Mkuu Senior boss,kwa mujibu wa wataalam wa haya makitu, akina Pasco, Rakims, Mshana jr na wengineo,meditation hukuwezesha uwezo wa kufanikisha mambo ambayo bila kuifanya hiyo kitu, si rahisi kuyafanikisha.
Mfano kuna vipawa ambavyo tunazaliwa navyo, ila kulingana na mazingira tunayokulia, tunashindwa kuving'amua au kuwa na uwezo wa kuvitumia. Sasa kwa mujibu wa wataalam hawa, meditation hukusaidia kung'amua vipawa hivi na kukupa uwezo wa kuvitumia.
Kwangu mimi hii sijaiprove kwangu mwenyewe au kwa watu wengine waliofanya hii kitu. Na ndio maana nikaileta hii mada hapa, labda naweza pata aliyefanikiwa kwanjia yoyote kupitia hii meditation ili nipate mwanga zaidi
Fanya hii itatatua matatizo yako mengi kama si yote Antidote For All - Free 7 Minute Guided Meditation
Tubu na urudi kwa Yesu,yeye atakuokoa na kukuongoza
soma Zaburi 32:8
Wanajamvi,
Hebu nisaidieni kufahamu faida za hii meditation katika maisha yetu ya kawaida. Nimejaribu kuifanya kwa miezi mitano sasa sijaona tofauti yeyote ya maisha yangu kabla ya meditation na sasa ninapoendelea nayo.
Nimewafuatilia sana Pasco, Rakim na mshana jr lakini naona patupu. Hebu waliofanikiwa nisaidieni(kama mtakuwepo), toka muijue hii meditation imeeasaidia nini na kwa njia zipi?.
Ok Bro.
Kaka mshana jr tafadhali naomba utuelimishe zaidi kuhusu hii kitu. Iko vp ? How does it work exactly ?? Thanks.
Kwanza niseme wazi kwamba mabandiko mengi ya meditation hapa jamvini na kwenye internet yabachanganya sana watu na mengi yako in deep na kitaalam sana... Na bahati mbaya sana wengi hupenda matokeo ya haraka
Pili meditation ni mchakato unaohitaji muda uvumilivu na mwalimu mahiri, inahitaji muda kwakuwa unadili na akili ambayo imeishi kwa zaidi ya miaka 20± imepokea mengi imefanya mengi imeona mengi imewaza mengi na kupanga mengi pia, imetawanyika katika nyanja mbalimbali...kwahiyo sasa unataka kuirudisha na kuwa kitu kimoja ni kazi ngumu mno
Tatu tunafanya meditation katikati ya changamoto za kimaisha na kifamilia kimtazamo kiimani na kimaisha, hivyo kupunguza uwezo wa kuweza kupata kile unachotaka
Lakini kwa kipindi hicho cha miezi mitano kwa Vyovyote utakuwa umepiga hatua kadhaa bila mwenyewe kufahamu hasa kiafya na namna ya kutenda na kuamua mambo mengi
Kwanza niseme wazi kwamba mabandiko mengi ya meditation hapa jamvini na kwenye internet yabachanganya sana watu na mengi yako in deep na kitaalam sana... Na bahati mbaya sana wengi hupenda matokeo ya haraka
Pili meditation ni mchakato unaohitaji muda uvumilivu na mwalimu mahiri, inahitaji muda kwakuwa unadili na akili ambayo imeishi kwa zaidi ya miaka 20± imepokea mengi imefanya mengi imeona mengi imewaza mengi na kupanga mengi pia, imetawanyika katika nyanja mbalimbali...kwahiyo sasa unataka kuirudisha na kuwa kitu kimoja ni kazi ngumu mno
Tatu tunafanya meditation katikati ya changamoto za kimaisha na kifamilia kimtazamo kiimani na kimaisha, hivyo kupunguza uwezo wa kuweza kupata kile unachotaka
Lakini kwa kipindi hicho cha miezi mitano kwa Vyovyote utakuwa umepiga hatua kadhaa bila mwenyewe kufahamu hasa kiafya na namna ya kutenda na kuamua mambo mengi
Mkuu Senior boss,kwa mujibu wa wataalam wa haya makitu, akina Pasco, Rakims, Mshana jr na wengineo,meditation hukuwezesha uwezo wa kufanikisha mambo ambayo bila kuifanya hiyo kitu, si rahisi kuyafanikisha.
Mfano kuna vipawa ambavyo tunazaliwa navyo, ila kulingana na mazingira tunayokulia, tunashindwa kuving'amua au kuwa na uwezo wa kuvitumia. Sasa kwa mujibu wa wataalam hawa, meditation hukusaidia kung'amua vipawa hivi na kukupa uwezo wa kuvitumia.
