Utajiri wenye uchungu

Utajiri wenye uchungu

Vitu vingine sio vya kuvifanyia siri jamaa amekufa kwa ujinga wake
 
mimi tangu mwanzo alipoanza kutumia uume wa bandia na kutafta sperm donor nilijua tu huko mwisho kutakua na tukio
Kabisa,maana kwa sperm donor kosa kubwa sana alilolifanya ni moja.
Aidha Dr. au Mike mmoja wapo alitakiwa astafishwe kuishi ili Dylan awe salama. Tofauti na hapo ni kimbembe.
 
NYEMO CHILONGANI

UTAJIRI WEMYE UCHUNGU

Sehemu ya Thelathini na Nne.

Kwa jinsi alivyokuwa, haikuwa rahisi kumkubalia, alionekana kuwa na hasira sana hivyo kuona kwamba kama wangemruhusu kuingia ndani basi angeweza kuanzisha timbwili huko ndani.

Wakati hayo yote yakiendelea, Dk. Fabian alikuwa katika chumba kingine na dereva, walikuwa wakizungumza lakini muda mwingi daktari huyo alionekana kuwa na mawazo tele.

Kitu kilichompa mawazo ni kuhusu Mike ambaye aliibuka tena na kuhitaji watoto wake. Alimfahamu kama bilionea lakini alisahau kwamba huyo mwanaume ndiye yule aliyemfuata kipindi cha nyuma na kumtoa mbegu zake za kiume.

Hakujua ni kitu gani alitakiwa kumwambia Dylan na mkewe, mwanamke hakujua kitu chochote kile kwani mchezo mzima ulipangwa na wao watatu tu. Alijua kwamba mwanaume huyo angeumia sana lakini hakuwa na jinsi, ilikuwa ni lazima amwambie ukweli kilichokuwa kimetokea.

Maofisa wa FBI walisubiri kwa dakika arobaini na tano, wakamchukua Dylan na kumpeleka katika chumba walichokuwa mwanaume yule, walitaka kuzungumza nao na kuwauliza kuhusu mahali watoto walipolekwa, walisema walichukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, mbona baba mwenyewe alisema kwamba hakuwa amewapata watoto hao?

“Ulisema kwamba watoto walipelekwa kwa baba yao, si ndiyo?” aliuliza afisa wa FBI, pembeni yake akiwepo Dylan na mkewe, Katty.

“Ndiyo!”

“Wazazi wao ndiyo hawa hapa, mbona wanasema hawakuwapata watoto wao?’ aliuliza afisa yule huku akiwaangalia.

“Mkuu! Ila sisi tuliambiwa kwamba wanapelekwa kwa baba yao!”

“Sasa mbona hajawapata? Baba yupi?”

“Baba yao!”

“Si ndiye huyu! Mbona hajawapata?”

“Hata sisi hatujui!”

Walichokifanya FBI ni kumchukua Dk. Fabian na kisha kuwapeleka katika chumba kingine cha mahojiano, huko walitaka kufahamu sababu za wao kutekwa kwa kuhisi kwamba kupitia wao wangeweza kupata kitu fulani.

Alipoulizwa dereva, alisema tu kwamba alikwenda kuwachukua watoto hao, ghafla akatekwa yeye na watoto na kupelekwa gereji, watoto wakachukuliwa na kupelekwa kwa baba yao, kitu ambacho aliona si kweli.

“Na wewe dokta?” aliuliza afisa, Dk. Fabian akakaa kimya, maofisa wote waliokuwa humo ndani wakabaki wakimwangalia, hawakujua sababu ya kukaa kimya, alipomaliza kuwa katika hali hiyo, akauinua uso wake na kuwaangalia.

“Naomba nionane na BwanaDylan!” aliwaambia maofisa wale.

Hilo halikuwa tatizo, kwa kuwa alimhitaji huyo, afisa mmoja akatoka na kwenda kumuita, baada ya dakika moja tu, akarudi akiwa na Bwana Dylan ambaye alikuwa akiongozana na mkewe.

