Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Ushindi wa Lema, aibu kwa Clouds FM

Hakuna redio nzuri kama Clouds fm hasa kipindi cha Power BREAK FAST! Jamaa hawa egemei itikadi yoyote!
 
Kama mnataka kusifiwa Chadema anzisheni redio yenu,pro chadema mmekua watu wa kuchukia watu wote ambao wapo analytical!
 
nimekuwa mshabiki kwa sehemu wa kusikiliza redio ya clouds FM asubuhi nikiwa kwenye foleni.Lakini leo nilijuta niliposikia maneno ya kejeli na dhihaka dhidi ya gazeti la Tanzania Daima lililoongea kuwa "hukumu ya Lema ni ya kihistoria".Hata kama asingeshinda mimi ningeona ni ya kihistoria kwa CDM tungekuwa tumenyang'anywa jimbo na Ikulu.Hii ilishatamkwa wazi na Lema na Ikulu haijapinga kwa lolote.Sasa Gerald akajifanya hakuna chochote kipya katika kesi hii na anashangaa gazeti na wananchi wa Arusha na wanachama wa CDM kushabikia kesi hii.SASA M4C TUMESHINDA.GERALD UNASEMAJE PAMOJA NA PJ WAKO?.Nyinyi ni vijana wenzetu,mbona tunakulana wenyewe?

Nilimsikia hata mie nikamshangaa sana. Huwa nawaheshimu sana hawa jamaa lakini leo nilishtuka sana. Uhistoria wa kesi ya Lema unatokana na mambo yafuatayo:
1. Hukuma za mahakama hutunga sheria yaani hukumu iliyopita na haikuwa challenged inaweza kutumika kutoa hukumu nyingine. Hii hukumu kila mtu hata CCM wenyewe walijua ni hukumu mbaya ni vile tu mahakimu/majaji wana kinga. Kusimama kwa hukumu hii kunge-set precedence mbaya iliyowahi kutokea katika sheria.
2. Lema alichaguliwa na wananchi kwa kura nyingi sana akimshinda Mama Buriani kwa mbali. Kwa kutumia haki ya asili (natural justice) haikuwa sahihi kuwanyang'anya wananchi wa Arusha Mbunge wao kwa sababu ambazo hazikuathiri matokeo kwa namna yoyote ile.
3. Mama Buriani hakuwahi kutokea mahakamani kutoa ushahidi wa kutukanwa na Lema, wala hakufungua kesi ya madai ya kudhalilishwa. Kosa kama hili ni lazima muhusika mwenyewe ajitokeze. Na hata hivyo adhabu yake haingekuwa kumvua Lema ubunge wake.
4. Kosa la kumtukana mtu ni la jinai. Mtuhumiwa anatakiwa ashitakiwe na Jamuhuri, aliyetukanwa anakuwa shahidi. Hakuna polisi waliomshika Lema na kumshitaki kwa kutenda kosa la jinai. Na hata hivyo adhabu yake ni faini, au kifungo au vyote kwa pamoja. Nadhani kila tusi ni kama miezi mitatu hivi.
5. Kushindwa kwa Lema kwenye rufaa hii kungeweka record mbaya kabisa katika utendaji wa mahakama.
6. Kushida kwa Lema kwenye kesi hii kunaweka record ya pekee ya ujasiri wa Majaji kuamua kwa uhuru kesi ambayo kwa namna kubwa Serikali ilikuwa na maslahi yake. Kwa hiyo Lema ameshinda kesi against all odds. Ni historia kwa kweli

Kwa hivyo Jerad Hando na PJ wawe wanafanya fair analysis badala ya kuponda kwa mrengo wa kupendelea upande fulani. Ushindi wa Lema ni ushindi wa mfumo wetu wa sheria na mahakama. Hiki siyo kitu kidogo hata, wakumbuke Jaji Mkuu alijitoa kwenye kesi hii. Tusifanye speculations lakini wahenga walisema ukiona moshi basi ujue kuna moto chini au dalili ya mvua ni mawingu au La kuvunda halina ubani. Tuwe makini hapo Clouds tufurahishe wasikilizaji lakini tukumbuke ku-balance mambo.
 