Kwangu mimi hii sijaiprove kwangu mwenyewe au kwa watu wengine waliofanya hii kitu. Na ndio maana nikaileta hii mada hapa, labda naweza pata aliyefanikiwa kwanjia yoyote kupitia hii meditation ili nipate mwanga zaidi
Habari mkuu. Kwa jinsi unavyofikiri ndio faida zake, ni tofauti kabisa na lengo lake. Ni sawa na idea ya rangi nyekundu na idea ya rangi (Havilingani ufahamu sawa lakini fina uhusiano fulani). Wengi wanajifunza meditation kwa malengo ambayo sio malengo ya meditation bali ni matokeo ya meditation. Na matokeo na malengo yake ni tofauti. Inakuwa ni tatizo hasa kwa wengi ambayo wana shauku ya kufahamu meditation. Walimu ni wengi lakini ile purpose kila mmoja atakudanganya kama alivyodanganywa. Au atakuambia kama naye alivyoambiwa, bila yeye mwenyewe naye kushuhudia.
Kabla ya kufanya meditation ni vyema kufahamu ni kwanini unafanya meditation. Kwani sababu yake itakupa hatua ya kwanza ya njia na matokeo sahihi.
Asante sana.
Nashukuru Apollo! Ila naona kama umeniacha solemba kidogo, hasa pale unaposema faida na malengo ya hii kitu ni tofauti, wawezafafanua kidogo?
Akhsante jibu murua hili, vipi wewe huwezi angalau nielezea mafanikio yako katika hii nyanja?
Lengo la Meditation ni simple. Lakini faida zake ni nyingi. Faida zake ni kutoka katika lengo moja. Na kila faida inaweza kuleta faida nyingine. Kuna faida kuu au lengo kuu ambalo matokeo mengine hutokea kama matawi. Ni kama mti na matawi. Lengo ni kuweza kutoa mshikilio uliopo akilini ambao kwa kawaida huonekani kwani tumezoea hali ya kushikilia akili zetu na hatuifahamu nature ya akili yetu.
Sio lengo ni kupata vipaji, sio kuwa na utajiri, sio kupata nguvu za ajabu, au jinsi wengi wanavyofikiri. Kuipata furaha ya kweli, kujitambua, kudhibiti hisia, mazoea, tamaa, hasira, chuki na ubinafsi, na kuweza kuiongoza akili yako. Hayo ni matokeo tu na faida za meditation zinazotoka katika faida kuu. Na faida hizo zinaweza kuzaa nyingine zaidi kama vile kuwa na tabia njema, kuacha mazoea mabaya, kujifahamu na kufahamu akili na ufahamu wa watu. Na faida hizo zinaweza kuleta faida zaidi kama kuwa na maisha mazuri kwani unaweza kujithibiti na unaishi vyema kwa akili na busara, unaweza kushirikiana na watu, unaweza kujidhibiti na kujitawala na kuwa mtu wa haki na msimamo. Pia unakuwa mwepesi kuisikia nafsi / intuition.
Kinachowarudisha nyuma wengi ni kuwa hawapitii kwanza maelezo ya mwanzo ya kuyafahamu kama vile akili ni nini, ina nini, ufahamu ni nini, una nini na nini. Akili ipoje na Ubongo? Ubongo na milango ya ufahamu vimeungana vipi na ufahamu? Chanzo cha mawazo ni nini? Ufahamu upoje na akili? Akili na mwili vimeunganika wapi? Wazo ni nini? Kulala ni nini? Nini kitatokea usipolala? Ndoto ni nini? Baada ya kupitia introduction kidogo ya kufahamu sayansi hiyo ndipo utatambua meditation ni nini na kwanini kuna meditation. Wengi huanza kusomea meditation bila kufahamu maelezo ya mwanzo katika kujifahamu na kufahamu ufahamu na akili ni nini.
Tafuta mtaalam aku guide katika hatua za mwanzo. Atasaidia kukurekbisha unapokosea. Kusoma tu kwenye vitabu au net itakuchukua mda sana. Nafikiri humu jf kuna wa kukusaidia au kukushauri wapi unaweza pata msaada.
Yapi sasa huwezi kuyaelezea?
asante gollocko kwa kuuliza kuhusu mada ambazo ziliwahi kuandikwa na Rakims pia mshana jr ambazo kama nilivyoeleza ktk uzi uliokuwa ukizungumzia ASTRAL PROJECTION kuwa mara nyingi na kwa miaka mingi MEDITATION imekuwa ikifanywa siri japokuwa Rakims na mshana jr na wengine wamejaribu kuelezea kadiri ya uwezo wao.
Meditation ni elimu pana tofauti na wengi wanavyofikiri na inahitaji kwanza kukubali na kuridhia mafunzo yake kwani tayari wengi wetu tumekuwa ni wagumu kuelewa na kukubali yale yanayoletwa na watu wajamii zetu au jamii za Asia na wengi tunakubali kwa haraka yale ya wazungu.
Ugumu huo umepelekea wengi kutoikubali elimu hii.
Kwa wanaoikubali wameona faida yake ambayo mara nyingi ni jambo la kukubali kwanza kiakili kabla ya kuanza kulitenda ili kufanya saikolojia yako kuendana sawa na kukubali kwako.
Tofauti na faida chache za meditation zinazoelezwa,zipo faida nyingine kama za kisaikolojia ktk zoezi la meditation.
Pia inategemea ni meditation ya aina gani uliyoifanya kwani zipo nyingi na je umefata njia zote za kufanya meditation kulingana na maditation unayofanya ?
Pia meditation huzalisha maswali mengi sana kabla hata ya kuianza kwake.