Utajiri wenye uchungu

Utajiri wenye uchungu

NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Mbili.

Dk. Fabian hakuwa na raha kabisa, muda wote alikuwa na mawazo tele, ujio wa Mike ndani ya hospitali ile ulimchanganya mno, hakuelewa ni kitu gani alitakiwa kufanya, hakujua kama alitakiwa kumwambia Dylan juu ya kilichokuwa kimetokea au alitakiwa kukaa kimya.

Alijifikiria, kichwa chake kilisumbuka sana, alijiuliza lipi lilikuwa sahihi lakini mwisho wa siku aliona ni bora kumwambia Dylan ukweli kwamba yule mtu ambaye alimuuzia mbegu, alifika ofisini kwake na kudai watoto wake.

“Ila wote si mabilionea! Watajuana wenyewe,” alisema Dk. Fabian na kisha kuchukua simu yake na kumpigia Dylan.

Simu ilipokelewa na sauti ya Dylan kuanza kusikika kutoka upande wa pili. Iliita na Dk. Fabian kuitikia. Walizungumza kidogo na alipotaka kumgusia kuhusu kile kilichokuwa kimetokea, alisita kufanya hivyo na mpaka anakata simu, hakuwa amemwambia lolote lile.

Moyo wake ulikuwa mzito sana, alijiona kuwa kwenye wakati mgumu mno. Alijitahidi kujisahaulisha lakini ilishindikana kabisa. Hakutaka kuendelea kukaa hospitalini hapo, akaondoka zake na kurudi nyumbani.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya wiki moja, akampigia simu mkewe na kumwambia kwamba alichukua likizo hivyo wangeondoka na kuelekea katika Visiwa vya Hawaii kwa ajili ya kula bata tu.

Safari hiyo ikapangwa ifanyike baada ya siku mbili, mkewe akajiandaa vilivyo kumsubiri mumewe ili wazungumze vizuri juu ya safari hiyo kwani naye alitamani kuwa na mumewe, waende sehemu, wakae huko kwa siku kadhaa kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya kitu hicho.

“Nakuja tupange,” alisema Dk. Fabian na kukata simu.

Hakutaka kubaki ofisini, kwa sababu muda wa kuondoka ulikuwa umefika, akatoka ofisini kwake, akachukua begi lake na kisha kutoka. Akaelekea sehemu ya kuegesha magari na kisha kulifuata gari lake huku tayari ikiwa imetimia saa mbili usiku.

Wakati amefungua gari lake na kutaka kuingia ndani, watu watatu waliovalia mavazi ya kidaktari, yaani mavazi marefu meupe wakamsogelea kule alipokuwa. Alibaki akiwaangalia, aliwafahamu madaktari wote wa hospitali hiyo lakini wale hawakuwa madaktari wa hapo kabisa.

“Nyie ni wakina na...” aliuliza lakini hata kabla hajamaliza kuuliza swali lake, akajikuta akionyeshea bastola ndogo aina ta Revolver na kutakiwa kunyamaza, vinginevyo angekufa.

“Shiiiiiii...” alitoa sauti hiyo mwanaume mmoja.

Walichokifanya ni kuingia naye ndani ya gari hilo na kuanza kuondoka naye huku wakimwambia akae katika kiti kingine. Gari likaendeshwa kwa mwendo wa kawaida tu, lilipita katika barabara kubwa ya St. George na baada ya dakika ishirini likaanza kuingia katika gereji moja kubwa ambapo ndani kulikuwa na wanaume wenye miili iliyojazia kama kumi na mbili, mikononi walishika spana na vifaa vingine vya kutengenezea magari. Aliposhushwa tu, wanaume wote hao wakamuonyeshea sura zilizokuwa na tabasamu pana.

“Karibu sana katika dunia yetu....ngoja nikwambie kwa kifupi tu, ukiwa humu, utasema tu tunachokihitaji kukijua, unaweza kusema kwamba hausemi, ila mwisho wa siku, unajikuta ukiwa umesema,” alisema mwanaume mmoja na kisha kumchukua, wakamuweka kwenye kiti, wakachukua bomba kubwa la kuchomelea magari, jamaa akafyatua kitufe, moto wa gesi ukatoa na kuanza kumsogelea Dk. Fabian katika kiti kile alichokuwa.

“Utakuwa tayari kutuambia tunachotaka kukijua?” aliuliza mwanaume mmoja. Dk. Fabian jasho lilimtoka.

“Ndiyo...ndiyo nitawaambia...” alisema huku akitetemeka mno.

“Sawa. Tulia tuanze kukuuliza maswali yetu,” alisema mwanaume huyo na kuuzima moto ule. Akavuta kiti na kutulia mbele ya Dk. Fabian.

Watu waliokuwa mbele yake hawakuonekana kuwa na masihara hata kidogo, walikuwa wazee wa kazi ambao mara wanapokuwa na uhitaji wa kufahamu kitu fulani kutoka kwako, ilikuwa ni lazima uwape ushirikiano kwani bila kufanya hivyo, hawakuwa na huruma hata kidogo.

Jamaa aliyekaa mbele yake, alikaa kitini huku akimwangalia Dk. Fabian, macho yake tu yalionyesha ni kwa kiasi gani hakuwa na maihara mahali hapo, alimwambia mapema sana kwamba alitaka kuambiwa kila kitu alichotaka kuambiwa kwani pasipo kupata alichokihitaji, ule moto wa gesi ungeishi mwilini mwake.

“Nani alipewa mtoto?” aliuliza mwanaume huyo.

“Mtoto gani?” aliuliza Dk. Fabian, hapohapo mwanaume yule akauwasha moto wa gesi, kwake, swali hilo lilikuwa kama dharau.

“Samahani Bwana mkubwa, sijajua unamzungumzia mtoto yupi,” alisema Dk. Fabian, kwani alijua kwa jinsi moto ulivyowashwa, ungeishia mwilini mwake.

“Nazungumzia zile mbegu za kiume ulizokuwa umepandikiza, mtoto alikwenda kwa nani?” aliuliza mwanaume huyo.

Hapo ndipo Dk. Fabian alipopata jibu juu ya watu wale, walikuwa wanaume ambao walitumwa na Mike Wamteka na awaambie mahali mtoto wake alipokuwa. Alikumbuka vilivyo, hakuwa na mtoto mmoja kama alivyohisi bali mbegu zake zilifanikiwa kuleta watoto wawili.

“Kumbe Mike ndiye ananifanyia hivi?” aliuliza Dk. Fabian.

“Sikiliza, una dakika chache sana za kutuambia mahali mtoto alipo, vinginevyo, utaacha mwili wako hapahapa,” alisema mwanaume yule.

Hakukuwa na utani, si huyo mwanaume aliyekaa mbele yake tu alionekana kuwa siriazi, hata wanaume wengine waliokuwa mahali hapo nao walionekana hivyohivyo kwamba hawakuwa na utani hata chembe.

Walitaka kujibiwa maswali yao, hawakutaka maelezo makubwa ambayo waliamini yasingewasaidia kwa chochote kile. Dk. Fabian akanyamaza, akaanza kuwaza kama lilikuwa jambo sahihi kuwaambia wanaume hao kila kitu, ila alivyoona jinsi hali mbaya iliyokuwa ikiendelea ndani ya gereji ile, hakuwa na jinsi.

“Ni kweli upandikizaji wa mbegu ulikamilika...” alisema Dk. Fabian.

“Baada ya hapo?”
“Mwanamke akajifungua...”
“Mwanamke yupi?”
“Mke wa Bwana Dylan..”
“Huyu bilionea?”

“Ndiyo!”

“Unamaanisha wale watoto wake mapacha, au siyo?”
“Ndiyo haohao.”

Hicho ndicho walichotaka kufahamu. Walichokifanya ni kumpigia simu Mike na kumwambia kila kitu walichoambiwa na daktari yule, walimueleza kwamba upandikizaji wa mbegu zile ulifanikiwa na matokeo yake kulikuwa na watoto mapacha, walipomwambia kwamba mtu aliyewekewa mbegu zile alikuwa mke wa Bwana Dylan, hata naye akashtuka.

“Unasemaje?”

“Hayo ndiyo maelezo tuuliyopewa.”

“Sawa! Endeleeni kumshikilia, ninakuta tupange mipango!”

Simu zikakatwa, upande wa pili, Mike alikuwa na mawazo tele, hakuamini kama kweli watoto wa Bwana Dylan ndiyo walikuwa watoto wake. Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kufungua laptop yake, akaunganisha na tovuti ya Google na kisha kuandika ‘Bilionaire Dylan’s Family’. Hapohapo picha za Bwana Dylan na familia yake zikaanza kuonekana kwenye laptop yake.

Aliwaangalia vizuri watoto mapacha aliokuwa nao, kwa mbali walionekana kufanana naye kwa kila kitu, alibaki akishangaa, upandikizaji ule ulimfanya kupata watoto wawili mapacha, hakukuwa na kitu kingine alichokitaka kwa wakati huo zaidi ya watoto wake tu.

Akawasiliana na vijana walewale waliomteka Dk. Fabian na kuwapa kazi nyingine kwamba alitaka kuwaona watoto wake ambao walikuwa wakubwa na walikuwa wakisoma shule ya msingi kipindi hicho.

Hilo halikuwa tatizo, vijana hao walikuwa tayari mua wowote ule hivyo wakahakikisha kwamba kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa kwenda.

Wakaanza kuwafuatilia, kila siku ilikuwa ni lazima kuwafuatilia shuleni, kitu ambacho kiliwapa wakati mgumu ni kwamba watoto hao walikuwa wakipelekwa na kurudishwa shuleni na baba yao ambaye bila shaka alikuwa na bastola.

Hawakutaka kukata tamaa, walimwambia wazi Mike kwamba kazi ilikuwa kubwa sana kwani walihisi kwamba bilionea huyo alikuwa na bastola kitu ambacho kingeweza kuhatarisha maisha yao, pia hawakutaka kufanya hivyo kwani kama angeanza kurushiana nao risasi, ingewezekana kabisa kukosea na hivyo kuwapiga watoto hao.

