Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #221
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
Sehemu ya Thelathini na Moja.
Maisha mapya yakaanza, Mike alionekana kuwa na furaha kupita kawaida, kila wakati alikuwa na mtoto wake, alimpenda Monica kuliko kitu chochote kile katika maisha yake.
Siku ziliendelea kukatika, hakuwa mtu wa kuwahi ofisini kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, mara kwa mara alipokuwa akiamka, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumchukua mtoto wake kisha kumbeba.
Kazi ya kumhudumia ilikuwa juu yake, hakutaka mpenzi wake, Aisha asumbuke kwa kitu chochote kile. Kutokana na mchanganyiko wa rangi aliokuwa nao, Monica alionekana kuwa mrembo tangu kipindi hicho alichokuwa mdogo.
Marafiki wa Mike kila siku walifika nyumbanii hapo kumpongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya, kwake, ilikuwa ni furaha tele. Aisha alikuwa na afya tele, hakutaka kuwasiliana na wazazi wake, alijaribu kusahau kila kitu kilichopita nchini Kuwait na hakutaka urudi tena huko.
Mpaka mwaka wa kwanza unakatimia, Monica alikuwa na uzuri wa sura yake ulionekana kwa kiasi kikubwa. Mike alikuwa na kazi kubwa ya kumpa maisha mazuri binti yake, huyo ndiye alikuwa mtu pekee aliyemthamini.
“Nitamlinda maisha yangu yote...” alisema Mike huku akiwa amembeba Monica katika bustani ya maua.
MIAKA MITANO BAADAYE
Monica alikuwa msichana mrembo mno, kila alipokwenda, kulikuwa gumzo, alikuuwa na sura nzuri, nusu alikuwa mtu mweusi na nusu alikuwa Mzungu. Maisha yake yalikuwa ya kifahari, kila siku baba yake alikuwa na jukumu kubwa la kumfuata shuleni na kisha kumpeleka nyumbani.
Huyo ndiye alikuwa roho yake, alitamani sana kupata mtoto wa pili na walikubaliana mpaka huyo atakapofikisha umri wa miaka mitano, hivyo wakaanza kufanya jitihada za kumtafuta mtoto wa pili.
Siku moja akiwa ofisini, akapigiwa simu na kupewa taarifa kwamba mpenzi wake, Aisha alikuwa hoi, alikuwa akitokwa na damu sehemu za siri na haikujulikana tatizo lilikuwa nini.
Hakukuwa na muda wa kumsubiri daktari wa familia afike bali alichomwambia mfanyakazi wa ndani ni kumpeleka hospitali na haraka sana kitu hicho kufanyika.
Ofisini hakukukalika tena, alichokifanya ni kuondoka na kwenda katika Hospitali ya St. Paul Medical Care ambapo huko akamkuta Aisha akiwa kitandani.
Muda mwingi alikuwa akilia kwa maumivu makali, Mike akamuuliza juu ya tatizo alilokuwa nalo lakini mwanamke huyo hakujibu chochote kile zaidi ya kuonyesha dalili zote kwamba alikuwa akisikia maumivu mno.
Madaktari waliingia kwa zamu, walimtibu na mwisho wa siku kumwambia tatizo alilokuwa nalo, lilikuwa ni miscarriage, yaani kutoka kwa mimba. Pasipo kujua, kumbe Aisha alikuwa na mimba ila kwa bahati mbaya kabisa, mimba hiyo ilikuwa imeharibika kabisa.
“Unasemaje?” aliuliza Mike.
“Mkeo alikuwa na mimba, ila imeharibika,” alijibu daktari.
Mike akaumia moyoni mwake, hakuamini alichokisikia, alibaki akimwangalia daktari yule mara mbilimbili, alihisi kama alikuwa ndotoni. Alihitaji sana mtoto wa pili lakini tatizo lililotokea, lilikiumiza sana kichwa chake.
“Haiwezekani...”
“Ndiyo hivyo!”
****
Mike alitakiwa kukubaliana na matokeo kwamba mchumba wake alikuwa na mimba na bahati mbaya iliharibika na kutoka, moyo wake ulimuuma sana kwani hakukuwa na kitu alichokuwa akikihitaji katika kipindi hicho kama kumuona mchumba wake akizaa tena.
