Swet-R
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 5,613
- 8,048
....Nakuambia wana matusi hao. Ukiwashtukia ni wakali hatari. Wanatukana na matusi ambayo hayapo duniani.Hahahhahaaa.....dah....imebidi nicheke tu best
Mmoja juzi kati kajichanganya kwangu ananiambia mimi mtendaji huku kwako,mbona hujajaza na hujalipia zile form za kurasmisha kupewa hati?. Akaniambia bahati nzuri niko na maafisa ardhi hapa,kwa hiyo ili kukusaidia nitumie hela nikujazie form leo ndio siku ya mwisho waondoke nazo. Nikamuuliza ni kiasi gani?. Akajibu ya miaka 99 ni 60+ na miaka 33 no 30+. Sasa shida ilikuwa kila nikifikia kumuuliza eneo gani na wapi?. Anajibu aaah...! Bwana kwani wewe hukujui kwako?. Anakata simu,anapiga simu tena baadae. Nikamwambia nina maeneo sehemu nyingi,wewe ni wa wapi? Anakata simu.
Baadae nikamwambia kamteperi mamako. Weeee...mtendaji yule alishusha matusi makubwa hatari.
Sasa huyu nae kidogo kidogo anamsogeza jamaa ampige. Nimemshtua jamaa anakaribia kupigwa.
Ukitaka kuwajua ni wale wale wa tuma humu,ukiwashtukia tu kwanza wanapanick,yanaaanza matusi mdogo mdogo. Hapo atakuja na tusi kubwaaaaa,subiri muda tu