Utajiri wenye uchungu

Utajiri wenye uchungu

NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Ishirini na Tisa.

"Tunaondoka, nadhani hautorudi tena huku," alisema Sam huku akimwangalia Aisha ambaye uso wake ulikuwa na tabasamu pana.

"Na sitotaka kurudi tena, hata kama nikifa, ni bora kuzikwa hukohuko," alisema msichana huyo huku tabasamu lake likiendelea kuwepo usoni mwake.

****

Hali ya mawingu haikuwa nzuri hata kidogo, anga ilichafuka, hakukuwa na amani hata kidogo. Marubani wawili waliokuwa wakiiendesha ndege hiyo walichanganyikiwa, hawakuamini kama kweli anga hiyo ilichafuka kiasi hicho.

Walifanya kazi ya urubani kwa zaidi ya miaka ishirini, hata anga ilipokuwa ikichafuka kwa kujaa mawingu huku mvua iliyoambatana na upepo mkali inaponyesha, hawakuwa wakiogopa lakini kwa siku hiyo, hali ilionekana kuwa tofauti kabisa.

Radi zilikuwa zikipiga kila kona, waliogopa, walihisi kwamba ndege hiyo ingepoteza muelekeo, walijitahidi kuiweka sawa kwani upepo mkali uliokuwa ukivuma ulikuwa ukiiyumbisha ndege ile kupita kawaida.

Tayari hali ya hatari ikaanza kuonekana, walichokifanya ni kuitoa ndege ile kutoka katika usawa wa nchi kavu na kuipeleka katika usawa wa bahari ya Atlantiki.

Hali ya hewa haikutulia, siku hiyo ilionekana kuwa na mkosi kwao, juhudi zao za kuiweka sawa ndege ile zilikuwa zikiendelea zaidi, mbaya zaidi, kitu kilichowatisha ni kuona injini moja ya ndege ile ikianza kuzima na kuwaka mara kwa mara.

"Vipi?" aliuliza rubani mmoja.

"Injini inazima na kuwaka, Mungu wangu! Tuombe Mungu, hali hii sijawahi kuiona tangu nazaliwa," alisema rubani mwingine.

"Hebu tuishushe ndege chini kidogo, inaweza kusaidia," alisema rubani huyo na hivyo kuanza kufanya hivyo.
Walichokuwa wakitaka ni kutoka katika wingu zito ambalo liliambatana na upepo mkali, wakaishusha ndege ile kwa chini kidogo, kama mita hamsini kutoka baharini, yote hiyo walifanya ili kuepukana na upepo huo mkali lakini cha ajabu, injini ile iliyokuwa ikiwaka na kuzima, ikazima kabisa.

"Mungu wangu! Injini imezima..." alisema rubani.

"Unasemaje?"

Huku nyuma, kila mtu alikuwa akishangaa, hali iliyokuwa ikionekana ilimtisha kila mmoja, Aisha alibaki akipiga kelele, hewa safi ya oksijeni ikaanza kupotea hivyo kuvuta mipira ya hewa safi na kujivisha midomoni na puani mwao.

"Tunakufa..." alisema Aisha huku akianza kulia.

"Hatuwezi kufa....hebu tuchukue maboya," alisema Shawn.

Hicho ndicho walichofanya, walijua kwamba kwa namna moja au nyingine marubani wale wasingeweza kuirudisha ndege ile katika hali ya kawaida kutokana na upepo mkali kuendelea kuvuma hivyo walichokifanya ni kuchukua maboya kwa kuamini kwamba kama ndege hiyo ingeanguka basi ingeangukia baharini.

"Vaa haraka Aisha...injini imezima," alisema Shawn huku akimsisitiza Aisha kuvaa boya lile. Hata kabla hawajakaa sawa, ndege ile ikaanza kushuka baharini kwa kasi, kila mtu akaogopa, tayari walikiona kifo kuwa mlangoni, baada ya sekunde kadhaa, kilichosikika kilikuwa ni puuuuu, ndege ikaangukia baharini na kuanza kuzama.

****

Mike alichanganyikiwa, hakuelewa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, mara ya mwisho kuzungumza na Shawn alimwambia kwamba walikuwa ndani ya ndege wakiivuka Bahari ya Atlantiki ila kitu kilichomshangaza ni kwamba kwa kipindi hicho, simu ya mtu huyo haikuwa ikipatikana.

Hali hiyo ilimpa hofu moyoni mwake na kuhisi kwamba inawezekana kuna kitu kibaya kilichotokea, akili yake ikamwambia kwamba inawezekana kulikuwa na ajali ndiyo maana simu haikuwa ikipatikana.

Alichanganyikiwa mno, alichokifanya ni kuwasiliana na watu wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JFK wa hapo New York ili kuona kama walikuwa na mawasiliano na marubani waliokuwa wakirusha ndege hiyo.

“Una hofu ya nini?” alisikika mwanaume mmoja akiuliza kwenye simu.

“Kuna ndege yangu ilikuwa ikitoka Dubai, nashangaa siwapati kwenye simu, kuna tatizo lolote?” aliuliza Mike huku akionekana kuchanganyikiwa.

“Ndege aina gani?”

“Ndogo!”

“Aina?”

“Ultra-long-range G550.”

“Asante! Nitakupigia tafadhali.”

Simu ikakatwa, bado Mike alikuwa na hofu moyoni mwake, alikuwa na uhakika kwamba kulikuwa na kitu kilikuwa kimetokea, kila alipokaa, moyo wake ulikosa amani kabisa, hakutaka kukubali, alichokifanya nii kuondoka kuelekea huko uwanja wa ndege.

Alipofika huko, moja kwa moja akaelekea katika uongozi wa uwanja huo na kuwaambia kilichokuwa kimetokea hivyo kuchukua simu na kuwapigia watu wa mawasiliano ili waambie mahali ndege hiyo ilipokuwa kwa kipindi hicho.

“Hakuna mawasiliano...” alisema jamaa mmoja mara baada ya kujaribu kuwapigia marubani waliokuwa ndani ya ndege hiyo.
“Hamuwapati kabisa?”
“Ndiyo mkuu! Labda kuna tatizo la hali ya hewa, tutaendelea kuwatafuta,” alijibu jamaa wa upande wa pili.

Mike hakutaka kuondoka mahali hapo, alitaka kufuatilia mpaka mwisho, alihitaji kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, moyo wake ulikuwa mzito mno, kuna kipindi alisikia sauti ikimwambia kwamba ndege hiyo ilipata ajali lakini wakati mwingine alipiga moyo konde na kusema kwamba hayo yalikuwa mawazo ya kijinga tu.

