Nikweli sikuwahi kuongea privately na Major General Silas Mayunga ingawa nilimfahamu mara tu alipoteuliwa kua katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro na mimi nilikua mkoani humo tukafamiana kwa kawaida tu. Ni kweli pia alikua 'mtata' ( yaani mtamaduni hasaa, nadhani naeleweka).Hukuwahi kuongea na Mayunga privately. Yeye mwenyewe alikuwa mtata pamoja na kwamba alikuwa kamanda wangu mzuri sana kwenye uhamasishaji. Na hili nakubaliana na wewe kwamba wakati wa vita kama vile wakati mwingine wowote wa shughuli ngumu, kuna slogans lazima zitumike katika kufairji na kutia hamasa. Joka kuu is something else kama nduli etc zenye lengo la kutukana kwa lengo lakuondoa nyongo chungu mioyoni mwa watu.
Lakini, ulishawahi kusikia kuna watu wanakula nyama za binadamu katika ulimwengu huu huu, tabia ambayo si ya kawaida lakini inafanyika kutokaa na vichocheo vya nguvu?
Vitani yanatokea mengi, sitaki kuyasema kwanza ni muda mrefu. Unaweze kuamini kuna mahala watu wanamkamata mateka wanawambia akate nyama yake kutoka paja lake mwenyewe atengeneze nyama choma yake mwenyewe?
Watu wana hulka nyingi. Huwezi kukataa tu kwa sababu unakataa pale mtu katili anaposemekana kufanay ukatili usiouwazia wewe? Unaweza kukanusha kwamba kwenye jokofu la idi amini kulikuwa vichwa vya binadamu? Tabia hii haifanywi na mtu wa kawaida. Na kama anaweza kufnya hili, bila shaka anauwezo usiompaka wa kufanya ushetani mwingie wowote. Sikuwepo akila nyama za watu lakini mazingira yanatengeneza mwelekeo chanya kwenye hizi allegations. Or else wewe ulikuwa miongoni mwa kikosi chamauaji cha huyu jamaa ambaye unajua alikuwa akifanya nini na miili ya watu wale walikuwa wakipotea mysteriously. La sivyo huwezi kukanusha kwa kuwa hujui.
Nchi za Magharibi hazikumchukia Amini!? U need to read and research more. Support gani Uingereza ilitoa kwa Uganda wakati ule? Kama ni msaada labda waliwauzia silaha kama mabeberu wafanyavyo popote kwenye vita, pande zote zinazopigana zinaweza kuuziwa silaha na kampuni moja. Kwa taarifa yako pamoja na tofauti za kiitikadi kati ya Tanzania ya Nyerere na nchi za Magharibi walikua wakimheshimu sana sana Mwalimu na hawakujiunga na Amini kuipiga Tanzaniawewe bwana mwongo nchi za magharibi hazikumchukia Amin mana zilimwona ndiye haswaa angeweza kupambana na Nyerere mcomunisti na ndo maana Uingereza ilimsaidia pia wakati wa vita ya Kagera
mkuu...wacha watu waendelee kumkenulia meno ngedere.UNAUMIA JINSI WANAVYOMSHANGILIA? NISIKILIZE MIMI.
Baada ya Idd Amin kumpindua aliyekuwa Rais wa kwanza wa Uganda (Milton Obote) kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende.
Inaaminika kuwa kati ya Madikteta wataalamu katika ushawishi ni pamoja na Idd Amin Dadaa,
Alikuwa ana uwezo wa ajabu sana katika kupepeta mdomo huku akijiamini sana.
Ghafla wananchi wa Uganda walianza kumpenda na kumuona mkombozi wao, kila aliyeinuka kumpinga alitengenezewa propaganda za uongo na hatimaye kuonekana sio mzalendo.
Yeyote aliyesimama kumkanusha wananchi walikuwa tayari kumpiga hata mawe.
Kwakuwa alitengeneza mazingira ya kusikilizwa yeye peke yake ilikuwa rahisi kwake kusema uongo.
