Ushauri wa bure kwa Waislam

Ushauri wa bure kwa Waislam

Status
Not open for further replies.
Asante sana Mkandara. Sasa Jukwaa limepata watu wenye akili huru katika kufikiria. Sasa ndugu yangu ulikuwa wapi siku zote hizi. Kama ungetokea mapema tusingetumia nguzu zote hizi. Hakika Mkandara, ulichosema ndio hasa madai yetu. Na tuna omba Marafiki zetu na Maadui zetu watuelewe hivyo.

Kamwe hata siku moja, Waislamu na Uislamu hauna uadui na Wakristo au wasikua na dini. Waislamu siku zote Mpaka Mwisho wa Dunia, watakua wanapambana na wale wanao wazuia kutekeleza matakwa ya dini yao na kufanya ibada zao.

Asante sana Mkandara Mimi MZIMU waKiwangwa, nimekuelewa sana. Na naomba Mejor General kahtaan, Field Mashal peri, Comandoo Ritz na Wanaharakati wengine wote tumpe heshima yake Huyu Bwana Mkandara. Bwana Mkandara, hizi sentensi chache ulizo ziandika hapa, tunaomba uzirudie rudie katika Bunge La Katiba kila upatapo nafasi.
Mkuu MZIMU.

Mkubwa wetu Mkandara tupo nae muda mrefu humu kwenye Jihadi toka 2008.
 
Last edited by a moderator:

Wewee hicho kilikua kiini macho, kuzifanya ni shule za serekali lakini mkakati ulikua kuhakisha wanafunzi wa kiisalamu wanapungua kadri wanavyo zidi kupanda madarasa. Mwisho wasiku, wakati wanafunzi wote walianza darasa la kwanza almost 50- 50, Watoto wa Kislamu waliokua wanafanikiwa kupenya hadi chuo kikuuu, walikua chini ya 12%.

Matokoe yake Ngazi zote muhimu za serekali na Mashirika ya Umma zilishikwa na Wakristo huku waislamu wakiambiwa hawaja soma. Nawaliosoma pia, walihakikisha hawashiki nafasi nyeti serekalini. Halii ilikua Mbaya hadi Rais Ali Hasan Mwinyi alipoingia Madarakani na kuanza kufuta baadhi ya hizo athari. Kama unakumbuka vizuri na huna akili za kushikiwa, Raisi Ali Hassani Mwinyi hakuwa na Maelewano Mazuri na Nyerere hadi ikafikia hatua ya kupigana vijembe hadharani.

Kama unakumbuka, Nyerere aliwahi kunukuliwa akisema nchi inaongozwa na Mwanamke katika hatua zake za Kumprovoke Ali hassani Mwinyi.

Kwaupande wake yeye Mwinyi aliwahi kumjibu huyu Mheshimiwa sana, katika Sherehe zilizofanyika Uwanja wa Taifa kwa Kusema, '' Ukiwa Mtoni unaoga, akaja kichaa akachukua Nguo zako, Usimfukuze. Nyote Mtaonekana Vichaa''.

Dogo upo?. Kwa taarifa yako hali unayo iona sasa katika Serekali iliyopo sio Bahati mbaya. Yote hiyo ni Mikakati ya Waisilamu kuvunja adhari za Makanisa na ukiristo katika Mifumo ya Serekali na Utendaji, kama inavyo julikana kwa sasa MFUMO KRISTO.

Baada ya kibao kimeguaka, Makanisa na Wafuasi wake wakanza kugeukia katika Propaganda mbalimbali zikiwemo za vyombo vya Habari kuweka vijana wao walio brainwashed kua Yesu ni Mungu, na kueneza chuki dhidi ya Uisalamu na Waislamu na kujaribu kumchafua Ali Hassani Mwinyi kua haja fanya lolote katika nchi hii, wakati aliichukua nchi ipo kwenye njaa, watu wanapanga foleni kutafuta bidhaa muhimu, kama vile unga, sukari, mafuta ya taa n.k.

Wakati Ali Hassani Mwinyi anachukua nchi, bidhaa kama Sabuni za kuogea na dawa za meno zilikua ni bidhaa za anasa mtu wa kawaida alikua hawezi kua nazo.

