Utafiti mpya: Lowassa aongoza tena mbio za urais

Utafiti mpya: Lowassa aongoza tena mbio za urais

Gazeti la Rostam Aziz,mkurugenzi wake Hussein Bashe ambaye nd'o mtu wa kati,kati ya Lowassa na Rostam Aziz sasa mnategemea nini hapo? Msitoke povu bure,Lowassa peke yake anaweza kuvinunua hivi vyombo vya maamuzi times and again,na kumbukeni hawa jamaa wamejipanga kivyotevyote tu,shida iliyopo ni kuwa watanzania tumezoea kurubuniwa na ni wachache wanaeeza kuona mbali.Na hata hao wachache wanaoweza kuona mbali wananunulika kuhadaika kirahisi tu,kwa ajili ya matumbo yao wapo tayari hata kushabikia upuuzi kama huu kwa sababu ya kurutubisha tu matumbo yao.

take msg inatosha
 
Huyo mwizi labda awe rais wa wala rushwa,kabla ya uchaguzi mkuu tutaskia na kuona kila aina ya vimbwanga vya tafiti uchwara.gazeti la rai linamilikiwa na rostam hatutarajii jipya
 
kwani hamjui kuwa RAI ni miongoni mwa magazeti ya Lowasa?
It's true.

New habari corporation, ambayo ndiyo inayomiliki magazeti ya Mtanzania na Rai, wamiliki wake wakubwa ni Rostam Aziz,ambaye ndiye mwenye hisa nyingi, na anayefuatia kwa hisa nyingi ni huyo mzee wa mamvi.

Kwa hiyo haishangazi hata kidogo, kwa gazeti hilo la Rai, kumpandisha chati na kujipendekeza kwa bosi wao, mzee wa mamvi, kwa kuchapisha hizo tafiti ambazo hazina tofauti na uliokuwa utabiri wa mnajimu, Marehemu Sheikh Yahya!
 
lengo lako ni kuuza gazeti au? kama umeweza kusema hayo kwa nini usiseme yote? kwa nini usingekaa kimya tu ili watu wasome hilo RAI?


Kama yeye sio mhusika alishindwa nini kuwataja wahusika?.Kwanza hata huo niudhaifu unatosha kumpiga chini kwa sabb nimnafiki,muoga,mficha wezi wenzie na sio mzarendo! Safari hii nizamu ya Ukawa hatutakuwa tayari kuongozwa nawalanguzi
 
Hata hao mnaompigia kampeni mnatofauti gani namkewake Kama hela ya kuhemea Mboga na unga,kuvaa na kunywa anawapa yeye kwanini msiitwe wakezake?Amewaahidi vyeo kwanini msiitwe michepuko yake?.Wanaume wazima mnaishi kwa kukinga bakuri kwanini msiitwe wakezake?
 
wakuu mbona wabishi nyinyi na manakataa ukweli, mbona lipo wazi kuwa LOWASSA kwa CCM hana MPINZANI?
Msiwe kama Yule ndege anayeficha kichwa na kuacha ------ nje!
 
It's true.

New habari corporation, ambayo ndiyo inayomiliki magazeti ya Mtanzania na Rai, wamiliki wake wakubwa ni Rostam Aziz,ambaye ndiye mwenye hisa nyingi, na anayefuatia kwa hisa nyingi ni huyo mzee wa mamvi.

Kwa hiyo haishangazi hata kidogo, kwa gazeti hilo la Rai, kumpandisha chati na kujipendekeza kwa bosi wao, mzee wa mamvi, kwa kuchapisha hizo tafiti ambazo hazina tofauti na uliokuwa utabiri wa mnajimu, Marehemu Sheikh Yahya!

Hiyo kampuni ya New Habari Co. Inamilikiwa na Rostam Aziz 100% wala hana share na mtu... tatizo inatumika na mtandao wa walanguzi wa rasilimali za taifa.
 
Atachaguliwa na mke wake siyo watanzania kama anavyodhani wanakaa wanapika utafiti halafu wanapotosha watu.


Wewe na familia yako ndo hamtamchagua lowassa ila watanzania tuliowengi tunaiman nae....
 
Alafu mimi tu niseme kitu kimoja,,kwa upande wa Ccm,akipandishwa lowasa kuwania urais hata wapinzani watagawanyika! huo ndo ukweli jamaa anakubalika hata mkiweka promo za kumchafua mnajisumbua!!!
 
Alafu mimi tu niseme kitu kimoja,,kwa upande wa Ccm,akipandishwa lowasa kuwania urais hata wapinzani watagawanyika! huo ndo ukweli jamaa anakubalika hata mkiweka promo za kumchafua mnajisumbua!!!

Mkuu na hili ni baada ya wananchi kushtukia kwamba lowassa alionewa ndio wakaamuwa kuonyesha kwamba bado wanamuhitaji atuvushe hapa tulipo.Lowassa kanyaga baba kanyaga twende
 
Utafiti wa Urais uliochapishwa na gazeti la Rai linalomilikiwa na Rostam Azizi unaoonesha Lowassa anaongoza kwa 52% akifuatiwa na Dr Slaa na January Makamba umetajwa kuwa ni kiinimacho na hadaa kwa watanzania, imebainika.

Utafiti huu uliokataliwa na wahariri wa magazeti karibu yote kuandikwa inasemekana inayokana mapungufu yafuatayo ambayo hayakupata majibu kutoka kwa waandaaji :-

1.Umeandaliwa na vijana was Lowassa wanaofanya kazi mtandaoni.

2.Kura ilikua haina ukomo, unaweza kupiga mara nyingi uwezavyo

3.Vijana wa Lowassa waliandaliwa utaratibu wa kupiga kura usiku na mchana ili tu mgombea wao aongoze kwa mbali sana.

4.Admin au muendeshaji wa kura hiyo alikua na mamlaka ya kuingia na kutazama na hata kudhibiti nani aendelee kuongoza na nani afuatie.

5.Dr Slaa ametengenezwa aonekane anafuatia nyuma ya Lowassa ili ionekane kuwa CCM isipomsimamisha Lowassa basi wapinzani watachukua nchi.

Baada ya waandishi na wahariri wote kukataa kuchapisha Utafiti huo wa hovyo wakihoji nani kauandaa na ulipimwa kwa vigezo gani vya kisayansi, ni gazeti la Rai pekee linalomilikiwa na Rostam Azizi, rafiki mkubwa wa Lowassa ndilo pekee limechapisha habari hiyo.
Lowassa ajajitekenya na kucheka mwenyewe.
 
Ifikie wakati sasa wahariri watueleze ukweli. Lowasa ni fisadi ambaye fedha zake zinamuwasha mwili mzima
 
Kama Lowassa aliweza kupika habari na kumlisha maneno Mkapa kuwa ameongea na CITIZEN TV ya Kenya kuhusu nani anayeona anafaa kugombea Urais mwakani atashindwa nini kwa sasa? akamlisha maneno mkapa kuwa "....Maana tuhuma zingine upuuzi kweli kweli"...
 
Back
Top Bottom