Usiogope wanavyomshangilia

Usiogope wanavyomshangilia

"The challenge of leadership is to be strong, but not rude; be kind, but not weak; be bold, but not bully; be thoughtful, but not lazy; be humble, but not timid; be proud, but not arrogant; have humor, but without folly." - Jim Rohn
 
Tuombe Mungu tusifike huko........maana visa vya Iddi Amin jamani sikieni tu, msiombe kuona.
 
Hukuwahi kuongea na Mayunga privately. Yeye mwenyewe alikuwa mtata pamoja na kwamba alikuwa kamanda wangu mzuri sana kwenye uhamasishaji. Na hili nakubaliana na wewe kwamba wakati wa vita kama vile wakati mwingine wowote wa shughuli ngumu, kuna slogans lazima zitumike katika kufairji na kutia hamasa. Joka kuu is something else kama nduli etc zenye lengo la kutukana kwa lengo lakuondoa nyongo chungu mioyoni mwa watu.

Lakini, ulishawahi kusikia kuna watu wanakula nyama za binadamu katika ulimwengu huu huu, tabia ambayo si ya kawaida lakini inafanyika kutokaa na vichocheo vya nguvu?

Vitani yanatokea mengi, sitaki kuyasema kwanza ni muda mrefu. Unaweze kuamini kuna mahala watu wanamkamata mateka wanawambia akate nyama yake kutoka paja lake mwenyewe atengeneze nyama choma yake mwenyewe?

Watu wana hulka nyingi. Huwezi kukataa tu kwa sababu unakataa pale mtu katili anaposemekana kufanay ukatili usiouwazia wewe? Unaweza kukanusha kwamba kwenye jokofu la idi amini kulikuwa vichwa vya binadamu? Tabia hii haifanywi na mtu wa kawaida. Na kama anaweza kufnya hili, bila shaka anauwezo usiompaka wa kufanya ushetani mwingie wowote. Sikuwepo akila nyama za watu lakini mazingira yanatengeneza mwelekeo chanya kwenye hizi allegations. Or else wewe ulikuwa miongoni mwa kikosi chamauaji cha huyu jamaa ambaye unajua alikuwa akifanya nini na miili ya watu wale walikuwa wakipotea mysteriously. La sivyo huwezi kukanusha kwa kuwa hujui.
Nikweli sikuwahi kuongea privately na Major General Silas Mayunga ingawa nilimfahamu mara tu alipoteuliwa kua katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro na mimi nilikua mkoani humo tukafamiana kwa kawaida tu. Ni kweli pia alikua 'mtata' ( yaani mtamaduni hasaa, nadhani naeleweka).
Lakini hapa sasa tukubaliane kutokukubaliana. Inawezekana uliongea nae privately akakwambia alivokwambia na inawezekana pia ikawa ni kweli, lakini kwa namna hiyo watu tumeambiwa meengi sana kuhusu viongozi wetu. Kuna kiongozi mmoja aliwahi kunambia privately kua kiongozi mmoja hapa nchini alisaini hati chache sana za watu waliohukumiwa kunyongwa ili hukumu hiyo itekelezwe juu yao. Kwamba alikua haipendi hukumu ya kifo! Lakini jamaa akanambia kiongozi huyo alipoteza na kauwa watu wengi sana kimyakimya na akatoa maelezo meengi sana! Mimi mpaka leo sijamuamini na siwezi kumuamini sababu sikuweza wala sikua na namna ya kuthibitisha, niliona ni porojo tu
Nakubaliana na wewe pia vitani kuna ukatili wa ajabu sana na wakinyama hasa! Lakini hiyo ndio vita, ukishasema vitani basi hakuna ubinaadamu na uongo pia unakua mwingi kwakweli na Mungu Atuepushe na vita, ila sasa propaganda zinazoendeshwa ni mbinu za kummaliza adui
 
wewe bwana mwongo nchi za magharibi hazikumchukia Amin mana zilimwona ndiye haswaa angeweza kupambana na Nyerere mcomunisti na ndo maana Uingereza ilimsaidia pia wakati wa vita ya Kagera
Nchi za Magharibi hazikumchukia Amini!? U need to read and research more. Support gani Uingereza ilitoa kwa Uganda wakati ule? Kama ni msaada labda waliwauzia silaha kama mabeberu wafanyavyo popote kwenye vita, pande zote zinazopigana zinaweza kuuziwa silaha na kampuni moja. Kwa taarifa yako pamoja na tofauti za kiitikadi kati ya Tanzania ya Nyerere na nchi za Magharibi walikua wakimheshimu sana sana Mwalimu na hawakujiunga na Amini kuipiga Tanzania
 
UNAUMIA JINSI WANAVYOMSHANGILIA? NISIKILIZE MIMI.

