Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,172
- 34,277
NYEMO CHILONGANI.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
Sehemu ya Kwanza.
“All people who live at the beach have to leave immediately because tsunami will come. Once you hear this announcement, tell your colleague,” (Watu wote mnaoishi katika ufukwe mnatakiwa muondoke haraka iwezekanavyo kwa sababu tsunami itakuja. Unaposikia tangazo hili mtaarifu na mwenzako,)” ilisikika sauti ya mwanamke aliyekuwa akitangaza katika Kituo cha Redio cha Orange Fm nchini Marekani.
Watu wote waliokuwa wakiishi katika fukwe mbalimbali katika Jiji la New Orleans nchini Marekani walitakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo kwani tayari mamlaka ya hali ya hewa ya nchini humo (National Weather Service) ilitangaza hali ya hatari ambayo ingelipata jiji hilo pamoja na majiji mengine yaliyokuwa katika fukwe mbalimbali ikiwemo Miami.
Hakukuwa na mtu aliyepuuzia taarifa hiyo, wengi wakaanza kuondoka kwa ajili ya kuyaokoa maisha yao kwani bado kumbukumbu juu ya kimbunga cha Katrina ambacho kilipiga miezi michache iliyopita bado ziliendelea kubaki vichwani mwao.
Mitaani kulikuwa na purukushani, kila mtu alitaka kuyaokoa maisha yake. Kumbukumbu juu ya tsunami zilikuwa vichwani mwao, walisoma kwenye historia miaka ya nyuma kwamba balaa hilo liliwahi kuikumba China na Japan na matokeo yake watu wengi walifariki dunia.
Serikali ya Marekani ikaagiza magari makubwa na kuwataka watu wote waondoke katika sehemu za ufukwe na kukimbia umbali wa kilometa ishirini kutoka ufukweni kwani pasipo kufanya hivyo ilikuwa ni lazima tsunami iwakumbe na kufariki dunia.
Watu waliondoka, helkopta zilipita kila kona ndani ya jiji hilo, mtu mmoja aliyekuwa akitangaza kwenye kipaza sauti alisikika akiwaambia watu kwamba huo ulikuwa ni muda wa kuondoka, kulikimbia jiji hilo kutokana na maafa ambayo yalitarajiwa kulikumba jiji hilo, tena saa mbili zijazo.
“Where is Catherine?” (Catherine yupo wapi?) alisikika mwanamke mmoja akiuliza.
“I don’t know . She told me that she would go to James, maybe she went there (Sifahamu. Aliniambia kwamba angekwenda kwa James, labda alikwenda huko) alijibu mwanaume mmoja.
Hakutaka kujali sana, kwa kuwa aliambiwa kwamba msichana huyo alikwenda kwa mwanaume aitwaye James, hakutaka kuuliza zaidi ya kuendelea na safari yao ya kuyaokoa maisha yao kwani lilikuwa limebaki saa moja kabla ya janga hilo kulikumba Jiji la New Orleans na miji yote ambayo ilikuwa karibu na bahari.
Mamlaka ya hali ya hewa nchini Marekani haikukaa kimya, bado iliendelea kutoa onyo kwamba watu wote waliokuwa wakiishi pembezoni mwa bahari ya Atlantic walitakiwa kuondoka kwani tsunami liliendelea kuja kwa kasi kwa kipimo cha 4.11 ambacho kilikuwa ni kikubwa mno huku mawimbi yake yakiwa na urefu wa mita mia moja kwenda juu ambayo yalikuwa yakienda kwa kasi ya kilometa 2 kwa dakika tano.
Huko lilipoanzia nchini China, Thailand na nchi nyingine barani Asia, liliacha vilio, zaidi ya watu milioni mbili walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya huku makazi ya watu wengi yakiharibiwa mno.
Maafa yaliyotokea nchini China kipindi hicho waliyaona kwenye televisheni, waliogopa na kuhisi kwamba inawezekana tsunami hilo lingefika mpaka nchini Marekani kwani hata wao kulikuwa na miji ambayo ilikuwa pembezoni mwa bahari, kweli ikawa hivyo.
“Mnatakiwa kuchukua vitu vilivyokuwa muhimu kwenu, ambavyo havina umuhimu viacheni na serikali itawasaidia kwa kila kitu,” bado tangazo lilikuwa likitolewa kutoka kwa mtu aliyekuwa kwenye helkopta ambaye alitumia kipaza sauti kilichosikika vizuri kabisa na kila mtu.
