The Festival
Member
- Aug 30, 2021
- 27
- 98
Nawasalimu ndugu zangu popote pale mulipoš¤š½. Nina matumaini ni wazima wa afya, na kwa wale waliopata mtihani wa maradhi basi tunawaombea siha njema kwa MwenyeziMungu (Mtukufu, Aliye juu, Aliye mkuu).
(Picha kwa hisani ya: Gift of Herbert J. Harris, 1986)
Hii ni ngoma ya kijiji chetu. Kila azaliwaye kijijini kwetu hupaswa kuwa na ufundi wa kuicheza. Ngoma hii yasifika utamu wake hasa ukiwa katikati ya kiwanja ukiicheza kufuatana na midundo yake. Wanakijiji wa vijiji jirani nao hucheza ngoma zao na hakika hunufaika. Mfano mzuri ni wanakijiji wa Uchinani, wanaicheza vizuri ngoma yao na sasa imewasaidia wako pahala poa kabisa. Wengine ni wanakijiji wa kiarabu, nao wanaicheza vizuri ngoma yao na si haba matunda ya kuserebuka kwao tunayaona. Vijiji vya Amerika na Ulaya wanaicheza kweli kweli na hatua kubwa wamepiga katika vijiji vyao. Hii inanikumbusha maneno ya bibi pale alipokua akiniambia, utamu wa ngoma uingie ucheze. Hivo kwa yeyote ambaye atakua akisifia uhondo wa ngoma basi inatupasa tufahamu ya kwamba, msifiaji huyo alibahatika kuwemo na bado yumo kiwanjani akitimbwirika kwa miondoko murua kupata utamu halisi wa midundo ya ngoma hiyo hadi kuisifia.
Lakini katika kijiji chetu hali ni tofauti kwa baadhi ya wenzetu waliopata vigoda vya kukalia. Wenzetu hao wanaonekana kutojali kabisa kujumuika pamoja nasi kiwanjani kuburudika na midundo mitamu ya ngoma hii, bali wao huona raha kutazama wachezaji huku wakihamasisha na kuipamba ngoma hii kwa mashairi na mapambio mbali mbali ili watu wasiokua miongoni mwao waingie kati kurindima na kuicheza ngoma hii.
Hali ilipofika sasa ni ya ukakasi na ninapata maswali mazito hadi ninashindwa kabisa kuyajibu: shida ni nini mpka wao wenye vigoda hawavishughulishi viungo vyao kuja kurindima na sisi? Ni kwanini hawa walio kalia vigoda kutoka pwani na bara wala hawajishughulishi kuserebuka na mdundo wa ngoma hii, ili kusudi wakiisifia wawe na uwezo wa kujenga hoja madhubuti ya kwamba ngoma ni tamu haswa na wote twaicheza kwa mitindo na mizuka mbali mbali? Au wamesahau ahadi zao kedekede kwetu, wakituaminisha ya kwamba wao ni wachezaji wazuri wa ngoma na tukiwaazima vigoda basi watatuonesha ufundi wao wa kuicheza ngoma hii ipaswavyo na wala hawatabweteka? Au wenzetu wana hofu wataanguka kama wakiicheza huku wamekalia vigoda? Au wana wasiwasi wakiicheza watanyanyuka kwa midadi na kisha kanuni ya kwenye daladala itafata, ukiinuka sisi tunakaa? Au wamesahau ya kwamba vigoda vina muda maalumu wa kukaliwa na ni dhamana na wala si miliki yao milele daima? Ni kwa nini wanaisifia sana ngoma hii na wala wao hatuwaoni kiwanjani wakijimwagamwaga kuicheza?
Naona na wenzetu wasiokua na vigoda vya kukalia kwa kiasi kikubwa wameamua kuacha kuicheza ngoma, kwa kuwa wale wenye vigoda ambao ndio walipaswa kuwa vinara wa kucheza ngoma hii hawaichezi hata thumni. Huku ni kufanya nini huku? Huku ni kuisusia ngoma ambayo ndio chachu ya mambo mazuri tuyatakayo.