Muda ulizidi kwenda mbele, baada ya saa mbili, matokeo wala hayakubadilika, yaliendelea kubaki vilevile kwamba marubani hao hawakupatikana.

“Kuna tatizo?” aliuliza Mike.

“Inawezekana ndege imepata ajali na kuzama baharini. Ngoja tuwasiliane na watu wa usalama wa majini,” alisema kiongozi wa mahali hapo na kuanza kuwasiliana.

Uchunguzi ukaanza kufanyika haraka sana, baada ya saa sita, wakapewa taarifa kwamba kulikuwa na ndege iliyokuwa imepata ajali na kuanguka baharini, walipoambiwa wataje iliandikwa vipi kwa nyuma, wakasema G550.

“Ndiyo yenyewe....” alisema Mike, akajikuta miguu ikiishiwa nguvu na kukaa chini.

Machozi yakaanza kumtoka, hakuamini kilichokuwa kimetokea, alimsubiri kwa hamu mpenzi wake, alitaka kumsubiri, ampokee kwa mabusu mfululizo, sasa ilikuwaje ndege aliyopanda ipate ajali, tena katika siku ambayo kwake ilionekana kuwa ya thamani kuliko siku nyingine.

Walichokifanya ni kuwasiliana na watu wa majini na kwenda huko kufuatilia kama kuna mtu yeyote aliyepona. Mike hakutaka kukubali, hakutaka kuletewa taarifa tu bali alichokifanya na yeye kuelekea huko ili kujionea mwenyewe.

Helkopta ikaandaliwa na ndani ya dakika chache walianza safari ya kuelekea huko. Njia nzima Mike alikuwa akilia tu, hakuwa akiamini kile kilichokuwa kikiendelea kwamba mpenzi wake na mtoto wake mtarajiwa walikuwa wamekufa.

“Hivi ni kweli Aisha amekufa?” alijikuta akiwauliza watu aliokuwa nao humo ndani.

“Hatujui, lakini hakuna aliyekufa, kama kweli ilipata ajali muda saa chache zilizopita, wote watakuwa salama,” alijibu jamaa mmoja, maneno yake yalikuwa yenye kutia moyo ila kwa Mike, yaligonga mwamba.

Walichukua saa mbili mpaka kufika mahali ambapo ndege hiyo ilipokuwa imepata ajali alfajiri ya siku hiyo. Walipofika hapo, waliikuta ndege hiyo, lakini kitu cha ajabu hawakukuta mwili wa mtu hata mmoja zaidi ya nguo za marubani ambazo zilionekana kuraruliwa hali iliyoonyesha kwamba walikuwa wametafunwa na papa.

“Kitu cha kwanza ni kutafuta kiboksi cheusi,” alisema jamaa ambaye alionekana kuwa kongozi wao.

Vijana wawili waliokuwa na mitungi ya hewa safi wakaingia ndani ya maji, huko, wakaanza kutafuta hicho kiboksi cheusi ambacho waliambiwa wakitafute, wala hawakuchukua muda mwingine wakakipata na hivyo kuanza kuitafuta miili miili ya watu waliokuwa ndani ya ndege hiyo.

Zoezi hilo lilikuwa kubwa na gumu, walitafuta zaidi na zaidi, walikwenda huku na kule lakini hawakuweza kuiona miili hiyo kitu kilichowafanya kuwa na wasiwasi mno.

Kati ya watu wote waliokuwa mahali hapo, Mike ndiye alionekana kuwa makini, alikuwa akiangalia huku na kule, moyo wake ulimuomba sana Mungu kwamba afanikiwe kumuona mpenzi wake lakini hilo wala halikuwezekana.

Walikaa huko kwa saa tatu lakini hawakufanikiwa kitu, hivyo Mike kuhisi kwamba mpenzi wake na watu aliokuwa amewatuma, wote walikufa katika ajali hiyo, hivyo wakarudi nchini Marekani huku akiwa na uchungu mkali moyoni mwake.

****

“Usiogope Aisha....usiogope...” ilisikika sauti kutoka kwa Shawn.

“Ninakufa...ninakufa...niokoe...” alipiga kelele Aisha.

“Huwezi kufa, hauwezi kufa....”

Walikuwa kwenye maji, walijitahidi kujitoa ndani ya ndege ile na wote wanne kuanza kuogelea. Hawakujua marubani walikuwa wapi, walichokuwa wakikiangalia kwa wakati huo ni kuyaokoa maisha yao tu.

Waliendelea kuogelea, maboya waliyoyavaa yaliwasaidia sana kuogelea. Mawimbi yalikuwa yakipiga huku na kule, kwa Shawn na wenzake hakukuwa na tatizo lolote lile lakini kwa Aisha, ilibidi ashikwe ili asiweze kupelekwa na mawimbi hayo.
Waliendelea kuogelea kwa zaidi ya saa moja na nusu na ndipo kwa mbali sana wakaweza kukiona kisiwa, hawakujua kilikuwa kisiwa gani, kilikuwa kidogo sana, hivyo wakaanza kuelekea huko.

“Ni lazima twende kule,” alisema Shawn.

“Baridi litaniua...”
“Usife...huwezi kufa, jitahidi kuvumilia Aisha. Ukifa wewe, safari yetu ya kuja Kuwait itakuwa bure kabisa, vumilia,” alisema Shawn huku akiwa amemshika mkono Aisha, waliendelea kusonga mbele kukifuata kisiwa kile.

****

Hali ilikuwa mbaya kisiwani, baridi kali lilikuwa likipiga kupita kawaida, muda wote Aisha alikuwa akitetemeka, alitoka katika nchini Kuwait, moja ya nchi za kiarabu iliyokuwa na joto kali kutokana na hali ya jangwa iliyokuwepo huko.

Kwa Shawn na wenzake, hali haikuwa mbaya sana, walichokifanya ni kuelekea katika kipori kidogo kilichokuwa kisiwani humo na kisha kuchukua kuni na kurudi.

Walizungukwa na maji kila kona na kila walipoangalia, hakukuwa na dalili za meli au mtumbwi wowote ule. Walipelekwa huko bila kutaka, hawakujua Mashariki ilikuwa upande gani, Magharibi wala upande wowote ule.

Wakawasha moto kwa njia za kusaga mawe na kisha kuanza kuota moto. Hakukuwa na aliyelala, usiku mzima walikuwa mahali hapo, walichoka, njaa iliwauma lakini hawakuwa na jinsi, walikuwa wakisubiri msaada wowote ule, uwe meli, boti au chochote kile.