Alibaki kwenye kiti huku akihuzunika, alishindwa kabisa kuyazuia machozi yake akajikuta akianza kulia mahali hapo. Daktari aliyemfuata na kumpa taarifa ndiye aliyekuwa akimpoza, alijua ni kwa namna gani aliumia moyoni mwake hivyo kumfariji lilikuwa jambo la msingi sana.
Baada ya dakika kadhaa, akanyamaza, akaelekea bafuni na kunawa uso wake kisha kurudi tena kule kwenye korido, akachukuliwa na kupelekwa katika chumba alicholazwa mchumba wake, alipomuona, machozi yakaanza kutiririka tena mashavuni mwake.
Akamsogelea na kuanza kumwangalia, maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake yakaongezeka maradufu, hakuamini kama ingetokea siku ambayo angekuja kuumia kama siku hiyo hasa mara baada ya kumpata msichana huyo wa maisha yake.
“Aisha mpenzi....kwa nini lakini?” alijikuta akiuliza kwa sauti ndogo huku macho yake yakiwa yametua usoni mwa mpenzi wake.
Aisha alikuwa kimya kitandani pale, Mike hakutaka kuondoka, alibaki palepale huku muda mwingi akitumia kumwangalia mpenzi wake. Hakujali kama kulikuwa na baadhi ya majukumu hayakuwa yakiendelea ofisini kwake, kilichokuwa cha muhimu kwa wakati huo kilikuwa afya ya mpenzi wake tu.
Aisha alikaa hospitalini kwa siku mbili na ndipo alipotoka na kurudishwa nyumbani. Maisha yake yalikuwa na huzuni kubwa, mara kwa mara alikuwa mtu wa kulia tu, mpenzi wake ndiye alikuwa mfariji wake mkubwa, alipolia na kuumia moyoni mwake, mwanaume huyo ndiye alikuwa mfariji wake.
Maisha yaliendelea kama kawaida, ukaribu wao haukupungua, kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo walivyoendelea kupendana kila siku. Baada ya miezi sita kupita, wakaamua kuanza tena harakati za kumtafuta mtoto wa pili.
Usiku na mchana kazi yao ilikuwa hiyohiyo lakini kila baada ya wiki mbili Aisha alipokwenda kupima hospitalini, hakukuwa na dalili zozote za mimba. Hilo liliwaumiza sana lakini hawakujali, juhudi zao ziliendelea kila siku lakini matokeo yalikuwa yaleyale kwamba Aisha hakupata mimba.
Hilo likawatisha sana, wakahisi kwamba kulikuwa na tatizo na hivyo kwenda kumuona daktari wa familia, Dk. Cassie ambaye alipomnguza Aisha kwa vipimo vyake akaonekana kuwa na tatizo.
“Kuna nini?” aliuliza Mike.
“Mkeo ana tatizo...”
“Tatizo gani?” aliuliza Mike huku akionekana kuchanganyikiwa.
Wakati daktari aliposema hivyo, moyo wa Aisha ukapiga paa, hakuamini alichokisikia, kitendo cha daktari yule kusema kwamba alikuwa na tatizo, tayari akakosa amani moyoni mwake, mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu huku wakati mwingine akitamani kutoka ndani ya chumba kile ili asimsikie daktari akitoa majibu ya vipimo vile.
“Mkeo hatoweza kuzaa tena,” alisema Dk. Cassie huku hata kwa kumwangalia tu machoni mwake, alionekana kuwaonea huruma.
“Unasemaje?”
“Tumejaribu kumpima, tumegundua kwamba viunga vyake vya uzazi vimeharibika, mkeo alishawahi kupata tatizo lolote la kiafya katika mfumo wake wa uzazi?” aliuliza Dk. Cassie.
“Ndiyo! Miezi sita iliyopita, alipata mimba ila ilitoka kwa bahati mbaya,” alijibu Mike.
“Poleni sana, hilo ndilo tatizo lililosababisha haya yote, mfumo wake wa uzazi umeharibika,” alisema daktari huku akifungua faili lake.
Kilisikika kilio kikubwa kutoka kwa Aisha, hakuamini alichokisikia, alimwangalia daktari mara mbilimbili lakini majibu yake hayakubadilika, yalikuwa yaleyale kwamba hakuwa na uwezo wa kuzaa tena.
Mike ndiye alikuwa mfariji wake, hakutaka kumuacha katika kipindi kigumu kama hicho, alimfariji, matatizo aliyokuwa akipitia, hakutakiwa kutengwa, alitakiwa kutiwa moyo na kufarijiwa kila siku.