Baada ya Idd Amin kumpindua aliyekuwa Rais wa kwanza wa Uganda (Milton Obote) kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende.

Inaaminika kuwa kati ya Madikteta wataalamu katika ushawishi ni pamoja na Idd Amin Dadaa,
Alikuwa ana uwezo wa ajabu sana katika kupepeta mdomo huku akijiamini sana.

Ghafla wananchi wa Uganda walianza kumpenda na kumuona mkombozi wao, kila aliyeinuka kumpinga alitengenezewa propaganda za uongo na hatimaye kuonekana sio mzalendo.

Yeyote aliyesimama kumkanusha wananchi walikuwa tayari kumpiga hata mawe.

Kwakuwa alitengeneza mazingira ya kusikilizwa yeye peke yake ilikuwa rahisi kwake kusema uongo.

Alitunga uongo mwingi na kuumwaga kwa wananchi ili wampende huku akimzuia yeyote kuinuka kwa lengo la kumkanusha.

Hata pale wasomi walipoonya kuhusu masuala kadhaa hususani ya kiuchumi waligeuka kuwa maadui zake.

Mfano ni pale alipomuua gavana wa Benki kuu kwa kosa la kumwambia kuwa fedha hamna na hali ya uchumi ni mbaya.

Katika kutafuta uungwaji mkono na wananchi alidiriki hata kutengeneza matatizo na kuyatatua ili aonekane ni Rais anayejali.

Kwa mfano anapokuwa kwenye ziara zake humuandaa mtu atakayedanganya kuwa ni mgonjwa alafu anamlilia akiomba msaada kwa Rais na hapo utamuona Idd Amin anaandika cheki hapo hapo na kumpatia akatibiwe kumbe yote ni maigizo.

Katika matukio kama hayo wananchi hujikuta wanamshangilia huku wakimuona ni mwenye huruma.

Wakati mwingine alikuwa anawaua baadhi ya wapinzani wake hata wale waliokuwa waandamizi kwenye serikali yake huku akiwa wa kwanza kumwaga machozi wakati wa misiba ya aliowaua.

Mfano ni Pale alipomuua waziri wake wa Afya na kisha kulia machozi huku akitangaza kiama kwa waliofanya tukio lakini baadae ilibainika kuwa kichwa cha waziri huyo kilikuwa kwenye Jokofu la Amin huko kwake. Yaani amemla nyama.

Pamoja na propaganda zote na maigizo kibao bado wapo watu waliokuwa ni waaminifu kwa Milton Obote wakiwemo maaskari na wanajeshi pia...

THE LAST KING OF SCOTLAND...

Hii ni Movie iliyoigiza maisha ya Idd Amin na kupata tuzo nyingi kuliko movie zote zilizomuigiza Amin kwani ilikuwa ni kama uhalisia kwa wale waliowahi kumfahamu Idd Amin Dadaa.

Movie hii ina kijana aliyeitwa Nicholas Gharigan ambaye anakuja Uganda kujitolea kufanya huduma ya kidaktari katika nchi maskini za Afrika.

Alipotua Uganda anapokelewa na Daktari mwingine ambaye anakuwa kama mwenyeji wake kwani japokuwa naye pia ni mzungu lakini yeye ameshalowea kwa muda kiasi ndani ya Uganda naye akitoa huduma za tiba.

Wakiwa kwenye pitapita zao wakakutana na watu wakiwa wanajiandaa kwa kuimba nyimbo na shamrashamra kibao.

Dr Nicholaus Gariggan akamuuliza mwenyeji wake. Kulikoni?

Alijibiwa kuwa wanajiandaa kumpokea Rais Amin kwani anakuja hapo kijijini siku hiyo.

Dr Garigan aliomba wabaki kidogo ili nao wamuone huyo Amin.

Baada ya muda kidogo Gari nyingi zilianza kuingia pale huku watu wakimwagika kwa nderemo na vifijo huku vumbi likitimka kwa nyimbo na kucheza.
Ngoma zilisikika huku msafara wa magari ukiendelea kumiminika.

Baadae Jitu kubwa, Refu,Jeusi lililovalia mavazi ya Kijenerali wa Jeshi lilipanda jukwaani huku likishangiliwa kwa nguvu mnooo....

Uganda hoyeeeeeeee
Hoyeeeeeeee...

Ni sauti ya Amin akiwasalimu watu wa kijiji kile.

Butwaa lilimshika Dr Garigan ambaye ilibidi amuulize mwenyeji wake...

