Usiogope wanavyomshangilia

Usiogope wanavyomshangilia

IDD Amini alikua na mabaya yake mengi lakini pia mengi dhidi yake yalikua ni propaganda chafu na uwongo dhidi yake kama hilo la kula nyama za watu. Hiyo movie The Last King Of Scotland ina exaggerations nyiingi tu zingine kweli zingine uongo. Kama ni kupata tuzo nyingi inaeleweka nchi za magharibi hazikumpenda kabisa mtu huyu na wazungu wakikuchukia mambo yako yote huwa mabaya na atakaekuchafua watampa tuzo lukuki. Wapo watu Uganda tena kwa mamilioni wanamkumbuka kwa mazuri Idd Amini Dadda
Kwa hiyo unataka kusema nini, tumpende Idi Amin hata anapotaka kumwua Lissu?
 
UNAUMIA JINSI WANAVYOMSHANGILIA? NISIKILIZE MIMI.

Baada ya Idd Amin kumpindua aliyekuwa Rais wa Uganda (Milton Obote) kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende.

Inaaminika kuwa kati ya Madikteta wataalamu katika ushawishi ni pamoja na Idd Amin Dadaa,
Alikuwa ana uwezo wa ajabu sana katika kupepeta mdomo huku akijiamini sana.

Ghafla wananchi wa Uganda walianza kumpenda na kumuona mkombozi wao, kila aliyeinuka kumpinga alitengenezewa propaganda za uongo na hatimaye kuonekana sio mzalendo.

Yeyote aliyesimama kumkanusha wananchi walikuwa tayari kumpiga hata mawe.

Kwakuwa alitengeneza mazingira ya kusikilizwa yeye peke yake ilikuwa rahisi kwake kusema uongo.

Alitunga uongo mwingi na kuumwaga kwa wananchi ili wampende huku akimzuia yeyote kuinuka kwa lengo la kumkanusha.

Hata pale wasomi walipoonya kuhusu masuala kadhaa hususani ya kiuchumi waligeuka kuwa maadui zake.

Mfano ni pale alipomuua gavana wa Benki kuu kwa kosa la kumwambia kuwa fedha hamna na hali ya uchumi ni mbaya.

Katika kutafuta uungwaji mkono na wananchi alidiriki hata kutengeneza matatizo na kuyatatua ili aonekane ni Rais anayejali.

Kwa mfano anapokuwa kwenye ziara zake humuandaa mtu atakayedanganya kuwa ni mgonjwa alafu anamlilia akiomba msaada kwa Rais na hapo utamuona Idd Amin anaandika cheki hapo hapo na kumpatia akatibiwe kumbe yote ni maigizo.

Katika matukio kama hayo wananchi hujikuta wanamshangilia huku wakimuona ni mwenye huruma.

Wakati mwingine alikuwa anawaua baadhi ya wapinzani wake hata wale waliokuwa waandamizi kwenye serikali yake huku akiwa wa kwanza kumwaga machozi wakati wa misiba ya aliowaua.

Mfano ni Pale alipomuua waziri wake wa Afya na kisha kulia machozi huku akitangaza kiama kwa waliofanya tukio lakini baadae ilibainika kuwa kichwa cha waziri huyo kilikuwa kwenye Jokofu la Amin huko kwake. Yaani amemla nyama.

Pamoja na propaganda zote na maigizo kibao bado wapo watu waliokuwa ni waaminifu kwa Milton Obote wakiwemo maaskari na wanajeshi pia...

THE LAST KING OF SCOTLAND...

Hii ni Movie iliyoigiza maisha ya Idd Amin na kupata tuzo nyingi kuliko movie zote zilizomuigiza Amin kwani ilikuwa ni kama uhalisia kwa wale waliowahi kumfahamu Idd Amin Dadaa.

Movie hii ina kijana aliyeitwa Nicholas Gharigan ambaye anakuja Uganda kujitolea kufanya huduma ya kidaktari katika nchi maskini za Afrika.

Alipotua Uganda anapokelewa na Daktari mwingine ambaye anakuwa kama mwenyeji wake kwani japokuwa naye pia ni mzungu lakini yeye ameshalowea kwa muda kiasi ndani ya Uganda naye akitoa huduma za tiba.

Wakiwa kwenye pitapita zao wakakutana na watu wakiwa wanajiandaa kwa kuimba nyimbo na shamrashamra kibao.

Dr Nicholaus Gariggan akamuuliza mwenyeji wake. Kulikoni?

Alijibiwa kuwa wanajiandaa kumpokea Rais Amin kwani anakuja hapo kijijini siku hiyo.

Dr Garigan aliomba wabaki kidogo ili nao wamuone huyo Amin.

Baada ya muda kidogo Gari nyingi zilianza kuingia pale huku watu wakimwagika kwa nderemo na vifijo huku vumbi likitimka kwa nyimbo na kucheza.
Ngoma zilisikika huku msafara wa magari ukiendelea kumiminika.

Baadae Jitu kubwa, Refu,Jeusi lililovalia mavazi ya Kijenerali wa Jeshi lilipanda jukwaani huku likishangiliwa kwa nguvu mnooo....

Uganda hoyeeeeeeee
Hoyeeeeeeee...

Ni sauti ya Amin akiwasalimu watu wa kijiji kile.

Butwaa lilimshika Dr Garigan ambaye ilibidi amuulize mwenyeji wake...

"Hivi wanampenda sana huyu Raisi eeenh"

Jibu alilojibiwa ni kwamba...

"Hata Obote akija wanamshangilia hivi hivi"

Hivyo basi...


USISHTUSHWE NA JINSI WANAVYOMSHANGILIA!
SOUR GRAPES.
 
Mr haambiliki naye na Idd Amin hawachekani.. Kila sehemu anayoenda lazima waandaliwe watu wa kumweleza matatizo yao naye hujifanya anayatatua palepale
 
Mr haambiliki naye na Idd Amin hawachekani.. Kila sehemu anayoenda lazima waandaliwe watu wa kumweleza matatizo yao naye hujifanya anayatatua palepale
Ujanja wa 1970's yeye ndo anaapply miaka hii.. MTU wa ajabu sana, anadhani sote ni wajinga hatujui janja yake, no wonder anaogopa hata kusema anajenga SGR kwa mkopo.
 
Back
Top Bottom