Enyi mlio na vigoda kumbukeni mkataa pema pabaya panamwita. Nawanasihi muicheze ngoma. Kwani hivyo mfanyavyo, kuisifu tu na kuipamba ngoma si utaratibu tulio achiwa na wale waasisi wa ngoma hii. Waasisi kama vile Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa kijiji chetu aliicheza ngoma hii kwelikweli ndani na nje ya kijiji tangu mwaka 1922 mwezi wa 04 tarehe 13 hadi pale mauti yalipo mkuta mwaka 1999 mwezi wa 10 tarehe 14. Abeid Amani Karume, Mtu kazi, baharia mzoefu nae hakupoa kabisa katika kurindima viwanjani kwa miondoko ya kipwani tangu mwaka 1905 mwezi wa 08 tarehe 04 mpaka pale alipoaga dunia mwaka 1972 mwezi wa 04 tarehe 07. Bibi Titi Mohammed, mwanamke wa shoka asiyeimbwa na wengi, aliserebuka na kuicheza kwa mikogo ngoma hii tangu mwaka 1926 mwezi wa 06 hadi pale alipofikwa na umauti mwaka 2000 mwezi wa 06 tarehe 05. Hakika nakiri ya kwamba, ardhi imemeza watu. Hao ni baadhi tu ya wengi waliokua wamekalia vigoda na bado walidumisha kuicheza ngoma sambamba na wale wasio na vigoda. Lakini sasa mambo si shwari tena, kwani nyinyi wenye vigoda kwa kutoicheza ngoma hii kwa vitendo, munawashawishi wasio na vigoda nao kutoicheza ngoma ipasavyo. Kwa heshima na taadhima, enyi wenye vigoda naomba mjitafakari sana kwenye kuicheza ngoma hii na si kuwashawishi wengine tu nanyi mmo pembeni tulii.
Enyi ambao hamna vigoda, nawanasihi ya kwamba musiache kuicheza ngoma yetu hii, japokuwa ni ngumu sana kuicheza ngoma hii huku ukimwona alieshiba kakalia kigoda cha dhamana akikutizama wala hajishughulishi kuicheza ilihali alipaswa kuwa kiwanjani akitimua vumbi kwa kuicheza ngoma. Nafahamu baadhi yenu mwatamani kukalia vigoda lakini hilo si lengo kuu, muhimu kijiji kichangamke yaani kisipoe hata chembe. Hivyo kwa unyenyekevu nawaomba tuendelee kuicheza ngoma yetu bila kujali kama yupo mwenye kigoda ana icheza ngoma au la.
Madhara ya kutoicheza ngoma hii ni makubwa mno kwani huhatarisha maslahi mapana ya leo na kesho yetu, na pia huhatarisha maslahi ya kijiji chetu chote kwa ujumla. Naweza sema ya kwamba, kwa kuwa sisi tupo viwanjani kuicheza ngoma, wasioicheza wanaweza kupata mwanya wa kwenda majumbani mwetu ambapo tumeacha mali zetu, wakatuchukulia mali zetu bila ya ridhaa zetu. Vile vile kijiji chetu kitakosa mchezaji, hivo ngoma itadorora na kijiji kitapoa na kukosa thamani inayo stahiki.
Hamasa ya mshikamano itapungua kwani kwa kutoicheza kwetu kwa pamoja hata huo umoja tutaukosa. Masikilizano na maelewano baina yetu yatapotea kwani midundo ya ngoma hii inahamasisha umuhimu wa maskilizano na maelewano. Rasilimali za kijiji chetu zitapotea kwa kuwa ngoma hii inachochea kukipenda na kukithamini kijiji chetu.
Utamaduni utabadilika na kuharibika, hivyo vizazi vijavyo vitashindwa kufahamu namna bora ya kuicheza ngoma hii. Ulinzi na usalama utatoweka kwani ngoma hii inahamasisha wanakijiji shupavu kupenda kujitolea kulinda amani ya kijiji chetu. Vitendo vya rushwa vitashamiri kwa kuwa ngoma hii ikivuma sana haipasuki bali huelekeza watu kutokomeza tabia za ubinafsi na urasimu. Madhara ni mengi mno tutakesha kuyasema na ngoma ndio hivo tena imenoga.
Nakaribisha wanajukwaa wote kutoa maoni ya nini kifanyike kutokana na tafsiri walioipata katika bandiko hili, nami mwandishi nitatoa tafsiri hapa hapa kwenye bandiko. Pia nawaomba mpige kura kwa ajili ya bandiko letu hili. Wino umekwisha, naweka kalamu chini.
