Utabiri: Tanzania kwenda total lockdown mwezi April

Utabiri: Tanzania kwenda total lockdown mwezi April

Ndugai kwenye kikao cha jana kawaasa wabunge wawe makini na maamuzi ya lockdown sababu amekiri hatuna kiburi cha lockdown jee utabiri wako vp

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwani Ndugai ndiyo nani? Angekuwa Mungu sawa. Lakini kama ni huyu kazi ndugai, basi ya kwake tupa kule.

Tusubirie May 1. Kwani ni mbali basi?
 
Mtabiri naanza kuamini maneno yako..Mana kwa wenzetu huko Uganda Hali ya lockdown imeshaanza.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu maneno ya Ramaphosa ni ya muhimu sana: "lockdown haiepukiki. Inavyocheleshwa gharama kwa hasara ya maisha ya watu na katika hali zote itakuwa kubwa zaidi".

Hakuna faida yoyote kwenye kuchelewesha lockdown.

Ni aibu kuwa bunge linaendelea na posho zinalipwa. Posho hizi zingesaidia support kwenye lockdown.

Bunge kuendelea ni mfano mbaya kabisa katika hali ya sasa.

Hatupaswa kuendekeza mikusanyiko yoyote kwa jina lolote kwa sasa.
 
Mwanzisha mada angalia kwenye historia ya ukoo wenu kama mna gwiji wa uchawi. Si bure amekurithisha bila kujijua.wewe ni msukule.
 
kujifungia ndani ni solution ndio ila sio solution pekee, kwani ukimwi ulivyoingia bongo watu waliacha kufanya mapenzi? Cha muhimu ni kuchukua tu precautions, lockdown tutakula nini sio kila mtu ana uwezo wa kuweka stock kubwa ya nusu mwaka

Sent using Jamii Forums mobile app

mkuu tofautisha ukimwi na corona , lakini pia nakuunga mkono sio kila mtu anaweza kukaa ndani, kwa mfano mimi chakula changu kila siku ni cha kununua lazima nitoke mara 3 kwa siku


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lockdown alafu tule Nini? Tubun njia mbadala

Sent using Jamii Forums mobile app


Mkuu, hili limeelezwa kinaga ubaga mara nyingi kweli kweli.

Waliolileta mwanzo, wameelewa ndiyo maana wameunga mkono juhudi.

Hukuona mabandiko yaliyokuwa yakionyesha tutakachokula pamoja vipi hakuna atakaye kufa njaa?

Kama hukuona sema tukurejeshee tena mabandiko hayo.
 
Naona umeanza mafumbo mkuu.

Kumbe Android alikoroga mambo. Nilimaanisha hivi:

"Nasita kukurejea kama mkuu. Ila umerukia treni kwa mbele.

Vipi umenusurika lakini?"

Hapana fumbo hapo - kila kitu wazi wazi.
 
Kumbe Android alikoroga mambo. Nilimaanisha hivi:

"Nasita kukurejea kama mkuu. Ila umerukia treni kwa mbele.

Vipi umenusurika lakini?"

Hapana fumbo hapo - kila kitu wazi wazi.
Oh ok ngoja niondoke mbele ya treni.
 
lockdown haitakaa iwepo tanzania, huko Italy na Marekani vifo vimeanza kupungua, wiki mbili zijazo corona itabaki historia
 
Mwanzisha mada angalia kwenye historia ya ukoo wenu kama mna gwiji wa uchawi. Si bure amekurithisha bila kujijua.wewe ni msukule.

Ila wewe siyo msukule? Ama kweli ajidhaniaye amesimama.
 
Back
Top Bottom