Hoja zao zikaeleweka kwa Mike lakini akawataka waendelee kufuatilia zaidi pasipo kumuachia huru Dk. Fabian kwani walijua kwamba kama wangemuachia huru basi angekwenda kusema kila kitu kilichokuwa kimetokea.

Baada ya wiki moja tangu walipoanza kufuatilia ndipo wakafanikiwa kugundua kwamba siku hiyo watoto walipokuwa wakipelekwa shuleni, hawakuwa wakiendeshwa na baba yao bali alikuwepo dereva.

Hiyo ikawafurahisha, walichokifanya ni kuvuta subira kwa kuona kwamba pia ua ilikuwa ni lazima wakamilishe mpango wao wakati wa kutoka shuleni, hivyo wakavumilia.

Pembeni ya shule waliyokuwa wakisoma Patrick na Patricia kulikuwa na mgahawa wa McDonald hivyo wakaelekea hapo na kuanza kunywa kahawa huku macho yao yakiwa katika geti la shule hiyo kubwa.

Nje, katika sehemu ya kuegeshea magari waliweza kuliona gari la Bwana Dylan likianza kuingia mahali hapo, wakaangalia ndani, hakuwepo zaidi ya dereva tu aliyefika mahali hapo kwa ajili ya kuwachukua.

Hawakutaka kuchelewa, nao wakatoka katika mgahawa ule na moja kwa moja kuanza kulifuata. Bastola zilikuwa mikoni mwao, siku hiyo ilikuwa ni lazima wakamilishe kile walichokuwa wakikihitaji, wawateke watoto hao na kisha kuondoka nao.
Walipolifikia gari hilo, jamaa mmoja akakifuata kioo na kuanza kukigonga huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana ambalo lilimfanya dereva kutokugundua kama mtu huyo alikuwa mbaya, tena alikuwa na wenzake waliojificha. Akashusha kioo.

“Nikusaidie nini kaka?” aliuliza dereva huku akimwangalia mtu huyo.

“Hakuna chochote, ninataka tu utulie hivyohivyo!”
“Kwa nini?”

Mwanaume huyo hakuzungumza kitu kingine chochote kile zaidi ya kutoa bastola yake na kumnyooshea dereva huyo ambaye akaanza kuogopa kwani tangu azaliwe, hakuwahi kuonyeshewa bastola hata mara moja.

“Kaka, gari siyo yangu! Ni ya bosi wangu,” alijitetea.

“Hatuhitaji gari...”
“Hamuhitaji?”

Hapohapo wenzake wakajitokeza, wote walikuwa na bunduki, wakafungua milango na kuingia ndani huku wakimtaka dereva huyo atulie hivyohivyo na hata watoto hao watakapokuja, awatambulishe kwamba wao walikuwa marafiki zake. Dereva akatii kwani pasipo kufanya hivyo, aliamini angeweza kuuawa.

Je, nini kitafuata?
Tukutane sehemu ijayo.
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Mbili.

Dk. Fabian hakuwa na raha kabisa, muda wote alikuwa na mawazo tele, ujio wa Mike ndani ya hospitali ile ulimchanganya mno, hakuelewa ni kitu gani alitakiwa kufanya, hakujua kama alitakiwa kumwambia Dylan juu ya kilichokuwa kimetokea au alitakiwa kukaa kimya.

Alijifikiria, kichwa chake kilisumbuka sana, alijiuliza lipi lilikuwa sahihi lakini mwisho wa siku aliona ni bora kumwambia Dylan ukweli kwamba yule mtu ambaye alimuuzia mbegu, alifika ofisini kwake na kudai watoto wake.

“Ila wote si mabilionea! Watajuana wenyewe,” alisema Dk. Fabian na kisha kuchukua simu yake na kumpigia Dylan.

Simu ilipokelewa na sauti ya Dylan kuanza kusikika kutoka upande wa pili. Iliita na Dk. Fabian kuitikia. Walizungumza kidogo na alipotaka kumgusia kuhusu kile kilichokuwa kimetokea, alisita kufanya hivyo na mpaka anakata simu, hakuwa amemwambia lolote lile.

Moyo wake ulikuwa mzito sana, alijiona kuwa kwenye wakati mgumu mno. Alijitahidi kujisahaulisha lakini ilishindikana kabisa. Hakutaka kuendelea kukaa hospitalini hapo, akaondoka zake na kurudi nyumbani.
Siku zikaendelea kukatika, baada ya wiki moja, akampigia simu mkewe na kumwambia kwamba alichukua likizo hivyo wangeondoka na kuelekea katika Visiwa vya Hawaii kwa ajili ya kula bata tu.

Safari hiyo ikapangwa ifanyike baada ya siku mbili, mkewe akajiandaa vilivyo kumsubiri mumewe ili wazungumze vizuri juu ya safari hiyo kwani naye alitamani kuwa na mumewe, waende sehemu, wakae huko kwa siku kadhaa kwani ni muda mrefu ulikuwa umepita pasipo kufanya kitu hicho.

“Nakuja tupange,” alisema Dk. Fabian na kukata simu.

Hakutaka kubaki ofisini, kwa sababu muda wa kuondoka ulikuwa umefika, akatoka ofisini kwake, akachukua begi lake na kisha kutoka. Akaelekea sehemu ya kuegesha magari na kisha kulifuata gari lake huku tayari ikiwa imetimia saa mbili usiku.

Wakati amefungua gari lake na kutaka kuingia ndani, watu watatu waliovalia mavazi ya kidaktari, yaani mavazi marefu meupe wakamsogelea kule alipokuwa. Alibaki akiwaangalia, aliwafahamu madaktari wote wa hospitali hiyo lakini wale hawakuwa madaktari wa hapo kabisa.

“Nyie ni wakina na...” aliuliza lakini hata kabla hajamaliza kuuliza swali lake, akajikuta akionyeshea bastola ndogo aina ta Revolver na kutakiwa kunyamaza, vinginevyo angekufa.

“Shiiiiiii...” alitoa sauti hiyo mwanaume mmoja.

Walichokifanya ni kuingia naye ndani ya gari hilo na kuanza kuondoka naye huku wakimwambia akae katika kiti kingine. Gari likaendeshwa kwa mwendo wa kawaida tu, lilipita katika barabara kubwa ya St. George na baada ya dakika ishirini likaanza kuingia katika gereji moja kubwa ambapo ndani kulikuwa na wanaume wenye miili iliyojazia kama kumi na mbili, mikononi walishika spana na vifaa vingine vya kutengenezea magari. Aliposhushwa tu, wanaume wote hao wakamuonyeshea sura zilizokuwa na tabasamu pana.

“Karibu sana katika dunia yetu....ngoja nikwambie kwa kifupi tu, ukiwa humu, utasema tu tunachokihitaji kukijua, unaweza kusema kwamba hausemi, ila mwisho wa siku, unajikuta ukiwa umesema,” alisema mwanaume mmoja na kisha kumchukua, wakamuweka kwenye kiti, wakachukua bomba kubwa la kuchomelea magari, jamaa akafyatua kitufe, moto wa gesi ukatoa na kuanza kumsogelea Dk. Fabian katika kiti kile alichokuwa.

“Utakuwa tayari kutuambia tunachotaka kukijua?” aliuliza mwanaume mmoja. Dk. Fabian jasho lilimtoka.

“Ndiyo...ndiyo nitawaambia...” alisema huku akitetemeka mno.

“Sawa. Tulia tuanze kukuuliza maswali yetu,” alisema mwanaume huyo na kuuzima moto ule. Akavuta kiti na kutulia mbele ya Dk. Fabian.

Watu waliokuwa mbele yake hawakuonekana kuwa na masihara hata kidogo, walikuwa wazee wa kazi ambao mara wanapokuwa na uhitaji wa kufahamu kitu fulani kutoka kwako, ilikuwa ni lazima uwape ushirikiano kwani bila kufanya hivyo, hawakuwa na huruma hata kidogo.

Jamaa aliyekaa mbele yake, alikaa kitini huku akimwangalia Dk. Fabian, macho yake tu yalionyesha ni kwa kiasi gani hakuwa na maihara mahali hapo, alimwambia mapema sana kwamba alitaka kuambiwa kila kitu alichotaka kuambiwa kwani pasipo kupata alichokihitaji, ule moto wa gesi ungeishi mwilini mwake.

“Nani alipewa mtoto?” aliuliza mwanaume huyo.

“Mtoto gani?” aliuliza Dk. Fabian, hapohapo mwanaume yule akauwasha moto wa gesi, kwake, swali hilo lilikuwa kama dharau.

“Samahani Bwana mkubwa, sijajua unamzungumzia mtoto yupi,” alisema Dk. Fabian, kwani alijua kwa jinsi moto ulivyowashwa, ungeishia mwilini mwake.

“Nazungumzia zile mbegu za kiume ulizokuwa umepandikiza, mtoto alikwenda kwa nani?” aliuliza mwanaume huyo.

Hapo ndipo Dk. Fabian alipopata jibu juu ya watu wale, walikuwa wanaume ambao walitumwa na Mike Wamteka na awaambie mahali mtoto wake alipokuwa. Alikumbuka vilivyo, hakuwa na mtoto mmoja kama alivyohisi bali mbegu zake zilifanikiwa kuleta watoto wawili.

“Kumbe Mike ndiye ananifanyia hivi?” aliuliza Dk. Fabian.

“Sikiliza, una dakika chache sana za kutuambia mahali mtoto alipo, vinginevyo, utaacha mwili wako hapahapa,” alisema mwanaume yule.

Hakukuwa na utani, si huyo mwanaume aliyekaa mbele yake tu alionekana kuwa siriazi, hata wanaume wengine waliokuwa mahali hapo nao walionekana hivyohivyo kwamba hawakuwa na utani hata chembe.

Walitaka kujibiwa maswali yao, hawakutaka maelezo makubwa ambayo waliamini yasingewasaidia kwa chochote kile. Dk. Fabian akanyamaza, akaanza kuwaza kama lilikuwa jambo sahihi kuwaambia wanaume hao kila kitu, ila alivyoona jinsi hali mbaya iliyokuwa ikiendelea ndani ya gereji ile, hakuwa na jinsi.

“Ni kweli upandikizaji wa mbegu ulikamilika...” alisema Dk. Fabian.

