
 
Zipo dalili za kuonesha kuwa huyu tajiri/mteja ni tapeli, wanakuwaga na maneno mengi ili umuone ana nia njema. Anaweza kutoa malipo ya awali nusu ukadhani atamalizia nusu iliyobaki. Kazi ikikamilika mgogoro wa madai unaanza
 
Hii ni kweli kabisa!!
Kuna ndugu yangu alikimbia project Arusha kisa hii michezo.
Ni fundi, kafanya kazi dakika za jioooni katafutiwa weakness kidogo boss akashika hapohapo!!

Ilibidi tuforce nauli ili arudi Dar kwa mbinde sana.

Sema yeye sio fundi systematic ni hawa wa elimu ya hapa na pale... Na ndio victim wakubwa kwenye hii michezo.
 
Kazi za ujenzi ni ngumu sana na inabidi kuwa na uangalifu sana. Migogoro mingi inahusu malipo na ubora wa kazi. Kuna hatua kadhaa inabidi kuzichukua.

1. Kabla ya kazi kuwa na mkataba ulioandikwa.
2. Kuwe na hesabu ya kazi iliyoandikwa ikielezea kazi zinazotakiwa kufanyika na gharama zake.
3. Malipo yafanyike kupitia benki au miamala ya simu, Malipo yafuatiwe na risiti.
4. Hakikisha kuna mtu wa kati, ambaye ataangalia kazi anaweza kuwa Architect au Engineer. Huyu ana ueleewa kuhusu kazi na anasaidia kutatua migogoro baina ya mjenzi na mwenye nyumba.
5. Kama mwenye nyumba ananunu vifaa, hakikisha usalama wa vifaa na ulinzi uwe juu yake.
6. Mabadiliko yoyote yasifanyike mpaka kwanza bei yake imejulikana kwa pande zote
7. Kata bima
8. Hakikisha unatumia pesa kwa ajili ya kazi na kwa mujibu wa makubaliano
Mkuu umechambua vizuri sana.

Shida inakuja kwenye ugumu wa maisha fundi ana zaidi ya miezi sita hajawahi fanya kazi nzuri zaidi ya vijideiwaka vya hapa na pale.

Halafu anatokea mshua anakupa mchongo wa Kujenga kasri lake,fundi hapo ana uhakika wa kupata Ada za watoto,kulipa pango pamoja na kupunguza madeni.

Anajikuta anavamia kazi bila kufuata uliyoainisha hapo juu,keshashikishwa advance million moja . mengine mbele Kwa mbele.

Na asilimia nyingi za mafundi ni walevi hivyo kutumia laki tano Kwa siku haoni hasara halafu Kesho anaomba umwazime elfu ishirini aiachie familia.
 
Sitaki kuhalalisha ila kuna kibwana mdogo kimoja ,kilikuja kufunga camera kwenye ofisi na biashara za mnene mmoja .Kufikia wakati wa malipo mnene akaanza kuleta gozigozi .Kibwana mdogo wakakitupa ngome wakadai pia kimekwiba na kimetapeli.Ilibidi tukichangie mpaka nauli ya kurudi Dar.
Aisee
 
  • Thanks
Reactions: EEX
Zipo dalili za kuonesha kuwa huyu tajiri/mteja ni tapeli, wanakuwaga na maneno mengi ili umuone ana nia njema. Anaweza kutoa malipo ya awali nusu ukadhani atamalizia nusu iliyobaki. Kazi ikikamilika mgogoro wa madai unaanza
Ndivyo mchezo unavyokuwa hivyo.
 
Back
Top Bottom