Aisha akakosa raha, furaha aliyokuwa nayo ikapotea, mtoto wake, Monica ndiye alikuwa mfariji wake na ndiye alikuwa mtoto pekee aliyekuwa naye. Kila alipomwangalia, alijiona kuwa na kila sababu ya kumpenda kuliko kitu chochote kile.
Hakukuwa na mwingine, huyo ndiye alikuwa wake wa pekee. Siku zilikatika zaidi, kuna wakati Aisha alimwambia mumewe, Mike kwamba kama alikuwa na kiu ya kupata mtoto basi angefanya lolote, hata kutembea na msichana mwingine ili mradi apate kile alichokuwa akikitaka lakini Mike hakukubali kabisa. Kwake, Aisha alikuwa kila kitu.
“Mtoto si tatizo,” alisema Mike.
“Ila nahisi unaumia.”
“Hapana mpenzi! Siumii kabisa, kama mtoto si tunaye? Sasa kuna tatizo gani?’ aliuliza Mike huku akimwangalia mkewe usoni.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi wake, hakutaka kumsaliti mpenzi wake, alitaka kuendelea kuwa naye milele yote. Japokuwa kulikuwa na uwezekano wa kutembea na msichana yeyote kutokana na utajiri aliokuwa nao lakini hakuonekana kuwa tayari kufanya hivyo.
Wakati akiwa kwenye mawazo mengi ndipo kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma kabisa. Akakumbuka kwamba kabla ya kupata utajiri aliwahi kutoa mbegu zake ambazo daktari alimwambia kwamba zingepandikizwa katika yai la mwanamke na hatimaye kutengeneza mtoto kwani mume wa mwanamke huyo alihitaji sana mtoto.
Alipokumbuka hilo, akatoa tabasamu pana, moyo wake ulikuwa na uhakika kwamba kile alichokifanya daktari yule kilifanikiwa kwa asilimia mia moja, hivyo ilikuwa ni lazima amtafute daktari yule na kumwambia mahali alipokuwa mtoto wake.
“Ni lazima niende huko hospitali! Kama fedha ninazo, kumtunza mtoto wa damu yangu haitokuwa tatizo kabisa,” alijisemea.
Hakutaka kufanya siri, alichokifanya ni kumwambia mke wake, alimhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea, tangu alipokuwa amepigika, alipofuatwa na watu asiowafahamu na kisha kupewa fedha kwa kazi ambayo alitakiwa kuifanya.
“Kwa hiyo ukatoa?” aliuliza Aisha.
“Ndiyo! Nilitoa na hizo fedha ndizo zilibadilisha maisha yangu. Ni lazima niitafute damu yangu,” alijibu Mike.
Alidhamiria kuitafuta damu yake. Alikumbuka vilivyo kwamba kazi hiyo ya upandikizaji wa mbegu ulifanyika katika Hospitali ya Marie Stopes iliyokuwa hapo New York na daktari aliyemfanyia kazi hiyo aliitwa kwa jina la Fabian.
“Ni lazima nimtafute...” alijisemea Mike, hakutaka kuchelewa, alichokifanya, siku hiyohiyo ni kuondoka kuelekea katika hospitali hiyo.
****
Njiani, Mike alikuwa na mawazo tele, kila kitu kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kilimhuzunisha mno, aliona kabisa kwamba angepata msongo wa mawazo kwa jinsi alivyochanganyikiwa.
Mawazo yake yalikuwa kwa daktari aliyezichukua mbegu zake na kwenda kuzipandikiza katika yai la uzazi la mwanamke, hakuwa na matokeo lakini aliamini kwamba zoezi lile lilikamilika na hivyo mimba kutungwa na mtoto kuzaliwa.
Hakuchukua muda mwingi, akaegesha gari katika eneo la Hospitali ya Marie Stopes ambapo akateremka na kuanza kuelekea ndani. Jina lake lilikuwa kubwa na alijulikana kutoka na utajiri mkubwa aliokuwa nao hivyo kila alipopita, watu walibaki wakimwangalia na wengine kujipitisha karibu naye na kumsalimia.