Nakumbuka hata sabuni za kufulia kulikua hakuna. Tulikua tunafulia Majani ya Migomba. Daftari za kuandikia iliku hakuna, tulikua tunaandikia makaratasi ya Mifuko ya cement.

Rais Ali Hassani Mwinyi alipoingi Madarakani, akaiondoa hali hiyo mara moja. Akaruhusu kuanziswa kwa vituo vya Television.

Hali ya nchi ilikua imeanza kubadilika na kua nchi yenye neema. Kama Mgonjwa alieanza kupata nafuu.

Kuona hivyo, Baraza la Maaskofu KKKT, wakachapisha waraka kua nchi imejaa Rushwa, nchi inanuka.

Hilo hakika lilimuuzi sana Rais Ali Hassani Mwinyi. Akaamua kuwaondelea uvivu Maaskofu na Wakristo wote. Aliitisha Mkutano wa Wazee wa Dar- es -salaam Pale katika Hotel ya STAR LIGHT jioni saa kumi. Rais Ali Hassani Mwinyi aliongea kwa Masaa mawili bila kukaa kwa hasira. Aka wauliza Maaskofu, Nchi hii inanuka, imejaa rushwa mmeiona leo. Wakati watu wanapanga foleni za mawe kutafuta bidhaa Muhimu, nyinyi mlikua wapi?. Wakati Colgate ni bidhaa ya anasa, Nyinyi mlikua wapi?.

Akawaambia, Ndugu zangu Maaskofu, Ya Kaizari mpeni Kaizari na ya Musa mpeni Musa.

Mpaka hapo unaelewa hilo?. Sio mnakuja humu na kuropoka tu. Hamjui tumetoka wapi wala tunaenda wapi?.
Hii bayana naichukuwa kama data kwa siku za baadae.
 
Mmepata ufadhili wa ISIS,BOKO HARAM au AL SHAABAB? Muulizen sheikh farid raha ya ndoa ikoje huko aliko
Mkandara yupo JF wakati wewe bado upo kijijini kwenu haujui Jambo Forums ni nini, teh teh teh!!
 

Wewee hicho kilikua kiini macho, kuzifanya ni shule za serekali lakini mkakati ulikua kuhakisha wanafunzi wa kiisalamu wanapungua kadri wanavyo zidi kupanda madarasa. Mwisho wasiku, wakati wanafunzi wote walianza darasa la kwanza almost 50- 50, Watoto wa Kislamu waliokua wanafanikiwa kupenya hadi chuo kikuuu, walikua chini ya 12%.
.

Huo upuuzi mwingine ulioandika sina haja ya kucomment na kujaza page.. Hilo la kupenya hadi chuo kikuu ni kutokana na mwamko wa waislamu wengi kwenda shule kipindi kile. Na mtakumbuka maneno ya Prof. Kapuya na Makamba enzi zile walivyowaambia acheni kuilaumu serikali haiwasaidii waislamu, kazaneni muende shule..

Mimi nimesoma shule mbali mbali, na katika hizo shule including vyuo vya elimu ya juu, wengi wetu tutatambua ubaguzi wa kidini ambao umekuwa ukiendeshwa na hii inatokana na watu kuwa na mawazo mgando kama yenu kuwa "tunaonewa". Group discussions badala ya kukazana kuungana au kuwa na mix ya watu wenye uwezo, watu wanakomaa na watu wa dini zao...

Hebu tuache kueneza propaganda za kidini kaeni chini mfanye kazi na kuacha kukaa barazani kunywa kahawa mkitegemea serikali itawakomboa...

Ushauri; siku nyingine jibu hoja kwa hoja na sio porojo.. Ungejibu maswali yangu ningeona una malengo ya kujadiliana kwa hoja..
 