“Baada ya hapo?”
“Mwanamke akajifungua...”
“Mwanamke yupi?”
“Mke wa Bwana Dylan..”
“Huyu bilionea?”

“Ndiyo!”

“Unamaanisha wale watoto wake mapacha, au siyo?”
“Ndiyo haohao.”

Hicho ndicho walichotaka kufahamu. Walichokifanya ni kumpigia simu Mike na kumwambia kila kitu walichoambiwa na daktari yule, walimueleza kwamba upandikizaji wa mbegu zile ulifanikiwa na matokeo yake kulikuwa na watoto mapacha, walipomwambia kwamba mtu aliyewekewa mbegu zile alikuwa mke wa Bwana Dylan, hata naye akashtuka.

“Unasemaje?”

“Hayo ndiyo maelezo tuuliyopewa.”

“Sawa! Endeleeni kumshikilia, ninakuta tupange mipango!”

Simu zikakatwa, upande wa pili, Mike alikuwa na mawazo tele, hakuamini kama kweli watoto wa Bwana Dylan ndiyo walikuwa watoto wake. Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kufungua laptop yake, akaunganisha na tovuti ya Google na kisha kuandika ‘Bilionaire Dylan’s Family’. Hapohapo picha za Bwana Dylan na familia yake zikaanza kuonekana kwenye laptop yake.

Aliwaangalia vizuri watoto mapacha aliokuwa nao, kwa mbali walionekana kufanana naye kwa kila kitu, alibaki akishangaa, upandikizaji ule ulimfanya kupata watoto wawili mapacha, hakukuwa na kitu kingine alichokitaka kwa wakati huo zaidi ya watoto wake tu.

Akawasiliana na vijana walewale waliomteka Dk. Fabian na kuwapa kazi nyingine kwamba alitaka kuwaona watoto wake ambao walikuwa wakubwa na walikuwa wakisoma shule ya msingi kipindi hicho.

Hilo halikuwa tatizo, vijana hao walikuwa tayari mua wowote ule hivyo wakahakikisha kwamba kila kitu kinakwenda kama kinavyotakiwa kwenda.

Wakaanza kuwafuatilia, kila siku ilikuwa ni lazima kuwafuatilia shuleni, kitu ambacho kiliwapa wakati mgumu ni kwamba watoto hao walikuwa wakipelekwa na kurudishwa shuleni na baba yao ambaye bila shaka alikuwa na bastola.

Hawakutaka kukata tamaa, walimwambia wazi Mike kwamba kazi ilikuwa kubwa sana kwani walihisi kwamba bilionea huyo alikuwa na bastola kitu ambacho kingeweza kuhatarisha maisha yao, pia hawakutaka kufanya hivyo kwani kama angeanza kurushiana nao risasi, ingewezekana kabisa kukosea na hivyo kuwapiga watoto hao.

Hoja zao zikaeleweka kwa Mike lakini akawataka waendelee kufuatilia zaidi pasipo kumuachia huru Dk. Fabian kwani walijua kwamba kama wangemuachia huru basi angekwenda kusema kila kitu kilichokuwa kimetokea.

Baada ya wiki moja tangu walipoanza kufuatilia ndipo wakafanikiwa kugundua kwamba siku hiyo watoto walipokuwa wakipelekwa shuleni, hawakuwa wakiendeshwa na baba yao bali alikuwepo dereva.

Hiyo ikawafurahisha, walichokifanya ni kuvuta subira kwa kuona kwamba pia ua ilikuwa ni lazima wakamilishe mpango wao wakati wa kutoka shuleni, hivyo wakavumilia.

Pembeni ya shule waliyokuwa wakisoma Patrick na Patricia kulikuwa na mgahawa wa McDonald hivyo wakaelekea hapo na kuanza kunywa kahawa huku macho yao yakiwa katika geti la shule hiyo kubwa.

Nje, katika sehemu ya kuegeshea magari waliweza kuliona gari la Bwana Dylan likianza kuingia mahali hapo, wakaangalia ndani, hakuwepo zaidi ya dereva tu aliyefika mahali hapo kwa ajili ya kuwachukua.

Hawakutaka kuchelewa, nao wakatoka katika mgahawa ule na moja kwa moja kuanza kulifuata. Bastola zilikuwa mikoni mwao, siku hiyo ilikuwa ni lazima wakamilishe kile walichokuwa wakikihitaji, wawateke watoto hao na kisha kuondoka nao.
Walipolifikia gari hilo, jamaa mmoja akakifuata kioo na kuanza kukigonga huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana ambalo lilimfanya dereva kutokugundua kama mtu huyo alikuwa mbaya, tena alikuwa na wenzake waliojificha. Akashusha kioo.

“Nikusaidie nini kaka?” aliuliza dereva huku akimwangalia mtu huyo.

“Hakuna chochote, ninataka tu utulie hivyohivyo!”
“Kwa nini?”

Mwanaume huyo hakuzungumza kitu kingine chochote kile zaidi ya kutoa bastola yake na kumnyooshea dereva huyo ambaye akaanza kuogopa kwani tangu azaliwe, hakuwahi kuonyeshewa bastola hata mara moja.

“Kaka, gari siyo yangu! Ni ya bosi wangu,” alijitetea.

“Hatuhitaji gari...”
“Hamuhitaji?”

Hapohapo wenzake wakajitokeza, wote walikuwa na bunduki, wakafungua milango na kuingia ndani huku wakimtaka dereva huyo atulie hivyohivyo na hata watoto hao watakapokuja, awatambulishe kwamba wao walikuwa marafiki zake. Dereva akatii kwani pasipo kufanya hivyo, aliamini angeweza kuuawa.

Je, nini kitafuata?
Tukutane sehemu ijayo.
Shukrani mrembo
 
NYEMO CHILONGANI
UTAJIRI WENYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Tatu.

Kama kawaida yao, Patrick na Patricia walitoka darasani na kuanza kuelekea katika sehemu ya kupakia magari ndani ya eneo hilo kwa ajili ya kuingia ndani ya gari lao na kisha kuondoka mahali hapo. Walikuwa wakirukaruka, hivyo ndivyo walivyokuwa wakifanya kila walipoachwa watembee pamoja.

Walikuwa wamependeza mno, walivutia, kufanana kwao ilikuwa vigumu mno kugundua yupi alikuwa mwanaume na yupi mwanamke kwani hata Patricia mwenye hakutaka kuachia nywele ndefu, zilikuwa fupifupi kama zilivyokuwa za ndugu yake.

Mara baada ya kulifikia gari lile, mlango ukafunguliwa na kisha kuingia ndani. Kwanza wakashtuka, hawakumkuta dereva peke yake kama ilivyokuwa asubuhi, walimkuta akiwa na wanaume wengine watatu, ingawa sura zao zilionyesha tabasamu pana lakini hawakutaka kuamini kama watu wale walikuwa wazuri.

“Kaka, ni wakina nani hawa?” aliuliza Partick huku akimwangalia mtu mmojammoja ndani ya gari hilo.

“Ni marafiki wa baba, twendeni,” alisema dereva yule.

Hawakubisha, wakaingia ndani na kisha safari ya kuelekea nyumbani kuanza. Walionekana kuwa na hofu, hawakuonekana kujiamini hata kidogo, kila walipowaangalia watu hao, walizidi kuogopa na kuona kwamba watu hao hawakuwa marafiki hata kidogo.
Hawakuchukua barabara ile waliyozoea ya kurudia nyumbani, wakachukua barabara nyingine, na sehemu zote walizokuwa wakipita, dereva ndiye aliyekuwa akiambiwa nenda huku, kata huku, nenda kule.

“Tunakwenda wapi?” aliuliza Patricia huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Nyumbani!” alijibu dereva kwa kifupi.

“Hapana! Ila huku siyo nyumbani, kaka turudishe nyumbani,” alisema Patricia huku hofu yake ikionekana dhahiri machoni mwake.

Dereva hakuwa na la kufanya, alikuwa akiambiwa nini cha kufanya na wapi pa kupita, walipofika umbali fulani, wakamwambia atoke katika kile kiti na jamaa mmoja kukalia.

Hawakutaka kumuacha hapo, walijua kwamba kama wangefanya hivyo basi ingekuwa ni rahisi kutoa taarifa kituo cha polisi, wakaondoka naye, walipofika katika ile gereji ambayo ndani yake bado walimshikilia Dk. Fabian, wakamuingiza na dereva huyo na kumwambia atulie na wao kuendelea na safari yao.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea, Patrick na Patricia walikuwa wakikifuatilia kwa karibu mno, walikuwa wakilia tu, walitaka kurudishwa nyumbani lakini hakukuwa na mtu aliyewasikiliza zaidi ya kuambiwa kwamba huko walipokuwa wakipelekwa ndipo palikuwa kwa baba yao.

“Tunataka kumuona mama, turudisheni nyumbani, tunataka kumuona mama...” alisema Patricia huku akilia mfululizo, si yeye tu, hata Patrick naye alikuwa akilia tu.

“Nyamazeni, huku tunapokwenda ndipo kwa baba yenu,” alisema jamaa mmoja.

Hawakunyamaza, kilio chao kilikuwa hichohicho lakini hakukuwa na aliyewaelewa, baada ya dakika kadhaa, gari hilo likaanza kuingizwa katika jumba moja kubwa, lilikuwa ni zaidi ya nyumba waliyokuwa wakiishi, kulikuwa na bwawa la kuogelea, walinzi, mbwa na vitu vingine vingi.

Baada ya gari kutembea kwa umbali fulani ndani ya eneo kubwa la nyumba hiyo, likasimamishwa na kisha kuteremshwa kutoka ndani ya gari hilo. Walikuwa kwenye hofu, wakachukuliwa na kuingizwa ndani, wakaambiwa wakae kwenye makochi yaliyokuwa hapo sebuleni.

Baada ya dakika kadhaa, Mike akatokea sebuleni hapo, alikuwa na mpenzi wake, Aisha. Alipowaona watoto hao, akashindwa kuvumilia, alifanana nao sana, akawasogelea na kisha kuwakumbatia.

Walimwangalia mwanaume huyo, hawakumfahamu alikuwa nani, ndiyo kwanza ilikuwa mara yao ya kwanza kumuona. Aisha alisimama pembeni, muda wote uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana, alipowaangalia watoto hao, alikuwa na uhakika walikuwa watoto wa mpenzi wake kwani kama kufanana, walifanana naye sana.

