TUJITEGEMEE
Platinum Member
- Nov 6, 2010
- 27,504
- 28,436
......
Kwa vile umeishajua mustakabali wako Chadema na kiukweli hatimaye utaondoka, sisi baadhi ya tunaokukubali, tunakuomba na kukusihi, usiendelee kuibomoa Chadema!. Chadema ina wenyewe ambao udini kwao sio tatizo, ukabila kwao sio tatizo wala ukanda kwao sio tatizo!, pigania haki yako, ili uondoke Chadema kwa heshima bila kunyea kambi!.
........
Pasco.
Naona mmejifunga vibwebwe kulitumbukiza taifa hili la Tanzania kwenye machafuko kwa nguvu zenu zote.....Kwa nini akili zenu zinawatuma kutumia propaganda za kishenzi/wildness yaana za kuchochea machafuko kwa nija ya kidini, ukabila, ukanda na propaganda za kishenzi kama hizo hali ninyi waandishi ndiyo hasa mnatakiwa kuubiri amani, umoja, mshikamano, kuvumiliana kusaidiana baina ya waafrika wazaliwa na waamiaji wa Tanzania? Kwa nini..!
Nakumbuka ulishawahi kuonywa huko nyuma juu ya propaganda zako hizi za kishenzi, ulisikia na ukaacha. Sijaelewa ni nini kimekusibu. Kwa ulichoandika hapa...natangaza kupatika ARAP SANG WA BONGO mwingine akimfuata THE BIG SHOW. Kwa kuwakumbusha tu...ARAP SANG ni mtangazaji na mwandishi wa habari wa Kenya ambaye ameshitakiwa huko ICC-The Hague kwa kutumia matangazo yake ya redio kuchochea maauaji ya wakenya baada ya Uchaguzi mkuu nchini humo
Kwa nguvu zangu zote popote nitakapo pata nafasi nitapinga utumiaji wa Propaganda za Kishenzi za udini, ukabila, n.k zinazoelekea kuleta machafuko nchi.
Ndugu wananchi, waafrika, watanzania wenzangu...TUWAPIGE VITA WALE WOTE WANAOENEZA UDINI, UKABILA, na mengine kama hayo ili kuleta machafuko nchi kwa kisingizio chochote kile. Kwa hili tuanze na Pasco wa JF na mwenzake THE BIG SHOW.
Nina imani tutaishinda vita hii maana tunaweza bila hata kuwewezeshwa na ndugu zetu wa mataifa ya nje.