Alitunga uongo mwingi na kuumwaga kwa wananchi ili wampende huku akimzuia yeyote kuinuka kwa lengo la kumkanusha.
Hata pale wasomi walipoonya kuhusu masuala kadhaa hususani ya kiuchumi waligeuka kuwa maadui zake.
Mfano ni pale alipomuua gavana wa Benki kuu kwa kosa la kumwambia kuwa fedha hamna na hali ya uchumi ni mbaya.
Katika kutafuta uungwaji mkono na wananchi alidiriki hata kutengeneza matatizo na kuyatatua ili aonekane ni Rais anayejali.
Kwa mfano anapokuwa kwenye ziara zake humuandaa mtu atakayedanganya kuwa ni mgonjwa alafu anamlilia akiomba msaada kwa Rais na hapo utamuona Idd Amin anaandika cheki hapo hapo na kumpatia akatibiwe kumbe yote ni maigizo.
Katika matukio kama hayo wananchi hujikuta wanamshangilia huku wakimuona ni mwenye huruma.
Wakati mwingine alikuwa anawaua baadhi ya wapinzani wake hata wale waliokuwa waandamizi kwenye serikali yake huku akiwa wa kwanza kumwaga machozi wakati wa misiba ya aliowaua.
Mfano ni Pale alipomuua waziri wake wa Afya na kisha kulia machozi huku akitangaza kiama kwa waliofanya tukio lakini baadae ilibainika kuwa kichwa cha waziri huyo kilikuwa kwenye Jokofu la Amin huko kwake. Yaani amemla nyama.
Pamoja na propaganda zote na maigizo kibao bado wapo watu waliokuwa ni waaminifu kwa Milton Obote wakiwemo maaskari na wanajeshi pia...
THE LAST KING OF SCOTLAND...
Hii ni Movie iliyoigiza maisha ya Idd Amin na kupata tuzo nyingi kuliko movie zote zilizomuigiza Amin kwani ilikuwa ni kama uhalisia kwa wale waliowahi kumfahamu Idd Amin Dadaa.
Movie hii ina kijana aliyeitwa Nicholas Gharigan ambaye anakuja Uganda kujitolea kufanya huduma ya kidaktari katika nchi maskini za Afrika.
Alipotua Uganda anapokelewa na Daktari mwingine ambaye anakuwa kama mwenyeji wake kwani japokuwa naye pia ni mzungu lakini yeye ameshalowea kwa muda kiasi ndani ya Uganda naye akitoa huduma za tiba.
Wakiwa kwenye pitapita zao wakakutana na watu wakiwa wanajiandaa kwa kuimba nyimbo na shamrashamra kibao.
Dr Nicholaus Gariggan akamuuliza mwenyeji wake. Kulikoni?
Alijibiwa kuwa wanajiandaa kumpokea Rais Amin kwani anakuja hapo kijijini siku hiyo.
Dr Garigan aliomba wabaki kidogo ili nao wamuone huyo Amin.
Baada ya muda kidogo Gari nyingi zilianza kuingia pale huku watu wakimwagika kwa nderemo na vifijo huku vumbi likitimka kwa nyimbo na kucheza.
Ngoma zilisikika huku msafara wa magari ukiendelea kumiminika.
Baadae Jitu kubwa, Refu,Jeusi lililovalia mavazi ya Kijenerali wa Jeshi lilipanda jukwaani huku likishangiliwa kwa nguvu mnooo....
Uganda hoyeeeeeeee
Hoyeeeeeeee...
Ni sauti ya Amin akiwasalimu watu wa kijiji kile.
Butwaa lilimshika Dr Garigan ambaye ilibidi amuulize mwenyeji wake...
"Hivi wanampenda sana huyu Raisi eeenh"
Jibu alilojibiwa ni kwamba...
"Hata Obote akija wanamshangilia hivi hivi"
Hivyo basi...