“Naomba tupewe chumba cha siri, tuna mazungumzo binafsi...” alisema Dk. Fabian, hata Bwana Dylan akabaki akishangaa, kwanza kitendo cha kumuona daktari huyo hapo polisi, kilimchanganya.

Wakapelekwa katika chumba kimoja cha siri, hakukuwa na kamera za CCTV wala hakukuwa na vinasa sauti. Huko wakatulia, muda wote Bwana Dylan alikuwa akimwangalia daktari yule, alihisi kulikuwa na kitu.

“Kuna nini?” aliuliza.

“Mike amerudi!”

“Mike! Ndiye nani?”

“Yule bilionea!”

“Unamzungumza huyu Mike bilionea, amerudi kutoka wapi sasa?” aliuliza Bwana Dylan.

“Unakumbuka zile mbegu tulizozitoa, zilikuwa zake na ndiye yeye aliniteka na kuniuliza nilimuwekea nani mbegu zile, nilikataa kusema, akatishia kuniua..” alijibu Dk. Fabian na kuhadithia kila kitu kilichotokea.

Bwana Dylan alibaki kimya, mwili ulikuwa ukimtetemeka, japokuwa ndani ya chumba kile kulikuwa na kiyoyozi lakini alihisi kijasho chembamba kikimtoka. Hakuamini alichokisikia kwamba yule Mike ambaye alifanikisha zoezi zima la upatikanaji wa watoto wale eti alirudi na kuwataka watoto wake.

“Haiwezekani! Nilimalizana naye, wale ni watoto wangu na si wake ni wangu,” alisema Dylan huku akionekana kuchanganyikiwa.

Hali ya hewa ilibadilika, wakatoka ndani ya kile chumba, kwa jinsi alivyokuwa Dylan kipindi kifupi kilichopita, alionekana kuwa tofauti kabisa na kipindi hiki. Alionekana kuwa mwingi wa hasira, hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

“Kuna nini?” aliuliza afisa mkuu wa FBI, Bwana Pierre August.

“Nataka nizungumze na wewe...” alijibu Dk. Fabian.

“Kuhusu nini?”

“Aliyewateka watoto.”

“Unamjua?”

“Ndiyo!”

“Ni nani?”

“Bilionea Mike...”

“Unasemaje?”

“Ndiyo hivyo! Ila kuna kitu....”

“Kitu gani?”

“Mtafuteni yeye kwanza...” alisema Dk. Fabian.

Maofisa wa FBI hawakutaka kusubiri, waliambiwa juu ya mtuu aliyekuwa amewateka watoto hao, alikuwwa bilionea mkubwa, hawakujua sababu ya kuwateka hivyo walichokifanya ni kuanza kwenda nyumbani kwake.

Huku nyuma, Dylan alikuwa amechanganyikiwa, akaona kama dunia ikiimgeuka, hakuamini kama mwisho wa kila kitu ungekuwa namna ile, alimwangalia mke wake, alionekana kuwa mtu mwenye maswali mengi lakini hakutaka kuzungumza kitu chochote kile.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilikuwa siri kubwa na muda huo ulionyesha kabisa kwamba ile siri iliyodumu kwa miaka yote ilikuwa ikienda kujulikana, angefanya nini? Hakujua.

Polisi na maofisa wa FBI wakaelekea mpaka nyumbani kwa Mike, wakaoba kuonana naye, wakaruhusiwa kuingia ndani. Walipofika sebuleni, macho yao yakatua kwa watoto waliokuwa wakiwatafuta, walionekana kuwa kawaida, hawakuwa na furaha wala hawakuwa na huzuni.

Mike alikuwa sebuleni hapo pamoja na mkewe, Aisha, walikuwa wakizungumza mambo mengi na watoto wale, kwa kutumia maneno mengi, bado Mike alikuwa akiwaambia kwamba yeye alikuwa baba yao.

