smart tv haihusuani na resolution ya tv, smart tv inamaana tv yako inakuwa na operating system na kuweza kufanya task kama kuangalia video online, kuplay movies na interface nzuri nk.
mfabo wa operating system za tv ni kama tizen ya samsung, web os ya lg, firefox os ya mozilla na android tv ya google.
ila kwa uzoefu wangu mimi smart tv zinauzwa bei ghali sana, unaweza nunua tv ya kawaida then ukanunua na tv box/cast na kuifanya tv iwe smart bila gharama kubwa.
ukisema HD, FHD na UHD hizi ni resolution au kwa lugha rahisi ni idadi ya pixel ambayo tv yako inayo
HD- 1280x720. hapo inamaana kiupana kuna pixel 1280 na kiurefu pixel 720 ukizidisha hapo inamaana jumla tv ina pixel milioni moja
FHD- 1920x1080 ambayo ni pixel milioni 2
UHD- 3840x2160 ambayo ni roughly pixel milioni 8
kwa majina mengine hd ni 1 megapixel, fhd ni 2 megapixel na Uhd ni 8 megapixel
3d au 3 dimension ni ngumu sana kuielezea kwa maneno ila kiufupi unaona vitu kama reality, mfano kwenye movie mtu karusha kisu upande wako unaweza kuinama sababu unafeel kabisa kinakupiga wewe, ili uone 3d kwa tv itabidi uwe na miwani ambayo mara nyingi inakuja na tv.