"Hivi wanampenda sana huyu Raisi eeenh"

Jibu alilojibiwa ni kwamba...

"Hata Obote akija wanamshangilia hivi hivi"

Hivyo basi...


USISHTUSHWE NA JINSI WANAVYOMSHANGILIA!
mkuu...wacha watu waendelee kumkenulia meno ngedere.

yatakapoanza kuwasibu ndipo wataelewa, lakini by then itakuwa too little too late!
 
Yule alianza kutumia mitama na kupiga roba enzi za JK akapewa tabasamu na cheo cha ukuu wa wilaya. Walimchekea bila kumuonya walipendezwa na kitendo.

Ameshika bunduki ananyemelea kuwa waziri wa mambo ya ndani. Ndio njia zake maana vyeti hana.
....maana yake watawala tulionao ndio style wanazopenda kututawala kihalifu
 
1. Serikali hii ya JK Ni dhaifu, nchi inahitaji Raisi dikteta ili isonge mbele - Mnyika

2. Nchi inahitaji Raisi anayeweza kufanya maamuzi magumu bila woga- Mbowe

3. Tunamuhitaji rais mwenye uwezo wa kukemea wasaidizi wake Na wakamtii- Lema


Sasa mnalalamika nn was....nge nini??
...wewe unaamini huyu anakemea wasaidizi wake?/ anachofanya nikukemea asiowapenda
 
1. Serikali hii ya JK Ni dhaifu, nchi inahitaji Raisi dikteta ili isonge mbele - Mnyika

2. Nchi inahitaji Raisi anayeweza kufanya maamuzi magumu bila woga- Mbowe

3. Tunamuhitaji rais mwenye uwezo wa kukemea wasaidizi wake Na wakamtii- Lema


Sasa mnalalamika nn was....nge nini??

Serikali hii ya JK Ni dhaifu, nchi inahitaji Raisi dikteta ili isonge mbele - Mnyika
- Kwa hiyo hii inasonga mbele au inarudi nyuma?
  • Bei ya sukari ikoje,
  • biashara na uwekezaji umeongezeka au unapungua? Uwekezaji kutoka nje umepungua kwa zaidi ya asilimia 9;
  • kasi ya kufunga maduka hapa nchini haijawahi kutokea tangu Tanzania kuwepo;
  • Udhaifu wa sarafu yetu umeendelea kuwepo; Malory zaidi ya asilimia 35 hayana kazi baada ya kukosa mizigo ya kusafirisha,

2. Nchi inahitaji Raisi anayeweza kufanya maamuzi magumu bila woga- Mbowe
- Ila hayo maamuzi yafanyike baada ya tafakuri ya kina ili yalete tija. Unaweza vipi kuanzisha miradi lukuki ya fedha nyingi ambazo huna na wakati huo huo unawadanganya wananchi kuwa miradi hiyo inagharamiwa kwa fedha za ndani?

3. Tunamuhitaji rais mwenye uwezo wa kukemea wasaidizi wake Na wakamtii- Lema
- Amemkemea nani? Kudhalilisha viongozi mbele ya wananchi ni kuwakemea? Vitendo vya DAB vinalalamikiwa na wengi amefanya nini?

Tumuunge rais kwa yale mazuri anayofanya lakn siyo kila kitu anafanya sawa. Anataka kuleta chembechembe za ubaguzi kwa wananchi wake, hili tulipinge kwa kulipigia kelele. Atafakari kabla ya kusema, aache kuongea uwongo, afuate katiba, miongozo, sheria na taratibu ili nchi isonge mbele

Pia akubali kukosolewa, kukosea sio dhambi wala kukosolewa sio dhambi.
 
UNAUMIA JINSI WANAVYOMSHANGILIA? NISIKILIZE MIMI.

Baada ya Idd Amin kumpindua aliyekuwa Rais wa Uganda (Milton Obote) kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende.

Inaaminika kuwa kati ya Madikteta wataalamu katika ushawishi ni pamoja na Idd Amin Dadaa,
Alikuwa ana uwezo wa ajabu sana katika kupepeta mdomo huku akijiamini sana.

Ghafla wananchi wa Uganda walianza kumpenda na kumuona mkombozi wao, kila aliyeinuka kumpinga alitengenezewa propaganda za uongo na hatimaye kuonekana sio mzalendo.

Yeyote aliyesimama kumkanusha wananchi walikuwa tayari kumpiga hata mawe.

Kwakuwa alitengeneza mazingira ya kusikilizwa yeye peke yake ilikuwa rahisi kwake kusema uongo.