Siku ya kwanza ikakatika, walikuwa hapohapo kisiwani, siku ya pili nayo ikaingia lakini hakukuwa na dalili zozote zile. Walionekana kukata tamaa, wakati mwingine Aisha aliyaona mateso ya kukaa kisiwani hapo kuwa makubwa, ilikuwa ni afadhali kuuawa kule Kuwait kuliko kukutana na mateso makali aliyokuwa akikutana nayo mahali hapo.

Siku ya tatu ikaingia, napo hali ilikuwa mbaya zaidi, hakukuwa na chakula chochote kile, miili yao ikaanza kudhoofika, ikaanza kukosa nguvu kwani kama maji, walijitahidi kuyanywa hayohayo japokuwa yalikuwa ya chumvi lakini kuhusu chakula, hawakuwa na jinsi, waliendelea kubaki njaa hivyohivyo.

“Hatuwezi kuvumilia, ni lazima tuvue samaki,” alisema Shawn huku akiwaangalia wenzake.

“Hatuna nyavu!”
“Kwani kuvua samaki mpaka nyavu? Hakuna, hata kwa kutengeneza mikuki, tutaweza kuvua,” alisema.

Hicho ndicho walichokifanya, walikuwa majasusi, wenye mafunzo mengi, walifunduishwa namna ya kupambana katika kipindi kigumu kama hicho hivyo kitu walichokifanya kilikuwa ni kukata miti, wakaichonga kwa kutumia meno yao, walipoona kidogo imepata ncha kali, wakaingia baharini.

Uvuaji huo ambao ulitumika sana katika nchi zisizoendelea ndiyo walioutumia. Ulikuwa mgumu sana lakini waliweza kuufanya hivyohivyo. Siku hiyo ya kwanza ilikuwa ngumu kwao lakini wakafanikiwa kupata samaki waliowatosha na hivyo kurudi kisiwani na kuwachoma kisa kula.

Maisha yalikuwa hivyohivyo, hakukuwa na chakula kingine zaidi ya samaki ambao waliwala pasipo chumvi, hapo hawakuangalia ladha, walichokiangalia kilikuwa ni kushiba tu.
Mpaka siku ya nne inaingia, wakipigwa baridi kali nyakati za usiku lakini hakukuwa na msaada wowote ule uliokuja, waliendelea kuishi humohumo mpaka kuyazoea maisha ya humo kisiwani.

“Tutachukua muda gani mpaka kuondoka hapa?” aliuliza Aisha.

“Inategemea.”
“Na nini?”

“Na msaada tutakaoupata, kama utachukua siku kumi, tutakaa kwa siku hizo, kama utachukua mwaka mzima, hatuna jinsi,” alijibu Shawn.

Aisha alikata tamaa, alichokuwa akikitaka ni kufarijiwa na Shawn kwamba hata kama walijua kusingekuwa na msaada wowote ule lakini aambiwe tu kwamba msaada ungepatikana.

“Wiki moja imekatika, bado tupo hukuhuku kisiwani!” alisema Aisha huku mwili wake ukiwa umekonda kwa ajili ya mawazo na tabu za mule kisiwani.

“Ndiyo hivyo Aisha! Ninajaribu kuwatafuta kwenye simu, hakuna network,” alisema Shawn.

Walikuwa na simu, yenye uwezo mkubwa ambayo haikuwa ikipitisha maji, haikutumia betri la umeme bali sola hivyo ilivyofika mchana ilikuwa ni lazima kuichaji.

“Nahisi tutakufa hapa,” alisema Aisha huku akionekana kukata tamaa kabisa.
“Haiwezekani! Hatuwezi kufa hapa!”

“Tutaupata wapi msaada?”
“Sijui! Lakini kufa hapa! Haiwezekani Aisha, tutapata msaada tu.”

Wiki ya tatu ilipoingia, Aisha akaanza kujisikia vibaya, kizunguzungu kikaanza, tumbo likaanza kumuuma mno. Alilia siku nzima, Shawn na wenzake ndiyo waliokuwa wakimpoza na kumsaidia katika kila kitu.

Hakukuwa na dawa mahali hapo, walichokifanya ni kutumia mizizi ya miti iliyokuwa kisiwani hapo kama dawa za kumtibu Aisha ambaye kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele, hali yake iliendelea kuwa mbaya sana.

“Vipi Shawn?” aliuliza Sam.

“Network inakuja na kukata, inakuja na kukata....” alijibu Shawn.

Hiyo ilikuwa ni saa kumi alfajiri, hawakulala usiku mzima, ni Aisha tu ndiye aliyelala tena kwa usingizi wa mang’amung’amu. Wao walikesha wakiiangalia simu ambayo ilikuwa inashika network na kupotea.

“Fanya kitu kimoja.”
“Kipi?”
“Mtumie meseji Mike.”
“Hakuna network.”
“Wewe mtumie, kama network ikija, meseji itakwenda tu.”

Hakuwa na jinsi, alichoambiwa kilikuwa sahihi kabisa hivyo kutuma meseji hiyo ambayo wala haikwenda kutokana na eneo hilo kukosekana kwa network.

****

Mike alichanganyikiwa, hakuamini kama kweli alimpoteza msichana aliyekuwa akimpenda kwa moyo wote lakini kilichomuumiza zaidi ni kupotea kwa mtoto wake ambaye angetarajiwa kuzaliwa miezi michache ijayo.
Akakosa furaha, akawa mtu wa kulia tu, kila siku akawa anaomboleza, wakati mwingine aliona kama Mungu akimuonea tu. Alitumia gharama kubwa mno kumuokoa Aisha kutoka katika kifo nchini Kuwait mpaka huko lakini mwisho wa siku, hata kabla hajaingia nchini Marekani, tayari msichana huyo alikufa njiani.
“Mungu! Mlaze mpenzi wangu mahali pema peponi,” alisema Mike.

Hakuwa na jinsi, moyo wake ulimwambia kwamba alimpoteza mpenzi wake, hakukuwa na kingine alichokifanya zaidi ya kumtaka Mungu amlinde Aisha huko alipokuwa.

Wiki ya kwanza ikakatika, hakukuwa na taarifa zozote zile, wiki ya pili ikakatika, hakukuwa na taarifa zozote kutoka huko walipokuwa. Ilipofika wiki ya tatu, tena katikati, saa mbili asubuhi akiwa ofisini kwake huku akiwa na mawazo, akasikia mlio wa meseji ukiwa umelia kuashiria kwamba kuna meseji imeingia.

Akaichukua simu yake na kuifungua meseji hiyo, akakutana na ujumbe mfupi ulioandikwa ‘WE STILL ALIVE IN THE ISLAND’ (BADO TUPO HAI KISIWANI) Mike akashtuka, alipoangalia namba, ilikuwa ni ya Shawn.

Je, nini kitaendelea?
 