D2050 nikupongeze kidogo wewe hujatukana sana kma kawaida ya wanaitwa waislamu halisi......mimi nina rafiki yangu ni muislam safi wa swala 5 na surual fupi....huwa ananambia mahakama ya kadhi wengi wasiyoitaka ni waislamu wasomi na wenye uelewa wa haki za binadamu.huwa anaelezea mambo meng sana....mengine si vizur kuandika....ila mimi naona moja ya madhara hayo ni ...
1. Kuvunjika kwa umoja wa kitaifa uliopo kati ya waislam, wakristu na wapagani
2. Ugomvi wa kimaslahi kati ya wakristu, wapagani na waislam. Endapo Mahakama ya kadhi itaingizwa kwenye katiba ya nchi ni wazi itagharamiwa na serikali na hivyo viongozi wa dini ya kiislam ambao ndiyo watakuwa makadhi watatumia fedha za walipa kodi wa Tanzania ambao ni waislam, wakristu na wapangani kujinufaisha wenyewe kwa kujitengenezea ajira. Vipi kuhusu viongozi wa dini za wakristu Maaskofu, Mapadri, Wachungaji na Viongozi wa dini za Jadi nao watakuwa wanalipwa na Serikali?
3. Kutoweka kwa wakristu kutokana na utawala wa sharia, sababu hukumu iliyo tawala kwenye sharia ni kifo hivyo wakristu watauwawa kwa kuwa hawatakubali kuishi tamaduni za kiislam.
 
Mkandara yupo JF wakati wewe bado upo kijijini kwenu haujui Jambo Forums ni nini, teh teh teh!!
Ritz na wewe unalalamikia suala la elimu? Labda benno malisa aje atusaidie
 
Last edited by a moderator:
Huo upuuzi mwingine ulioandika sina haja ya kucomment na kujaza page.. Hilo la kupenya hadi chuo kikuu ni kutokana na mwamko wa waislamu wengi kwenda shule kipindi kile. Na mtakumbuka maneno ya Prof. Kapuya na Makamba enzi zile walivyowaambia acheni kuilaumu serikali haiwasaidii waislamu, kazaneni muende shule..

Mimi nimesoma shule mbali mbali, na katika hizo shule including vyuo vya elimu ya juu, wengi wetu tutatambua ubaguzi wa kidini ambao umekuwa ukiendeshwa na hii inatokana na watu kuwa na mawazo mgando kama yenu kuwa "tunaonewa". Group discussions badala ya kukazana kuungana au kuwa na mix ya watu wenye uwezo, watu wanakomaa na watu wa dini zao...

Hebu tuache kueneza propaganda za kidini kaeni chini mfanye kazi na kuacha kukaa barazani kunywa kahawa mkitegemea serikali itawakomboa...

Ushauri; siku nyingine jibu hoja kwa hoja na sio porojo.. Ungejibu maswali yangu ningeona una malengo ya kujadiliana kwa hoja..

Ndugu yangu wewe unamakengeza ua vipi?. Uislamu sio Majina, tumia akili yako vizuri. Ulishamuona mtu akawa Muislamu akamiliki Bendi ya Muziki, au kufunga ndoa na Mkristo au asiekua Muislamu.
 
MZIMU pole sana kwa pigo takatifu la karne,vipi mkuu,jihadi imeishia wapi au jeshi limesambaratika,niliona ulianza kugawa vyeo vya kijeshi
 
Last edited by a moderator:
Nakupa angalizo dogo tu kwamba hii katiba ni ya miaka hamsini ijayo,nina imani katika maisha yako mpaka unakufa hutalishuhudia taifa hili likiwa na taasisi yenye mandhari ya udini
 
Last edited by a moderator:
hizo jumuiya kama zitakuwa hazitambuliwi kisheria zitakuwa hazina maana.huwezi kuunda jumuiya inayo towa taraka kwa waislam pindi wakiachana kisha ukienda mahakamani unaambiwa taraka hiyo batili.

mahakama ya kadhi haiwahusu nyinyi wakristo,tunahusika sisi waislam.

Sheria ya mirathi kwa waislamu mtoto wa asie zaliwa ndani ya ndoa haruhusiwi kurisi mali ya marehem.je mahakama za serikali inalitambuwa hilo?

Wakristo kwanini mnapinga mahakama ya kadhi wakati haiwahusu?tukisema mna husda nyinyi wakristo mtabisha?