Kipindi cha michezo saa 3 (sports roundup) usiku tu ndio kimebeba uhai wa hii redio station otherwise ni station ya kihuni,mfano kipindi chao cha Power breakfast ni hatari sana kwa maadili ya Kitanzania,Gerald Hando ni janga!
 
Binafsi hata mimi sikuyapenda maneno yao ya kejeli ya leo mana wameponda hadi basi kwamba Tz Daima inamaliza wino bure hakuna historia hapo watu wanatumia hela kuja toka Arusha hizo hela bora watumie kwa sikukuu daa mpaka nkahisi nimenyeshewa ila siku zote dhuluma haiwezi kuishinda haki. Kwa kweli leo clouds mmejidhalilisha sana kwa kuwa na ushabiki wa kinafiki hata hiyo miaka 13 mnayoiadhimisha bora muanze upya
 
huyo gerald hajui lolote kuhusu tasnia ya habar,na hata kama ana diploma itakuwa ya vyuo vya uchochoron na cyo vnavyotambulika na tcu,
 
haija wai tokea, redio ya wafu ikasifia chama makini, achana na mabwege, vibonde, vibaraka, watumwa wa mafisadi, nawe km ni mmoja wao kufie mbali!!!!!! alaaaaaa!!!!!
 
Redio hawatakiwi kuwa wanaaa hebu Jiulize hivi kutokana na makala hii huwaoni kama hao watangazaji ni wazembe?;

Hakika kuna haja ya uteuzi wa Majaji kuchunguzwa upya hii ni aibu kwa Mheshimiwa Rais na washauri wake kwani huu ni mfano mmoja tu wa majaji uozo, Je, wako wangapi wa sampuli yake?


Swali la msingi la kujiuliza ni:
Je, ni raia wema wangapi wameathiriwa na hukumu butu kama hizi hizi za Jaji Gabriel Rwakibalira na wakatumikia adhabu zisizo sahihi kwa kukosa utetezi wa mawakili makini?

Tupo pamoja katika kumpongeza ndugu yetu Lema na jopo lake la mawakili lakini hapo nilipo bold naweza sema ndio maana kuna rufaa kutokana na kwamba mahakama moja inaweza ikatafsiri kesi vingine kutokana na hoja zilivyoletwa kwa wakati huo na ndio maana mtu asiporidhika anakata rufaa kwa tafsiri zaidi ya kisheria based on hukumu iliyotolewa. (sheria inatambua kabisa kwa akili za binadamu jaji anaweza akafanya maamuzi kinyume na matarajio na ndio maana ikatoa nafasi nyingine ya kukata rufaa)
 
wadau bado mnasikiliza hiyo redio?kwani wanatofauti na TBC?they all bunch of losers.
 
Ni watu ambao ukiwasikiliza vizuri, utagundua mara nyingi wanadhani yale wanayoyasema na kuyafikiri ndo sahihi, na shida yao kubwa ni kutopenda kujifunza.Nadhani waelimishwe kiundani nini maana ya neno historia.
 
Tangu wapike ushindi wa Ma-DJ wa radio, sijawahi sikiliza hiyo radio hata ktk gari ya mtu au ya kulipia.Kw aujumla sijui hata siku hizi sikumbuki hata frequency zao.

Wasomi wa bongo wamekuwa wajinga wajinga kw akusikiliza vipindi vyao asubuhi,wale watoto wa magorofani wakiongea ujinga kama kawaida yao.Wakiwa wadogo waliongolea movie za van Dame na Arnold, wachache pia na Rambo, sasa wanaongea move za kijinga za Nape, na mwigulu huku wakimsogeza karibu Zitto na Makamba.Kuna cha mwanamume hapo kusikiliza?
 