Asante madame ila sehemu ya 28 ni kama imerukwa
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini.

Mike akashtuka, hakuamini kile alichokiona kwamba watu aliokuwa amewatafuta kwa wiki nzima walikuwa katika kisiwa sehemu fulani. Kwanza akainuka na kuisoma vizuri meseji ile, alitaka kuona alisoma kama ilivyoandikwa au alikuwa amechanganya, akairudia na kurudia, kweli ilisema vilevile kwamba watu hao walikuwa kisiwani.

Hakujua ni kisiwa gani walichokuwepo, hakutaka kupoteza muda humo ofisini, moja kwa moja akawasiliana na watu wa baharini na kuwaambia kwamba alipokea ujumbe wa maneno kuwa watu aliowatuma walikuwa hai kisiwani.

“Wapo na huyo msichana?” aliuliza jamaa wa idara ya ulinzi wa baharini.

“Bado sijajua, nimeuliza lakini meseji haiendi, nafikiri hakuna network,” alisema Mike.

Hakukuwa na muda wa kupoteza tena, walichokifanya ni kuingia ndani ya helkopta na kuanza safari ya kuelekea huko. Njiani, kila mmoja hakujua ni kisiwa gani ambacho walikuwepo watu hao. Ndani ya Bahari ya Atlantiki kulikuwa na zaidi ya visiwa hamsini, je ni kisiwa gani walichokuwepo watu hao, hawakujua.

“Kuna zaidi ya visiwa hamsini, sasa watakuwa kisiwa gani?” aliuliza rubani.

“Nafikiri kimojawapo, hasa kile kisichokaliwa na watu,” alijibu Mike.

Ilikuwa kazi kubwa kukisia, hawakuelewa mahali walipokuwa watu hao, walichanganyikiwa, alichokifanya Mike ni kuchukua ramani iliyokuwemo ndanii ya helkopta ile na kuanza kuangalia visiwa vilivyokuwa ndani ya bahari hiyo.

Kulikuuwa na visiwa vingi kama Braza, Fogo, West Point, Sea Lion na vingine vingi lakini kati ya hivyo vyote, vilikuwa vikikaliwa na watu, hivyo huko kungekuwa na network, walichotaka kujua wao, ni kile kisiwa ambacho hakikuwa kikikaliwa na watu na ambacho hakikuwa na network yoyote ile.

“Hivyo vyote ulivyovitaja, vinakaliwa na watu,” alisema rubani.

“Sasa kipi ambacho hakikaliwi na watu?”
“Hata mimi sijui kwa kweli, wewe twendeni tu, tutaona mbele ya safari,” alisema kiongozi wa ulinzi katika bahari hiyo, Paul.
Safari iliendelea, walipita katika visiwa vingi, kulikuwa na watu wengi, hawakutaka kutua huko, hakukuwa sehemu sahihi ambayo watu waliopotea walipokuwa.

Baada ya saa nne wakiwa angani, wakafika katika kisiwa ambacho kwa mbali hakukuwa na mtu wala jengo lolote lile, wakajua kwamba inawezekana hicho ndicho kisiwa walichokuwa wameambiwa.

Harakaharaka helkopta ikaanza kuteremka, hakukuwa na mtu zaidi ya miti, kilionekana kuwa kisiwa kilichotengwa ambacho kilikuwa mbali kabisa na visiwa vingine.

Wakateremka na kuanza kuangalia huku na kule, hakukuwa na mtu yeyote yule, walijitahidi kuangalia zaidi na zaidi tena huku wakiita, hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia.

“Kweli watakuwa katika kisiwa hiki?” aliuliza rubani.

“Sidhani! Hebu twendeni katika kisiwa kingine, ila hiki kimetelekezwa sana mpaka network napo hakuna,” alisema Paul.

Hawakuwa na jinsi, wakaanza kupiga hatua kurudi kwenye helkopta ile, hawakuwa na uhakika kama watu hao walikuwa kwenye kisiwa hicho au la, japokuwa walitumia saa nyingi, hawakuwa na jinsi, walitakiwa kuondoka kuelekea katika kisiwa kingine.

****

“Sam...unasikia sauti helkopta?” aliuliza Shawn.

“Hapana!”

“Hebu sikiliza vizuri...”

Kwa mbali walikuwa wakisikia sauti ya helkopta kutoka katika upande mwingine kabisa, nyuma ya kisiwa hicho. Walikuwa na uhakika kwamba sauti waliyokuwa wakiisikia ilikuwa ni ya helkopta kweli lakini haikuwa katika upande waliokuwepo, ilikuwa katika upande wa pili kabisa.

Kila mmoja akawa na nguvu isipokuwa mtu mmoja tu, huyu alikuwa Aisha ambaye kwa kipindi walichokuwa humo kisiwani, hali yake haikuwa nzuri kabisa.

Walimpa mizizo kama dawa lakini hakukuwa na kilichobadilika, hali ilikuwa mbaya mno na hakukuwa na kitu chochote alichokisubiria mahali hapo zaidi ya kifo.

Kwa kasi ya ajabu Sam akatoka mahali hapo na kuanza kuelekea upande wa pili. Kilikuwa kisiwa kikubwa mno, hata alipozunguka, alichoka sana lakini hakutaka kusimama, alikimbia ufukwe kwa ufukwe huku akiita ili kama watu hao wakisikia, basi wasimame na hivyo kuwasiaidia.

“Tusaidieni...tusaidieniiiii” aliita Sam huku akikimbia kwa kasi.

Mike na wenzake tayari walikuwa wamepanda ndani ya helkopta ile, mlio wake ulikuwa mkubwa ambao uliimeza kabisa sauti ya Sam ambaye alikuwa akielekea kule walipokuwa.

Mike hakuridhika, moyo wake ulikuwa mzito mno, hakuamini kama kweli katika kisiwa hicho hakukuwa na mtu aliyekuwa akiishi, aliamini kabisa kwamba mpenzi wake na watu aliowatuma walikuwa mahali hapo.

“Moyo wangu mzito sana,” alisema Mike huku akiwaangalia wenzake.

“Kwa nini?”
“Nadhani wapo humu.”
“Hapana! Si unaona tumeangalia kote!” alisema Paul.

“Hapana! Hatujaangalia, ila kama mnataka twende kwingine, hakuna tatizo,” alisema Mike kwa sautio ya chini, moyo wake ulikuwa mzito mno.

Helkopta ikaanza kuinuka tayari kwa kuondoka mahali hapo. Macho ya Mike yalikuwa chini, hakuamini kama kweli walikuwa wakiondoka pasipo kuwaona watu hao.