USISHTUSHWE NA JINSI WANAVYOMSHANGILIA!
....maana yake watawala tulionao ndio style wanazopenda kututawala kihalifuYule alianza kutumia mitama na kupiga roba enzi za JK akapewa tabasamu na cheo cha ukuu wa wilaya. Walimchekea bila kumuonya walipendezwa na kitendo.
Ameshika bunduki ananyemelea kuwa waziri wa mambo ya ndani. Ndio njia zake maana vyeti hana.
...wewe unaamini huyu anakemea wasaidizi wake?/ anachofanya nikukemea asiowapenda1. Serikali hii ya JK Ni dhaifu, nchi inahitaji Raisi dikteta ili isonge mbele - Mnyika
2. Nchi inahitaji Raisi anayeweza kufanya maamuzi magumu bila woga- Mbowe
3. Tunamuhitaji rais mwenye uwezo wa kukemea wasaidizi wake Na wakamtii- Lema
Sasa mnalalamika nn was....nge nini??
Uongo habari za Kijiji cha Buzi ni hekaya tuuWanaokula nyama za watu wapo na hasa baadhi ya mkoa wa kagera na uganda (wachawi)
Obote siyo rais wa kwanza wa Uganda.Rais wa kwanza ni Kabaka Edward Mutesa na yeye alipinduliwa na Obote.



1. Serikali hii ya JK Ni dhaifu, nchi inahitaji Raisi dikteta ili isonge mbele - Mnyika
2. Nchi inahitaji Raisi anayeweza kufanya maamuzi magumu bila woga- Mbowe
3. Tunamuhitaji rais mwenye uwezo wa kukemea wasaidizi wake Na wakamtii- Lema
Sasa mnalalamika nn was....nge nini??
nimecheka hapo mwishoni mzungu akimjibu mwenzakeNdio.Na wewe ulikuwepo?
NimekuelewaUNAUMIA JINSI WANAVYOMSHANGILIA? NISIKILIZE MIMI.
Baada ya Idd Amin kumpindua aliyekuwa Rais wa Uganda (Milton Obote) kazi kubwa aliyokuwa nayo ni kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende.
Inaaminika kuwa kati ya Madikteta wataalamu katika ushawishi ni pamoja na Idd Amin Dadaa,
Alikuwa ana uwezo wa ajabu sana katika kupepeta mdomo huku akijiamini sana.
Ghafla wananchi wa Uganda walianza kumpenda na kumuona mkombozi wao, kila aliyeinuka kumpinga alitengenezewa propaganda za uongo na hatimaye kuonekana sio mzalendo.
Yeyote aliyesimama kumkanusha wananchi walikuwa tayari kumpiga hata mawe.
Kwakuwa alitengeneza mazingira ya kusikilizwa yeye peke yake ilikuwa rahisi kwake kusema uongo.
Alitunga uongo mwingi na kuumwaga kwa wananchi ili wampende huku akimzuia yeyote kuinuka kwa lengo la kumkanusha.
Hata pale wasomi walipoonya kuhusu masuala kadhaa hususani ya kiuchumi waligeuka kuwa maadui zake.
Mfano ni pale alipomuua gavana wa Benki kuu kwa kosa la kumwambia kuwa fedha hamna na hali ya uchumi ni mbaya.
Katika kutafuta uungwaji mkono na wananchi alidiriki hata kutengeneza matatizo na kuyatatua ili aonekane ni Rais anayejali.
Kwa mfano anapokuwa kwenye ziara zake humuandaa mtu atakayedanganya kuwa ni mgonjwa alafu anamlilia akiomba msaada kwa Rais na hapo utamuona Idd Amin anaandika cheki hapo hapo na kumpatia akatibiwe kumbe yote ni maigizo.
Katika matukio kama hayo wananchi hujikuta wanamshangilia huku wakimuona ni mwenye huruma.