Alichotaka muda huo ni kuonana na Dk. Fabian na kumwambia kile kilichomfanya kuwa ndani ya hospitali hiyo siku hiyo. Alikuwa na hamu ya kuambiwa kile alichokuwa akikitaka na ndiyo maana baada ya kukumbuka hilo hakutaka kupoteza muda.
Baada ya kuzungumza na nesi mmoja na kumuelekeza mahali ofisi ya daktari huyo ilipokuwa, akaamua kwenda huko. Hakukuta mtu yeyote hivyo akapiga hodi na kuingia ndani.
Sura yake haikuwa ngeni kwa Dk. Fabian, walibaki wakiangaliana tu. Dk. Fabian alimfahamu mwanaume aliyesimama mbele yake, alikuwa bilionea mkubwa lakini hakukumbuka kama mtu huyo ndiye yule ambaye alitoa mbegu zake na kisha kupandikizwa katika yai la Katty.
“Karibu sana Bwana Mike...” alimkaribisha, Mike akakaa kitini.
Kwanza wakaanza kuzungumza mambo mengine kabisa, katika stori zote, Dk. Fabian alitumia muda wake kumsifia Mike kutokana na uchapakazi aliokuwa nao mpaka kumfanya miongoni mwa mabilionea wakubwa duniani.
Katika kumwambia kile alichokuwa amekifuata mahali hapo, hakuanza moja kwa moja, alianzia mbali kabisa tangu alipokuwa msikini, alimwambia mambo mbalimbali aliyoyapitia, maisha magumu aliyokuwa nayo kabla ya kuwa bilionea mkubwa.
Dk. Fabian uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana, kila alichokuwa akiambiwa kilionekana kumfurahisha lakini baada ya Mike kuanza kuzungumzia kile kilichomleta mahali pale, Dk. Fabian akaonekana kushtuka.
“Unakumbuka lakini?” aliuliza Mike.
“Kumbe ni wewe?”
“Ndiyo! Naomba uniambie, mtoto wangu yupo wapi,” alisema Mike huku akimwangalia daktari huyo usoni.
Dk. Fabian hakujibu kitu chochote kile, alikumbuka kwamba mara ya mwisho kuzungumza na mtu huyo alimwambia wazi kwamba mbegu zile aliziuza na kila kitu kilichoendelea siku ile kilikuwa siri kubwa, sasa iweje mtu huyo aje na kumwambia kwamba alihitaji mtoto wake?
“Hapana! Unakumbuka tulichokubaliana?” aliuliza Dk. Fabian.
“Kipi?”
“Kwamba iwe siri!”
“Sawa! Itaendelea kuwa siri, kwani nimemwambia mtu?”
“Hapana! Ila zile mbegu ziliuzwa, unakumbuka?” aliuliza Dk. Fabian.
Kwanza Mike hakutaka kuzungumza kitu, alibaki akimwangalia daktari huyo, hasira zake zikaanza kuonekana waziwazi usoni mwake, alimuona daktari huyo kuwa mpumbavu mkubwa.
“Hivi zile ni mbegu za nani?” aliuliza Mike.
“Zilikuwa zako!”
“Mtoto aliyezaliwa ana vinasaba vya nani?”
“Vyako!”
“Sasa kwa nini mtoto asiwe wangu?”
“Lakini tulikubaliana!”
“Najua! Niambie ni nani mwenye mtoto wangu!” alisema Mike huku akimwangalia daktari huyo kwa macho yaliyojaa chuki.
“Hapana! Hiyo ni siri ya hospitali, na ni siri ya taaluma yangu, siwezi kufanya hivyo,” alijibu daktari huyo, macho yake tu yalionyesha kumaanisha alichokuwa akikisema.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Mike hakutaka kuzungumza kitu, kadiri alivyomwangalia daktari yule ndivyo alivyokasirika zaidi, alichokifanya ni kuinuka na kuondoka mahali hapo. Moyo wake ulikuwa na hasira kali, japokuwa ni kweli aiziuza mbegu zile kipindi cha nyuma lakini kipindi hicho aliona kama amedhulumiwa haki yake hivyo ilikuwa ni lazima aipate tena.
“Nitajua la kufanya!” alisema Mike na kuingia ndani ya gari lake, alichokifanya ni kuondoka hospitalini hapo huku moyo wake ukiwa umejaa hasira kali.
Je, nini kitaendelea?
UTAJIRI WENYE UCHUNGU
Sehemu ya Thelathini na Moja.
