Ushauri wa Zitto kwa Lema na RC Gambo

Ushauri wa Zitto kwa Lema na RC Gambo

Kuna watu wanataka wamwambie Rais Magufuli nani awe RC wa arusha. Hilo halipo
 
Hili lisipite bila mimi kutoa mawazo yangu.

reaction ya Lema haikubaliki kabisa, alichofanya Lema ni too medieval. Angesubiri jamaa amalize yake kwa heshima ya wale wageni waliokaa pale, then angewaeleza privately mustakabali wa kisiasa ulivyo.

Sioni tofauti ya mtu kufanya kituko cha ajabu mbele ya wakwe zako. say kuvua nguo

sasa hata wewe umepoteza dila ya mawazo kabisaaa na nyumbani kwangu usikanyage !!!!!!!!!!!!!!.
umkaribishe mtu kwako halafu yeye awe ndiyo kidume , walahi haiwezekani.
 
sasa hata wewe umepoteza dila ya mawazo kabisaaa na nyumbani kwangu usikanyage !!!!!!!!!!!!!!.
umkaribishe mtu kwako halafu yeye awe ndiyo kidume , walahi haiwezekani.
kupandisha mori mbele ya wafadhili kama alivyofanya unaona ni sawa? si wafadhili wataona wanadeal na mtu ambaye weledi wake wa diplomasia ni hafifu
 
Hili lisipite bila mimi kutoa mawazo yangu.

reaction ya Lema haikubaliki kabisa, alichofanya Lema ni too medieval. Angesubiri jamaa amalize yake kwa heshima ya wale wageni waliokaa pale, then angewaeleza privately mustakabali wa kisiasa ulivyo.

Sioni tofauti ya mtu kufanya kituko cha ajabu mbele ya wakwe zako. say kuvua nguo
I second you,kwangu wote wana makosa,Mkuu wa mkoa kwa kutokurecognize efforts za mbunge na kw Mbunge kutokuweza kujicontrol emotions zake,kulikua na shida gani asubiri mpaka Gambo amalize then aongee na kueleza ukweli?Kuwa kiongozi inahitajika hekima ya hali ya juu,Ni vizuri viongozi wakawa na skill ya "Intellectual emotions".
 
Hili lisipite bila mimi kutoa mawazo yangu.

reaction ya Lema haikubaliki kabisa, alichofanya Lema ni too medieval. Angesubiri jamaa amalize yake kwa heshima ya wale wageni waliokaa pale, then angewaeleza privately mustakabali wa kisiasa ulivyo.

Sioni tofauti ya mtu kufanya kituko cha ajabu mbele ya wakwe zako. say kuvua nguo
I thought you would be objective. Hivi RC alifanya kitu sahihi? Simtetei Lema, nilitarajia ungewachambua wote wawili.
 
Haikupendeza lakini kuwa mpinzani wa kweli Tanzania lazima uwe na "ujasiri & ukichaa" wa aina fulani. Haya yote yasingesemwa na tusingeyajua kama Lema angenyamaza halafu asipewe nafasi ya kusema pale. Watu wa aina ya GL na TL hunipa matumaini hata mimi nisio na chama na sipendezwi na mwendo wa chama dola.
 
I thought you would be objective. Hivi RC alifanya kitu sahihi? Simtetei Lema, nilitarajia ungewachambua wote wawili.
kwa Gambo siwezi kumchambua...ni sawa na mtu alikuwa anaendelea kuongea ili tujue atamaliza vipi. Mara nyingi siwezi kumhukumu mtu kwa sentensi mbili na hata kama alikuwa tayari amekwishakosea kwa kusema ardhi imetolewa ma mawala advocates, tungesubiri amalize halafu Lema atoe masahihisho,

mbona magufuli kwenye msiba wa masaburi alitoa masahihisho mwishoni even if alikuwa ameshapewa fursa ya kuongea awali? sisi wapinzani tunahitaji kujifunza siasa safi
 
Hili lisipite bila mimi kutoa mawazo yangu.

reaction ya Lema haikubaliki kabisa, alichofanya Lema ni too medieval. Angesubiri jamaa amalize yake kwa heshima ya wale wageni waliokaa pale, then angewaeleza privately mustakabali wa kisiasa ulivyo.

Sioni tofauti ya mtu kufanya kituko cha ajabu mbele ya wakwe zako. say kuvua nguo
Alichokifanya Lema ndiyo sahihi kwa watu wote ambao wanajifanya Miungu hapa duniani. Kama hata mkono alimruka ya nini asubiri B aadaye. Malizia yote hapo hapo kila mtu akiona na kusikia,B aadaye yatakuwa majungu.
 
Alichokifanya Lema ndiyo sahihi kwa watu wote ambao wanajifanya Miungu hapa duniani. Kama hata mkono alimruka ya nini asubiri B aadaye. Malizia yote hapo hapo kila mtu akiona na kusikia,B aadaye yatakuwa majungu.
Upo sahihi mkuu!!Hakukuwa na mbadala!!
 