Huo ndo upuuzi wa karne ya zamani kutaka utumike hadi leo. Huyo mtoto wa nje ya ndoa yukoje ktk dunia hii ya sasa? Yaani kwa upuuzi wa huyo anayeitwa marehemu,mndi iwe sababu ya yeye kukosa haki ya babanyake?
 
Huo ndo upuuzi wa karne ya zamani kutaka utumike hadi leo. Huyo mtoto wa nje ya ndoa yukoje ktk dunia hii ya sasa? Yaani kwa upuuzi wa huyo anayeitwa marehemu,mndi iwe sababu ya yeye kukosa haki ya babanyake?

Ushasema huu upuz so hata huyo mtoto ni mpuuzi.sisi waislam hatuwatambui watoto wanaotokana na upuuz
 
Wandugu kinachosababisha watu watake hii mahakama iwe kwenye taratibu za ngazi za mahakama ni kufanya mambo ya waislamu ya kijamii yahukumiwe katika utaratibu uliopo kwenye quran tukufu.
Kuna watu wengi wanaunganisha familia (ndoa) kwa hiyari yao wenyewe katika taratibu za kiislamu, lakini unapofika wakati wa mashtaka wanakimbilia serikalini ambayo haina sheria hata moja ya kiislamu.
Kama mti akiua mathalani anaweza kufunguliwa kesi kwenye mahakama ya wilaya, atasomewa mashtaka lakini ataambiwa hatakiwi kujibu chochote mpaka hapo kesi itakapohamishiwa mahakama kuu.
Sasa kwanini isiwezekane mtu kufungua kesi ya mirathi au talaka mahakama ya wilaya akaambiwa kesi hiyo itahamishiwa mahakama ya kadhi? Je unaweza kuweka mfumo kama huu katika mahakama halafu uendeshaji wake usihusishe mapato yanayokusanywa katika taratibu za kiserikali?
Tafakari!
Kwa namna Serikali haiwezi kuruhusu kila mtu kuwa na mahakama anayojisikia yeye kuwanayo. Kama Waislam wanaona hawatendewi haki na mahakama zilizopo kwa mujibu wa Quran hata Wakristo watadai mahakama yao kwasababu mahakama zilizopo haziwatendei haki kwa mujibu wa Biblia Takatifu. Mfano Biblia imetuagiza kusamehe 7x70, lakini mahakama zilizopo hazitusamehe hata mara moja labda ukae jela miaka kadhaa ndipo huruma ya rahisi ikupitie. Kwa mantiki Wakristo tunataka mahakama ambazo tutakuwa tunasameheana 7x70. Je na wakristo wadai mahakama yao iwepo kwenye katiba? Iwapo serikali itaruhusu kila dini kuwa na mahakama yake, Je mahakama zilizopo zifungwe au zifutwe ili kila dini itumie mahakama yake ya dini?
 
MZIMU pole sana kwa pigo takatifu la karne,vipi mkuu,jihadi imeishia wapi au jeshi limesambaratika,niliona ulianza kugawa vyeo vya kijeshi

Nakupa angalizo dogo tu kwamba hii katiba ni ya miaka hamsini ijayo,nina imani katika maisha yako mpaka unakufa hutalishuhudia taifa hili likiwa na taasisi yenye mandhari ya udini

Mzimu tupo usifikir tumekuacha Ila hatujaona jipya tunaona wanaropokaropoka tu

Haya bwana! Asiekubali kushindwa si mshindani, kipa kauza timu, sasa sisi tutafanyaje. Ila mark my words. You have just won a battle, the War still rages on.

Ila najua mnajua na mnakiri kua tupo sahihi, ila mnashindwa kutuunga mkono, kwa sababu kuna watu kama hao ndani ya jitihada zetu.
 
Kidumee Sheikh Farid akisalisha . Nyuma walo maamuma Karume na Shein Leo watanganyika wamemlawiti.... uhaini mkubwa na shari kubwa kwa uislam

Mbona unakauli chafu mkuu?

Turudi kwenye, unadhani kunaulazima gani wa mahakama yakadhi kuwepo kwenye katiba?
 