“Na mama yetu ni nani?” aliuliza Patrick.

“Huyo aliyewazaa...”

“Nini kilitokea?” aliuliza Patricia.

“Ni stori ndefu sana, ila nataka mfahamu kwamba mimi ndiye baba yenu,” alisema Mike.

Maofisa hao waliposimama kwa muda, waliimwangalia Mike na mkewe, hawakuonekana kuhofia kitu chochote kile, walichokifanya, hapohapo wakamwambia juu ya kile kilichotokea kwamba alikuwa akishutumiwa kuwateka watoto.

“Sikuwateka watoto...” alijibu Mike.

“Kumbe wamefikaje hapa?”

“Nilikwenda kuwachukua, hivi kweli kuna mtu anaweza kuwateka watoto wake?” aliuliza Mike huku akiwaangalia maofisa hao.

“Watoto wako hawa?”

“Ndiyo!”

Kila mmoja alionekana kumshangaa, walichokifanya ni kumchukua na kumpeleka katika kituo cha polisi huku akiongozana na mapacha wale. Mike hakuonekana kuogopa hata mara moja, njia nzima uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana.

Walipofika katika kituo hicho, wakaingizwa ndani ambapo huko wakakutana na Bwana Dylan akiwa na mkewe, Katty. Patrick na Patricia walipomuona mama yao, wakamfuata na kumkumbatia, walionekana kuwa na furaha mno.

“Mlikuwa wapi?” aliuliza mwanamke huyo.

“Tulikuwa kwa baba...”

“Baba gani?”

“Baba yetu....”

“Yupi?”

“Huyu hapa!” walijibu huku wakimnyooshea mkono Mike.

Hakukuwa na kitu kilichomuuma Dylan kama kuona watoto wake wakimtaja mwanaume mwingine kwamba ndiye baba yao. Aliyasikia maumivu makali moyoni mwake, yaani kitendo cha Mike kukaa na watoto hao kwa muda mfupi tu tayari aliwaambia maneno mengi, kuwashawishi kwa mifano mpaka watoto wote kuamini kwamba yeye alikuwa baba yao.

Dylan hakujibu kitu, alikwenda pembeni na kutulia kwenye kiti. Muda wote machozi yalikuwa yakimtoka, hakuamini kile kilichokuwa kikiendelea mahali pale.

Katty alibaki na maswali mengi, alipomwangalia Mike, uso wake ulikuwa kwenye tabasamu pana lakini alipoyapeleka macho kwa mumewe, alikuwa akilia kwa uchungu, hakujua kitu gani kilitokea, katika kumbukumbu zake, hakukumbuka kama alikwishawahi kuonana na Mike, sasa iweje hao watoto wawe wake? Kila alichojiuliza, akakosa jibu.

“Wewe unasema watoto hawa ni wako! Si ndiyo?” alisema Bwana August huku akimwangalia Mike.

“Ndiyo!”

“Kivipi?”

“Dylan anaelewa kila kitu! Watoto ni wangu! Hii ni damu yangu!” alijibu Mike huku akionekana kujiamini.

“Unanichanganya!”

“Angalia hata sura zetu, huoni kama nafanana nao sana...”

“Hilo si tatizo!”

“Basi muulize Dylan, hawa ni watoto wa nani!” alisema Mike.

Bwana August akamgeukia Dylan ambaye alikuwa pembeni akilia tu. Kila mmoja alimuonea huruma lakini ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane kwamba hao watoto walikuwa wa nani.

Mke wake mwenyewe alibaki akimwangalia, hakujua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mahali hapo. Bado alichanganyikiwa, kwa nini mumewe ajiumeume na wakati alijua fika kwamba watoto wale alizaa nao. Kila Dylan alipoulizwa, alibaki kimya.

“Hawa ni watoto wangu! Dk. Fabian, hebu eleza kila kitu kilivyokuwa!” alisema Mike huku bado tabasamu lake likionekana kuwa usoni mwake.

