Ngalikihinja,
Usipoishi propprtional na hela zako, hasa kama una hela halafu unaishi kama huna hela, lazima uonekane mchawi....
Hii kauli umeiweka too general unless if your target audience is Africa, kama umefika nchini Marekani kuna mji unaitwa Silicon Valley unapatikana kusini mwa eneo la San Francisco ktk jimbo la California. Huku ndiko kiini cha ugunduzi na teknolojia, ni kawaida kabisa kukutana na mtu mwenye ukwasi wenye thamani zaidi ya trilioni 10 za ki-Tanzania na anatembea kavaa flip flops, kaptura na plain t-shirt kwenda ofisini kwake kwa mfano kuna watu wanaitwa Jack Dorsey na mwenzie Biz Stone ukikutana nao mtaani utadhani wahuni wa mtaani kumbe ndo wagunduzi na watendaji wakuu wa mtandao wa Twitter . Pia kuna mtu anaitwa Gabe Newell huyu naye ni mtu mzito sana ni mwanzilishi wa kampuni ya Valve inayotengeneza video games ukikutana nae utadhani ni maskini yeye anaishi mji wa Bellevue, jiji la Waashington.
Hoja yangu hapa ni kwamba watu wenye ukwasi mkubwa wengi wao hawanaga flashy lifestyle unless labda wawe new money yaani umeupata ukwasi huna kipindi kirefu au wewe ni mtu wa sanaa au kipaji kama mpira au mwanasiasa mwizi mwizi ndo utaishi Maisha ya mbwembwe to maintain your status and fame. Matajiri walio wengi wanaishi Maisha ya kawaida as long as unapata mahitaji ya msingi huna haja ya kujionyesha kama shughuli zako hazikuhitaji kujionyesha nunua gari ambalo ni practical kukutoa mahala A kwenda mahala B labda kama wewe ni mtu unayependa magari same applies to house sio lazima uwe na lijumba kubwa kisa una pesa hata kama hulihitaji.
Tafuta kitabu kinaitwa The millionaire Next Door kimeandikwa na Thomas J. Stanley na mwenzake William D. Danko. Utashangazwa sana na watu wanavyoweza kutengeneza ukwasi mkubwa kwa ku-avoid the high life na kuwa more practical Zaidi ili kukwepa expenses zisizo za lazima ambazo zitakufanya uwe ktk endless consumption treadmill.