“Watoto wangu! Hatimaye mpo mikononi mwangu,” alisema Mike huku akiwaangalia, bado Patrick na Patricia walionekana kuwa na wasiwasi.

“Tunataka kwenda nyumbani!”

“Hapa ndiyo nyumbani kwenu!”

“Hapana! Tunataka kumuona mama na baba...” alisema Patricia.

“Mimi ndiye baba yenu! Patricia, mimi ni baba yako, niangalie, huoni kama tunafanana?” alisema Mike huku akimwangalia Patricia usoni, hakuishia hapo, maneno hayohayo akamwambia na Patrick.

Ni kweli, walipokuwa wakimwangalia mwanaume huyo aliyesimama mbele yao walifanana naye sana lakini hiyo haikutosha kumaanisha kwamba alikuwa baba yao, walifahamu fika kwamba Dylan ndiye alikuwa baba yao, sasa kwa nini mwanaume huyo aseme kwamba alikuwa baba yao, kwao, hilo lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo.

****

Bado Dylan na mkewe walikuwa kwenye mawazo lukuki, kitendo cha watoto wao kutokuonekana kiliwachanganya sana, walikuwa kwenye majonzi makubwa, walijitahidi kuwasiliana na polisi lakini hao wala hawakusaidia kitu chochote kile, bado mbele yao kulikuwa na giza nene, hawakujua watoto hao walikuwa mahali gani.

Polisi chini ya Interpool walihangaika lakini hawakufanikiwa, walijaribu hata kuwasiliana na polisi wa nchi nyingine za jirani kama Canada na Mexico ili kuona kama watoto hao watakuwa wamepelekwa huko lakini majibu yalikuwa bila kwa bila.

Hawakutulia, waliposhindwa kabisa, wakawaachia maofisa wa FBI wafuatilie ili kuona kama wangeweza kufanikiwa, wakaingia katika kazi ya kuwatafuta watoto hao, walitakiwa kufanya juu chini lakini mwisho wa siku watoto hao wanapatikana, tena wakiwa salama kabisa.

“Mtu wa kwanza atafutwe dereva, huyu ndiye atakuwa mtu muhimu sana,” alisema afisa mmoja.

Hicho ndicho walichotaka kukifanya, mtu wa kwanza ambaye alitakiwa kupatikana kwa wakati huo alikuwa huyo dereva, naye, kupatikana kwake ilikuwa ngumu sana kitu kilichowafanya maofisa wa FBI kuchukua namba yake ya simu kutoka kwa Dylan ili waweze kuitraki namba hiyo na wafahamu mahali alipokuwa.

“Kama tukifanya hivyo, tutafanikiwa,” alisema afisa wa FBI na kisha kuondoka kuelekea nyumbani kwa Dylan huku wakiwa na uhakika kwamba watafanikiwa kumpata dereva huyo kabla ya kumpata mtu aliyewateka watoto hao.

****

Mara baada ya kuondoka kuelekea nyumbani kwa Dylan, wakaonana naye na kumwambia mikakati kabambe ambayo walitaka kuifanya kipindi hicho, ilikuwa ni lazima waitraki simu ya dereva huyo kujua alikuwa mahali gani kipindi hicho.

Wakapewa namba na moja kwa moja kurudi makao makuu. Huko, wakakaa chini. Suala la kutekwa kwa watoto wa Dylan lilikuwa kubwa, Marekani ikaonekana kama kutikisika kwani Dylan hakuwa mtu mdogo, alikuwa bilionea mkubwa hivyo suala lake lilichukuliwa na kuwa kubwa mno.

Wakaanza kazi mara moja, ilikuwa ni lazima wakamilishe mchakato wao. Vijana wa IT wakakaa katika kompyuta zao, walikuwa ni vijana wenye uwezo ambao waliajiriwa kwa ajili ya kazi hiyo tu.
Walikuwa na PhD ya masuala ya kompyuta, hawakuwa watu wa mchezo hata mara moja. Wakati wao wakihangaika kuitafuta simu hiyo, maofisa wengine wa FBI walikuwa wakifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

“Simu inaita...” alisema kijana mmoja.

Hapohapo wakaingiza katika system yao, ilikuwa ni afadhali simu kuzimwa kuliko kuwa hewani, kitendo cha kuita tu, tayari mambo yakaanza kwenda sawa katika kompyuta zao.

Kwanza ikatokea dunia, ikaanza kujizungusha, ilipofika katika Bara la Marekani ya Kaskazini, ikatulia na hapohapo kuanza kujivuta mpaka katika Jiji la New York, bado ilikuwa ikitafuta mahali simu hiyo ilipokuwa, ikaanza kupita katika mitaa mingi na mwisho wa siku kusimama katika gereji moja iliyokuwa katika Mtaa wa Hampishire ambao ulikaliwa na Waingereza wengi.

“Yupo hapa,” alisema kijana mmoja, mshale ulisimama katika gereji hiyo.

Hapohapo simu zikaanza kupigwa, maofisa wa FBI wakawasiliana na wenzao ambao waliwataka kwenda katika gereji hiyo mara moja, hakukuwa na uda wa kupoteza, haraka sana wakaanza kwenda huko, kila kitu kilichokuwa kikiendelea, taarifa ilikuwa ikitolewa.

****

Dereva alihisi simu yake ikiita mfukoni mwake, ilikuwa katika mtetemo (vibration) kiasi kwamba hakukuwa na mtu mwingine aliyeligundua hilo. Hakuweza kuipokea, mikono yake ilifungwa kamba na aliiacha iendelee kuita huku akihisi kwamba mpiga alikuwa bosi wake, Dylan.

Hakujua nani mwingine alikuwa mahali hapo, uso wake ulifunikwa kwa kitambaa cheusi, hakuwa akiona kitu chochote kile, hata yule Dk. Fabian ambaye naye alifungwa kamba hakujua kama aliendelea kuwa mahali hapo au alitolewa.

Aliwasikia watu wakizungumza, mazungumzo yao mengi yalikuwa ni kuhusu malipo ambayo walipewa, yalikuwa makubwa ambayo hawakudhani kama kuna siku kungetokea mtu ambaye angewalipa kiasi kikubwa cha fedha kama walicholipwa kwa kufanya kazi nyepesi kama ile ambayo waliifuatilia kwa kipindi cha mwezi mzima.

Mpaka kufikia hatua hiyo, dereva akabaki akijiuliza maswali mengi, hao watu walikuwa nani na kwa nini waliwateka watoto? Hakujua. Muda ulizidi kwenda mbele, hofu yake iliendelea kuwa moyoni mwake na kuna kipindi alihisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yake.

“Jamani...mnataka nini kutoka kwetu?” aliuliza dereva yule huku akitaka kufahamu kile hasa kilichomfanya kuwa hapo kwani kama suala lilikuwa ni watoto, walichukuliwa na kupelekwa sehemu.

“Wewe! Hebu nyamaza, tutasambaratisha ubongo wako,” alijibu mwanaume mmoja huku akimsogelea, alipomfikia, akampiga teke la uso.

Ilipofika saa kumi jioni, mara honi zikaanza kusikika kutoka nje ya gereji hiyo, walipotazama kupitia kamera zilizokuwa humo ndani, macho yao yakatua katika gari moja la kifahari ambalo lilionekana kubondeka mbele.

Dereva wa gari hilo alikuwa akipiga honi, alitaka kufunguliwa kwa ajili ya kuliingiza gari lake ndani na kufanyiwa matengenezo. Kila mmoja alionekana kukasirika, hawakutegemea kupata gari lolote lile japokuwa hiyo ilikuwa ni gereji.

“Ni nani huyo?” aliuliza jamaa mmoja.

“Sijui! Hebu kamfungulie usikie anataka nini,” alisema jamaa mwingine.

Jamaa huyo akatoka na kuelekea nje ambapo akalifungua geti kwa kuelekea juu, akalifuata gari hilo na kuanza kuzungumza na dereva. Hakutaka kusikia chochote zaidi ya kumwambia kwamba hakuna huduma yoyote iliyokuwa ikitolewa kwa siku hiyo.

Wakati akiwa anazungumza na dereva huyo, wenzake walikuwa ndani wakifuatilia, walitaka kufahamu kama mtu huyo kweli alihitaji kutengenezewa gari au kulikuwa na jingine.

“Sikiliza...” alisema mwanaume aliyekuwa ndani ya gari pamoja na mwenzake.

“Kuna nini tena?”
“Unaliona gari hilo hapo mbele...”

“Limefanyaje?”
“Linahitaji matengenezo.”
“Sawa! Ila gereji imefungwa.”
“Inafungwaje na wakati nilitoa taarifa kwamba nitaleta gari langu?” aliuliza mwanaume huyo, alionekana kumfahamu mtu aliyehusika na gereji hiyo.

“Tumefunga.”
“Kwani wewe ni nani?”
“Mhusika wa hii gereji!”
“Acha ujinga, tangu lini ukawa mhusika wa gereji hii?” aliuliza mwanaume huyo huku akiteremka kutoka ndani ya gari.

Mwenzake hakubaki, naye akatoka, wale vijana wawili waliokuwa ndani ya gereji hiyo ambao walikuwa wakifuatilia kila kitu kwenye televisheni iliyounganishwa na kamera za CCTV, nao wakatoka na kwenda kule nje kwani walihisi kulikuwa na kitu kibaya.

“Kuna nini tena?” aliuliza mwanaume mmoja ambaye ndiye alionekana kuwa kiongozi.

“Nataka kuingiza gari ndani!”

“Ili?”
“Litengenezwe, huoni lilivyo?” alijibu.

“Tumefunga.”
“Kwani nyie ni nani? Mbona hamjakaa kiufundi?” aliuliza.

Wakati mwanaume huyo akijiandaa kujibu, akajikuta akiwekwa chini ya ulinzi na mwanaume yule aliyekuwa upande wa pili. Wenyewe walishtuka, hawakujua hao walikuwa wakina nani, walichokifahamu ni kwamba walikuwa wateja ambao walifika kwa ajili ya kulitengeneza gari lao bovu, sasa iweje wawaweke chini ya ulinzi.

