Kwanini Rais Mstaafu Kikwete anaudharau sana Upinzani wa Tanzania?

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,986
142,002
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem
 
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem
Vyama vyenyewe havipo serious ukweli upo wazi, chadema kimekusanya viongozi ambao wengi wao wanaamini kwenye mabavu , matusi na ujuaji na ni kama chama cha kifamilia au kikanda wamepoteza mvuto kwa wananchi

Act wakiwa serious nawaona mbali sana wamejikita kwenye hoja na siasa zenye ushawishi na wanajitaji muda mrefu sana kuweka mizizi kiasi cha kushindana na ccm may be next 50 years
 
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem
Kikwete anyamaze tu, ameshindwa kutunza mke na familia, anasubiri serekali imlelee mke na watoto! Mke kaona hapati matunzo kaamua kwenda kudai malipo kwa wenza wa wastaafu. Mtoto ndio huyo domo zege kaenda kuzeekea bungeni.
 
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem

Ni propaganda tu za kuwafanya watu waamini hivyo ili hata wakiiba kura watu wanajua ni kuwa CCM wameshinda.

Kama upinzani siyo tishio ni kwa nini wanahangaika kuiba kura tena waziwaz, kupitisha wabunge bila kupingwa na kugawa majimbo kuwafever CCM.

Kama upinzani siyo tishio kwa nini hawataki kubadilisha katiba ili tuwe na katiba inayoendana na wakati badala ile yenye sheria za mkoloni.

KJ asijifanye mjuaji hapa. Kila mtu anajua kuwa 2010 aligalagazwa na Dr. Slaa mpaka akazuia matokeo kutangzwa kutoka vituoni na matokeo yakacheleweshwa ili wayapike vizuri.

Pamoja na wizi wote wa kura Statistics zinaonyesha kuwa CCM wamekuwa wakipata kura chache kila uchaguzi kulinganisha na uchaguzi ulipita. Hii ndiyo sababu iliyomfanya Mwendazake kuweka mpira kwapani 2020.
 
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem
Anawajua ni wachumia tumbo nyuma ya pazia wakitengewe juice ikulu kila kitu kimekwisha ni maigizo majukwaani!
 
Mara kwa mara mzee Kikwete amekuwa akisema vyama vya Upinzani Siyo tishio kwa CCM na havina ubavu wa kuishinda kwenye uchaguzi mkuu

Kwenye kumuaga Hayati Mwinyi pale Uwanja wa Uhuru Mzee Kikwete alisema vyama vya Upinzani vinajifurahisha tu Lakini kamwe haviwezi kuishinda CCM

Jana katika kuadhimisha miaka 3 ya Rais Samia mzee Kikwete amesema CCM Kushindwa na Upinzani labda uje muujiza

Ikumbukwe wakati wa Utawala wake Chadema walikuwa wanakwenda Ikulu mara kwa mara na kuenjoy Juice ya Ceres na Samosa

Ramadan Kareem

Hadharau wala, ni mwanasiasa tu
 
Vyama vyenyewe havipo serious ukweli upo wazi, chadema kimekusanya viongozi ambao wengi wao wanaamini kwenye mabavu , matusi na ujuaji na ni kama chama cha kifamilia au kikanda wamepoteza mvuto kwa wananchi

Act wakiwa serious nawaona mbali sana wamejikita kwenye hoja na siasa zenye ushawishi na wanajitaji muda mrefu sana kuweka mizizi kiasi cha kushindana na ccm may be next 50 years
Ccm ingekuwa ina uwezo huo usemao tusingeingia kwenye aibu ya mchele wenye virutubisho. Chama kina miaka 50+ madarakani, lakini bado kinategemea katiba outdated kukaa madarakani!
 
Kikwete anyamaze tu, ameshindwa kutunza mke na familia, anasubiri serekali imlelee mke na watoto! Mke kaona hapati matunzo kaamua kwenda kudai malipo kwa wenza wa wastaafu. Mtoto ndio huyo domo zege kaenda kuzeekea bungeni.
Hapo kwenye domo zege umesema ukweli sina hakika kama umefunga kwa uzushi huu wa kusema kikwete kashindwa kulea!
 
vyama vya upinzani bado havijitambui

uzuri watanzania hufanya mamuzi ya kuvibwaga kipindi cha uchaguzi
Kwa zile chaguzi za kihayawani ccm itaendelea kukaa madarakani hata miaka 100. Uzuri wananchi wamegundua kuendelea kushiriki hizi chaguza a kishenzi huku ccm ikipora chaguzi, ni kuipa uhalali isiyostahili. Kwa sasa wanaojitambua hawana muda wa kupoteza kushiriki huo upuuzi. Tutapata njia nyingine ya kupata viongozi. Kwa sasa uchaguzi ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
 