Muda ulizidi kwenda mbele, dakika arobaini na tano baadaye, ukimya mkubwa ulitawala kila kona ndani ya jiji hilo, hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika, si binadamu tu bali hata wanyama hawakuwepo, watu walikimbia na kwenda katika Mji wa Gonzales uliokuwa kilometa ishirini kutoka hapo New Orleans.
“Jamani naomba mnisaidie, namtafuta binti yangu...” alisema mwanamke mmoja, kwa kumwangalia tu alionekana kuwa na hofu moyoni mwake, alikuwa akimwambia mmoja wa wanajeshi ambao waliwachukua watu kutoka New Orleans.
“Anaitwa nani?”
“Catherine, mara ya mwisho kabla tangazo halijatolewa, alikwenda kwa mpenzi wake, sijui kama yupo naye kwa sababu hata wazazi wa mpenzi wake tulionana nao wakasema kwamba hata kijana wao hayupo nao,” alisema mwanamke huyo.
Hiyo ilikuwa kazi nyingine kabisa, alichokifanya mwanajeshi huyo ni kuonana na wazazi wa huyo kijana ambaye alikuwa mpenzi wa Catherine aitwaye James na kuanza kuzungumza nao.
Kama alivyoambiwa na mama yake Catherine ndivyo alivyoambiwa hata na wazazi hao kwamba kijana wao aitwaye James hakuwa akionekana. Hiyo ikawatia hofu kwa kuhisi kwamba japokuwa mahali hapo waliona kwamba kila mtu alikuwa hapo kumbe kuna wawili ambao hawakuwa hapo.
Walichokifanya ni kuanza kuyaita majina yao kila kona kwa kupitia kipaza sauti. Kila aliyesikia, akabaki akimwangalia mwenzake kwa kuhisi labda huyo ndiye aliyekuwa akihitajika.
Zaidi ya watu milioni nne waliokuwa wamekimbia katika jiji hilo, ni watu wawili tu ndiyo ambao hawakuwa wakionekana, kwani familia zote zilikuwepo na kila moja walitimia isipokuwa familia mbili ambazo watu wawili hawakuonekana.
Tayari kukaonekana kuwa na tatizo sehemu, mwanajeshi yule akawapa taarifa wenzake kwamba watu wawili hawakuwa wakionekana mahali hapo hivyo walitakiwa kwenda kuwatafuta katika jiji hilo, hata kama kuwaita walitakiwa kufanya hivyo ilimradi wawapate na kuwaleta pale walipokuwa.
“Zimebaki dakika ngapi kabla ya Tsunami kuipiga New Orleans?” aliuliza mwanajeshi mmoja.
“Dakika ishirini!”
“Chukueni helkopta haraka muende kuwatafuta...”
Hicho ndicho kilichofanyika, hakukuwa na muda wa kupoteza mahali hapo, kwa haraka sana wanajeshi sita wakaingia katika helkopta moja kubwa na kuanza kurudi ndani ya jiji hilo kwa ajili ya kuwatafuta watu wawili tu, msichana mjauzito aliyeitwa Catherine na mwanaume aliyeitwa James.
Walipofika katika jiji hilo, wakachukua darubini na kuanza kuangalia, kila kona, hakukuwa na mtu yeyote, hakukuwa na mnyama, ni nyumba na magari machache ndivyo vilivyokuwa vimebaki.
Hawakukata tamaa, waliendelea kuwatafuta huku wakiita kwa sauti kubwa tena kwa kutumia kipaza sauti lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia au hata kutoka na kuwapungia mikono kuonyesha kwamba alitaka msaada.
Dakika ziliendelea kukatika, zilipofika dakika kumi na tisa tu, kwa mbali baharini likaanza kuonekana wimbi kubwa na zito likija kwa kasi. Waliliangalia wimbi lile, lilikuwa kubwa zaidi ya mita mia moja ambayo ilitangazwa na mamlaka ya hali ya hewa.
Lilikuwa likija kwa kasi mno na hata muungurumo wake ulikuwa mkubwa. Halikuwa likija peke yake bali lilikuwa likija na meli kadhaa kubwa zilizokuwa baharini ambazo nazo zilisombwa na tsunami hiyo.
“It is coming...it is coming...” (Linakuja...linakuja..) alisema mwanajeshi mmoja, rubani akageuza helkopta ile na kuanza kuondoka kwani kwa jinsi wimbi lile lilivyokuwa likija kwa kasi, tena huku likiwa kubwa namna ile, walijua kabisa wangeweza kupata tatizo, hivyo wakaondoka huku wakiahirisha kuwatafuta watu hao ambao ukweli wenyewe ni kwamba walikuwa hai, tena msichana Catherine akiwa kwenye uchungu mkubwa wa kujifungua mbele ya mpenzi wake, James.