Maisha mapya yakaanza, Mike alionekana kuwa na furaha kupita kawaida, kila wakati alikuwa na mtoto wake, alimpenda Monica kuliko kitu chochote kile katika maisha yake.
Siku ziliendelea kukatika, hakuwa mtu wa kuwahi ofisini kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma, mara kwa mara alipokuwa akiamka, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumchukua mtoto wake kisha kumbeba.
Kazi ya kumhudumia ilikuwa juu yake, hakutaka mpenzi wake, Aisha asumbuke kwa kitu chochote kile. Kutokana na mchanganyiko wa rangi aliokuwa nao, Monica alionekana kuwa mrembo tangu kipindi hicho alichokuwa mdogo.
Marafiki wa Mike kila siku walifika nyumbanii hapo kumpongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya, kwake, ilikuwa ni furaha tele. Aisha alikuwa na afya tele, hakutaka kuwasiliana na wazazi wake, alijaribu kusahau kila kitu kilichopita nchini Kuwait na hakutaka urudi tena huko.
Mpaka mwaka wa kwanza unakatimia, Monica alikuwa na uzuri wa sura yake ulionekana kwa kiasi kikubwa. Mike alikuwa na kazi kubwa ya kumpa maisha mazuri binti yake, huyo ndiye alikuwa mtu pekee aliyemthamini.
“Nitamlinda maisha yangu yote...” alisema Mike huku akiwa amembeba Monica katika bustani ya maua.
MIAKA MITANO BAADAYE
Monica alikuwa msichana mrembo mno, kila alipokwenda, kulikuwa gumzo, alikuuwa na sura nzuri, nusu alikuwa mtu mweusi na nusu alikuwa Mzungu. Maisha yake yalikuwa ya kifahari, kila siku baba yake alikuwa na jukumu kubwa la kumfuata shuleni na kisha kumpeleka nyumbani.
Huyo ndiye alikuwa roho yake, alitamani sana kupata mtoto wa pili na walikubaliana mpaka huyo atakapofikisha umri wa miaka mitano, hivyo wakaanza kufanya jitihada za kumtafuta mtoto wa pili.
Siku moja akiwa ofisini, akapigiwa simu na kupewa taarifa kwamba mpenzi wake, Aisha alikuwa hoi, alikuwa akitokwa na damu sehemu za siri na haikujulikana tatizo lilikuwa nini.
Hakukuwa na muda wa kumsubiri daktari wa familia afike bali alichomwambia mfanyakazi wa ndani ni kumpeleka hospitali na haraka sana kitu hicho kufanyika.
Ofisini hakukukalika tena, alichokifanya ni kuondoka na kwenda katika Hospitali ya St. Paul Medical Care ambapo huko akamkuta Aisha akiwa kitandani.
Muda mwingi alikuwa akilia kwa maumivu makali, Mike akamuuliza juu ya tatizo alilokuwa nalo lakini mwanamke huyo hakujibu chochote kile zaidi ya kuonyesha dalili zote kwamba alikuwa akisikia maumivu mno.
Madaktari waliingia kwa zamu, walimtibu na mwisho wa siku kumwambia tatizo alilokuwa nalo, lilikuwa ni miscarriage, yaani kutoka kwa mimba. Pasipo kujua, kumbe Aisha alikuwa na mimba ila kwa bahati mbaya kabisa, mimba hiyo ilikuwa imeharibika kabisa.
“Unasemaje?” aliuliza Mike.
“Mkeo alikuwa na mimba, ila imeharibika,” alijibu daktari.
Mike akaumia moyoni mwake, hakuamini alichokisikia, alibaki akimwangalia daktari yule mara mbilimbili, alihisi kama alikuwa ndotoni. Alihitaji sana mtoto wa pili lakini tatizo lililotokea, lilikiumiza sana kichwa chake.
“Haiwezekani...”
“Ndiyo hivyo!”
****
Mike alitakiwa kukubaliana na matokeo kwamba mchumba wake alikuwa na mimba na bahati mbaya iliharibika na kutoka, moyo wake ulimuuma sana kwani hakukuwa na kitu alichokuwa akikihitaji katika kipindi hicho kama kumuona mchumba wake akizaa tena.