Hawakuwa na jinsi, wakatakiwa kulala chini tena kifudifudi na mikono ikiwa kichwani. Wwalishindwa kufahamu hao walikuwa wakina nani lakini baada ya kutamka kwamba walikuwa FBI, tayari wakajiona kukamatwa.

Wakafungwa pingu na kisha kutulizwa pembeni, kilichofanyika ni kuingia ndani na kisha kuwatoa vitambaa mateka hao ambao ni Dk. Fabian na dereva wa Dylan, kilichofuata ni kupigwa simu makao makuu ambapo baada ya muda, polisi wakafika na kisha kuwachukua na kuwapeleka kituoni.

“Tuambieni watoto wapo wapi?” waliulizwa wanaume hao.

“Hawakuwa pale, walichukuliwa na baba yao,” alijibu mwanaume mmoja.

“Baba yao?”
“Ndiyo!”

Wakaweka wazi kwamba wao walipewa kazi ya kuwateka watoto hao kwa kuwa baba yao alikuwa akiwahitaji, sisi hatukuwa na jinsi, tuliangalia zaidi pesa hivyo kufanya kazi yetu, walipomleta dereva, wakaondoka na watoto hao na kusema wanawapeleka kwa baba yao.

Ofisa wa FBI hakutaka kuuliza swali jingine, hapohapo akachukua simu yake na kumpigia Dylan huku akimtaka mahali hapo kwani tayari dereva alipatikana, mbali na huyo, pia kulikuwa na wanaume wengine ambao ndiyo waliowateka watoto wao, nao walipatikana.

Ndani ya dakika kumi, Dylan, mkewe na Catherine wakafika mahali hapo. Kwa kumwangalia Dylan alionekana kuwa na hasira mno. Akataka kupelekwa ndani ya chumba hicho.

“Subiri kwanza...tumewauliza wale jamaa, wamesema kwamba watoto unao wewe...” alisema afisa wa FBI.

“Mimi?”
“Ndiyo!”
“Hebu nionane nao,” alisema Dylan.

Je, nini kitaendelea
 
NYEMO CHILONGANI

UTAJIRI WEMYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Nne.

Kwa jinsi alivyokuwa, haikuwa rahisi kumkubalia, alionekana kuwa na hasira sana hivyo kuona kwamba kama wangemruhusu kuingia ndani basi angeweza kuanzisha timbwili huko ndani.

Wakati hayo yote yakiendelea, Dk. Fabian alikuwa katika chumba kingine na dereva, walikuwa wakizungumza lakini muda mwingi daktari huyo alionekana kuwa na mawazo tele.

Kitu kilichompa mawazo ni kuhusu Mike ambaye aliibuka tena na kuhitaji watoto wake. Alimfahamu kama bilionea lakini alisahau kwamba huyo mwanaume ndiye yule aliyemfuata kipindi cha nyuma na kumtoa mbegu zake za kiume.

Hakujua ni kitu gani alitakiwa kumwambia Dylan na mkewe, mwanamke hakujua kitu chochote kile kwani mchezo mzima ulipangwa na wao watatu tu. Alijua kwamba mwanaume huyo angeumia sana lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima amwambie ukweli kilichokuwa kimetokea.

Maofisa wa FBI walisubiri kwa dakika arobaini na tano, wakamchukua Dylan na kumpeleka katika chumba walichokuwa mwanaume yule, walitaka kuzungumza nao na kuwauliza kuhusu mahali watoto walipolekwa, walisema walichukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, mbona baba mwenyewe alisema kwamba hakuwa amewapata watoto hao?

“Ulisema kwamba watoto walipelekwa kwa baba yao, si ndiyo?” aliuliza afisa wa FBI, pembeni yake akiwepo Dylan na mkewe, Katty.

“Ndiyo!”

“Wazazi wao ndiyo hawa hapa, mbona wanasema hawakuwapata watoto wao?’ aliuliza afisa yule huku akiwaangalia.

“Mkuu! Ila sisi tuliambiwa kwamba wanapelekwa kwa baba yao!”

“Sasa mbona hajawapata? Baba yupi?”

“Baba yao!”

“Si ndiye huyu! Mbona hajawapata?”

“Hata sisi hatujui!”

Walichokifanya FBI ni kumchukua Dk. Fabian na kisha kuwapeleka katika chumba kingine cha mahojiano, huko walitaka kufahamu sababu za wao kutekwa kwa kuhisi kwamba kupitia wao wangeweza kupata kitu fulani.

Alipoulizwa dereva, alisema tu kwamba alikwenda kuwachukua watoto hao, ghafla akatekwa yeye na watoto na kupelekwa gereji, watoto wakachukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, kitu ambacho aliona si kweli.

“Na wewe dokta?” aliuliza afisa, Dk. Fabian akakaa kimya, maofisa wote waliokuwa humo ndani wakabaki wakimwangalia, hawakujua sababu ya kukaa kimya, alipomaliza kuwa katika hali hiyo, akauinua uso wake na kuwaangalia.

“Naomba nionane na BwanaDylan!” aliwaambia maofisa wale.

Hilo halikuwa tatizo, kwa kuwa alimhitaji huyo, afisa mmoja akatoka na kwenda kumuita, baada ya dakika moja tu, akarudi akiwa na Bwana Dylan ambaye alikuwa akiongozana na mkewe.

“Naomba tupewe chumba cha siri, tuna mazungumzo binafsi...” alisema Dk. Fabian, hata Bwana Dylan akabaki akishangaa, kwanza kitendo cha kumuona daktari huyo hapo polisi, kilimchanganya.

Wakapelekwa katika chumba kimoja cha siri, hakukuwa na kamera za CCTV wala hakukuwa na vinasa sauti. Huko wakatulia, muda wote Bwana Dylan alikuwa akimwangalia daktari yule, alihisi kulikuwa na kitu.

“Kuna nini?” aliuliza.

“Mike amerudi!”

“Mike! Ndiye nani?”

“Yule bilionea!”

“Unamzungumza huyu Mike bilionea, amerudi kutoka wapi sasa?” aliuliza Bwana Dylan.

“Unakumbuka zile mbegu tulizozitoa, zilikuwa zake na ndiye yeye aliniteka na kuniuliza nilimuwekea nani mbegu zile, nilikataa kusema, akatishia kuniua..” alijibu Dk. Fabian na kuhadithia kila kitu kilichotokea.

Bwana Dylan alibaki kimya, mwili ulikuwa ukimtetemeka, japokuwa ndani ya chumba kile kulikuwa na kiyoyozi lakini alihisi kijasho chembamba kikimtoka. Hakuamini alichokisikia kwamba yule Mike ambaye alifanikisha zoezi zima la upatikanaji wa watoto wale eti alirudi na kuwataka watoto wake.

“Haiwezekani! Nilimalizana naye, wale ni watoto wangu na si wake ni wangu,” alisema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.

Hali ya hewa ilibadilika, wakatoka ndani ya kile chumba, kwa jinsi alivyokuwa Dylan kipindi kifupi kilichopita, alionekana kuwa tofauti kabisa na kipindi hiki. Alionekana kuwa mwingi wa hasira, hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

“Kuna nini?” aliuliza afisa mkuu wa FBI, Bwana Pierre August.

“Nataka nizungumze na wewe...” alijibu Dk. Fabian.

“Kuhusu nini?”

“Aliyewateka watoto.”

“Unamjua?”

“Ndiyo!”

“Ni nani?”

“Bilionea Mike...”

“Unasemaje?”

“Ndiyo hivyo! Ila kuna kitu....”

“Kitu gani?”

“Mtafuteni yeye kwanza...” alisema Dk. Fabian.

Maofisa wa FBI hawakutaka kusubiri, waliambiwa juu ya mtuu aliyekuwa amewateka watoto hao, alikuwwa bilionea mkubwa, hawakujua sababu ya kuwateka hivyo walichokifanya ni kuanza kwenda nyumbani kwake.

Huku nyuma, Dylan alikuwa amechanganyikiwa, akaona kama dunia ikiimgeuka, hakuamini kama mwisho wa kila kitu ungekuwa namna ile, alimwangalia mke wake, alionekana kuwa mtu mwenye maswali mengi lakini hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilikuwa siri kubwa na muda huo ulionyesha kabisa kwamba ile siri iliyodumu kwa miaka yote ilikuwa ikienda kujulikana, angefanya nini? Hakujua.

Polisi na maofisa wa FBI wakaelekea mpaka nyumbani kwa Mike, wakaoba kuonana naye, wakaruhusiwa kuingia ndani. Walipofika sebuleni, macho yao yakatua kwa watoto waliokuwa wakiwatafuta, walionekana kuwa kawaida, hawakuwa na furaha wala hawakuwa na huzuni.

Mike alikuwa sebuleni hapo pamoja na mkewe, Aisha, walikuwa wakizungumza mambo mengi na watoto wale, kwa kutumia maneno mengi, bado Mike alikuwa akiwaambia kwamba yeye alikuwa baba yao.

“Na mama yetu ni nani?” aliuliza Patrick.

“Huyo aliyewazaa...”

“Nini kilitokea?” aliuliza Patricia.

“Ni stori ndefu sana, ila nataka mfahamu kwamba mimi ndiye baba yenu,” alisema Mike.

Maofisa hao waliposimama kwa muda, waliimwangalia Mike na mkewe, hawakuonekana kuhofia kitu chochote kile, walichokifanya, hapohapo wakamwambia juu ya kile kilichotokea kwamba alikuwa akishutumiwa kuwateka watoto.

“Sikuwateka watoto...” alijibu Mike.

“Kumbe wamefikaje hapa?”

“Nilikwenda kuwachukua, hivi kweli kuna mtu anaweza kuwateka watoto wake?” aliuliza Mike huku akiwaangalia maofisa hao.

“Watoto wako hawa?”

“Ndiyo!”

Kila mmoja alionekana kumshangaa, walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka katika kituo cha polisi huku akiongozana na mapacha wale. Mike hakuonekana kuogopa hata mara moja, njia nzima uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana.

Walipofika katika kituo hicho, wakaingizwa ndani ambapo huko wakakutana na Bwana Dylan akiwa na mkewe, Katty. Patrick na Patricia walipomuona mama yao, wakamfuata na kumkumbatia, walionekana kuwa na furaha mno.