Ilikuwa ni lazima ukweli ujulikane, hata Catherine, mdogo wake Dylan alibaki kimya akiangalia kilichokuwa kikiendelea. Yeye mwenye alichanganyikiwa, kila alipowaangalia mapacha wale, walifanana mno na Mike ambaye alidai kwamba ndiye alikuwa baba wa watoto wale.

Hapo ndipo Dk. Fabian alipoanza kusimulia, alitakiwa kufanya hivyo, hakutakiwa kunyamaza au kuficha kitu chochote kile, alitakiwa kuzungumza ukweli juu ya kila kitu kilichotokea huko nyuma.

Kila mtu alibaki kimya akimsikiliza, muda wote huo, Dylan alijiinamia, machozi mfululizo yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake. Alikuwa tajiri mkubwa, aliyeheshimika, hapo ndipo akagundua kwamba utajiri haukuwa na maana yoyote ile.

Ulikuwa na uwezo wa kununua dawa ila si uhai, ulikuwa na uwezo wa kununua magari ila si furaha. Maneno aliyokuwa akizungumza Dk. Fabian yalimuumiza mno, kila alipoyasikiliza, alihisi kuna mtu alichukua mkuki wenye ncha kali iliyounguzwa na moto na kisha kuuchoma moyo wake.

Mpaka anamaliza kusimulia, Katty alikuwa akilia, hakuamini kilichokuwa kimesimuliwa. Yaani kila siku alijua kwamba watoto wale walikuwa wake na mume wake kumbe nyuma ya pazia kulikuwa na kitu kingine, kumbe alipandikiziwa mbegu katika mfumo wake wa uzazi.

Kilio kilisikika kwa sauti ya juu, hakukubali hata mara moja, akamfuata mumewe na kuanza kumgombeza huku akilia, moyo wake ulijisikia uchungu, kama mumewe alikuwa na tatizo, kwa nini hakumwambia kabla. Kila siku alikuwa akifanya naye mapenzi, alikuwa akifanya na nini? Kila alipojiuliza, alichanganyikiwa.

Dylan hakuzungumza kitu, hakutaka kubaki mahali hapo, akatoka nje na kuanza kuondoka huku dada yake akiwa nyuma akimfuata.

“Dylan, unakwenda wapi?” aliuliza Catherine, tayari Dylan alikuwa ndani ya gari, naye akaingia.

“Catherine, nitaishi vipi? Nitaificha wapi sura yangu?” aliuliza Dylan, alikuwa akiendelea kulia tu.

“Unakwenda wapi? Nijibu!”

“Niache, sioni umuhimu wa kuishi, sioni umuhimu wa kuwa tajiri. Nimeumia, utajiri hauna maana, ni utajiri wenye uchungu, utaniliza kila siku. Kwa nini? Kwani imekuwa hivi? Kwa nini Catherine?” aliuliza Dylan, alikuwa akilia mno, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali mno.

Catherine mwenye hakujibu maswali hayo, alibaki akimwangalia kaka yake, kwa jinsi alivyoonekana tu, alikuwa na maumivu makali moyoni mwake, hakujua nini cha kumwambia na hakutaka kumuache kaka yake kwani alijua ni kitu gani kingetokea endapo angemuacha, ilikuwa ni lazima ajiue kwani alikata tamaa, hakuona umuhimu wa kuishi.

Akawapigia simu wazazi wake, akawaelezea kwamba anahitaji msaada mkubwa kutoka kwao kwani vinginevyo Dylan angejiua. Wazazi wao walichanganyikiwa kusikia hivyo, wakaahidiana waonane nyumbani kwa Dylan.

“Naomba niendeshe gari tafadhali,” alisema Catherine, Dylan akampisha, akashikilia usukani na kuanza kuondoka.

