Prince! Maelezo yako ndio majibu niliyokuwa nayalenga. Nashukuru kwa darasa ulilonipa natumai na wengine watashuhudia ya kwao hii inatia moyo. Ila hebu nipe vikwazo ulivyokumbana nvyo mpaka unafikia hatua hiyo, maana naona kumaditate kwa saa 2 kila siku yataka moyo
kaka ni kweli kabisa kumeditate sio jambo rahisi kama wengine wanavyofikiri.
Mimi ilinigharimu 1 kuyalazimisha mawazo yangu ya kubaliane na kile ninacho kikusudia.
Haikua kazi raisi kaka wala halikua jambo la siku 1. Ilinichukua muda mrefu mpaka kuanza kuzoea hiyo hali.
Labda ni kupe mbinu iliyo ni saidia kwa uraisi.
Mimi ni mkristo.
Na ninapenda sana kutumia muda mwingi kufanya ibada na Mungu wangu.
Napenda sana kusoma neno la Mungu. Na kutafakari Neno la Mungu. Ihi ilinisaidia sana kwanza kuflash mawazo yote yasiyo na utukufu wa Mungu juu ya maisha yangu.
Hapa ndipo ili kua mwanzo wa kuanzia. Na neno lililo ni shep ni (Yoshua 1:8 na Zaburi 1:1-3)
Neno linasema:
- KITABU HIKI CHA TORATI KISIONDOKE KINYWANI MWAKO, BALI YATAFAKARI MANENO YAKE MCHANA NA USIKU, UPATE KUANGALIA KUTENDA SAWA SAWA NA MANENO YOTE YALIYO ANDIKWA HUMO, NDIPO UTAKAPO IFANIKISHA NJIA YAKO NA KUSTAWI SANA:
katika maneno haya ni kachukua:
1 - kujikiria mambo mazuri.
2 - kumeditate
3 - kujifunza
uho ndio ulikua mwanzo wa safari yangu ya mafanikio. Kwa kuwa eneo la maisha yangu kiroho liko vizuri.
Nikaamishia baadhi ya mambo katika eneo langu la uchumi kupitia mfumo ule ule wa kumeditate. Mambo ya kimaendeleo.
Na neno lililo ni sukuma zaidi lilikua (Mithali 21: 5)
- MAWAZO YA MWENYE BIDII HUUELEKEA UTAJIRI:
hapa sasa ni katenga chumba changu maalum. Ni kawa kila siku kuanzia saa 1 - 2 usiku. Nakaa peke yangu na kuanza kutafakari vitu ambavyo ni kivifanya vinaweza kunibariki na kubadilisha maisha yangu. Kutoka kwenye umaskini kwenda kwenye utajiri.
Nilikua na daftari langu na kalamu yangu. Nikaanza kutafakari shida mbali mbali zinazowakabili watu.na ni nini solution yake.
Na mimi nikajiweka kama mtatuzi wa hizo kero au shida za watu.
Gafla mawazo ya miradi ikawa inakuja kama maporomoko ya mto upitishao maji.
Ni kaanza kuandika miradi. Na kupiga hesabu - gharama na faida. Nikajikuta nimefungua miradi mingi na inayoniingizia pesa nyingi sana na kuagana na umaskini.
Sifanyi biashara kama sijui faida yake ni kiasi gani na nitawekeza kiasi gani. Ihi imenijengea tabia ya kujua ni faida kiasi gani nitapata kwenye kila uwekezaji ninao kusudia kuufanya.
Siwekezi bila kufanya tathimini kwanza. Haya yote ni faida ya Meditation.
Ukiamua yote yanawezekana.