Huku helkopta ikiwa imefika umbali wa mita hamsini kutoka katika kisiwa kile, kwa mbali Mike akamuona mtu akikimbia kwa kasi kuelekea kule walipokuwa wametua.

Kwanza akashtuka, hakuamini kama kweli yule alikuwa binadamu au kiumbe kingine kwani alikuwa akionekana kwa mbali kidogo. Hapohapo akawaambia wenzake kwamba kulikuwa na mtu aliyekuwa akikimbia kisiwani hivyo wasiondoke.

“Unasemaje?”
“Kuna mtu, yule kule chini,” alisema Mike kwa hamu, alitamani hata kujirusha kutoka katika helkopta ile.

Walipoangalia chini, kweli walimuona mtu mmoja akiwa anawapungia mikono, kila mmoja akaonekana kufurahi, kwa haraka sana, hapohapo helkopta ikaanza kushushwa, hata kabla hawajafika chini, Mike akaruka.

“Sam...” alimuita mtu huyo.

Sam hakuweza kuzungumza chochote kile, alibaki kimya, alikuwa akihema kwa nguvu, mwili wake ulichoka na alikuwa amekonda. Mike akasikia maumivu moyoni mwake, machozi yakaanza kumtoka.

“Aisha yupo wapi?” aliuliza Mike huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Unasema?”
“Aisha yupo wapi?” aliuliza Mike, Sam akabaki kimya kwa muda, kwa jinsi alivyoonekana, hofu kubwa ilimjaa moyoni mwake. Mike akaishiwa nguvu, akakaa chini kwani jibu alilohisi ndilo alilotegemea kupokea kutoka kwa Sam.

“Aisha amekufa...” ilikuwa ni sauti pekee iliyosikika moyoni mwa Mike.

****

Mike alibaki akitetemeka, alimwangalia Sam huku sauti ile ikiendelea kusikika moyoni mwake kwamba msichana aliyekuwa akimpenda alikuwa amekufa. Sam hakujibu kitu, alikuwa amechoka na muda wote alikuwa akihema kwa nguvu.

Mike alikuwa na shauku ya kusikia jibu juu ya kile alichokuwa amekiuliza, alibaki akimwangalia mwanaume huyo, alipopumzika kwa dakika moja, akampa jibu lililompa faraja kubwa moyoni mwake kwamba msichana huyo alikuwa hai, ila alikuwa hoi.

“Unasemaje?” aliuliza Mike.

“Twendeni...” alisema Sam.

Wakaondoka na kuelekea huko aliposema Sam. Japokuwa hakuwa akipafahamu lakini Mike ndiye alikuwa mtu wa mbele kabisa, alikuwa akipiga hatua za harakaharaka, alitamani sana kumuona mpenzi wake, alimpenda kwa mapenzi ya dhati hivyo kuona akifariki dunia, kilikuwa moja ya vitu asivyopenda kabisa vitokee.

Walichukua dakika kadhaa wakafika upande wa pili, macho ya Mike yakatua kwa watu watatu akiwemo mpenzi wake ambaye alikuwa hoi chini. Kwa hatua za harakaharaka Mike akamsogelea mpenzi wake pale chini alipokuwa.

Mwili wake ulikonda mno, kwa kumwangalia tu alionekana kuwa mgonjwa, pasipo kutarajia, Mike akaanza kutokwa na machozi yaliyochanganyikana na vitu viwili, cha kwanza kilikuwa ni furaha hasa baada ya kumuona mpenzi wake lakini cha pili kilikuwa ni maumivu makali hasa baada ya kumkuta mpenzi wake akiwa kwenye hali ile.

“nini kimetokea?” aliuliza Mike.

“Mimba inaweza kuharibika...”

“Unasemaje?” aliuliza Mike huku akionekana kutokuamini.

“Mimba yake ipo kwenye hali ya hatari!”

Mike alipoambiwa hivyo akachanganyikiwa, akamwambia rubani arudi kule alipokuwa, kuichukua helkopta ile na kuipeleka katika upande mwingine wa kisiwa ili wamchukue Aisha na kuondoka naye, hicho kikafanyika haraka sana.

“Aisha...Aisha mpenzi nipo hapa kwa ajili yako...” alisema Mike huku akimwangalia mpenzi wake machoni mwake.

Aisha aliyafumbua macho kwa mbali sana, alikuwa hoi, aliumwa sana na wakati mwingine alihisi kama angekufa, kidogo uso wake ukajawa na tabasamu pana.

Wala haukuchukua muda mrefu, helkopta ikaletwa, wakampakiza Aisha na kuondoka. Ndani ya helkopta, muda wote Mike alikuwa amemuegemeza mpenzi wake katika mapaja yake, kila alipomwangalia, alimuonea huruma na alisikia maumivu makali moyoni mwake.

Helkopta iliondoka na baada ya dakika kumi, Kisiwa cha West Point kikaanza kuonekana machoni mwao. Safari ya kuelekea Marekani ilikuwa ndefu sana na wasingeweza kufanya hivyo kwa kuhisi kwamba Aisha angeweza kufa hata njiani, hivyo kilichofanyika ni kutua katika kisiwa hicho kwa ajili ya matibabu.

Helkopta ilipotua tu, wakamshusha na kumbeba na kumpeleka katika hospitali ambayo haikuwa mbali na mahali hapo helkopta ilipotua. Watu wa kisiwa hicho walibaki wakiwaangalia tu, hawakujua hao walikuwa wakina nani, walitoka wapi na walifuata nini mahali hapo.

“Anaumwa nini?” aliuliza nesi mara baada ya kufika hospitalini hapo.

“Anaumwa njaa, kingine ni kwamba mimba inataka kuharibika...” alijibu Mike, hata Shawn mwenyewe hakuwa na nguvu za kujibu.

Machela ikasukumwa mpaka katika chumba kimoja ambapo huko Aisha akalazwa katika kitanda kimoja, kitu cha kwanza kabisa kufanyika ni kuchomwa sindano ya glucose kwa ajili ya kuupa nguvu mwili wake.

“Dokta, atapona?” aliuliza Mike, kwa kumwangalia tu alionekana kuchanganyikiwa.

“Atapona tu, wala usijali!”

Mike hakutaka kuondoka hospitalini hapo, aliwaagiza wenyeji wa kisiwani hapo, Shawn na wenzake wapelekwe katika hoteli ya gharama, wale na kufanya mambo mengine wakati yeye akiendelea kuwa hospitalini hapo.

Hicho ndicho kilichofanyika, wakaondoka huku yeye akiendelea kubaki pale hospitali, kitu alichokitaka ni kuona mpenzi wake angeishia wapi. Alibaki akimuomba Mungu, hakukuwa na kitu kilichokuwa kikimuumiza kama kuona mpenzi wake akiwa hoi kitandani.