Huku ndani, Katty hakujua afanye nini, alibaki kimya huku akiwaangalia watoto wake, kila alichokisikia hakukiamini, alimchukua mumewe, Dylan kwa kile alichomfanyia, uamuzi wa kuondoka mahali hapo na watoto wake ndiyo uliomjia kichwani, hakutaka kurudi nyumbani, alipanga kuondoka haraka sana kuelekea Los Angeles.

“Katty...samahani sana kwa kilichotokea, hakikuwa dhumuni langu, najua umeumia sana lakini haina jinsi, naomba unisamehe kwa kila kitu,” alisema Mike huku akimwangalia mwanamke huyo.

“Usijali...”

“Sasa unakwenda wapi?”

“Ni lazima niende Los Angeles, siwezi kubaki hapa...”

“Na watoto wangu?”

“Ni watoto wangu pia...”

“Najua! Lakini ningependa kuwa nao karibu!”

“Najua!”

“Kwa hiyo tufanye nini?”

Moyoni mwake aliumia, kila kitu alichokiacha nyumbani, hakutaka kukirudia, aliamua kuondoka kuelekea Los Angeles. Watoto hao hawakuwa wake peke yake, bali baba yao alikuwa Mike ambaye naye alikuwa bilionea mkubwa.

Wakapanga mikakati ni kwa namna gani wangewatunza watoto hao, hivyo siku hiyohiyo Mike kumsindikiza kuelekea Los Angeles kwa ndege yake binafsi. Huku nyuma, hata vijana ambao walifanya utekaji wakaachiwa huru kwani kesi yenyewe ikagundulika kwamba watoto hawakutekwa bali walichukuliwa na baba yao, mjadala ukaishia hapo.

Wakafika mpaka Los Angeles ambapo wakapanga apartment na kuishi huko. Kwa kuwa Mike aliwapenda sana watoto wake, akaamua kuwanunulia nyuma ya kifahari, kuwawekea kila kitu na kumtaka Katty aishia nao huko.

Kila siku Katty akawa mtu wa kupokea meseji na kupigiwa simu na Dylan na kumuomba msamaha kwa kila kitu kilichotokea, hakujibu meseji hizo kwani mwanaume huyo alimuumiza moyo wake kupita kawaida.

Siku zikaendelea, watoto wakakua, Dylan akaendelea na maisha yake yenye uchungu, ya kulia kila siku. Hakuwa na furaha hata siku moja, aliwakumbuka Patrick na Patricia lakini hakuwa na jinsi, hawakuwa watoto wake.

Hayo mambo yalimalizwa kimyakimya, hata maofisa wa FBI walipewa fedha nyingi kutunza siri, hakikutakiwa kujulikana kitu chochote kile. Kutokana na kuwa na msongo wa mawazo, afya ya Dylan ikaanza kuzorota, akaanza kukonda, akawa hali na baada ya kwenda hospitali kupimwa, akagundulika kuwa na shinikizo la damu ambalo lilimfanya kudhoofika kila siku mpaka kufikia hatua ya kupelekwa hospitali.

Afya yake haikubadilika, bado aliendelea kuumia kila siku, akakosa amani, furaha ikapotea, fedha hazikumsaidia, hazikuweza kuinunua afya na kurudi kama zamani.

Kuumwa kwake ukawa gumzo duniani kote, kila kona watu walimzungumzia yeye, kila mmoja alisema lake, kwa jinsi alivyokuwa amedhoofika kitandani pale kila mmoja aliamini kwamba Bwana Dylan asingeweza kupona, angekufa palepale kitandani.

Maneno ya watu hao yakawa kama sumu kwani tangu watu wawe na hofu namna hiyo na kutamka maneno mabaya, Dylan hakuchukua muda mrefu, akafariki kitandani hapo.

Ilikuwa ni huzuni mno, watu walisikitika kwani alikuwa mtu mwema, aliyewasaidia watu wengi ila mwisho wa siku, shinikizo la damu likamuua kitandani hapo.