“Mlikuwa wapi?” aliuliza mwanamke huyo.

“Tulikuwa kwa baba...”

“Baba gani?”

“Baba yetu....”

“Yupi?”

“Huyu hapa!” walijibu huku wakimnyooshea mkono Mike.

Hakukuwa na kitu kilichomuuma Dylan kama kuona watoto wake wakimtaja mwanaume mwingine kwamba ndiye baba yao. Aliyasikia maumivu makali moyoni mwake, yaani kitendo cha Mike kukaa na watoto hao kwa muda mfupi tu tayari aliwaambia maneno mengi, kuwashawishi kwa mifano mpaka watoto wote kuamini kwamba yeye alikuwa baba yao.

Dylan hakujibu kitu, alikwenda pembeni na kutulia kwenye kiti. Muda wote machozi yalikuwa yakimtoka, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea mahali pale.

Katty alibaki na maswali mengi, alipomwangalia Mike, uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana lakini alipoyapeleka macho kwa mumewe, alikuwa akilia kwa uchungu, hakujua kitu gani kilitokea, katika kumbukumbu zake, hakukumbuka kama alikwishawahi kuonana na Mike, sasa iweje hao watoto wawe wake? Kila alichojiuliza, akakosa jibu.

“Wewe unasema watoto hawa ni wako! Si ndiyo?” alisema Bwana August huku akimwangalia Mike.

“Ndiyo!”

“Kivipi?”

“Dylan anaelewa kila kitu! Watoto ni wangu! Hii ni damu yangu!” alijibu Mike huku akionekana kujiamini.

“Unanichanganya!”

“Angalia hata sura zetu, huoni kama nafanana nao sana...”

“Hilo si tatizo!”

“Basi muulize Dylan, hawa ni watoto wa nani!” alisema Mike.

Bwana August akamgeukia Dylan ambaye alikuwa pembeni akilia tu. Kila mmoja alimuonea huruma lakini ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane kwamba hao watoto walikuwa wa nani.

Mke wake mwenyewe alibaki akimwangalia, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mahali hapo. Bado alichanganyikiwa, kwa nini mumewe ajiumeume na wakati alijua fika kwamba watoto wale alizaa nao. Kila Dylan alipoulizwa, alibaki kimya.

“Hawa ni watoto wangu! Dk. Fabian, hebu eleza kila kitu kilivyokuwa!” alisema Mike huku bado tabasamu lake likionekana kuwa usoni mwake.

Ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane, hata Catherine, mdogo wake Dylan alibaki kimya akiangalia kilichokuwa kikiendelea. Yeye mwenye alichanganyikiwa, kila alipowaangalia mapacha wale, walifanana mno na Mike ambaye alidai kwamba ndiye alikuwa baba wa watoto wale.

Hapo ndipo Dk. Fabian alipoanza kusimulia, alitakiwa kufanya hivyo, hakutakiwa kunyamaza au kuficha kitu chochote kile, alitakiwa kuzungumza ukweli juu ya kila kitu kilichotokea huko nyuma.

Kila mtu alibaki kimya akimsikiliza, muda wote huo, Dylan alijiinamia, machozi mfululizo yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake. Alikuwa tajiri mkubwa, aliyeheshimika, hapo ndipo akagundua kwamba utajiri haukuwa na maana yoyote ile.

Ulikuwa na uwezo wa kununua dawa ila si uhai, ulikuwa na uwezo wa kununua magari ila si furaha. Maneno aliyokuwa akizungumza Dk. Fabian yalimuumiza mno, kila alipoyasikiliza, alihisi kuna mtu alichukua mkuki wenye ncha kali iliyounguzwa na moto na kisha kuuchoma moyo wake.

Mpaka anamaliza kusimulia, Katty alikuwa akilia, hakuamini kilichokuwa kimesimuliwa. Yaani kila siku alijua kwamba watoto wale walikuwa wake na mume wake kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na kitu kingine, kumbe alipandikiziwa mbegu katika mfumo wake wa uzazi.

Kilio kilisikika kwa sauti ya juu, hakukubali hata mara moja, akamfuata mumewe na kuanza kumgombeza huku akilia, moyo wake ulijisikia uchungu, kama mumewe alikuwa na tatizo, kwa nini hakumwambia kabla. Kila siku alikuwa akifanya naye mapenzi, alikuwa akifanya na nini? Kila alipojiuliza, alichanganyikiwa.

Dylan hakuzungumza kitu, hakutaka kubaki mahali hapo, akatoka nje na kuanza kuondoka huku dada yake akiwa nyuma akimfuata.

“Dylan, unakwenda wapi?” aliuliza Catherine, tayari Dylan alikuwa ndani ya gari, naye akaingia.

“Catherine, nitaishi vipi? Nitaificha wapi sura yangu?” aliuliza Dylan, alikuwa akiendelea kulia tu.

“Unakwenda wapi? Nijibu!”

“Niache, sioni umuhimu wa kuishi, sioni umuhimu wa kuwa tajiri. Nimeumia, utajiri hauna maana, ni utajiri wenye uchungu, utaniliza kila siku. Kwa nini? Kwani imekuwa hivi? Kwa nini Catherine?” aliuliza Dylan, alikuwa akilia mno, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno.

Catherine mwenye hakujibu maswali hayo, alibaki akimwangalia kaka yake, kwa jinsi alivyoonekana tu, alikuwa na maumivu makali moyoni mwake, hakujua nini cha kumwambia na hakutaka kumuache kaka yake kwani alijua ni kitu gani kingetokea endapo angemuacha, ilikuwa ni lazima ajiue kwani alikata tamaa, hakuona umuhimu wa kuishi.

Akawapigia simu wazazi wake, akawaelezea kwamba anahitaji msaada mkubwa kutoka kwao kwani vinginevyo Dylan angejiua. Wazazi wao walichanganyikiwa kusikia hivyo, wakaahidiana waonane nyumbani kwa Dylan.

“Naomba niendeshe gari tafadhali,” alisema Catherine, Dylan akampisha, akashikilia usukani na kuanza kuondoka.

Huku ndani, Katty hakujua afanye nini, alibaki kimya huku akiwaangalia watoto wake, kila alichokisikia hakukiamini, alimchukua mumewe, Dylan kwa kile alichomfanyia, uamuzi wa kuondoka mahali hapo na watoto wake ndiyo uliomjia kichwani, hakutaka kurudi nyumbani, alipanga kuondoka haraka sana kuelekea Los Angeles.

“Katty...samahani sana kwa kilichotokea, hakikuwa dhumuni langu, najua umeumia sana lakini haina jinsi, naomba unisamehe kwa kila kitu,” alisema Mike huku akimwangalia mwanamke huyo.

“Usijali...”

“Sasa unakwenda wapi?”

“Ni lazima niende Los Angeles, siwezi kubaki hapa...”

“Na watoto wangu?”

“Ni watoto wangu pia...”

“Najua! Lakini ningependa kuwa nao karibu!”

“Najua!”

“Kwa hiyo tufanye nini?”

Moyoni mwake aliumia, kila kitu alichokiacha nyumbani, hakutaka kukirudia, aliamua kuondoka kuelekea Los Angeles. Watoto hao hawakuwa wake peke yake, bali baba yao alikuwa Mike ambaye naye alikuwa bilionea mkubwa.

Wakapanga mikakati ni kwa namna gani wangewatunza watoto hao, hivyo siku hiyohiyo Mike kumsindikiza kuelekea Los Angeles kwa ndege yake binafsi. Huku nyuma, hata vijana ambao walifanya utekaji wakaachiwa huru kwani kesi yenyewe ikagundulika kwamba watoto hawakutekwa bali walichukuliwa na baba yao, mjadala ukaishia hapo.

Wakafika mpaka Los Angeles ambapo wakapanga apartment na kuishi huko. Kwa kuwa Mike aliwapenda sana watoto wake, akaamua kuwanunulia nyuma ya kifahari, kuwawekea kila kitu na kumtaka Katty aishia nao huko.

Kila siku Katty akawa mtu wa kupokea meseji na kupigiwa simu na Dylan na kumuomba msamaha kwa kila kitu kilichotokea, hakujibu meseji hizo kwani mwanaume huyo alimuumiza moyo wake kupita kawaida.

Siku zikaendelea, watoto wakakua, Dylan akaendelea na maisha yake yenye uchungu, ya kulia kila siku. Hakuwa na furaha hata siku moja, aliwakumbuka Patrick na Patricia lakini hakuwa na jinsi, hawakuwa watoto wake.

Hayo mambo yalimalizwa kimyakimya, hata maofisa wa FBI walipewa fedha nyingi kutunza siri, hakikutakiwa kujulikana kitu chochote kile. Kutokana na kuwa na msongo wa mawazo, afya ya Dylan ikaanza kuzorota, akaanza kukonda, akawa hali na baada ya kwenda hospitali kupimwa, akagundulika kuwa na shinikizo la damu ambalo lilimfanya kudhoofika kila siku mpaka kufikia hatua ya kupelekwa hospitali.

Afya yake haikubadilika, bado aliendelea kuumia kila siku, akakosa amani, furaha ikapotea, fedha hazikumsaidia, hazikuweza kuinunua afya na kurudi kama zamani.

Kuumwa kwake ukawa gumzo duniani kote, kila kona watu walimzungumzia yeye, kila mmoja alisema lake, kwa jinsi alivyokuwa amedhoofika kitandani pale kila mmoja aliamini kwamba Bwana Dylan asingeweza kupona, angekufa palepale kitandani.

Maneno ya watu hao yakawa kama sumu kwani tangu watu wawe na hofu namna hiyo na kutamka maneno mabaya, Dylan hakuchukua muda mrefu, akafariki kitandani hapo.

Ilikuwa ni huzuni mno, watu walisikitika kwani alikuwa mtu mwema, aliyewasaidia watu wengi ila mwisho wa siku, shinikizo la damu likamuua kitandani hapo.