UTAJIRI WENYE UCHUNGU.
Sehemu ya Kwanza.
“All people who live at the beach have to leave immediately because tsunami will come. Once you hear this announcement, tell your colleague,” (Watu wote mnaoishi katika ufukwe mnatakiwa muondoke haraka iwezekanavyo kwa sababu tsunami itakuja. Unaposikia tangazo hili mtaarifu na mwenzako,)” ilisikika sauti ya mwanamke aliyekuwa akitangaza katika Kituo cha Redio cha Orange Fm nchini Marekani.
Watu wote waliokuwa wakiishi katika fukwe mbalimbali katika Jiji la New Orleans nchini Marekani walitakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo kwani tayari mamlaka ya hali ya hewa ya nchini humo (National Weather Service) ilitangaza hali ya hatari ambayo ingelipata jiji hilo pamoja na majiji mengine yaliyokuwa katika fukwe mbalimbali ikiwemo Miami.
Hakukuwa na mtu aliyepuuzia taarifa hiyo, wengi wakaanza kuondoka kwa ajili ya kuyaokoa maisha yao kwani bado kumbukumbu juu ya kimbunga cha Katrina ambacho kilipiga miezi michache iliyopita bado ziliendelea kubaki vichwani mwao.
Mitaani kulikuwa na purukushani, kila mtu alitaka kuyaokoa maisha yake. Kumbukumbu juu ya tsunami zilikuwa vichwani mwao, walisoma kwenye historia miaka ya nyuma kwamba balaa hilo liliwahi kuikumba China na Japan na matokeo yake watu wengi walifariki dunia.
Serikali ya Marekani ikaagiza magari makubwa na kuwataka watu wote waondoke katika sehemu za ufukwe na kukimbia umbali wa kilometa ishirini kutoka ufukweni kwani pasipo kufanya hivyo ilikuwa ni lazima tsunami iwakumbe na kufariki dunia.
Watu waliondoka, helkopta zilipita kila kona ndani ya jiji hilo, mtu mmoja aliyekuwa akitangaza kwenye kipaza sauti alisikika akiwaambia watu kwamba huo ulikuwa ni muda wa kuondoka, kulikimbia jiji hilo kutokana na maafa ambayo yalitarajiwa kulikumba jiji hilo, tena saa mbili zijazo.
“Where is Catherine?” (Catherine yupo wapi?) alisikika mwanamke mmoja akiuliza.
“I don’t know . She told me that she would go to James, maybe she went there (Sifahamu. Aliniambia kwamba angekwenda kwa James, labda alikwenda huko) alijibu mwanaume mmoja.
Hakutaka kujali sana, kwa kuwa aliambiwa kwamba msichana huyo alikwenda kwa mwanaume aitwaye James, hakutaka kuuliza zaidi ya kuendelea na safari yao ya kuyaokoa maisha yao kwani lilikuwa limebaki saa moja kabla ya janga hilo kulikumba Jiji la New Orleans na miji yote ambayo ilikuwa karibu na bahari.
Mamlaka ya hali ya hewa nchini Marekani haikukaa kimya, bado iliendelea kutoa onyo kwamba watu wote waliokuwa wakiishi pembezoni mwa bahari ya Atlantic walitakiwa kuondoka kwani tsunami liliendelea kuja kwa kasi kwa kipimo cha 4.11 ambacho kilikuwa ni kikubwa mno huku mawimbi yake yakiwa na urefu wa mita mia moja kwenda juu ambayo yalikuwa yakienda kwa kasi ya kilometa 2 kwa dakika tano.
Huko lilipoanzia nchini China, Thailand na nchi nyingine barani Asia, liliacha vilio, zaidi ya watu milioni mbili walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa vibaya huku makazi ya watu wengi yakiharibiwa mno.
Maafa yaliyotokea nchini China kipindi hicho waliyaona kwenye televisheni, waliogopa na kuhisi kwamba inawezekana tsunami hilo lingefika mpaka nchini Marekani kwani hata wao kulikuwa na miji ambayo ilikuwa pembezoni mwa bahari, kweli ikawa hivyo.
“Mnatakiwa kuchukua vitu vilivyokuwa muhimu kwenu, ambavyo havina umuhimu viacheni na serikali itawasaidia kwa kila kitu,” bado tangazo lilikuwa likitolewa kutoka kwa mtu aliyekuwa kwenye helkopta ambaye alitumia kipaza sauti kilichosikika vizuri kabisa na kila mtu.