.....kumbe!!!!!! ni redio ya udaku na kujikombakomba...chini ya mhimili ya washereshaji.....
 
Nilimsikia hata mie nikamshangaa sana. Huwa nawaheshimu sana hawa jamaa lakini leo nilishtuka sana. Uhistoria wa kesi ya Lema unatokana na mambo yafuatayo:
1. Hukuma za mahakama hutunga sheria yaani hukumu iliyopita na haikuwa challenged inaweza kutumika kutoa hukumu nyingine. Hii hukumu kila mtu hata CCM wenyewe walijua ni hukumu mbaya ni vile tu mahakimu/majaji wana kinga. Kusimama kwa hukumu hii kunge-set precedence mbaya iliyowahi kutokea katika sheria.
2. Lema alichaguliwa na wananchi kwa kura nyingi sana akimshinda Mama Buriani kwa mbali. Kwa kutumia haki ya asili (natural justice) haikuwa sahihi kuwanyang'anya wananchi wa Arusha Mbunge wao kwa sababu ambazo hazikuathiri matokeo kwa namna yoyote ile.
3. Mama Buriani hakuwahi kutokea mahakamani kutoa ushahidi wa kutukanwa na Lema, wala hakufungua kesi ya madai ya kudhalilishwa. Kosa kama hili ni lazima muhusika mwenyewe ajitokeze. Na hata hivyo adhabu yake haingekuwa kumvua Lema ubunge wake.
4. Kosa la kumtukana mtu ni la jinai. Mtuhumiwa anatakiwa ashitakiwe na Jamuhuri, aliyetukanwa anakuwa shahidi. Hakuna polisi waliomshika Lema na kumshitaki kwa kutenda kosa la jinai. Na hata hivyo adhabu yake ni faini, au kifungo au vyote kwa pamoja. Nadhani kila tusi ni kama miezi mitatu hivi.
5. Kushindwa kwa Lema kwenye rufaa hii kungeweka record mbaya kabisa katika utendaji wa mahakama.
6. Kushida kwa Lema kwenye kesi hii kunaweka record ya pekee ya ujasiri wa Majaji kuamua kwa uhuru kesi ambayo kwa namna kubwa Serikali ilikuwa na maslahi yake. Kwa hiyo Lema ameshinda kesi against all odds. Ni historia kwa kweli

Kwa hivyo Jerad Hando na PJ wawe wanafanya fair analysis badala ya kuponda kwa mrengo wa kupendelea upande fulani. Ushindi wa Lema ni ushindi wa mfumo wetu wa sheria na mahakama. Hiki siyo kitu kidogo hata, wakumbuke Jaji Mkuu alijitoa kwenye kesi hii. Tusifanye speculations lakini wahenga walisema ukiona moshi basi ujue kuna moto chini au dalili ya mvua ni mawingu au La kuvunda halina ubani. Tuwe makini hapo Clouds tufurahishe wasikilizaji lakini tukumbuke ku-balance mambo.

Jerad Hando ninayemfahamu toka ameingia hapa jijini kutoka Arusha alikokulia hana weledi wa kufahamu mambo makubwa kama haya. Na hii ni tatizo kwa fani nzima ya waandishi habari kuwa na akili ndogo wengi ambao wameachiwa uhuru mkubwa kuipotosha jamii na ukizingatia wananchi wetu wengi wanasumbuliwa na ujinga na umasikini!
 
Gerald Hando ni classmate wangu Azania Secondary, O level, he is more than 40yrs now lkn mambo yake utafikiri rika la Diamond...
 
hapa nadhani mnawachafua clauds bure,tafadhali mfanye tena utafiti wa kina kujua mnachokisema kama ni sawa

Wewe vipi, waliosikiliza ndiyo wanaotoa ushahidi,unataka utafiti upi tena?
 
Back
Top Bottom