Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,945
- 4,499
Mwenye e-mail ya Zimbwera wa East Africa radio aniwekee hapa ili nimrushie hii link aone jamii ilivyokereka na washindani wenzake.
Ngoja niwacheck Prosper au Bishangazi
Mwenye e-mail ya Zimbwera wa East Africa radio aniwekee hapa ili nimrushie hii link aone jamii ilivyokereka na washindani wenzake.
mwenye cloudz si ni ccm damu na wafanyakazi wake nao wanafuata mkumbo kulinda kibarua
Unajua weakness ya Chombo cha habari kama Clouds ni kwamba wanaokota Ma-DJ wenye umaarufu wa kijinga jinga na Washereheshaji wa Kitchen parties na kuwageuza waandishi. Hivyo ni u kanjanja kwenda mbele. Wengi shule hakuna pale wala hakuna mwenye mafunzo ya Ki taaluma kutoka kwenye chuo vinavyoeleweka. Na matokeo yake ni rahisi kutambua matundu ya udhaifu wao pale inapotekea mijadala unakuta hata uwezo wao wa kuchambua mambo unakuwa very limited na wamekuwa wakipwaya kwa kiasi kikubwa.
Mi huwa hata siwasilizagi kwa kweli vihiyo hawa wa Cloud. Wamejaa misifa ya kimjini mjini na ushakumpe.
Wanahitaji kubadilisha mtazamo na ku reshape chombo hiki kama wanataka watu makini wawachukulie serious kwa kweli.
Hao ni wachambuzi wa magazeti,sio wachambuzi wa habari
litakaloandikwa la kipropaganda wanatiririka nalo,hawajitegemei kiakili,kiuelewa
Kweli leo ni ushindi wa Godbless Lema...Huyu huwa anakuwa kama Guest leo katoka mafichoni chezea ushindi wa kamanda Lema wewe, sikukuu mi nitalia Kishumundu Yesu na Maria
There are currently 405 users browsing this thread. (218 members and 187 guests)
Ukishaguandua bidhaa uliyotumia ni feki unaiacha mara moja. Ukiwasikiliza tena kesho hujawakomoa, bali umewaongezea soko. Namna bora kabisa ya kupambana na vitu kama hivi ni kuwasusia kabisa. Wakikosa wasikilizaji wajirekebisha au watafunga kituo.Nimewasikia sana hasa yule Gerald Hando amekandia sana habari iliyoandikwa Tz daima, hukumu ya kihistoria kusomwa leo,nataka na kesho niwasikie watasemaje.aibu yao magamba hao
Wameishaweka Breaking News kwenye Fun Page yao kwa Facebook! East Africa Radio | Facebook
Kweli leo ni ushindi wa Godbless Lema...
Leo asubuhi kwenye kipindi cha Power breakfast watangazaji wa Clouds FM wameongea mengi ya kumbeza Lema na kesi yake. Sijui sasa hivi wanajisikiaje baada ya hukumu kusoma.
Ombi langu kwa vyombo vya habari:
Msioneshe waziwazi kwamba mnaegemea upande fulani wa chama cha kisiasa kwani vyombo vyenu hivyo ni vya kibiashara. Jamii ikigundua kuwa mna mlengo flani itawasusa.
Mwana JF aliyesikiliza kipindi hicho anaweza akaongeza yale yalokuwa yakiongelewa..
Ukiona Clouds fm wamekandia kitu juu maslahi yao hayakupewa nafasi,kuna kale kampuni kao ka kupiga fedha nyingi katika deal za matangazo na uhamisishaji,inawezekana waliuza wazo kwa Maige la kupiga pesa akawatolea nje na visa vikaanzia happo wakaona nafasi imepatikana ya kummaliza,Clouds ni mkono wa pili wa mafisadi ndani ya CCM.Tujaribu kidogo kufikiria nje ya box,kuna siku clouds wanakandia ccm,na kuna sk chadema pia.Kwa leo sijaona kosa lao.Hando alikua tu anajaribu kupinga upotoshaji au ukuzaji habari usio na msingi.Saa nyengine magazeti yanakuza mambo bila msingi.That ws the point...mbona walimkomaliaga waziri maige wa ccm hadi akaondoka.