Muda ulizidi kwenda mbele, dakika arobaini na tano baadaye, ukimya mkubwa ulitawala kila kona ndani ya jiji hilo, hakukuwa na sauti yoyote iliyosikika, si binadamu tu bali hata wanyama hawakuwepo, watu walikimbia na kwenda katika Mji wa Gonzales uliokuwa kilometa ishirini kutoka hapo New Orleans.
“Jamani naomba mnisaidie, namtafuta binti yangu...” alisema mwanamke mmoja, kwa kumwangalia tu alionekana kuwa na hofu moyoni mwake, alikuwa akimwambia mmoja wa wanajeshi ambao waliwachukua watu kutoka New Orleans.
“Anaitwa nani?”
“Catherine, mara ya mwisho kabla tangazo halijatolewa, alikwenda kwa mpenzi wake, sijui kama yupo naye kwa sababu hata wazazi wa mpenzi wake tulionana nao wakasema kwamba hata kijana wao hayupo nao,” alisema mwanamke huyo.
Hiyo ilikuwa kazi nyingine kabisa, alichokifanya mwanajeshi huyo ni kuonana na wazazi wa huyo kijana ambaye alikuwa mpenzi wa Catherine aitwaye James na kuanza kuzungumza nao.
Kama alivyoambiwa na mama yake Catherine ndivyo alivyoambiwa hata na wazazi hao kwamba kijana wao aitwaye James hakuwa akionekana. Hiyo ikawatia hofu kwa kuhisi kwamba japokuwa mahali hapo waliona kwamba kila mtu alikuwa hapo kumbe kuna wawili ambao hawakuwa hapo.
Walichokifanya ni kuanza kuyaita majina yao kila kona kwa kupitia kipaza sauti. Kila aliyesikia, akabaki akimwangalia mwenzake kwa kuhisi labda huyo ndiye aliyekuwa akihitajika.
Zaidi ya watu milioni nne waliokuwa wamekimbia katika jiji hilo, ni watu wawili tu ndiyo ambao hawakuwa wakionekana, kwani familia zote zilikuwepo na kila moja walitimia isipokuwa familia mbili ambazo watu wawili hawakuonekana.
Tayari kukaonekana kuwa na tatizo sehemu, mwanajeshi yule akawapa taarifa wenzake kwamba watu wawili hawakuwa wakionekana mahali hapo hivyo walitakiwa kwenda kuwatafuta katika jiji hilo, hata kama kuwaita walitakiwa kufanya hivyo ilimradi wawapate na kuwaleta pale walipokuwa.
“Zimebaki dakika ngapi kabla ya Tsunami kuipiga New Orleans?” aliuliza mwanajeshi mmoja.
“Dakika ishirini!”
“Chukueni helkopta haraka muende kuwatafuta...”
Hicho ndicho kilichofanyika, hakukuwa na muda wa kupoteza mahali hapo, kwa haraka sana wanajeshi sita wakaingia katika helkopta moja kubwa na kuanza kurudi ndani ya jiji hilo kwa ajili ya kuwatafuta watu wawili tu, msichana mjauzito aliyeitwa Catherine na mwanaume aliyeitwa James.
Walipofika katika jiji hilo, wakachukua darubini na kuanza kuangalia, kila kona, hakukuwa na mtu yeyote, hakukuwa na mnyama, ni nyumba na magari machache ndivyo vilivyokuwa vimebaki.
Hawakukata tamaa, waliendelea kuwatafuta huku wakiita kwa sauti kubwa tena kwa kutumia kipaza sauti lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia au hata kutoka na kuwapungia mikono kuonyesha kwamba alitaka msaada.
Dakika ziliendelea kukatika, zilipofika dakika kumi na tisa tu, kwa mbali baharini likaanza kuonekana wimbi kubwa na zito likija kwa kasi. Waliliangalia wimbi lile, lilikuwa kubwa zaidi ya mita mia moja ambayo ilitangazwa na mamlaka ya hali ya hewa.
Lilikuwa likija kwa kasi mno na hata muungurumo wake ulikuwa mkubwa. Halikuwa likija peke yake bali lilikuwa likija na meli kadhaa kubwa zilizokuwa baharini ambazo nazo zilisombwa na tsunami hiyo.
“It is coming...it is coming...” (Linakuja...linakuja..) alisema mwanajeshi mmoja, rubani akageuza helkopta ile na kuanza kuondoka kwani kwa jinsi wimbi lile lilivyokuwa likija kwa kasi, tena huku likiwa kubwa namna ile, walijua kabisa wangeweza kupata tatizo, hivyo wakaondoka huku wakiahirisha kuwatafuta watu hao ambao ukweli wenyewe ni kwamba walikuwa hai, tena msichana Catherine akiwa kwenye uchungu mkubwa wa kujifungua mbele ya mpenzi wake, James.