Ahsante sana & Karibu.
(Picha kwa hisani ya: Gift of Herbert J. Harris, 1986)
Hii ni ngoma ya kijiji chetu. Kila azaliwaye kijijini kwetu hupaswa kuwa na ufundi wa kuicheza. Ngoma hii yasifika utamu wake hasa ukiwa katikati ya kiwanja ukiicheza kufuatana na midundo yake. Wanakijiji wa vijiji jirani nao hucheza ngoma zao na hakika hunufaika. Mfano mzuri ni wanakijiji wa Uchinani, wanaicheza vizuri ngoma yao na sasa imewasaidia wako pahala poa kabisa. Wengine ni wanakijiji wa kiarabu, nao wanaicheza vizuri ngoma yao na si haba matunda ya kuserebuka kwao tunayaona. Vijiji vya Amerika na Ulaya wanaicheza kweli kweli na hatua kubwa wamepiga katika vijiji vyao. Hii inanikumbusha maneno ya bibi pale alipokua akiniambia, utamu wa ngoma uingie ucheze. Hivo kwa yeyote ambaye atakua akisifia uhondo wa ngoma basi inatupasa tufahamu ya kwamba, msifiaji huyo alibahatika kuwemo na bado yumo kiwanjani akitimbwirika kwa miondoko murua kupata utamu halisi wa midundo ya ngoma hiyo hadi kuisifia.
Lakini katika kijiji chetu hali ni tofauti kwa baadhi ya wenzetu waliopata vigoda vya kukalia. Wenzetu hao wanaonekana kutojali kabisa kujumuika pamoja nasi kiwanjani kuburudika na midundo mitamu ya ngoma hii, bali wao huona raha kutazama wachezaji huku wakihamasisha na kuipamba ngoma hii kwa mashairi na mapambio mbali mbali ili watu wasiokua miongoni mwao waingie kati kurindima na kuicheza ngoma hii.
Hali ilipofika sasa ni ya ukakasi na ninapata maswali mazito hadi ninashindwa kabisa kuyajibu: shida ni nini mpka wao wenye vigoda hawavishughulishi viungo vyao kuja kurindima na sisi? Ni kwanini hawa walio kalia vigoda kutoka pwani na bara wala hawajishughulishi kuserebuka na mdundo wa ngoma hii, ili kusudi wakiisifia wawe na uwezo wa kujenga hoja madhubuti ya kwamba ngoma ni tamu haswa na wote twaicheza kwa mitindo na mizuka mbali mbali? Au wamesahau ahadi zao kedekede kwetu, wakituaminisha ya kwamba wao ni wachezaji wazuri wa ngoma na tukiwaazima vigoda basi watatuonesha ufundi wao wa kuicheza ngoma hii ipaswavyo na wala hawatabweteka? Au wenzetu wana hofu wataanguka kama wakiicheza huku wamekalia vigoda? Au wana wasiwasi wakiicheza watanyanyuka kwa midadi na kisha kanuni ya kwenye daladala itafata, ukiinuka sisi tunakaa? Au wamesahau ya kwamba vigoda vina muda maalumu wa kukaliwa na ni dhamana na wala si miliki yao milele daima? Ni kwa nini wanaisifia sana ngoma hii na wala wao hatuwaoni kiwanjani wakijimwagamwaga kuicheza?
Naona na wenzetu wasiokua na vigoda vya kukalia kwa kiasi kikubwa wameamua kuacha kuicheza ngoma, kwa kuwa wale wenye vigoda ambao ndio walipaswa kuwa vinara wa kucheza ngoma hii hawaichezi hata thumni. Huku ni kufanya nini huku? Huku ni kuisusia ngoma ambayo ndio chachu ya mambo mazuri tuyatakayo.