Alibaki kwenye kiti huku akihuzunika, alishindwa kabisa kuyazuia machozi yake akajikuta akianza kulia mahali hapo. Daktari aliyemfuata na kumpa taarifa ndiye aliyekuwa akimpoza, alijua ni kwa namna gani aliumia moyoni mwake hivyo kumfariji lilikuwa jambo la msingi sana.
Baada ya dakika kadhaa, akanyamaza, akaelekea bafuni na kunawa uso wake kisha kurudi tena kule kwenye korido, akachukuliwa na kupelekwa katika chumba alicholazwa mchumba wake, alipomuona, machozi yakaanza kutiririka tena mashavuni mwake.
Akamsogelea na kuanza kumwangalia, maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake yakaongezeka maradufu, hakuamini kama ingetokea siku ambayo angekuja kuumia kama siku hiyo hasa mara baada ya kumpata msichana huyo wa maisha yake.
“Aisha mpenzi....kwa nini lakini?” alijikuta akiuliza kwa sauti ndogo huku macho yake yakiwa yametua usoni mwa mpenzi wake.
Aisha alikuwa kimya kitandani pale, Mike hakutaka kuondoka, alibaki palepale huku muda mwingi akitumia kumwangalia mpenzi wake. Hakujali kama kulikuwa na baadhi ya majukumu hayakuwa yakiendelea ofisini kwake, kilichokuwa cha muhimu kwa wakati huo kilikuwa afya ya mpenzi wake tu.
Aisha alikaa hospitalini kwa siku mbili na ndipo alipotoka na kurudishwa nyumbani. Maisha yake yalikuwa na huzuni kubwa, mara kwa mara alikuwa mtu wa kulia tu, mpenzi wake ndiye alikuwa mfariji wake mkubwa, alipolia na kuumia moyoni mwake, mwanaume huyo ndiye alikuwa mfariji wake.
Maisha yaliendelea kama kawaida, ukaribu wao haukupungua, kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele na ndivyo walivyoendelea kupendana kila siku. Baada ya miezi sita kupita, wakaamua kuanza tena harakati za kumtafuta mtoto wa pili.
Usiku na mchana kazi yao ilikuwa hiyohiyo lakini kila baada ya wiki mbili Aisha alipokwenda kupima hospitalini, hakukuwa na dalili zozote za mimba. Hilo liliwaumiza sana lakini hawakujali, juhudi zao ziliendelea kila siku lakini matokeo yalikuwa yaleyale kwamba Aisha hakupata mimba.
Hilo likawatisha sana, wakahisi kwamba kulikuwa na tatizo na hivyo kwenda kumuona daktari wa familia, Dk. Cassie ambaye alipomnguza Aisha kwa vipimo vyake akaonekana kuwa na tatizo.
“Kuna nini?” aliuliza Mike.
“Mkeo ana tatizo...”
“Tatizo gani?” aliuliza Mike huku akionekana kuchanganyikiwa.
Wakati daktari aliposema hivyo, moyo wa Aisha ukapiga paa, hakuamini alichokisikia, kitendo cha daktari yule kusema kwamba alikuwa na tatizo, tayari akakosa amani moyoni mwake, mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu huku wakati mwingine akitamani kutoka ndani ya chumba kile ili asimsikie daktari akitoa majibu ya vipimo vile.
“Mkeo hatoweza kuzaa tena,” alisema Dk. Cassie huku hata kwa kumwangalia tu machoni mwake, alionekana kuwaonea huruma.
“Unasemaje?”
“Tumejaribu kumpima, tumegundua kwamba viunga vyake vya uzazi vimeharibika, mkeo alishawahi kupata tatizo lolote la kiafya katika mfumo wake wa uzazi?” aliuliza Dk. Cassie.
“Ndiyo! Miezi sita iliyopita, alipata mimba ila ilitoka kwa bahati mbaya,” alijibu Mike.
“Poleni sana, hilo ndilo tatizo lililosababisha haya yote, mfumo wake wa uzazi umeharibika,” alisema daktari huku akifungua faili lake.
Kilisikika kilio kikubwa kutoka kwa Aisha, hakuamini alichokisikia, alimwangalia daktari mara mbilimbili lakini majibu yake hayakubadilika, yalikuwa yaleyale kwamba hakuwa na uwezo wa kuzaa tena.
Mike ndiye alikuwa mfariji wake, hakutaka kumuacha katika kipindi kigumu kama hicho, alimfariji, matatizo aliyokuwa akipitia, hakutakiwa kutengwa, alitakiwa kutiwa moyo na kufarijiwa kila siku.
