barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,739
- 32,936
Wewe comte mbona unaharibu jina,huyu comte alikuwa mmoja kati ya wanafalsafa wakubwa,ana nasharia nyingi za kufikirisha.Mbona hulitendei haki hilo jina?HIVI MUNGU HAJUI NANI KAFANYA NINI MPAKA TUTUMIE NGUVU ZOTE HIZI KUONYESHA NANI KAFANYA NINI? HIVI HUU MRADI NDIO UTAMFANYA LEMA ADUMU KUWA MBUGE? MBONA AMEKUWA MBUNGE BILA YA HUO MRADI KUWEPO?
KAMA ALIVYOSEMA ZITO HII NI AIBU KWA VIJANA
Unamjua Yesu Vizuri wewe au unakisia tu,hataYesu mwenyewe kabla ya kuachana na wanafunzi wake alitaka "Recognition".Yesu alitaka kujua je hata wale walio karibu yake wanajua yeye ni nani na mchango wake ni upi?Ndio maana aliwauliza wale wanafunzi wake "Eti mimi ni nani na watu wanasema mimi ni nani?
Wale wanafunzi wake wengine wakasema aaaa wewe wanasema Nabii Elia,mara Musa mara ooo!!Yesu akamuuliza Petro...Petro mimi ni nani?Pale pale Petro akasema,wewe ni Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye juu...Hata kabla hajamaliza,pale pale Yesu akampa Petro "shavu"...Kwamba wewe ndio Peteo (Kefa) na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa,utakalolifunga duniani na mbinguni litafungwa.....Yaani baada ya "Recognition" tu,Yesu akampa shavu Petro...