Katika mazishi yake, Katty hakuacha kwenda, alikwenda ila hakwenda na watoto kwa kuwa huyo hakuwa baba yao, ndugu za Dylan walikuwa wakimwangalia kwa jicho baya lakini hakutaka kujali, alichojua alikwenda hapo kwa ajili ya kuonyesha ushirikiano na kwa kuwa alimpenda Dylan, hakukuwa na kingine.

Baada ya siku mbili, Dylan akazikwa katika makaburi ya Victoria Cementary yaliyokuwa New Orleans ambapo ndipo alipokuwa amezaliwa, sehemu ambayo wazazi wake walikuwa wakiishi hata kabla ya kupata utajiri.

Baada ya mazishi hayo, Katty akarudi zake Los Angeles ambapo aliendelea kuwalea watoto wake. Hakuhitaji urithi, hakuhitaji kitu chochote kutoka katika familia ya Bwana James, aliwaacha na utajiri wao, yeye aliendelea kufanya vitu vyake huku Mike akimtunza na kumfungulia biashara mbalimbali za kufanya ambazo zilimuingizia kiasi kikubwa cha fedha.

MWISHO.

Inahuzunisha sana...

Hii simulizi inafundisha kwamba, Japo maisha siyo kutesa kila kila siku, hata pesa nayo, inaweza ikawa siyo kila kitu...


Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Inahuzunisha sana...
Hii simulizi inafundisha kwamba, Japo maisha siyo kutesa kila kila siku, hata pesa nayo, inaweza ikawa siyo kila kitu...
Chapter Closed...
Cc: mahondaw
ni kweli na pamoja na pesa zote bado ameshindwa kujitibu tatizo lake lakini pengine angekubaliana na hali yake akaadopt tu mtoto pengine angempa faraja asingefariki hivo
 
ni kweli na pamoja na pesa zote bado ameshindwa kujitibu tatizo lake lakini pengine angekubaliana na hali yake akaadopt tu mtoto pengine angempa faraja asingefariki hivo

Ukiwa na pesa kuna mambo mengine ni ngumu sana kuyakubali au kuyaacha yapite tu hivyo hivyo...

Utatumia kila njia na uwezo wako wote, mambo yaende na kuonekana sawa hata kama haiwezekani...



Cc: mahondaw
 
Hiko ndio kimemcost dylan sasa s angekua wazi tu ana hiyo kadhia pengine angependwa hivohivo
Ukiwa na pesa kuna mambo mengine ni ngumu sana kuyakubali au kuyaacha yapite tu hivyo hivyo...
Utatumia kila njia na uwezo wako wote, mamb yaende na kuonekana sawa hata kama haiwezekani...
Cc: mahondaw
 
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.

Sehemu ya Kwanza.