Enyi mlio na vigoda kumbukeni mkataa pema pabaya panamwita. Nawanasihi muicheze ngoma. Kwani hivyo mfanyavyo, kuisifu tu na kuipamba ngoma si utaratibu tulio achiwa na wale waasisi wa ngoma hii. Waasisi kama vile Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Baba wa kijiji chetu aliicheza ngoma hii kwelikweli ndani na nje ya kijiji tangu mwaka 1922 mwezi wa 04 tarehe 13 hadi pale mauti yalipo mkuta mwaka 1999 mwezi wa 10 tarehe 14. Abeid Amani Karume, Mtu kazi, baharia mzoefu nae hakupoa kabisa katika kurindima viwanjani kwa miondoko ya kipwani tangu mwaka 1905 mwezi wa 08 tarehe 04 mpaka pale alipoaga dunia mwaka 1972 mwezi wa 04 tarehe 07. Bibi Titi Mohammed, mwanamke wa shoka asiyeimbwa na wengi, aliserebuka na kuicheza kwa mikogo ngoma hii tangu mwaka 1926 mwezi wa 06 hadi pale alipofikwa na umauti mwaka 2000 mwezi wa 06 tarehe 05. Hakika nakiri ya kwamba, ardhi imemeza watu. Hao ni baadhi tu ya wengi waliokua wamekalia vigoda na bado walidumisha kuicheza ngoma sambamba na wale wasio na vigoda. Lakini sasa mambo si shwari tena, kwani nyinyi wenye vigoda kwa kutoicheza ngoma hii kwa vitendo, munawashawishi wasio na vigoda nao kutoicheza ngoma ipasavyo. Kwa heshima na taadhima, enyi wenye vigoda naomba mjitafakari sana kwenye kuicheza ngoma hii na si kuwashawishi wengine tu nanyi mmo pembeni tulii.
Enyi ambao hamna vigoda, nawanasihi ya kwamba musiache kuicheza ngoma yetu hii, japokuwa ni ngumu sana kuicheza ngoma hii huku ukimwona alieshiba kakalia kigoda cha dhamana akikutizama wala hajishughulishi kuicheza ilihali alipaswa kuwa kiwanjani akitimua vumbi kwa kuicheza ngoma. Nafahamu baadhi yenu mwatamani kukalia vigoda lakini hilo si lengo kuu, muhimu kijiji kichangamke yaani kisipoe hata chembe. Hivyo kwa unyenyekevu nawaomba tuendelee kuicheza ngoma yetu bila kujali kama yupo mwenye kigoda ana icheza ngoma au la.
Madhara ya kutoicheza ngoma hii ni makubwa mno kwani huhatarisha maslahi mapana ya leo na kesho yetu, na pia huhatarisha maslahi ya kijiji chetu chote kwa ujumla. Naweza sema ya kwamba, kwa kuwa sisi tupo viwanjani kuicheza ngoma, wasioicheza wanaweza kupata mwanya wa kwenda majumbani mwetu ambapo tumeacha mali zetu, wakatuchukulia mali zetu bila ya ridhaa zetu. Vile vile kijiji chetu kitakosa mchezaji, hivo ngoma itadorora na kijiji kitapoa na kukosa thamani inayo stahiki.
Hamasa ya mshikamano itapungua kwani kwa kutoicheza kwetu kwa pamoja hata huo umoja tutaukosa. Masikilizano na maelewano baina yetu yatapotea kwani midundo ya ngoma hii inahamasisha umuhimu wa maskilizano na maelewano. Rasilimali za kijiji chetu zitapotea kwa kuwa ngoma hii inachochea kukipenda na kukithamini kijiji chetu.
Utamaduni utabadilika na kuharibika, hivyo vizazi vijavyo vitashindwa kufahamu namna bora ya kuicheza ngoma hii. Ulinzi na usalama utatoweka kwani ngoma hii inahamasisha wanakijiji shupavu kupenda kujitolea kulinda amani ya kijiji chetu. Vitendo vya rushwa vitashamiri kwa kuwa ngoma hii ikivuma sana haipasuki bali huelekeza watu kutokomeza tabia za ubinafsi na urasimu. Madhara ni mengi mno tutakesha kuyasema na ngoma ndio hivo tena imenoga.
Nakaribisha wanajukwaa wote kutoa maoni ya nini kifanyike kutokana na tafsiri walioipata katika bandiko hili, nami mwandishi nitatoa tafsiri hapa hapa kwenye bandiko. Pia nawaomba mpige kura kwa ajili ya bandiko letu hili. Wino umekwisha, naweka kalamu chini.
Ahsante sana & Karibu.