Pale alipokuwa, mapigo ya Aisha yakaanza kupata nguvu ya kudunda, yalikuwa mafanikio makubwa, akasafishwa sehemu zake za siri na kupewa dawa zenye nguvu ya kuua bakteria walioanza kushambulia sehemu hiyo.

Hawakuishia hapo, waliendelea hata kumchunguza kwa ndani zaidi kuona kama kulikuwa na tatizo kubwa, walipoona kwamba hakuna tatizo la kutisha, wakamuwekea dawa nyingine yenye nguvu zaidi.

Siku ya kwanza ikapita huku Aisha akiwa hoi kitandani pale, Mike hakutaka kutoka, aliendelea kubaki chumbani palepale mpaka usiku ulipoingia. Kesho yake, akaamka akiwa kwenye kiti, akasimama na kumsogelea Aisha pale kitandani alipokuwa amelala, akamsogelea, hapohapo Aisha akayafumbua macho yake.

“Umeamka hatimaye!” alisema Mike huku akimwangalia msichana huyo usoni.

Aisha hakuzungumza kitu, aliyafumbua macho yake lakini hakuwa na nguvu zozote za kuongea, akabaki akimwangalia mpenzi wake tu. Kidogo moyo wake ukafarijika, ile furaha ambayo ilipotea ikaanza kurudi upya moyoni mwake.

Baada ya siku tatu, kidogo Aisha alionekana kupata nafuu na hivyo kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani. Mpaka wanaingia, Aisha alionekana kuwa mwenye furaha mno, hakuamini kwamba mwanzo wa safari ile ndefu hatimaye angefika nchini Marekani, sehemu ambayo kulikuwa na watu wengi duniani walikuwa wakiililia.

Maisha yakaanza upya nchini humo, Aisha hakutakiwa kuonekana, kuwa kwake nchini humo ilikuwa siri kubwa, aliishi na Mike kama mke na mume.

Mimba ya Aisha iliendelea kukua, kila siku Mike alikuwa pembeni yake, kuwa karibu na msichana huyo lilikuwa jambo lililompa furaha sana maishani mwake, hakuamini kama mwisho wa siku naye alikuwa akienda kuitwa baba.

“Daktari amesemaje?” aliuliza Mike.

“Mtoto wa kike!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Ataitwa Monica...ninakupenda mpenzi wangu!” alisema Mike huku akitoa tabasamu pana.

Siku zikaendelea kwenda mbele, miezi ikakatika na baada ya mimba kufikisha miezi tisa, Aisha akaanza kujisikia uchungu ambapo akachukuliwa na kupelekwa hospitali.

Mike alipopigiwa simu na kuambiwa kilichokuwa kimetokea, hakuamini, akatoka ofisini kwake, hata kabla dereva wake hajafika, akaingia ndani ya gari na kuondoka kuelekea hospitali. Alitaka kufuatilia kila hatua, alipofika, akachukuliwa na kuambiwa kusubiri nje ya chumba cha leba.

“Hakuna tatizo!” alisema Mike na kutulia mahali hapo, baada ya saa moja, akaanza kusikia sauti ya mtoto akilia, akashindwa kuvumilia, akapiga magoti na kumshukuru Mungu! Hatimaye akafanikiwa kuwa baba.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini.

Mike akashtuka, hakuamini kile alichokiona kwamba watu aliokuwa amewatafuta kwa wiki nzima walikuwa katika kisiwa sehemu fulani. Kwanza akainuka na kuisoma vizuri meseji ile, alitaka kuona alisoma kama ilivyoandikwa au alikuwa amechanganya, akairudia na kurudia, kweli ilisema vilevile kwamba watu hao walikuwa kisiwani.

Hakujua ni kisiwa gani walichokuwepo, hakutaka kupoteza muda humo ofisini, moja kwa moja akawasiliana na watu wa baharini na kuwaambia kwamba alipokea ujumbe wa maneno kuwa watu aliowatuma walikuwa hai kisiwani.

“Wapo na huyo msichana?” aliuliza jamaa wa idara ya ulinzi wa baharini.

“Bado sijajua, nimeuliza lakini meseji haiendi, nafikiri hakuna network,” alisema Mike.

Hakukuwa na muda wa kupoteza tena, walichokifanya ni kuingia ndani ya helkopta na kuanza safari ya kuelekea huko. Njiani, kila mmoja hakujua ni kisiwa gani ambacho walikuwepo watu hao. Ndani ya Bahari ya Atlantiki kulikuwa na zaidi ya visiwa hamsini, je ni kisiwa gani walichokuwepo watu hao, hawakujua.

“Kuna zaidi ya visiwa hamsini, sasa watakuwa kisiwa gani?” aliuliza rubani.

“Nafikiri kimojawapo, hasa kile kisichokaliwa na watu,” alijibu Mike.

Ilikuwa kazi kubwa kukisia, hawakuelewa mahali walipokuwa watu hao, walichanganyikiwa, alichokifanya Mike ni kuchukua ramani iliyokuwemo ndanii ya helkopta ile na kuanza kuangalia visiwa vilivyokuwa ndani ya bahari hiyo.

Kulikuuwa na visiwa vingi kama Braza, Fogo, West Point, Sea Lion na vingine vingi lakini kati ya hivyo vyote, vilikuwa vikikaliwa na watu, hivyo huko kungekuwa na network, walichotaka kujua wao, ni kile kisiwa ambacho hakikuwa kikikaliwa na watu na ambacho hakikuwa na network yoyote ile.

“Hivyo vyote ulivyovitaja, vinakaliwa na watu,” alisema rubani.

“Sasa kipi ambacho hakikaliwi na watu?”
“Hata mimi sijui kwa kweli, wewe twendeni tu, tutaona mbele ya safari,” alisema kiongozi wa ulinzi katika bahari hiyo, Paul.
Safari iliendelea, walipita katika visiwa vingi, kulikuwa na watu wengi, hawakutaka kutua huko, hakukuwa sehemu sahihi ambayo watu waliopotea walipokuwa.

Baada ya saa nne wakiwa angani, wakafika katika kisiwa ambacho kwa mbali hakukuwa na mtu wala jengo lolote lile, wakajua kwamba inawezekana hicho ndicho kisiwa walichokuwa wameambiwa.

Harakaharaka helkopta ikaanza kuteremka, hakukuwa na mtu zaidi ya miti, kilionekana kuwa kisiwa kilichotengwa ambacho kilikuwa mbali kabisa na visiwa vingine.

Wakateremka na kuanza kuangalia huku na kule, hakukuwa na mtu yeyote yule, walijitahidi kuangalia zaidi na zaidi tena huku wakiita, hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia.