Wakati mwingine alikuwa anawaua baadhi ya wapinzani wake hata wale waliokuwa waandamizi kwenye serikali yake huku akiwa wa kwanza kumwaga machozi wakati wa misiba ya aliowaua.
Mfano ni Pale alipomuua waziri wake wa Afya na kisha kulia machozi huku akitangaza kiama kwa waliofanya tukio lakini baadae ilibainika kuwa kichwa cha waziri huyo kilikuwa kwenye Jokofu la Amin huko kwake. Yaani amemla nyama.
Pamoja na propaganda zote na maigizo kibao bado wapo watu waliokuwa ni waaminifu kwa Milton Obote wakiwemo maaskari na wanajeshi pia...
THE LAST KING OF SCOTLAND...
Hii ni Movie iliyoigiza maisha ya Idd Amin na kupata tuzo nyingi kuliko movie zote zilizomuigiza Amin kwani ilikuwa ni kama uhalisia kwa wale waliowahi kumfahamu Idd Amin Dadaa.
Movie hii ina kijana aliyeitwa Nicholas Gharigan ambaye anakuja Uganda kujitolea kufanya huduma ya kidaktari katika nchi maskini za Afrika.
Alipotua Uganda anapokelewa na Daktari mwingine ambaye anakuwa kama mwenyeji wake kwani japokuwa naye pia ni mzungu lakini yeye ameshalowea kwa muda kiasi ndani ya Uganda naye akitoa huduma za tiba.
Wakiwa kwenye pitapita zao wakakutana na watu wakiwa wanajiandaa kwa kuimba nyimbo na shamrashamra kibao.
Dr Nicholaus Gariggan akamuuliza mwenyeji wake. Kulikoni?
Alijibiwa kuwa wanajiandaa kumpokea Rais Amin kwani anakuja hapo kijijini siku hiyo.
Dr Garigan aliomba wabaki kidogo ili nao wamuone huyo Amin.
Baada ya muda kidogo Gari nyingi zilianza kuingia pale huku watu wakimwagika kwa nderemo na vifijo huku vumbi likitimka kwa nyimbo na kucheza.
Ngoma zilisikika huku msafara wa magari ukiendelea kumiminika.
Baadae Jitu kubwa, Refu,Jeusi lililovalia mavazi ya Kijenerali wa Jeshi lilipanda jukwaani huku likishangiliwa kwa nguvu mnooo....
Uganda hoyeeeeeeee
Hoyeeeeeeee...
Ni sauti ya Amin akiwasalimu watu wa kijiji kile.
Butwaa lilimshika Dr Garigan ambaye ilibidi amuulize mwenyeji wake...
"Hivi wanampenda sana huyu Raisi eeenh"
Jibu alilojibiwa ni kwamba...
"Hata Obote akija wanamshangilia hivi hivi"
Hivyo basi...
USISHTUSHWE NA JINSI WANAVYOMSHANGILIA!
Hakuna mfanano wowote hapo. Labda kwa bavicha kama wewe.Naona jinsi gani post hii imekuumiza kutokana na mfanano uliopo. Vumilia hizi ni tahadhari tu baada ya viashiria kuwa vingi.
Kama ulikuwepo basi lazima utafahamu kuwa makala imejaa uzushi na uongo wa kibavicha. Mimi wakati huo nilikuwa kidato cha nne kwa hiyo nilikuwa tayari najifahamu kiakili. Iddi Amin hakuwa na "kazi kubwa kueneza propaganda kwa wananchi wa Uganda ili wampende". Tangu siku ya kwanza ya mapinduzi watu walimwagika mtaani kushangilia kwa sababu Obote tayari alishapoteza imani ya wananchi. Mambo yalikuja kuharibika baadaye. Kama na wewe ulikuwepo nipo tayari hapa. Sida ganywi na uongo wa kitoto.Hata mimi nilikuwepo!
Nyinyi watoto mliozaliwa kipindi cha Jakaya mnamatatizo sana.Unafikiri ulikuwa peke yako wakati huo?