Utajiri wa masharti ni mateso

Utajiri wa masharti ni mateso

Ni bora ukawa na Mia mfukoni lakini umeipata kwa jasho.

Nimetembea hiyo Mikoa yote ni matajiri wachache sana wanaofurahia Pesa zao.

Lakini wengi Pesa zao ni za 'ndagu' zenye masharti lukuki ambayo ni ya kujitesa tu, Usitembee na mwanamke mwingine zaidi ya mke wako, Usivae viatu zaidi ya kandambili, Usinye choo cha nyumbani n.k

Sasa hayo ni mateso ndugu zangu , Raha Pesa uifurahie na sio ikupe Karaha.
Wewe umejuaje mkuu
 
Usitembee na mke zaidi ya mkeo
Usile nyama
Usile hotelini
Usilale gesti
Usivae nguo nzuri
Usinywe pombe
Usipeleke watoto shule za kulipia n.k n.k
Kwa masharti hayo unahitaji ndagu tena au ujinga tu
Waganga ni watu wajanja sana. Kwa masharti hayo umakuwa unabana matumizi ya fedha uliyonayo na itabaki kwenye mzunguko wa biashara tu. Utakosaje kuwa na pesa nyingi wakati unazalisha sana unakula kidogo. Tufunguke akili
 
Waganga ni watu wajanja sana. Kwa masharti hayo umakuwa unabana matumizi ya fedha uliyonayo na itabaki kwenye mzunguko wa biashara tu. Utakosaje kuwa na pesa nyingi wakati unazalisha sana unakula kidogo. Tufunguke akili
Fact mkuu, halafu mm nadhani hizi ni story tu nilishawahi fuatilia watu wanaosema Wana pesa hizi za kificho, nilichoona jamaa ni wachapakazi balaa, yaani wanafight ile mbaya ...nikawa najiuliza ni kweli yanayosemwa au ni wivu wa wanazengo Kama unapesa za masharti why ufanye kazi kwa kujituma namna hii
 
Ila mbona pale mlowo kuna kijana nae wanasema ana pesa yake niya hivyo lakini hayupo kwenye masharti ya hivyo

Ukimtazama anapiga pamba safi gari safi and coster za kumwaga mbeya tunduma

Labda hizi mambo zipo za aina tofauti sana

Ndivyo ilivyo.
 
Hapana yule dogo siyo ndagu namfahamu sana ameishi maishs magumu sana alipata mtaji baada ya kupiga udalali wa nyumba alipata around 20 mil ndo kachomoka.Kwa huko songwe king kong wa haya mandagu ni dingi mmoja wa vwawa mkinga anaitw chau.....nini sijui??
Ilasiiiii
 
Back
Top Bottom