Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep Quite!, Don't Ridicule Them!.

Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep Quite!, Don't Ridicule Them!.

Pasco unanisikitisha sana, una upeo wa hali juu sana kuliko haya uliyoandika hapa, unamponza sana huyo kijana Z na wapuuzi wengine wa aina yako, this is too low for u bro, unajidhalilisha, najua lengo lako ni kuchochea kuni lakini mtashindwa vibaya,

CDM haiwezi kufa kwaajili ya ZZK, au yyt yule. Sijaamini ni wewe umeandika upumbavu mkuu kiasi hicho cha kuchochea udini na ukabila, ths is very unfair. Nyie ndio mnajifanya wanaharakati na wakosoajinlakini mna malengo yenu, imeniuma sana msomi kama wewe unatumika, too sad bro,

Naamini utabadilika maana hata Hata kule Arumeru uliongea maneno kama haya ya kujipa moyo kwamba CDM itashindwa kwaajili ya baba yako EL bt nothing happened ukabaki kujishau, so hata mwisho wa siku utabakibkujishau tu " tuliwakosoa ndio maana wako hapa" acha unafiki mkuu
Mkuu naona ume'base katika personnal attack zaidi.
kwanini usijibu kwa hoja mkuu?
 
Pasco wewe ni classmate wangu pale Mlimani,ila kwa mara ya kwanza,ntakukosea adabu.Hii post yako ni ya kichonganishi na ya kipuuzi.You need to balance a story kama mwandishi mahiri.Injuction ambayo ina timeframe ya kuexpire within 6 months,u can't call it ushindi wa kishindo.Pia sio kweli,kwamba CC haikuwa na haina mamlaka ya kumvua mtu vyeo ndani ya chama.It doesn't demand microscopic eyes to look at cdm katiba and reliase that.
Kwa nature ya kesi jinsi ilivyo,ni wazi sasa mpaka imalizike CDM watakuwa wamekwishafanya uchaguzi.
Turufu walionayo CDM ni kwamba,kwa kuwa kesi kuhusu uanachama wake iko mahakamani,Zitto will automatically be disqualified to contest any post.
 
Too late kwa alicho post fb tarehe 5 na baadae kukifuta

too late kwa anavyomtumia m/kiti wa cdm tmk na kuhusisha chama na 'kutekwa'

too late kwa kikao alichokua amefanya leo na aliyokua amepanga kabla ya hukumu kama matokeo yasingekua upande wake

Pasco mtu ajabu sana
 
Mr,nakupa hongera,lakini sasa unyamaze sio kuadhiriana na wenzio mmetoka mbali tulieni mjenge chama ndio tumaini la watanzania.sikupenda yale uliongea jana.Always patience pays.
 
Tunachosema viongozi na washabiku woote wa chadema waliotoka kilkmanjaro ni washamba wa siasa na watachelewa sana kuleta mabadiliko katika Nchi hii na msiote kwamba mtachukuwa dola kwa kutegemea upande kaskazini hilo msahau
 
Labda CUF waliopoteza mwelekeo ambao hata hawajijui wanafanya nini
Chama chochote atakachoenda Zitto ataangaliwa kwa jicho la umakini sana,na sidhani kama kuna chama kitakachompokea mtu wa namna hiyo!!!Ccm wameshamtumia kama toilet paper hawana haja naye tena.Hata aliyesaini mkataba wa IPTL alihongwa gari na Wa malaysia akasaini mkatba wa 3bn kila mwezi kuwapa IPTL.Miafrika tunatia aibu sana yaani unahongwa kigari tuu unasaliti wananchi wote!!Shame Upon Zitto &Co
 
Zitto has won this battle but CDM will eventually win this war. Smart people do not fight battles they can not win. CDM did not need to fight this one.

Any intelligent, smart, well informed person can never truly belong to one political party. Before you start to argue, remember, looks can be deceiving, and in political games, nothing is what it seems to be.

The more you think you know something in politics, the more deceived you are. Unless, you are the politician playing the game.
 
Tusisahau, umeme juu,Gasi juu na subirini impact yake viwandani,Mashambani n.k ili tujifunze kusimama na kushabikia ya msingi.Huyo Zitto anakwenda kunywa mvinyo wake baada ya ushindi na Msando alafu waandamanaji watakutana na giza majumbani mwao baada ya luku kukata ghafla kutokana na kuweka umeme wa kuungaunga!

Watanzania haya yanafaa kuwa madogo na yale yanayogusa maisha yetu yawe makubwa! Gesi 65,000/= , Umeme unit 8 ni 10,000/= , maji hakuna wiki sasa alafu habari kama hizi ndio zinageuka BIG ISSUE!

Acha watukaange hadi tutie akili na ikibidi sembe kilo moja iwe laki na maharage hivyo hivyo!!!!!!!!!!:doh::doh::doh::doh::doh:
Mmeamua kujadili ya ZZK badala ya mambo ya msingi, suala la ZZK ni picha picha za kutusahaulusha/ kufunga mdomo suala la umeme na mengineyo.
 