Waisilamu nchini wamekuwa wakiilamu serikali kwamba imewaundia chombo ambacho ni BAKWATA, na kwamba hawakitaki kwa kuwa hakijaundwa na waisilamu. Waisilamu hao hao wanaitaka serikali iwaanzishie chombo kinachoitwa Mahakama ya Kadhi. Sasa hapa naona kuna ujinga fulani. Unalalamika serikali kuwaingilia kwa kuanzisha BAKWATA, halafu unalalamika kwa nini serikali haiwaingilii kwa kuwaanzishia Kadhi. Waisilamu wawe wazi basi, wanapenda kuingiliwa au kutoingiliwa na serikali?

My take:
Kwa kuwa waisilamu wameshalalamika sana kwa suala la 'kuundiwa BAKWATA', naishauri serikali isijiingize kabisa kujaribu kuwasaidia tena, kwani watakuja kuilaumu tena na tena serikali kwa kuwaingilia. Waisilamu wajipange, waanzishe Mahakama ya Kadhi, waiendeshe wenyewe, wahukumiane wenyewe na hata hukumu zikiwa mbaya, walaumiane wenyewe

Wewe wacha hoja za kijinga na ukifuu.
Bakwata ni taasisi ya iliyo undwa kwa kiasi kikubwa na Nyerere lengi ikiwa udhibiti wa waislam wasipinge sera zake la kulinufasisha kanisa kama alivo liahidi.hata baada ya kuondoka yeye
Bakwata ni sawa na tawi la ccm limekuwa likichaguliwa viongozi kwa kuwekwa hata watu wasio soma mfano wa mufti wa sasa.
Hili waislam wamesha achana nalo na bakwata imebaki kutangaza siku ya eid kwa vile inakua holiday otherwise haina impact yoyote na kila muislam anaejijua ameachana nayo.

Tuje kwenye mahakama ya Kadhi.
Hii ni mahakama ya sheria.
Kama mahakama nyengine mfano mahakama ya chini ya juu yaani high court au mahakama ya appeal.
Pia ni sawa na mahakama ya kazi au mahakama ya watoto au mahakama ya biashara au mahakama ya ardhi.
Hizi zote ni mahakama lengo likiwa ni kuendesha mashtaka madai na kutoa hukumu kwa mujibu wa sheria zinazohusika.
Na serikali imezigawa court hizi ili kuleta ufanisi zaidi.
Mahakama ya kadhi nayo ni mahakama ya sheria itakayo simamia haki na sheria inazohusu ndoa na mirathi ya waislam.
Waislam wana utaratibu wao katika mambo hayo.
Katika nchi yenye serikali halali yenye katiba mambo yote yanayohusu sheria huwa chini ya serikali yenyewe ndio msimamizi wao ndio dola.
Mahakama hizi zitaajiri wanasheria na majaji walo somea islamic law kwa viwango vitavo wekwa kama majaji wengine wa sasa hivi. Hapa bakwata hawaingii wala sio suala la kuwaundia waislamu kama ilivo kuwa bakwata.
Sheria siku zote husimamiwa na serikali na mahakama zake..na hio hufanya hukumu zitolewazo kuwa halali kwa zinakuwa kwa mujibu wa katiba ya nchi na katiba inazilinda.
Njee ya mfumo wa serikali hakuna mahakama .
Hapo nyuma mahakama hizi zikikuwapo na hazikuleta problem yoyote.chuki ya nyerere kwa waislam ndio akazifuta bila ya sababu za msingi.
Chuki ile ndio amewarithisha leo mkaona mkatae tu .
Inavo elekea nchi hii waislam wao wakubali ku sacrifice mambo mengi ili kuleta umoja na uwelewano.mfano nchi za kiislam zinapumzika alkhmis na ijumaa ili wapate muda wa kusali siku ya ijumaa.vile vile nchi za kikristo wao hupumzika jumamosi na na jumapili ili wasabato na wakatoliki wapate muda wa kwenda kanisani.
Tanzania sio nchi ya kikristo ila mkoloni alikua mkristo akatuwekea utaratibu huu kwa vile alikuwa jumapili anaenda kanisani. Utaratibu huu tukaurithi mpaka leo na waislam wameridhia kama njia ya kustahamiliana.pia
Serikali imekua ikiingia mikataba mingi kwa niaba ya kanisa pia imekua ikiziendesha tasisi zake zake kwa mabilion kila mwaka inawalipa madaktari wote katika hospital za kanisa na hospital hizo hazitoi huduma bure ila kwa malipo na ni ghali mno na waislam pia hilo wanaliona sawa ni katika kuvumiliana.
Leo kuendesha mahakama yenye mahakimu wasio zidi 50 kulipa mshahara hawa watu basi wakristo wana mind sana !! Ilhali hizi mahakama kimsungi ni za madai hivyo kuna malipo yakufungulia kesi na pia kwenye urithi sehemu ya mali hukatwa kama kodi kwa serikali.
Wakristo wanaonesha chuki tu kwa visababu vya uongo uongo ili jambo hili lisipite wao wanadhani ndio wanauzuia uislam usisambae tanzania.
Tunahitaji kustahamiliana kuleta utengano katika nchi.
Haya tuyowafanyia waislam kwa vile mumehodhi bunge sio la kujisifia nchi inaenda kidogo kidogo kwenye mawazo ya hili la waislam na hili la wakristo..nchi moja njia tofauti hatutofika popote zaidi ya kuchukiana ndani ya nchi moja
 