Kikwete anyamaze tu, ameshindwa kutunza mke na familia, anasubiri serekali imlelee mke na watoto! Mke kaona hapati matunzo kaamua kwenda kudai malipo kwa wenza wa wastaafu. Mtoto ndio huyo domo zege kaenda kuzeekea bungeni.
Sasa hapo naona huna hoja zaidi ya porojo, wote tunajua kikwete ana mke na watoto na ana very stable happy family sasa huko kulea ameshindwa vipi mkuu?
Na mtoto wake ambae ni naibu waziri anafanya vizuri sana hata tukipita chalinze tunaona mabadiliko aliyoyaleta tangu achukue ubunge , uwekezaji umeongezeka , huduma za kijamii zimeongezeka
Kiongozi siyo lazima aongee sana anatakiwa awe mtendaji mzuri
 
A
Vyama vyenyewe havipo serious ukweli upo wazi, chadema kimekusanya viongozi ambao wengi wao wanaamini kwenye mabavu , matusi na ujuaji na ni kama chama cha kifamilia au kikanda wamepoteza mvuto kwa wananchi

Act wakiwa serious nawaona mbali sana wamejikita kwenye hoja na siasa zenye ushawishi na wanajitaji muda mrefu sana kuweka mizizi kiasi cha kushindana na ccm may be next 50 years
ACT siyo tishio sana kwa CCM kwa hiyo hawana sana shida nao hasa Bara, huwezi kushindana na CCM kama huna ubavu, Kwani CCM wanatumia mabavu, Mpaka sasa sijaona chama chochote kinachoweza mikiki mikiki ya CCM kiasi fulani CUF kilikuwa kimeanza kuwa chama chenye Mikiki mikiki ila kikazimishwa, CDM kina watu wengi wenye maisha mazuri hawapo tayari kujitoa muhanga. CCM haitatolewa madarakani na chama cha siasa ila kitakuja kutolewa madarakani kwa ambush baada ya idara zote zitakapo choka. Vyama vya siasa ni chachu tu ila wananchi wenyewe wanaweza kuanzisha vuguvugu ambalo ndilo litaindoa CCM, sababu ya kusema hivyo vyama vya siasa ni rahisi kuwanunua viongozi ila vuguvugu huwa halina kiongozi na anayelegea anawekwa kando watu wanasonga mbele.
 
Ushindi mkubwa na kazi kubwa wanayofanya ccm ni kuwa na hii tume ya uchaguzi. Kwao ccm kushinda uchaguzi ni kushinda kulazimisha hii tume. Sisi ni watu wazima hebu tuache unafiki na ujinga.

Serekali (ya ccm) hebu waruhusu tume huru ya uchaguzi na ndio hizi mada zitakuwa na maana
 
A

ACT siyo tishio sana kwa CCM kwa hiyo hawana sana shida nao hasa Bara, huwezi kushindana na CCM kama huna ubavu, Kwani CCM wanatumia mabavu, Mpaka sasa sijaona chama chochote kinachoweza mikiki mikiki ya CCM kiasi fulani CUF kilikuwa kimeanza kuwa chama chenye Mikiki mikiki ila kikazimishwa, CDM kina watu wengi wenye maisha mazuri hawapo tayari kujitoa muhanga. CCM haitatolewa madarakani na chama cha siasa ila kitakuja kutolewa madarakani kwa ambush baada ya idara zote zitakapo choka. Vyama vya siasa ni chachu tu ila wananchi wenyewe wanaweza kuanzisha vuguvugu ambalo ndilo litaindoa CCM, sababu ya kusema hivyo vyama vya siasa ni rahisi kuwanunua viongozi ila vuguvugu huwa halina kiongozi na anayelegea anawekwa kando watu wanasonga mbele.
Fact
 
Ushindi mkubwa na kazi kubwa wanayofanya ccm ni kuwa na hii tume ya uchaguzi. Kwao ccm kushinda uchaguzi ni kushinda kulazimisha hii tume. Sisi ni watu wazima hebu tuache unafiki na ujinga.

Serekali (ya ccm) hebu waruhusu tume huru ya uchaguzi na ndio hizi mada zitakuwa na maana
Bora hata ccm hicho chama kina mwenyekiti amekaa miaka 30 hatoki kwenye uenyekiti halafu leo tumpe nchi hivi tutakuwa wajinga wa aina gani?
 
Kikwete ni mwanasiasa haswa anajua namna ya kuwabinya mbupu wapinzani jukwaani. Ana medali za kucheza na akili za watu kwenye majukwaa.

Ila hayati alitumia ubabe na vyombo vya dola waziwazi. Japo alikuwa mtendaji na mfuatiliaji mzuri.
 
Bora hata ccm hicho chama kina mwenyekiti amekaa miaka 30 hatoki kwenye uenyekiti halafu leo tumpe nchi hivi tutakuwa wajinga wa aina gani?
Hiki chama kinawanyima usingizi sana eeenh?

We kwenye maelezo yangu umeona mahali nimetaja chadema? Kikwete alizungumzia upinzani hakuzungumzia chadema!
 
Back
Top Bottom