Pasco nimependa sana ushauri wako kaz kwake kupoteza au kulinda heshima yake kwa staili atakayoitumia kuondokea.

Namshauri kufanyia kazi ushauri wako kwan hata atoe siri zote hazitakuwa sababu ya kumrudisha sana sana atazidisha uadui na wasio na uelewa hawatamuelewa kabisaaaaa
 
Wanabodi,

Kwanza nampongeza sana Mhe. Zitto Zuberi Kabwe kwa ushindi wa kishindo mahakamani leo kwenye kesi dhidi ya Chadema!.

Tangu day one niliwaeleza humu kuwa maamuzi ya CC ya Chadema, ni maamuzi ya kipuuzi kabisa sijapata kuona!, niliuliza hiyo CC ilipata wapi mandate ya kumvua ZZK madaraka yake wakati haina uwezo huo?!. Kesi ya msingi nayo pia atashinda!, Chadema italazimishwa kumrejeshea vyeo vyake vyote, kisha ufuate utaratibu rasmi kumvua vyeo hivyo na hatimaye kumvua rasmi uanachama wake!.

Ushauri wangu wa bure kwa Zitto, nakuomba sana, be calm, keep quite, don't boast, don't ridicule Chadema!. Pia usiendelee kutoa siri nyingine zozote za viongozi wako zaidi ya zile ulizokwisha toa!.

Sijapenda jinsi ulivyo toa siri za M/Kiti wako alivyopokea mihela ya Rostam na Mkono!. Sijapenda 'ulivyonunua' lile gari la Mkono bila kueleza popote umelinunuaje na kwa nini ulinunue kwake!, na pia sijapenda jinsi 'unavyolikodisha' lile gari jingine, huku ukiendelea 'kulilipia bila matatizo' bla kueleza lolote!.

Mkuu, kwanza nashangaa kwa nini unatumia neno "Sijependa", Kwani wewe ni Zitto? Au unataka kutuambia kwamba wewe ndo mshauri mkuu wa Zitto afanye nini wakati gani? Pia unataka kutuambia kwamba dili zote anazopiga Zitto na wewe huwa unashiriki lakini hizi na mkono hakukushirikisha? Lastly, kwa hayo ambayo hujapenda tena ya Kifisadi kabisa na yanaelezea kwa namna zote Unafiki, uongo, ulaghai, Usaliti na Ulimbukeni wa zitto siyo tu kwa chama alichomo (kwa amri ya mahakama) na kwa wanachama wake bali pia kwa watanzania wote (Anadanganya hataki posho kumbe anapiga dili kubwa kubwa yeye na Mbowe - They are all the same) bado unamgrade Zitto kama mwanasiasa anaefaa mbele ya jamii pana ya watanzania?

Nakushauri baada ya kushinda kesi hii ya pingamizi, pia utashinda ile kesi ya msingi, ila Baraza Kuu, litakuvua rasmi vyeo vyako vyote na litakuvua uanachama wako, ambapo nafahamu utarudi tena mahakamani kuweka pingamizi mpaka 2015!.

Logics zako kama marehemu vile, wewe huyuhuyu unasema asiibomoe CHADEMA, lakini pia unasema lazima baraza kuu litamfukuza na kumvua kila kitu, pia unasema ataweka pingamizi hadi 2015 why na kwa manufaa ya nani? This is too narrow. Mnataka kumuua huyu kijana.

Kwa vile umeishajua mustakabali wako Chadema na kiukweli hatimaye utaondoka, sisi baadhi ya tunaokukubali, tunakuomba na kukusihi, usiendelee kuibomoa Chadema!. Chadema ina wenyewe ambao udini kwao sio tatizo, ukabila kwao sio tatizo wala ukanda kwao sio tatizo!, pigania haki yako, ili uondoke Chadema kwa heshima bila kunyea kambi!.

Unaweza kuthibitisha udini, ukabila, ukanda n.k wa CHADEMA? I would be happy utufahamishe au unionyeshe mahala popote, forms au kitu chochote kinachoonyesha kwamba ukitaka kujiunga CHADEMA lazima ujaze form na uwe approved unatoka ukanda,dini na kabila gani? This is also extreme pathetic for you to denounce them publicly like you did in this awkward post.

NB: Kukaa kimya kama ulivyomshauri Zitto wakati mwingine ni jibu. Wewe hukutakiwa kuandika haya. Yamekuacha uchi kuhusu weledi na nia yako kwa taifa hili na watanzania maskini.

NArudia tena, hongera sana Zitto Zuberi Kabwe!.

Congratulations!.

Pasco
 
Hongera Zitto.

Nami naungana na Pasco kukuomba umuache mbowe apumue kwa sasa,mishale uliyompiga kwa sasa inatosha.
Waache waseme lakini kwa sasa wewe wanyamazie hili tujiandae kwa case ya msingi na kule baraza kuu la chama.