ZITTOPP.png

Jana October 18 2016 kulifanyika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo ya Burka nje kidogo ya jiji la Arusha, lakini shughuli hiyo ilisimama baada mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema kusimama kupinga maelezo yaliyokuwa yakitolewa na mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Maelezo ya RC Gambo yalisema kwamba eneo la mradi ule limetokana na maono aliyokuwa nayo Marehemu Advocate Nyaga Mawala, maelezo ambayo mbunge Lemaalikuwa akiyapinga na kudai yeye amehusika kutafuta ardhi na wafadhili, Lema alidai maelezo hayo yamejaa imejaa upotoshwaji na siasa ndani. Unaweza kuangalia video hii hapa chini.

Leo October 19 2016, mbunge wa kigoma mjini na kiongozi mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa facebook ametoa ushauri kwa RC Gambo na Mbunge Lema, Zitto amesema…..…

Nachukizwa sana kuona viongozi vijana wanafanya mambo ya hovyo. Mkuu wa mkoa wa Arusha mdogo wangu Mrisho Gambo una dhamana zaidi Kwa vijana. Mnapofanya mambo ya kijinga mnaharibu nafasi ya vijana kuaminiwa zaidi. Kaa Na Mbunge Godbless Lema mnywe kahawa pale New Arusha Na muanze upya. Ndugu yangu Lema nashauri punguza munkari.

Juhudi zako Arusha haziwezi kufutika kirahisi. Nakushauri kaa chini Na Mkuu wa Mkoa wako mpige mstari muanze Kazi upya Kwa pamoja. Viongozi jiepusheni kuonyesha hasira zenu hadharani. Sio hekima.


Chanzo: Millard Ayo
 
Hili lisipite bila mimi kutoa mawazo yangu.

reaction ya Lema haikubaliki kabisa, alichofanya Lema ni too medieval. Angesubiri jamaa amalize yake kwa heshima ya wale wageni waliokaa pale, then angewaeleza privately mustakabali wa kisiasa ulivyo.

Sioni tofauti ya mtu kufanya kituko cha ajabu mbele ya wakwe zako. say kuvua nguo

Hakikubaliki kwako. Ni haki yako kutokukubali

Lakini ili ku - defend hadhi yake (Lema) kisiasa, ilikuwa ni LAZIMA kuukabili uhuni na upotoshaje ule wa RC palepale bila kusubiri kuja kutoa "press release!!"

Na unawezaje kumtetea Gambo kwa kitendo chake cha;

1. Kukataa kuitikia mwaliko wa wafadhiri wale kwenda kuzindua mradi ule wa maendeleo ulio ndani ya mkoa wake mpaka ashinikizwe na wakubwa zake eti tu kwa kuwa hataki alipo yeye, mbunge Lema awepo? Hatuoni kuwa huyu ni kiongozi asiyefaa kwa sbb anaweza kutumia mamlaka na madaraka yake vibaya kwa kuonea na kunyanyasa watu ambao hawapendi kama anavyofanya kwa Mbunge Lema??

2. Kukataa kumpa mbunge mkono wa salamu wakati akiwasalimia wengine wote waliokuwa pamoja na mbunge meza mkuu?

3. Kuvuruga itifaki iliyopangwa na wenye shughuli huku akitambua kuwa yeye ni mwalikwa tu kwa nafasi yake ya kiongozi wa serikali?

4. Kuchelewa kufika kwenye tukio kwa zaidi ya masaa 5?

Kumbuka kwa waliokuwepo, wanasema shughuli ilikuwa ianze saa 2:00asb, RC akafika saa 7mchana bila maelezo yoyote na bila kuomba radhi hata alipopata nafasi ya kuzungumza!!
 
Siasa nzuri zilete maendeleo. Siasa chafu/za maji taka zisiruhusiwe katika kukwaza fursa za maendeleo.

Ukizingatia kuwa huo ni mradi wa afya. Anayemkataa mwingine, anakataa huduma kuwagikia wananchi/wanufaika.

Swali. Kulikuwa na haja gani ya kuibuka mvutano?

Jibu la swali lako ni hili;

Hakukuwa na haja.

RC huyo, hata kama hampendi mbunge wa eneo hilo.....basi, focus yake ingepaswa kuwa kwenye shughuli iliyompeleka pale...kuzindua mradi ule kwa kufuata utaratibu uliowekwa na wenyeji wake!

Ni bahati mbaya kuwa, Mrisho Gambo inavyoonekana ni kuwa, tangu anatoka nyumbani kwake kichwani mwake na fikra zake zilikuwa zimejazwa na jina la Godbless Lema tu tena ktk mtazamo wa chuki zaidi na mwisho wa siku hekima na busara zikamkimbia yakatokea yaliyotokea!!
 
Back
Top Bottom