Alitunga uongo mwingi na kuumwaga kwa wananchi ili wampende huku akimzuia yeyote kuinuka kwa lengo la kumkanusha.

Hata pale wasomi walipoonya kuhusu masuala kadhaa hususani ya kiuchumi waligeuka kuwa maadui zake.

Mfano ni pale alipomuua gavana wa Benki kuu kwa kosa la kumwambia kuwa fedha hamna na hali ya uchumi ni mbaya.

Katika kutafuta uungwaji mkono na wananchi alidiriki hata kutengeneza matatizo na kuyatatua ili aonekane ni Rais anayejali.

Kwa mfano anapokuwa kwenye ziara zake humuandaa mtu atakayedanganya kuwa ni mgonjwa alafu anamlilia akiomba msaada kwa Rais na hapo utamuona Idd Amin anaandika cheki hapo hapo na kumpatia akatibiwe kumbe yote ni maigizo.

Katika matukio kama hayo wananchi hujikuta wanamshangilia huku wakimuona ni mwenye huruma.

Wakati mwingine alikuwa anawaua baadhi ya wapinzani wake hata wale waliokuwa waandamizi kwenye serikali yake huku akiwa wa kwanza kumwaga machozi wakati wa misiba ya aliowaua.

Mfano ni Pale alipomuua waziri wake wa Afya na kisha kulia machozi huku akitangaza kiama kwa waliofanya tukio lakini baadae ilibainika kuwa kichwa cha waziri huyo kilikuwa kwenye Jokofu la Amin huko kwake. Yaani amemla nyama.

Pamoja na propaganda zote na maigizo kibao bado wapo watu waliokuwa ni waaminifu kwa Milton Obote wakiwemo maaskari na wanajeshi pia...

THE LAST KING OF SCOTLAND...

Hii ni Movie iliyoigiza maisha ya Idd Amin na kupata tuzo nyingi kuliko movie zote zilizomuigiza Amin kwani ilikuwa ni kama uhalisia kwa wale waliowahi kumfahamu Idd Amin Dadaa.

Movie hii ina kijana aliyeitwa Nicholas Gharigan ambaye anakuja Uganda kujitolea kufanya huduma ya kidaktari katika nchi maskini za Afrika.

Alipotua Uganda anapokelewa na Daktari mwingine ambaye anakuwa kama mwenyeji wake kwani japokuwa naye pia ni mzungu lakini yeye ameshalowea kwa muda kiasi ndani ya Uganda naye akitoa huduma za tiba.

Wakiwa kwenye pitapita zao wakakutana na watu wakiwa wanajiandaa kwa kuimba nyimbo na shamrashamra kibao.

Dr Nicholaus Gariggan akamuuliza mwenyeji wake. Kulikoni?

Alijibiwa kuwa wanajiandaa kumpokea Rais Amin kwani anakuja hapo kijijini siku hiyo.

Dr Garigan aliomba wabaki kidogo ili nao wamuone huyo Amin.

Baada ya muda kidogo Gari nyingi zilianza kuingia pale huku watu wakimwagika kwa nderemo na vifijo huku vumbi likitimka kwa nyimbo na kucheza.
Ngoma zilisikika huku msafara wa magari ukiendelea kumiminika.

Baadae Jitu kubwa, Refu,Jeusi lililovalia mavazi ya Kijenerali wa Jeshi lilipanda jukwaani huku likishangiliwa kwa nguvu mnooo....

Uganda hoyeeeeeeee
Hoyeeeeeeee...

Ni sauti ya Amin akiwasalimu watu wa kijiji kile.

Butwaa lilimshika Dr Garigan ambaye ilibidi amuulize mwenyeji wake...

"Hivi wanampenda sana huyu Raisi eeenh"

Jibu alilojibiwa ni kwamba...

"Hata Obote akija wanamshangilia hivi hivi"

Hivyo basi...


USISHTUSHWE NA JINSI WANAVYOMSHANGILIA!
Nimekuelewa
 
Hata mimi nilikuwepo!
Kama ulikuwepo basi lazima utafahamu kuwa makala imejaa uzushi na uongo wa kibavicha. Mimi wakati huo nilikuwa kidato cha nne kwa hiyo nilikuwa tayari najifahamu kiakili. Iddi Amin hakuwa na "kazi kubwa kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende". Tangu siku ya kwanza ya mapinduzi watu walimwagika mtaani kushangilia kwa sababu Obote tayari alishapoteza imani ya wananchi. Mambo yalikuja kuharibika baadaye. Kama na wewe ulikuwepo nipo tayari hapa. Sida ganywi na uongo wa kitoto.
 
Back
Top Bottom