Aisha akakosa raha, furaha aliyokuwa nayo ikapotea, mtoto wake, Monica ndiye alikuwa mfariji wake na ndiye alikuwa mtoto pekee aliyekuwa naye. Kila alipomwangalia, alijiona kuwa na kila sababu ya kumpenda kuliko kitu chochote kile.
Hakukuwa na mwingine, huyo ndiye alikuwa wake wa pekee. Siku zilikatika zaidi, kuna wakati Aisha alimwambia mumewe, Mike kwamba kama alikuwa na kiu ya kupata mtoto basi angefanya lolote, hata kutembea na msichana mwingine ili mradi apate kile alichokuwa akikitaka lakini Mike hakukubali kabisa. Kwake, Aisha alikuwa kila kitu.
“Mtoto si tatizo,” alisema Mike.
“Ila nahisi unaumia.”
“Hapana mpenzi! Siumii kabisa, kama mtoto si tunaye? Sasa kuna tatizo gani?’ aliuliza Mike huku akimwangalia mkewe usoni.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi wake, hakutaka kumsaliti mpenzi wake, alitaka kuendelea kuwa naye milele yote. Japokuwa kulikuwa na uwezekano wa kutembea na msichana yeyote kutokana na utajiri aliokuwa nao lakini hakuonekana kuwa tayari kufanya hivyo.
Wakati akiwa kwenye mawazo mengi ndipo kumbukumbu zake zikaanza kurudi nyuma kabisa. Akakumbuka kwamba kabla ya kupata utajiri aliwahi kutoa mbegu zake ambazo daktari alimwambia kwamba zingepandikizwa katika yai la mwanamke na hatimaye kutengeneza mtoto kwani mume wa mwanamke huyo alihitaji sana mtoto.
Alipokumbuka hilo, akatoa tabasamu pana, moyo wake ulikuwa na uhakika kwamba kile alichokifanya daktari yule kilifanikiwa kwa asilimia mia moja, hivyo ilikuwa ni lazima amtafute daktari yule na kumwambia mahali alipokuwa mtoto wake.
“Ni lazima niende huko hospitali! Kama fedha ninazo, kumtunza mtoto wa damu yangu haitokuwa tatizo kabisa,” alijisemea.
Hakutaka kufanya siri, alichokifanya ni kumwambia mke wake, alimhadithia kila kitu kilichokuwa kimetokea, tangu alipokuwa amepigika, alipofuatwa na watu asiowafahamu na kisha kupewa fedha kwa kazi ambayo alitakiwa kuifanya.
“Kwa hiyo ukatoa?” aliuliza Aisha.
“Ndiyo! Nilitoa na hizo fedha ndizo zilibadilisha maisha yangu. Ni lazima niitafute damu yangu,” alijibu Mike.
Alidhamiria kuitafuta damu yake. Alikumbuka vilivyo kwamba kazi hiyo ya upandikizaji wa mbegu ulifanyika katika Hospitali ya Marie Stopes iliyokuwa hapo New York na daktari aliyemfanyia kazi hiyo aliitwa kwa jina la Fabian.
“Ni lazima nimtafute...” alijisemea Mike, hakutaka kuchelewa, alichokifanya, siku hiyohiyo ni kuondoka kuelekea katika hospitali hiyo.
****
Njiani, Mike alikuwa na mawazo tele, kila kitu kilichokuwa kikitokea katika maisha yake kilimhuzunisha mno, aliona kabisa kwamba angepata msongo wa mawazo kwa jinsi alivyochanganyikiwa.
Mawazo yake yalikuwa kwa daktari aliyezichukua mbegu zake na kwenda kuzipandikiza katika yai la uzazi la mwanamke, hakuwa na matokeo lakini aliamini kwamba zoezi lile lilikamilika na hivyo mimba kutungwa na mtoto kuzaliwa.
Hakuchukua muda mwingi, akaegesha gari katika eneo la Hospitali ya Marie Stopes ambapo akateremka na kuanza kuelekea ndani. Jina lake lilikuwa kubwa na alijulikana kutoka na utajiri mkubwa aliokuwa nao hivyo kila alipopita, watu walibaki wakimwangalia na wengine kujipitisha karibu naye na kumsalimia.