“All people who live at the beach have to leave immediately because tsunami will come. Once you hear this announcement, tell your colleague,” (Watu wote mnaoishi katika ufukwe mnatakiwa muondoke haraka iwezekanavyo kwa sababu tsunami itakuja. Unaposikia tangazo hili mtaarifu na mwenzako,)” ilisikika sauti ya mwanamke aliyekuwa akitangaza katika Kituo cha Redio cha Orange Fm nchini Marekani.
Watu wote waliokuwa wakiishi katika fukwe mbalimbali katika Jiji la New Orleans nchini Marekani walitakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo kwani tayari mamlaka ya hali ya hewa ya nchini humo (National Weather Service) ilitangaza hali ya hatari ambayo ingelipata jiji hilo pamoja na majiji mengine yaliyokuwa katika fukwe mbalimbali ikiwemo Miami.
Hakukuwa na mtu aliyepuuzia taarifa hiyo, wengi wakaanza kuondoka kwa ajili ya kuyaokoa maisha yao kwani bado kumbukumbu juu ya kimbunga cha Katrina ambacho kilipiga miezi michache iliyopita bado ziliendelea kubaki vichwani mwao.
Mitaani kulikuwa na purukushani, kila mtu alitaka kuyaokoa maisha yake. Kumbukumbu juu ya tsunami zilikuwa vichwani mwao, walisoma kwenye historia miaka ya nyuma kwamba balaa hilo liliwahi kuikumba China na Japan na matokeo yake watu wengi walifariki dunia.
Serikali ya Marekani ikaagiza magari makubwa na kuwataka watu wote waondoke katika sehemu za ufukwe na kukimbia umbali wa kilometa ishirini kutoka ufukweni kwani pasipo kufanya hivyo ilikuwa ni lazima tsunami iwakumbe na kufariki dunia.
Watu waliondoka, helkopta zilipita kila kona ndani ya jiji hilo, mtu mmoja aliyekuwa akitangaza kwenye kipaza sauti alisikika akiwaambia watu kwamba huo ulikuwa ni muda wa kuondoka, kulikimbia jiji hilo kutokana na maafa ambayo yalitarajiwa kulikumba jiji hilo, tena saa mbili zijazo.
“Where is Catherine?” (Catherine yupo wapi?) alisikika mwanamke mmoja akiuliza.
“I don’t know . She told me that she would go to James, maybe she went there (Sifahamu. Aliniambia kwamba angekwenda kwa James, labda alikwenda huko) alijibu mwanaume mmoja.
Hakutaka kujali sana, kwa kuwa aliambiwa kwamba msichana huyo alikwenda kwa mwanaume aitwaye James, hakutaka kuuliza zaidi ya kuendelea na safari yao ya kuyaokoa maisha yao kwani lilikuwa limebaki saa moja kabla ya janga hilo kulikumba Jiji la New Orleans na miji yote ambayo ilikuwa karibu na bahari.
Mamlaka ya hali ya hewa nchini Marekani haikukaa kimya, bado iliendelea kutoa onyo kwamba watu wote waliokuwa wakiishi pembezoni mwa bahari ya Atlantic walitakiwa kuondoka kwani tsunami liliendelea kuja kwa kasi kwa kipimo cha 4.11 ambacho kilikuwa ni kikubwa mno huku mawimbi yake yakiwa na urefu wa mita mia moja kwenda juu ambayo yalikuwa yakienda kwa kasi ya kilometa 2 kwa dakika tano.
Huko lilipoanzia nchini China, Thailand na nchi nyingine barani Asia, liliacha vilio, zaidi ya watu milioni mbili walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya huku makazi ya watu wengi yakiharibiwa mno.
Maafa yaliyotokea nchini China kipindi hicho waliyaona kwenye televisheni, waliogopa na kuhisi kwamba inawezekana tsunami hilo lingefika mpaka nchini Marekani kwani hata wao kulikuwa na miji ambayo ilikuwa pembezoni mwa bahari, kweli ikawa hivyo.
“Mnatakiwa kuchukua vitu vilivyokuwa muhimu kwenu, ambavyo havina umuhimu viacheni na serikali itawasaidia kwa kila kitu,” bado tangazo lilikuwa likitolewa kutoka kwa mtu aliyekuwa kwenye helkopta ambaye alitumia kipaza sauti kilichosikika vizuri kabisa na kila mtu.