“Kweli watakuwa katika kisiwa hiki?” aliuliza rubani.

“Sidhani! Hebu twendeni katika kisiwa kingine, ila hiki kimetelekezwa sana mpaka network napo hakuna,” alisema Paul.

Hawakuwa na jinsi, wakaanza kupiga hatua kurudi kwenye helkopta ile, hawakuwa na uhakika kama watu hao walikuwa kwenye kisiwa hicho au la, japokuwa walitumia saa nyingi, hawakuwa na jinsi, walitakiwa kuondoka kuelekea katika kisiwa kingine.

****

“Sam...unasikia sauti helkopta?” aliuliza Shawn.

“Hapana!”

“Hebu sikiliza vizuri...”

Kwa mbali walikuwa wakisikia sauti ya helkopta kutoka katika upande mwingine kabisa, nyuma ya kisiwa hicho. Walikuwa na uhakika kwamba sauti waliyokuwa wakiisikia ilikuwa ni ya helkopta kweli lakini haikuwa katika upande waliokuwepo, ilikuwa katika upande wa pili kabisa.

Kila mmoja akawa na nguvu isipokuwa mtu mmoja tu, huyu alikuwa Aisha ambaye kwa kipindi walichokuwa humo kisiwani, hali yake haikuwa nzuri kabisa.

Walimpa mizizo kama dawa lakini hakukuwa na kilichobadilika, hali ilikuwa mbaya mno na hakukuwa na kitu chochote alichokisubiria mahali hapo zaidi ya kifo.

Kwa kasi ya ajabu Sam akatoka mahali hapo na kuanza kuelekea upande wa pili. Kilikuwa kisiwa kikubwa mno, hata alipozunguka, alichoka sana lakini hakutaka kusimama, alikimbia ufukwe kwa ufukwe huku akiita ili kama watu hao wakisikia, basi wasimame na hivyo kuwasiaidia.

“Tusaidieni...tusaidieniiiii” aliita Sam huku akikimbia kwa kasi.

Mike na wenzake tayari walikuwa wamepanda ndani ya helkopta ile, mlio wake ulikuwa mkubwa ambao uliimeza kabisa sauti ya Sam ambaye alikuwa akielekea kule walipokuwa.

Mike hakuridhika, moyo wake ulikuwa mzito mno, hakuamini kama kweli katika kisiwa hicho hakukuwa na mtu aliyekuwa akiishi, aliamini kabisa kwamba mpenzi wake na watu aliowatuma walikuwa mahali hapo.

“Moyo wangu mzito sana,” alisema Mike huku akiwaangalia wenzake.

“Kwa nini?”
“Nadhani wapo humu.”
“Hapana! Si unaona tumeangalia kote!” alisema Paul.

“Hapana! Hatujaangalia, ila kama mnataka twende kwingine, hakuna tatizo,” alisema Mike kwa sautio ya chini, moyo wake ulikuwa mzito mno.

Helkopta ikaanza kuinuka tayari kwa kuondoka mahali hapo. Macho ya Mike yalikuwa chini, hakuamini kama kweli walikuwa wakiondoka pasipo kuwaona watu hao.

Huku helkopta ikiwa imefika umbali wa mita hamsini kutoka katika kisiwa kile, kwa mbali Mike akamuona mtu akikimbia kwa kasi kuelekea kule walipokuwa wametua.

Kwanza akashtuka, hakuamini kama kweli yule alikuwa binadamu au kiumbe kingine kwani alikuwa akionekana kwa mbali kidogo. Hapohapo akawaambia wenzake kwamba kulikuwa na mtu aliyekuwa akikimbia kisiwani hivyo wasiondoke.

“Unasemaje?”
“Kuna mtu, yule kule chini,” alisema Mike kwa hamu, alitamani hata kujirusha kutoka katika helkopta ile.

Walipoangalia chini, kweli walimuona mtu mmoja akiwa anawapungia mikono, kila mmoja akaonekana kufurahi, kwa haraka sana, hapohapo helkopta ikaanza kushushwa, hata kabla hawajafika chini, Mike akaruka.

“Sam...” alimuita mtu huyo.

Sam hakuweza kuzungumza chochote kile, alibaki kimya, alikuwa akihema kwa nguvu, mwili wake ulichoka na alikuwa amekonda. Mike akasikia maumivu moyoni mwake, machozi yakaanza kumtoka.

“Aisha yupo wapi?” aliuliza Mike huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Unasema?”
“Aisha yupo wapi?” aliuliza Mike, Sam akabaki kimya kwa muda, kwa jinsi alivyoonekana, hofu kubwa ilimjaa moyoni mwake. Mike akaishiwa nguvu, akakaa chini kwani jibu alilohisi ndilo alilotegemea kupokea kutoka kwa Sam.

“Aisha amekufa...” ilikuwa ni sauti pekee iliyosikika moyoni mwa Mike.

****

Mike alibaki akitetemeka, alimwangalia Sam huku sauti ile ikiendelea kusikika moyoni mwake kwamba msichana aliyekuwa akimpenda alikuwa amekufa. Sam hakujibu kitu, alikuwa amechoka na muda wote alikuwa akihema kwa nguvu.

Mike alikuwa na shauku ya kusikia jibu juu ya kile alichokuwa amekiuliza, alibaki akimwangalia mwanaume huyo, alipopumzika kwa dakika moja, akampa jibu lililompa faraja kubwa moyoni mwake kwamba msichana huyo alikuwa hai, ila alikuwa hoi.

“Unasemaje?” aliuliza Mike.

“Twendeni...” alisema Sam.

Wakaondoka na kuelekea huko aliposema Sam. Japokuwa hakuwa akipafahamu lakini Mike ndiye alikuwa mtu wa mbele kabisa, alikuwa akipiga hatua za harakaharaka, alitamani sana kumuona mpenzi wake, alimpenda kwa mapenzi ya dhati hivyo kuona akifariki dunia, kilikuwa moja ya vitu asivyopenda kabisa vitokee.

Walichukua dakika kadhaa wakafika upande wa pili, macho ya Mike yakatua kwa watu watatu akiwemo mpenzi wake ambaye alikuwa hoi chini. Kwa hatua za harakaharaka Mike akamsogelea mpenzi wake pale chini alipokuwa.

Mwili wake ulikonda mno, kwa kumwangalia tu alionekana kuwa mgonjwa, pasipo kutarajia, Mike akaanza kutokwa na machozi yaliyochanganyikana na vitu viwili, cha kwanza kilikuwa ni furaha hasa baada ya kumuona mpenzi wake lakini cha pili kilikuwa ni maumivu makali hasa baada ya kumkuta mpenzi wake akiwa kwenye hali ile.