Kwa kweli ningependa kuona sasa hivi una kuwa mtulivu na kuandaa nondo za kutosha kama kawaida yako.

Naomba utulie kwa sasa.

Hila ni vyema watu wakajua kuwa chanzo cha haya mambo kilianza kwenye ukaguzi wa mahesabu ya vyama na wanachadema kupitia media walianza kumtuhumu na kumkashifu zitto.

Aliye koleza moto alikuwa Godbless J Lema aliyekuja humu jamvini kumtuhumu zitto huku akiungwa mkono na makamanda wake wa Arusha na mimi binafsi niliwambia lema ndio atakuwa chanzo cha mgogoro mkubwa wa chadema, hakuishia hapo bali aliendelea kutoa tuhuma zake kwa kiongozi wake, pengine ilikuwa strategy ya kumuondoa zitto ndio maana lema hakukemewa bali alichekewa.

Nivyema Tundu Lissu akafanya kazi yake vyema ya kutoa ushauri mzuri kwa chadema lasivyo ataendelea kuhiingiza kwenye matatizo.

YANI MTU ANA PEWA ADHABU ALAF NDIO ANAITWA KUJITETEA?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu,

Kumtetea Zitto dhidi ya Chadema kwa mantiki ya hoja zinazoendana na UDINI,UKABILA na UKANDA ni UWENDAWAZIMU wa kiwango cha juu!

Sitaki niamini kuwa mtu ninayeamini ana 'hoja za nguvu' amekuwa MWENDAWAZIMU!

Pole!
 
Chadema msi sahau kuwa mahakama hime wasamehe pamoja na kuhidharau.
Tundu Lissu ni mwana sheria mzuri lakini muda mwingine anazi changanya sheri-jk
 
Last edited by a moderator:
Nawashauri viongozi wa chadema mwache ku-shout juu ya hukumu iliyotolewa, pray calm na mwacheni ZZK apeleke rufaa yake baraza kuu kama atakavyo na kama ni kweli katiba yenu ndivyo inavyoelekeza. Kama ZZK hakuwa na hila yoyote katika chama na that hatumiki na maccm Mungu atasimama na kumtetea and so atapata haki yake but otherwise kama anatumika na maccm Mungu ataitetea CDM na itasimama ili iwakomboe watanzania waliopigika.

Wajumbe pia kama kweli mna uchungu na chama kwamba chama kimekubaliwa na watanzania kwani wana matumaini kuwa kitawakomboa, mnatakiwa mumpime ZZK kwa tabia aliyoionesha kwa viongozi wake, kuanzia kwanza jitahada zake za kutaka uenyekiti akiwa kijana mdogo kabla hata Mbowe aliyemleta chamani hajamaliza term ya pili kwenye uenyekiti na huku akiwa anafanya vizuri na kujitoa kwa hali na mali, pili namna waraka ulivyoandikwa kwa kashfa kwa viongozi ambao wamekisaidia chama kukua (Hata kama anakana kushiriki kuuandaa ama kuufahamu) na tatu matusi aliyoyatoa kwa Mbowe baada ya taarifa ya Lisu juu ya magari aliyopewa na Mkono kana kwamba ni Mbowe aliyemtuhumu. Waweza kuona ni kiongozi wa namna gani.

Nionavyo mimi CDM ni chama cha ukombozi na kuna watu wamekipigania mpaka hapo kilipofika kwa hali na mali, issue kubwa hapa ni kuwatoa maccm na si kujifanya tunatafuta demokrasia na kama CDM ikiona kiongozi hafai mabadiliko yangefanyika kwa mujibu wa katiba na si nyaraka za matusi. Kuna kila dalili kwa uongozi uliopo kuwa maccm wataondoka 2015, waweza kuona kuwa kwa matumaini ambayo yamejengeka kwa watanzania kwa chadema pengine ni kweli ZZK ametumika na maccm kuleta mzozo ndani ya chama ili kisiwe na nguvu tena ya kuishinda ccm na coincidence ya matamko ya kina Wasira na Lukuvi na namna mzozo ulivyoanza inatia mashaka na mtu aweza kufikiri kuwa ZZK ametumika.

Kama kweli Zito umetumika ni vizuri ukutane na wazee wa chadema na kuomba radhi hata kama hutasema --------- ili chama kisivunjike na kushindwa kuwaondoa maccm na kuwakomboa watanzania kwenye ziki wanazopata. Na kama hutafanya hivyo (that umetumika na hutaki kuwahurumia watanzania that lengo lako/lenu chama kishindwe kuwakomboa), Mungu atakulaani. Chama kina malengo mazuri juu ya watanzania hata kama viongozi waweza kuwa na kasoro zao kwani wao si maraika.
 
Asanteni CHADEMA kwa kugombana, huyu kijana Zito alishatudanganya!Kumbe ni chui aliyevaa ngozi ya kondoo, hafai hata kuongoza kijiji! Kwa bahati nzuri anakwenda Masumbuko Lamwai Road, safari njema!
 
Back
Top Bottom