Muda ulizidi kwenda mbele, dakika arobaini na tano baadaye, ukimya mkubwa ulitawala kila kona ndani ya jiji hilo, hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika, si binadamu tu bali hata wanyama hawakuwepo, watu walikimbia na kwenda katika Mji wa Gonzales uliokuwa kilometa ishirini kutoka hapo New Orleans.
“Jamani naomba mnisaidie, namtafuta binti yangu...” alisema mwanamke mmoja, kwa kumwangalia tu alionekana kuwa na hofu moyoni mwake, alikuwa akimwambia mmoja wa wanajeshi ambao waliwachukua watu kutoka New Orleans.
“Anaitwa nani?”
“Catherine, mara ya mwisho kabla tangazo halijatolewa, alikwenda kwa mpenzi wake, sijui kama yupo naye kwa sababu hata wazazi wa mpenzi wake tulionana nao wakasema kwamba hata kijana wao hayupo nao,” alisema mwanamke huyo.
Hiyo ilikuwa kazi nyingine kabisa, alichokifanya mwanajeshi huyo ni kuonana na wazazi wa huyo kijana ambaye alikuwa mpenzi wa Catherine aitwaye James na kuanza kuzungumza nao.
Kama alivyoambiwa na mama yake Catherine ndivyo alivyoambiwa hata na wazazi hao kwamba kijana wao aitwaye James hakuwa akionekana. Hiyo ikawatia hofu kwa kuhisi kwamba japokuwa mahali hapo waliona kwamba kila mtu alikuwa hapo kumbe kuna wawili ambao hawakuwa hapo.
Walichokifanya ni kuanza kuyaita majina yao kila kona kwa kupitia kipaza sauti. Kila aliyesikia, akabaki akimwangalia mwenzake kwa kuhisi labda huyo ndiye aliyekuwa akihitajika.
Zaidi ya watu milioni nne waliokuwa wamekimbia katika jiji hilo, ni watu wawili tu ndiyo ambao hawakuwa wakionekana, kwani familia zote zilikuwepo na kila moja walitimia isipokuwa familia mbili ambazo watu wawili hawakuonekana.
Tayari kukaonekana kuwa na tatizo sehemu, mwanajeshi yule akawapa taarifa wenzake kwamba watu wawili hawakuwa wakionekana mahali hapo hivyo walitakiwa kwenda kuwatafuta katika jiji hilo, hata kama kuwaita walitakiwa kufanya hivyo ilimradi wawapate na kuwaleta pale walipokuwa.
“Zimebaki dakika ngapi kabla ya Tsunami kuipiga New Orleans?” aliuliza mwanajeshi mmoja.
“Dakika ishirini!”
“Chukueni helkopta haraka muende kuwatafuta...”
Hicho ndicho kilichofanyika, hakukuwa na muda wa kupoteza mahali hapo, kwa haraka sana wanajeshi sita wakaingia katika helkopta moja kubwa na kuanza kurudi ndani ya jiji hilo kwa ajili ya kuwatafuta watu wawili tu, msichana mjauzito aliyeitwa Catherine na mwanaume aliyeitwa James.
Walipofika katika jiji hilo, wakachukua darubini na kuanza kuangalia, kila kona, hakukuwa na mtu yeyote, hakukuwa na mnyama, ni nyumba na magari machache ndivyo vilivyokuwa vimebaki.
Hawakukata tamaa, waliendelea kuwatafuta huku wakiita kwa sauti kubwa tena kwa kutumia kipaza sauti lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia au hata kutoka na kuwapungia mikono kuonyesha kwamba alitaka msaada.
Dakika ziliendelea kukatika, zilipofika dakika kumi na tisa tu, kwa mbali baharini likaanza kuonekana wimbi kubwa na zito likija kwa kasi. Waliliangalia wimbi lile, lilikuwa kubwa zaidi ya mita mia moja ambayo ilitangazwa na mamlaka ya hali ya hewa.
Lilikuwa likija kwa kasi mno na hata muungurumo wake ulikuwa mkubwa. Halikuwa likija peke yake bali lilikuwa likija na meli kadhaa kubwa zilizokuwa baharini ambazo nazo zilisombwa na tsunami hiyo.
“It is coming...it is coming...” (Linakuja...linakuja..) alisema mwanajeshi mmoja, rubani akageuza helkopta ile na kuanza kuondoka kwani kwa jinsi wimbi lile lilivyokuwa likija kwa kasi, tena huku likiwa kubwa namna ile, walijua kabisa wangeweza kupata tatizo, hivyo wakaondoka huku wakiahirisha kuwatafuta watu hao ambao ukweli wenyewe ni kwamba walikuwa hai, tena msichana Catherine akiwa kwenye uchungu mkubwa wa kujifungua mbele ya mpenzi wake, James.
Du
 
Back
Top Bottom