Kuna kitu kimoja wengi wetu hatukijui kwamba mkristo hawezi kumshauri kitu muislam na muislam akakubali na muislam vile vile hawezi kumshauri kitu mkristo na mkristo akakubali lambda hilo lifanyike nje ya dini na bila kutumia jina la dini yeyote
 
Tatizo la watu wa imani hii kwanza hawaelewani, na hawaelewi hata imani yao inataka nini na kwanini. Kukosa kuelewa huko kumewafanya wakose hoja na kukosa hoja ndioko kumewafanya wajisikie inferior bila sababu na hivyo ndiyo maana kila wakati, mahala pote huwa wako suspicious na defensive na ndiko kutumia mabavu kwa kila jambo.

Ushauri hawashauriki hasa katika mema. Hakuna kitu utawashauri wakubali hata kama hawana hoja. (mfano, kwa nini mahakama zao ambazo ni ibada wanataka ziwekwe na serikali badala ya kuzifanya taasisi zao za kidini misikitini kama vile makanisa wanafanya), watakachokuambia ni matusi, na kutishia kufanya fujo kwa kisingizo kwamba wao wako wengi eti kwa kuwa hawanaga uzazi wa mpango, na vile wanavyotoa zawadi kwa muislam akioa mkristo.
Lakini kwamba wanahoja, hakuna.

Jambo lingine hawa watu si rahisi kuwashauri kutenda mema kwa sababu dini yao haina nguzo ya upendo. Wewe ukiwashaurim upendo, amani na kusameheana, halafu mwingine awashauri chuki, fujo visasi na mauaji, utashangaa watakavyochangamkia tenda za chuki, fujo, visasi na mauaji. Wanafanya hivyo hadi misikitini wao kwa wao wanamalizana halafu wanasingizia Westerners na Wakristo eti ndio wanawashauri hivyo. Hawatakumbuka kama kuna ushauri wa upendo, amani na msamaha. Ni jambo la ajabu sana kama dini yao inawafundisha upendo na amani, inakuwaje wanakimbilia kuwatii makafir wanaowafundisha chuki, mauaji na ushetani wote wakati hao makafir maisha yao yamejaa amani.

Kikubwa ili serikali iweze kusimamia vizuri vichwa vya namna hii, ni vyema ikae kwenye nafasi ya juu ya imani zote ili isimamie na kudhibiti pale ushetani unapotokelezea kwenye misiikiti kama Lyatonga. Katiba ni ya watanzania wote, habari za kadhi, misikitini.
screentouch

Wewe kama sio uislam ungebaki hukoo kijijini unalala na ngombe.
Jiangalie na mababu zako tuliwapokea na hatukuwa chinja...mlipokuwa na njaa na babu zako mlipolima vijijini na chakula hakizai ni muislam alo kufanya leo uwe na simu ya ku chat hapo babu yenu akisema ni anasa...ujinga mtupu..
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom