Ushauri wangu kwa Mzee Kikwete katika siasa za Tanzania ya Rais Samia

Yaani anaona kama 2025 atakuwepo
 
sahihi kabisa,,,
 
Hakuna utawala ambao ulikuwa bora kabisa kama wa jk. Aliweza kuajiri vijana wote bila kujali umetokea wapi. Walimu na madaktari walikuwa wanakombwa wote labda ukatae ajira mwenyewe jpm akaja kupiga pini ajira zote. Ni jk ndo alikuwa napandisha madaraja na mishahara kila mwaka. Ni jk ndo aliweza kuwaleta wawekezaji kila kona kiasi kwamba hakuna mtu aliyekuwa anataka kufanya kazi na asipate kazi ya kufanya unlike the jpm regime. Ni jk ndo uhuru na demokarasia ndo vilitamalaki mpaka tanzania ikawa kinara na ikapelekea mpaka raisi wa marekani na wa china wakatua kujifunza tanzania.
 
Usipo wasifia viongozi walioko madarakani hata kama hawafanyi vizuri ujue kuwa unaweka rehani uhai wako pamoja na mali zako hasa kwa watu wa aina ya Kikwete, kuwasifia sifia viongozi walioko madarakani kunaongezea siku za kuishi,ndio kama yale ya Mwinyi baba alikuwa Rais mtoto naye kawa Rais wa Zanzibar, mwisho baba mtu kasindikizwa kwa kujengewa nyumba ya kifahari na benz juu.
 
naunga mkono hoja......ya kukaa kimya lakini, hayo ya kwamba hakufanya chochote katika uraisi wake wa miaka kumi nayaacha nafsini mwa mtoa mada; aendelee kubishana nayo, yeye na Mungu wake anaemuamini. ila kwa upande wangu baadhi ya mambo ninayoyakumbuka kwa kikwete ni ujenzi wa mabarabara nchi nzima, ajira (ingawa siliangalii sana hili), ujenzi wa flyovers (nakumbuka kama sio 2010 basi 2011 nilishuhudia kwa macho yangu flyover ya tazara pale ikipimwa na kuwekwa tayari), hospitali nyingi tu km ile ya mloganzira, sijajua vizuri kuhusu chuo kikuu cha dodoma na shule za kata n.k

kwanini nami namtaka akae kimya?

jk anaandamwa, anachukiwa na kufuatiliwa mno na kundi lisilompenda lililoandaliwa vema kipindi kile (ingawa kwa wananchi wa kawaida jk wanamkubali sana.....ana nyota nao huku uswahilini tunasema). kuhusu hili nitaeleza kwa kirefu kidogo;

chuki na imani hii iliasisiwa wakati wa serikali ya awamu ya tano kwa nguvu kubwa; kilipondwa kila alichofanya, ulipigiwa kelele ya wizi kila mkataba wa mradi alioufanya wakati wake, lilisemwa dhaifu na tumepigwa katika kila jengo alilojenga.....tukawahi kuambiwa na kuonyeshwa ghorofa lililojengwa kwa mil.500 kama jitihada za kuhalalisha tuhuma hizo kwa kikwete ingawa nyumba ya kawaida tu std hujengwa mpaka mil.150. iweje ghorofa yenye floors kadhaa ijengwe kwa mil.500 hakuna aliyejua, na kwakuwa aliyesema alikuwa ni mwenye nguvu kuu akisaidiwa na uvivu wa kufikiri wa watanzania pamoja na uwekezaji wa kutosha wa kina musiba (aliyewahi kulipiwa mahali na jk), makonda, polepole, bashiru n.k, jina la kikwete likafanikiwa kuhusishwa moja kwa moja na ufisadi, wizi, unyang'anyi, kujuana, ulaghai n.k.

kina musiba waliandaliwa na kudhaminiwa vizuri tu waifanye kazi hiyokwa kurusha mamia ya clips kila leo yakimuhusisha jk na uovu na kila anayehusika na jk alikiona cha moto; ni wizi tu na uibaji. propaganda iliyopigwa kisawasawa kwa muda wa miaka mitano na ushee, huku mpigiwa propaganda akiwa hana pa kujitetea na usemaji (kwa vyombo vya habari n.k) ukiwa umezuiliwa vilivyo, matunda yalipatikana ya kutosha na jk akatambulika kama mwizi, laghai, asiye mzalendo n.k. haikuishia hapo tu, familia yake na waliokuwa wasaidizi wake walihusishwa pia na kila aina ya uovu.

baada ya raisi Magufuli kufariki (r.i.p), 'watesi' wake jk wameumia mno. kilichowaumiza kikubwa ni kutotimia kwa malengo yao ya muda mrefu waliyojiwekea (km vile kuandaa uhakika wa kula kwa muda mrefu (kupitia mpango wa kubadilisha katiba n.k)), kutompenda aliyeachiwa madaraka (kwa sababu ya ukanda, udini, jinsia n.k) na uwezekano wa kubumburuka kwa mamia ya uovu/madudu yao yaliyojificha chini ya kivuli cha kumkandia 'mharibifu' jk. kwa kutokuelewa au kuelewa msimamo wa raisi aliyopo madarakani sasa, wameamua kuja na kila aina tusi na shutuma mbaya kuwahi kutokea tangu pande hili la ardhi liumbwe ilimuradi tu kujaribu kuiambukiza jamii ya kitanzania hisia za kumchukia jk na familia yake na marafiki zake wote......yaani abaki pekee duniani hapa akisubiria kujifia na familia yake ipate tabu isiyo mithirika. katika kuhakikisha wanajaribu kumdhibiti jk na mama samia kwa ujumla (ili amuogope na kumuweka mbali jk kwa lolote lile na abaki tu akiwategemea kina polepole, bashiru n.k) yafuatayo yamezushwa:-

1. jk ndiye aliyemuua magufuli (ingawa haielezwi kivipi sababu marehemu alizungukwa vizuri na watu wake huku jk na wale walioitwa 'timu yake' walikuwa mbali kabisa na huo utawala)
2. jk ndiye anayeongoza nchi na mama ni 'remote' tu (lengo hapa ni kumshushia hadhi mama samia (sababu si wa kwao) mbele ya watanzania na kuendelea kumchonganisha jk kwa watanzania.
3. baada ya kuteuliwa makamba juzi kelele zimezidi kuwa ni yeye aliyesababisha hilo. wanasema hivyo huku wakisahau kuwa makamba (ambaye sasa anatangazwa mwizi kwa nguvu kubwa) aliteuliwa uwaziri na magufuli na kudumu nao kwa miaka 4........haieleweki kaiba nini (zaidi ya maneno tu ya musiba na timu yake walioandaliwa) na ni vipi aliteuliwa uwaziri na mtu anayesemwa kuwa ni 'muadilifu kuwahi kutokea dunia hii'. kuongeza chumvi katika jeraha, wanasema nape na ridhiwani hivi karibuni wataongezwa katika baraza la mawaziri (linasemwa hili basi tu katika jaribio la kumchanganya mama na kumkera jk) na mengine mengi yanayosemwa.

kivipi sasa unyamaze jk;

1. kwa sababu ya future ya kijana makamba. chuki na kila jina baya unalopewa wewe sasa yanapelekwa pia kwa makamba. anaitwa mwizi, anatukanwa n.k hayo yote wanayafanya kwa hisia kuwa ni kijana wako na sababu ya chuki waliyonayo kwako. kwa wewe kusema lolote kwa seriakli hii (hata kama utasema kile kile ulichokisema katika serikali zingine) basi kitapata muitikio wa hivyo. tulia brother na muachie Mungu mkuu....imetosha. simjui kwa undani makamba lakini kwa uchache namuona ni mtu stable sana anaweza kufanya kitu sahihi kumuaibisha shetani.

2. kumpunguzia matusi mama samia. anatukanwa mno na kundi fulani kwa kukutumia wewe (km nilivyosema hapo juu). kutia neno lolote, hata liwe la kawaida kiasi gani katika serikali hii, ni kuwapatia sababu maadui zako (walioandaliwa vizuri) ya kumshambulia na kumuaibisha mama pamoja na kukushambulia wewe. najua wewe ni mtoto wa mjini na unaweza tu kula nao sahani moja, lakini kausha brother kwani imetosha sasa acha karma tu ifanye kazi.

nakuuunga mkono mtoa mada, jk anyamaze!!
 
Ushauri mzuri sana lakini fahamu ili mtu ajirekebishe, lazima awe na akili timamu. Baadhi hwaoni makosa yao milele!
 
Mtoto kapata mama ila watanzania wanajifanya wasiri dah, duniani hakunaga siri
 
Orodha ya baadhi ya mambo aliyoyafanya JK (Smart president)

1. Daraja la Kigamboni
2. Daraja La Kilombero
3. Daraja la Umoja
4. Daraja la Maragarasi
5. Chuo Kikuu cha Dodoma
6. Hospitali ya Mloganzila
7. JNIA terminal III
8. DART(Mwendo kasi)
9. Sekondari za Kata nchi nzima kila kata ina shule.
10. Mradi mkubwa wa maji wa Ziwa Victoria
11. Songwe Airport
12. Kigoma Airport
13. Tabora Airport
14. Umeme wa REA
15. Benjamin Mkapa hospital Dodoma
16. Chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha
17. Dangote industry
18. Bomba la gesi Mtwara Dar
19. Kinyerezi I&II
20. Hospitali ya Moyo
21. MOI
22. Nchi nzima kuunganishwa kwa barabara za lami(zaidi km 14000 zilijengwa nchi nzima)
23. Umeme kwa makao makuu ya wilaya
24. Kuvusha Umeme Zanzibar
25. Ujenzi wa Mkongo wa taifa wa mawasiliano(leo tunajimwambafai na internet matunda ya JK)
26. JNICC Conference center(Ukumbi wa kisasa)
27. Hata CCM wenyewe aliwajengea ukumbi wa kisasa Dodoma.
28. Nyongeza ya mishahara kwa watumishi kila mwezi julai
29. Ajira kila mwaka
30. Annual Increment kila mwaka
32. Diplomasia ya kimataifa ilikuwa juu katika ukanda wa maziwa makuu.
33. Demokrasia iliyopevuka
34. Aliwagomea CCM na kuwaambia hoja za kisiasa hujibiwa kisiasa, sio kwa kipigo cha polisi.


Kama haujaridhika niongeze mengine.
 
Mgomo wa madaktari hadi kutekwa kwa ulimboka ilikuwa utawala wa nani? Kikwete alipoulizwa ajira alizotengeneza, nyingi alizotaja zilikuwa za wahudumu wa bar. Kwa nini wewe umeziona nyingi kuliko yeye?
 
Usihangaike na idadi, ni kiasi gani cha pesa kilitumika? Eti hata shule za kata alijenga, michango ya lazima aliyoisema Heche na Lissu umeiweka wapi?

Muhimu akae kimya! Muda wake ulipita kwa hayo ya kwake. Profesa Kikwete aliahidi akistaafu ataomba kufundisha chuo kikuu au ndo hiyo kuteuliwa kuwa Chancellor?
 
Eti wewe nae ni msomi?..kweli tz tunaenda pabaya.
 
Huyo anaitwa ni mzee wa kuwashwa-washwa! Sijui kama anaweza kaa kimya. Anataka kuongoza baada ya kustaafu badala ya kutuundia trust fund, yeye yumo tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…