Katika mazishi yake, Katty hakuacha kwenda, alikwenda ila hakwenda na watoto kwa kuwa huyo hakuwa baba yao, ndugu za Dylan walikuwa wakimwangalia kwa jicho baya lakini hakutaka kujali, alichojua alikwenda hapo kwa ajili ya kuonyesha ushirikiano na kwa kuwa alimpenda Dylan, hakukuwa na kingine.

Baada ya siku mbili, Dylan akazikwa katika makaburi ya Victoria Cementary yaliyokuwa New Orleans ambapo ndipo alipokuwa amezaliwa, sehemu ambayo wazazi wake walikuwa wakiishi hata kabla ya kupata utajiri.

Baada ya mazishi hayo, Katty akarudi zake Los Angeles ambapo aliendelea kuwalea watoto wake. Hakuhitaji urithi, hakuhitaji kitu chochote kutoka katika familia ya Bwana James, aliwaacha na utajiri wao, yeye aliendelea kufanya vitu vyake huku Mike akimtunza na kumfungulia biashara mbalimbali za kufanya ambazo zilimuingizia kiasi kikubwa cha fedha.

MWISHO.
 
NYEMO CHILONGANI

UTAJIRI WEMYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Nne.

Kwa jinsi alivyokuwa, haikuwa rahisi kumkubalia, alionekana kuwa na hasira sana hivyo kuona kwamba kama wangemruhusu kuingia ndani basi angeweza kuanzisha timbwili huko ndani.

Wakati hayo yote yakiendelea, Dk. Fabian alikuwa katika chumba kingine na dereva, walikuwa wakizungumza lakini muda mwingi daktari huyo alionekana kuwa na mawazo tele.

Kitu kilichompa mawazo ni kuhusu Mike ambaye aliibuka tena na kuhitaji watoto wake. Alimfahamu kama bilionea lakini alisahau kwamba huyo mwanaume ndiye yule aliyemfuata kipindi cha nyuma na kumtoa mbegu zake za kiume.

Hakujua ni kitu gani alitakiwa kumwambia Dylan na mkewe, mwanamke hakujua kitu chochote kile kwani mchezo mzima ulipangwa na wao watatu tu. Alijua kwamba mwanaume huyo angeumia sana lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima amwambie ukweli kilichokuwa kimetokea.

Maofisa wa FBI walisubiri kwa dakika arobaini na tano, wakamchukua Dylan na kumpeleka katika chumba walichokuwa mwanaume yule, walitaka kuzungumza nao na kuwauliza kuhusu mahali watoto walipolekwa, walisema walichukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, mbona baba mwenyewe alisema kwamba hakuwa amewapata watoto hao?

“Ulisema kwamba watoto walipelekwa kwa baba yao, si ndiyo?” aliuliza afisa wa FBI, pembeni yake akiwepo Dylan na mkewe, Katty.

“Ndiyo!”

“Wazazi wao ndiyo hawa hapa, mbona wanasema hawakuwapata watoto wao?’ aliuliza afisa yule huku akiwaangalia.

“Mkuu! Ila sisi tuliambiwa kwamba wanapelekwa kwa baba yao!”

“Sasa mbona hajawapata? Baba yupi?”

“Baba yao!”

“Si ndiye huyu! Mbona hajawapata?”

“Hata sisi hatujui!”

Walichokifanya FBI ni kumchukua Dk. Fabian na kisha kuwapeleka katika chumba kingine cha mahojiano, huko walitaka kufahamu sababu za wao kutekwa kwa kuhisi kwamba kupitia wao wangeweza kupata kitu fulani.

Alipoulizwa dereva, alisema tu kwamba alikwenda kuwachukua watoto hao, ghafla akatekwa yeye na watoto na kupelekwa gereji, watoto wakachukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, kitu ambacho aliona si kweli.

“Na wewe dokta?” aliuliza afisa, Dk. Fabian akakaa kimya, maofisa wote waliokuwa humo ndani wakabaki wakimwangalia, hawakujua sababu ya kukaa kimya, alipomaliza kuwa katika hali hiyo, akauinua uso wake na kuwaangalia.

“Naomba nionane na BwanaDylan!” aliwaambia maofisa wale.

Hilo halikuwa tatizo, kwa kuwa alimhitaji huyo, afisa mmoja akatoka na kwenda kumuita, baada ya dakika moja tu, akarudi akiwa na Bwana Dylan ambaye alikuwa akiongozana na mkewe.

“Naomba tupewe chumba cha siri, tuna mazungumzo binafsi...” alisema Dk. Fabian, hata Bwana Dylan akabaki akishangaa, kwanza kitendo cha kumuona daktari huyo hapo polisi, kilimchanganya.

Wakapelekwa katika chumba kimoja cha siri, hakukuwa na kamera za CCTV wala hakukuwa na vinasa sauti. Huko wakatulia, muda wote Bwana Dylan alikuwa akimwangalia daktari yule, alihisi kulikuwa na kitu.

“Kuna nini?” aliuliza.

“Mike amerudi!”

“Mike! Ndiye nani?”

“Yule bilionea!”

“Unamzungumza huyu Mike bilionea, amerudi kutoka wapi sasa?” aliuliza Bwana Dylan.

“Unakumbuka zile mbegu tulizozitoa, zilikuwa zake na ndiye yeye aliniteka na kuniuliza nilimuwekea nani mbegu zile, nilikataa kusema, akatishia kuniua..” alijibu Dk. Fabian na kuhadithia kila kitu kilichotokea.

Bwana Dylan alibaki kimya, mwili ulikuwa ukimtetemeka, japokuwa ndani ya chumba kile kulikuwa na kiyoyozi lakini alihisi kijasho chembamba kikimtoka. Hakuamini alichokisikia kwamba yule Mike ambaye alifanikisha zoezi zima la upatikanaji wa watoto wale eti alirudi na kuwataka watoto wake.

“Haiwezekani! Nilimalizana naye, wale ni watoto wangu na si wake ni wangu,” alisema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.

Hali ya hewa ilibadilika, wakatoka ndani ya kile chumba, kwa jinsi alivyokuwa Dylan kipindi kifupi kilichopita, alionekana kuwa tofauti kabisa na kipindi hiki. Alionekana kuwa mwingi wa hasira, hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

“Kuna nini?” aliuliza afisa mkuu wa FBI, Bwana Pierre August.

“Nataka nizungumze na wewe...” alijibu Dk. Fabian.

“Kuhusu nini?”

“Aliyewateka watoto.”

“Unamjua?”

“Ndiyo!”

“Ni nani?”

“Bilionea Mike...”

“Unasemaje?”

“Ndiyo hivyo! Ila kuna kitu....”

“Kitu gani?”

“Mtafuteni yeye kwanza...” alisema Dk. Fabian.

Maofisa wa FBI hawakutaka kusubiri, waliambiwa juu ya mtuu aliyekuwa amewateka watoto hao, alikuwwa bilionea mkubwa, hawakujua sababu ya kuwateka hivyo walichokifanya ni kuanza kwenda nyumbani kwake.

Huku nyuma, Dylan alikuwa amechanganyikiwa, akaona kama dunia ikiimgeuka, hakuamini kama mwisho wa kila kitu ungekuwa namna ile, alimwangalia mke wake, alionekana kuwa mtu mwenye maswali mengi lakini hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilikuwa siri kubwa na muda huo ulionyesha kabisa kwamba ile siri iliyodumu kwa miaka yote ilikuwa ikienda kujulikana, angefanya nini? Hakujua.

Polisi na maofisa wa FBI wakaelekea mpaka nyumbani kwa Mike, wakaoba kuonana naye, wakaruhusiwa kuingia ndani. Walipofika sebuleni, macho yao yakatua kwa watoto waliokuwa wakiwatafuta, walionekana kuwa kawaida, hawakuwa na furaha wala hawakuwa na huzuni.

Mike alikuwa sebuleni hapo pamoja na mkewe, Aisha, walikuwa wakizungumza mambo mengi na watoto wale, kwa kutumia maneno mengi, bado Mike alikuwa akiwaambia kwamba yeye alikuwa baba yao.

“Na mama yetu ni nani?” aliuliza Patrick.

“Huyo aliyewazaa...”

“Nini kilitokea?” aliuliza Patricia.

“Ni stori ndefu sana, ila nataka mfahamu kwamba mimi ndiye baba yenu,” alisema Mike.

Maofisa hao waliposimama kwa muda, waliimwangalia Mike na mkewe, hawakuonekana kuhofia kitu chochote kile, walichokifanya, hapohapo wakamwambia juu ya kile kilichotokea kwamba alikuwa akishutumiwa kuwateka watoto.

“Sikuwateka watoto...” alijibu Mike.

“Kumbe wamefikaje hapa?”

“Nilikwenda kuwachukua, hivi kweli kuna mtu anaweza kuwateka watoto wake?” aliuliza Mike huku akiwaangalia maofisa hao.

“Watoto wako hawa?”

“Ndiyo!”

Kila mmoja alionekana kumshangaa, walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka katika kituo cha polisi huku akiongozana na mapacha wale. Mike hakuonekana kuogopa hata mara moja, njia nzima uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana.

Walipofika katika kituo hicho, wakaingizwa ndani ambapo huko wakakutana na Bwana Dylan akiwa na mkewe, Katty. Patrick na Patricia walipomuona mama yao, wakamfuata na kumkumbatia, walionekana kuwa na furaha mno.

“Mlikuwa wapi?” aliuliza mwanamke huyo.

“Tulikuwa kwa baba...”

“Baba gani?”

“Baba yetu....”

“Yupi?”

“Huyu hapa!” walijibu huku wakimnyooshea mkono Mike.

Hakukuwa na kitu kilichomuuma Dylan kama kuona watoto wake wakimtaja mwanaume mwingine kwamba ndiye baba yao. Aliyasikia maumivu makali moyoni mwake, yaani kitendo cha Mike kukaa na watoto hao kwa muda mfupi tu tayari aliwaambia maneno mengi, kuwashawishi kwa mifano mpaka watoto wote kuamini kwamba yeye alikuwa baba yao.

Dylan hakujibu kitu, alikwenda pembeni na kutulia kwenye kiti. Muda wote machozi yalikuwa yakimtoka, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea mahali pale.