Alichotaka muda huo ni kuonana na Dk. Fabian na kumwambia kile kilichomfanya kuwa ndani ya hospitali hiyo siku hiyo. Alikuwa na hamu ya kuambiwa kile alichokuwa akikitaka na ndiyo maana baada ya kukumbuka hilo hakutaka kupoteza muda.
Baada ya kuzungumza na nesi mmoja na kumuelekeza mahali ofisi ya daktari huyo ilipokuwa, akaamua kwenda huko. Hakukuta mtu yeyote hivyo akapiga hodi na kuingia ndani.
Sura yake haikuwa ngeni kwa Dk. Fabian, walibaki wakiangaliana tu. Dk. Fabian alimfahamu mwanaume aliyesimama mbele yake, alikuwa bilionea mkubwa lakini hakukumbuka kama mtu huyo ndiye yule ambaye alitoa mbegu zake na kisha kupandikizwa katika yai la Katty.
“Karibu sana Bwana Mike...” alimkaribisha, Mike akakaa kitini.
Kwanza wakaanza kuzungumza mambo mengine kabisa, katika stori zote, Dk. Fabian alitumia muda wake kumsifia Mike kutokana na uchapakazi aliokuwa nao mpaka kumfanya miongoni mwa mabilionea wakubwa duniani.
Katika kumwambia kile alichokuwa amekifuata mahali hapo, hakuanza moja kwa moja, alianzia mbali kabisa tangu alipokuwa msikini, alimwambia mambo mbalimbali aliyoyapitia, maisha magumu aliyokuwa nayo kabla ya kuwa bilionea mkubwa.
Dk. Fabian uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana, kila alichokuwa akiambiwa kilionekana kumfurahisha lakini baada ya Mike kuanza kuzungumzia kile kilichomleta mahali pale, Dk. Fabian akaonekana kushtuka.
“Unakumbuka lakini?” aliuliza Mike.
“Kumbe ni wewe?”
“Ndiyo! Naomba uniambie, mtoto wangu yupo wapi,” alisema Mike huku akimwangalia daktari huyo usoni.
Dk. Fabian hakujibu kitu chochote kile, alikumbuka kwamba mara ya mwisho kuzungumza na mtu huyo alimwambia wazi kwamba mbegu zile aliziuza na kila kitu kilichoendelea siku ile kilikuwa siri kubwa, sasa iweje mtu huyo aje na kumwambia kwamba alihitaji mtoto wake?
“Hapana! Unakumbuka tulichokubaliana?” aliuliza Dk. Fabian.
“Kipi?”
“Kwamba iwe siri!”
“Sawa! Itaendelea kuwa siri, kwani nimemwambia mtu?”
“Hapana! Ila zile mbegu ziliuzwa, unakumbuka?” aliuliza Dk. Fabian.
Kwanza Mike hakutaka kuzungumza kitu, alibaki akimwangalia daktari huyo, hasira zake zikaanza kuonekana waziwazi usoni mwake, alimuona daktari huyo kuwa mpumbavu mkubwa.
“Hivi zile ni mbegu za nani?” aliuliza Mike.
“Zilikuwa zako!”
“Mtoto aliyezaliwa ana vinasaba vya nani?”
“Vyako!”
“Sasa kwa nini mtoto asiwe wangu?”
“Lakini tulikubaliana!”
“Najua! Niambie ni nani mwenye mtoto wangu!” alisema Mike huku akimwangalia daktari huyo kwa macho yaliyojaa chuki.
“Hapana! Hiyo ni siri ya hospitali, na ni siri ya taaluma yangu, siwezi kufanya hivyo,” alijibu daktari huyo, macho yake tu yalionyesha kumaanisha alichokuwa akikisema.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
Mike hakutaka kuzungumza kitu, kadiri alivyomwangalia daktari yule ndivyo alivyokasirika zaidi, alichokifanya ni kuinuka na kuondoka mahali hapo. Moyo wake ulikuwa na hasira kali, japokuwa ni kweli aiziuza mbegu zile kipindi cha nyuma lakini kipindi hicho aliona kama amedhulumiwa haki yake hivyo ilikuwa ni lazima aipate tena.
“Nitajua la kufanya!” alisema Mike na kuingia ndani ya gari lake, alichokifanya ni kuondoka hospitalini hapo huku moyo wake ukiwa umejaa hasira kali.
Je, nini kitaendelea?