“nini kimetokea?” aliuliza Mike.

“Mimba inaweza kuharibika...”

“Unasemaje?” aliuliza Mike huku akionekana kutokuamini.

“Mimba yake ipo kwenye hali ya hatari!”

Mike alipoambiwa hivyo akachanganyikiwa, akamwambia rubani arudi kule alipokuwa, kuichukua helkopta ile na kuipeleka katika upande mwingine wa kisiwa ili wamchukue Aisha na kuondoka naye, hicho kikafanyika haraka sana.

“Aisha...Aisha mpenzi nipo hapa kwa ajili yako...” alisema Mike huku akimwangalia mpenzi wake machoni mwake.

Aisha aliyafumbua macho kwa mbali sana, alikuwa hoi, aliumwa sana na wakati mwingine alihisi kama angekufa, kidogo uso wake ukajawa na tabasamu pana.

Wala haukuchukua muda mrefu, helkopta ikaletwa, wakampakiza Aisha na kuondoka. Ndani ya helkopta, muda wote Mike alikuwa amemuegemeza mpenzi wake katika mapaja yake, kila alipomwangalia, alimuonea huruma na alisikia maumivu makali moyoni mwake.

Helkopta iliondoka na baada ya dakika kumi, Kisiwa cha West Point kikaanza kuonekana machoni mwao. Safari ya kuelekea Marekani ilikuwa ndefu sana na wasingeweza kufanya hivyo kwa kuhisi kwamba Aisha angeweza kufa hata njiani, hivyo kilichofanyika ni kutua katika kisiwa hicho kwa ajili ya matibabu.

Helkopta ilipotua tu, wakamshusha na kumbeba na kumpeleka katika hospitali ambayo haikuwa mbali na mahali hapo helkopta ilipotua. Watu wa kisiwa hicho walibaki wakiwaangalia tu, hawakujua hao walikuwa wakina nani, walitoka wapi na walifuata nini mahali hapo.

“Anaumwa nini?” aliuliza nesi mara baada ya kufika hospitalini hapo.

“Anaumwa njaa, kingine ni kwamba mimba inataka kuharibika...” alijibu Mike, hata Shawn mwenyewe hakuwa na nguvu za kujibu.

Machela ikasukumwa mpaka katika chumba kimoja ambapo huko Aisha akalazwa katika kitanda kimoja, kitu cha kwanza kabisa kufanyika ni kuchomwa sindano ya glucose kwa ajili ya kuupa nguvu mwili wake.

“Dokta, atapona?” aliuliza Mike, kwa kumwangalia tu alionekana kuchanganyikiwa.

“Atapona tu, wala usijali!”

Mike hakutaka kuondoka hospitalini hapo, aliwaagiza wenyeji wa kisiwani hapo, Shawn na wenzake wapelekwe katika hoteli ya gharama, wale na kufanya mambo mengine wakati yeye akiendelea kuwa hospitalini hapo.

Hicho ndicho kilichofanyika, wakaondoka huku yeye akiendelea kubaki pale hospitali, kitu alichokitaka ni kuona mpenzi wake angeishia wapi. Alibaki akimuomba Mungu, hakukuwa na kitu kilichokuwa kikimuumiza kama kuona mpenzi wake akiwa hoi kitandani.

Pale alipokuwa, mapigo ya Aisha yakaanza kupata nguvu ya kudunda, yalikuwa mafanikio makubwa, akasafishwa sehemu zake za siri na kupewa dawa zenye nguvu ya kuua bakteria walioanza kushambulia sehemu hiyo.

Hawakuishia hapo, waliendelea hata kumchunguza kwa ndani zaidi kuona kama kulikuwa na tatizo kubwa, walipoona kwamba hakuna tatizo la kutisha, wakamuwekea dawa nyingine yenye nguvu zaidi.

Siku ya kwanza ikapita huku Aisha akiwa hoi kitandani pale, Mike hakutaka kutoka, aliendelea kubaki chumbani palepale mpaka usiku ulipoingia. Kesho yake, akaamka akiwa kwenye kiti, akasimama na kumsogelea Aisha pale kitandani alipokuwa amelala, akamsogelea, hapohapo Aisha akayafumbua macho yake.

“Umeamka hatimaye!” alisema Mike huku akimwangalia msichana huyo usoni.

Aisha hakuzungumza kitu, aliyafumbua macho yake lakini hakuwa na nguvu zozote za kuongea, akabaki akimwangalia mpenzi wake tu. Kidogo moyo wake ukafarijika, ile furaha ambayo ilipotea ikaanza kurudi upya moyoni mwake.

Baada ya siku tatu, kidogo Aisha alionekana kupata nafuu na hivyo kuendelea na safari ya kuelekea nchini Marekani. Mpaka wanaingia, Aisha alionekana kuwa mwenye furaha mno, hakuamini kwamba mwanzo wa safari ile ndefu hatimaye angefika nchini Marekani, sehemu ambayo kulikuwa na watu wengi duniani walikuwa wakiililia.

Maisha yakaanza upya nchini humo, Aisha hakutakiwa kuonekana, kuwa kwake nchini humo ilikuwa siri kubwa, aliishi na Mike kama mke na mume.

Mimba ya Aisha iliendelea kukua, kila siku Mike alikuwa pembeni yake, kuwa karibu na msichana huyo lilikuwa jambo lililompa furaha sana maishani mwake, hakuamini kama mwisho wa siku naye alikuwa akienda kuitwa baba.

“Daktari amesemaje?” aliuliza Mike.

“Mtoto wa kike!”
“Kweli?”
“Ndiyo!”

“Ataitwa Monica...ninakupenda mpenzi wangu!” alisema Mike huku akitoa tabasamu pana.

Siku zikaendelea kwenda mbele, miezi ikakatika na baada ya mimba kufikisha miezi tisa, Aisha akaanza kujisikia uchungu ambapo akachukuliwa na kupelekwa hospitali.

Mike alipopigiwa simu na kuambiwa kilichokuwa kimetokea, hakuamini, akatoka ofisini kwake, hata kabla dereva wake hajafika, akaingia ndani ya gari na kuondoka kuelekea hospitali. Alitaka kufuatilia kila hatua, alipofika, akachukuliwa na kuambiwa kusubiri nje ya chumba cha leba.

“Hakuna tatizo!” alisema Mike na kutulia mahali hapo, baada ya saa moja, akaanza kusikia sauti ya mtoto akilia, akashindwa kuvumilia, akapiga magoti na kumshukuru Mungu! Hatimaye akafanikiwa kuwa baba.

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Ijumaa
Aiseee nimejiskia raha
 
Back
Top Bottom