Katty alibaki na maswali mengi, alipomwangalia Mike, uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana lakini alipoyapeleka macho kwa mumewe, alikuwa akilia kwa uchungu, hakujua kitu gani kilitokea, katika kumbukumbu zake, hakukumbuka kama alikwishawahi kuonana na Mike, sasa iweje hao watoto wawe wake? Kila alichojiuliza, akakosa jibu.

“Wewe unasema watoto hawa ni wako! Si ndiyo?” alisema Bwana August huku akimwangalia Mike.

“Ndiyo!”

“Kivipi?”

“Dylan anaelewa kila kitu! Watoto ni wangu! Hii ni damu yangu!” alijibu Mike huku akionekana kujiamini.

“Unanichanganya!”

“Angalia hata sura zetu, huoni kama nafanana nao sana...”

“Hilo si tatizo!”

“Basi muulize Dylan, hawa ni watoto wa nani!” alisema Mike.

Bwana August akamgeukia Dylan ambaye alikuwa pembeni akilia tu. Kila mmoja alimuonea huruma lakini ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane kwamba hao watoto walikuwa wa nani.

Mke wake mwenyewe alibaki akimwangalia, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mahali hapo. Bado alichanganyikiwa, kwa nini mumewe ajiumeume na wakati alijua fika kwamba watoto wale alizaa nao. Kila Dylan alipoulizwa, alibaki kimya.

“Hawa ni watoto wangu! Dk. Fabian, hebu eleza kila kitu kilivyokuwa!” alisema Mike huku bado tabasamu lake likionekana kuwa usoni mwake.

Ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane, hata Catherine, mdogo wake Dylan alibaki kimya akiangalia kilichokuwa kikiendelea. Yeye mwenye alichanganyikiwa, kila alipowaangalia mapacha wale, walifanana mno na Mike ambaye alidai kwamba ndiye alikuwa baba wa watoto wale.

Hapo ndipo Dk. Fabian alipoanza kusimulia, alitakiwa kufanya hivyo, hakutakiwa kunyamaza au kuficha kitu chochote kile, alitakiwa kuzungumza ukweli juu ya kila kitu kilichotokea huko nyuma.

Kila mtu alibaki kimya akimsikiliza, muda wote huo, Dylan alijiinamia, machozi mfululizo yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake. Alikuwa tajiri mkubwa, aliyeheshimika, hapo ndipo akagundua kwamba utajiri haukuwa na maana yoyote ile.

Ulikuwa na uwezo wa kununua dawa ila si uhai, ulikuwa na uwezo wa kununua magari ila si furaha. Maneno aliyokuwa akizungumza Dk. Fabian yalimuumiza mno, kila alipoyasikiliza, alihisi kuna mtu alichukua mkuki wenye ncha kali iliyounguzwa na moto na kisha kuuchoma moyo wake.

Mpaka anamaliza kusimulia, Katty alikuwa akilia, hakuamini kilichokuwa kimesimuliwa. Yaani kila siku alijua kwamba watoto wale walikuwa wake na mume wake kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na kitu kingine, kumbe alipandikiziwa mbegu katika mfumo wake wa uzazi.

Kilio kilisikika kwa sauti ya juu, hakukubali hata mara moja, akamfuata mumewe na kuanza kumgombeza huku akilia, moyo wake ulijisikia uchungu, kama mumewe alikuwa na tatizo, kwa nini hakumwambia kabla. Kila siku alikuwa akifanya naye mapenzi, alikuwa akifanya na nini? Kila alipojiuliza, alichanganyikiwa.

Dylan hakuzungumza kitu, hakutaka kubaki mahali hapo, akatoka nje na kuanza kuondoka huku dada yake akiwa nyuma akimfuata.

“Dylan, unakwenda wapi?” aliuliza Catherine, tayari Dylan alikuwa ndani ya gari, naye akaingia.

“Catherine, nitaishi vipi? Nitaificha wapi sura yangu?” aliuliza Dylan, alikuwa akiendelea kulia tu.

“Unakwenda wapi? Nijibu!”

“Niache, sioni umuhimu wa kuishi, sioni umuhimu wa kuwa tajiri. Nimeumia, utajiri hauna maana, ni utajiri wenye uchungu, utaniliza kila siku. Kwa nini? Kwani imekuwa hivi? Kwa nini Catherine?” aliuliza Dylan, alikuwa akilia mno, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno.

Catherine mwenye hakujibu maswali hayo, alibaki akimwangalia kaka yake, kwa jinsi alivyoonekana tu, alikuwa na maumivu makali moyoni mwake, hakujua nini cha kumwambia na hakutaka kumuache kaka yake kwani alijua ni kitu gani kingetokea endapo angemuacha, ilikuwa ni lazima ajiue kwani alikata tamaa, hakuona umuhimu wa kuishi.

Akawapigia simu wazazi wake, akawaelezea kwamba anahitaji msaada mkubwa kutoka kwao kwani vinginevyo Dylan angejiua. Wazazi wao walichanganyikiwa kusikia hivyo, wakaahidiana waonane nyumbani kwa Dylan.

“Naomba niendeshe gari tafadhali,” alisema Catherine, Dylan akampisha, akashikilia usukani na kuanza kuondoka.

Huku ndani, Katty hakujua afanye nini, alibaki kimya huku akiwaangalia watoto wake, kila alichokisikia hakukiamini, alimchukua mumewe, Dylan kwa kile alichomfanyia, uamuzi wa kuondoka mahali hapo na watoto wake ndiyo uliomjia kichwani, hakutaka kurudi nyumbani, alipanga kuondoka haraka sana kuelekea Los Angeles.

“Katty...samahani sana kwa kilichotokea, hakikuwa dhumuni langu, najua umeumia sana lakini haina jinsi, naomba unisamehe kwa kila kitu,” alisema Mike huku akimwangalia mwanamke huyo.

“Usijali...”

“Sasa unakwenda wapi?”

“Ni lazima niende Los Angeles, siwezi kubaki hapa...”

“Na watoto wangu?”

“Ni watoto wangu pia...”

“Najua! Lakini ningependa kuwa nao karibu!”

“Najua!”

“Kwa hiyo tufanye nini?”

Moyoni mwake aliumia, kila kitu alichokiacha nyumbani, hakutaka kukirudia, aliamua kuondoka kuelekea Los Angeles. Watoto hao hawakuwa wake peke yake, bali baba yao alikuwa Mike ambaye naye alikuwa bilionea mkubwa.

Wakapanga mikakati ni kwa namna gani wangewatunza watoto hao, hivyo siku hiyohiyo Mike kumsindikiza kuelekea Los Angeles kwa ndege yake binafsi. Huku nyuma, hata vijana ambao walifanya utekaji wakaachiwa huru kwani kesi yenyewe ikagundulika kwamba watoto hawakutekwa bali walichukuliwa na baba yao, mjadala ukaishia hapo.

Wakafika mpaka Los Angeles ambapo wakapanga apartment na kuishi huko. Kwa kuwa Mike aliwapenda sana watoto wake, akaamua kuwanunulia nyuma ya kifahari, kuwawekea kila kitu na kumtaka Katty aishia nao huko.

Kila siku Katty akawa mtu wa kupokea meseji na kupigiwa simu na Dylan na kumuomba msamaha kwa kila kitu kilichotokea, hakujibu meseji hizo kwani mwanaume huyo alimuumiza moyo wake kupita kawaida.

Siku zikaendelea, watoto wakakua, Dylan akaendelea na maisha yake yenye uchungu, ya kulia kila siku. Hakuwa na furaha hata siku moja, aliwakumbuka Patrick na Patricia lakini hakuwa na jinsi, hawakuwa watoto wake.

Hayo mambo yalimalizwa kimyakimya, hata maofisa wa FBI walipewa fedha nyingi kutunza siri, hakikutakiwa kujulikana kitu chochote kile. Kutokana na kuwa na msongo wa mawazo, afya ya Dylan ikaanza kuzorota, akaanza kukonda, akawa hali na baada ya kwenda hospitali kupimwa, akagundulika kuwa na shinikizo la damu ambalo lilimfanya kudhoofika kila siku mpaka kufikia hatua ya kupelekwa hospitali.

Afya yake haikubadilika, bado aliendelea kuumia kila siku, akakosa amani, furaha ikapotea, fedha hazikumsaidia, hazikuweza kuinunua afya na kurudi kama zamani.

Kuumwa kwake ukawa gumzo duniani kote, kila kona watu walimzungumzia yeye, kila mmoja alisema lake, kwa jinsi alivyokuwa amedhoofika kitandani pale kila mmoja aliamini kwamba Bwana Dylan asingeweza kupona, angekufa palepale kitandani.

Maneno ya watu hao yakawa kama sumu kwani tangu watu wawe na hofu namna hiyo na kutamka maneno mabaya, Dylan hakuchukua muda mrefu, akafariki kitandani hapo.

Ilikuwa ni huzuni mno, watu walisikitika kwani alikuwa mtu mwema, aliyewasaidia watu wengi ila mwisho wa siku, shinikizo la damu likamuua kitandani hapo.

Katika mazishi yake, Katty hakuacha kwenda, alikwenda ila hakwenda na watoto kwa kuwa huyo hakuwa baba yao, ndugu za Dylan walikuwa wakimwangalia kwa jicho baya lakini hakutaka kujali, alichojua alikwenda hapo kwa ajili ya kuonyesha ushirikiano na kwa kuwa alimpenda Dylan, hakukuwa na kingine.

Baada ya siku mbili, Dylan akazikwa katika makaburi ya Victoria Cementary yaliyokuwa New Orleans ambapo ndipo alipokuwa amezaliwa, sehemu ambayo wazazi wake walikuwa wakiishi hata kabla ya kupata utajiri.

Baada ya mazishi hayo, Katty akarudi zake Los Angeles ambapo aliendelea kuwalea watoto wake. Hakuhitaji urithi, hakuhitaji kitu chochote kutoka katika familia ya Bwana James, aliwaacha na utajiri wao, yeye aliendelea kufanya vitu vyake huku Mike akimtunza na kumfungulia biashara mbalimbali za kufanya ambazo zilimuingizia kiasi kikubwa cha fedha.

MWISHO.
FUNZO KUBWA
Kujifungia ndani na tatizo kwa kulifanya siri sio suluhisho la kudumu.
 
Back
Top Bottom