hizo jumuiya kama zitakuwa hazitambuliwi kisheria zitakuwa hazina maana.huwezi kuunda jumuiya inayo towa taraka kwa waislam pindi wakiachana kisha ukienda mahakamani unaambiwa taraka hiyo batili.
mahakama ya kadhi haiwahusu nyinyi wakristo,tunahusika sisi waislam.
Sheria ya mirathi kwa waislamu mtoto wa asie zaliwa ndani ya ndoa haruhusiwi kurisi mali ya marehem.je mahakama za serikali inalitambuwa hilo?
Wakristo kwanini mnapinga mahakama ya kadhi wakati haiwahusu?tukisema mna husda nyinyi wakristo mtabisha?
Uko sawa kabisa kuwa Mahakama ya Kadhi haiwahusu wakristo, lakini kumbuka nchi yetu inamchanganyiko wa madhebu mbalimbali na wasiokuwa na dini. Nauliza maswali haya ukinijibu vyema bila kumuumiza mtu, nita amini unachokisema:-
1: Je, Kadhi Mkuu na Makadhi wa kuendesha mahakama hizo watapatikanaje, nani atawateua/atawachagua?
2: Je, gharama za uendeshaji zitagharamiwa na nani?
3: Pesa za kodi za Wananchi yaani waislamu, wakristo na wasio na dini zitatumika kuendesha mahakama hizo?
4: Kwa vile kuna ndoa za watu wa imani tofauti, je mwanandoa asiye mwislamu naye atahukumiwa katika mahakama hizo iwapo kutatokea mtafaruku katika ndoa yao?
5: Je, kwa mwislamu mwenye shauri katika mirathi au ndoa, ni LAZIMA apeleke shauri hilo kwa mahakama ya kadhi au atapewa rukhsa achague sehemu ya kulipeleka?
6: Mnasema Mahakama ya Kadhi itashughulikia Mirathi na Ndoa, je makosa ya kijinai yanayohusu "jamii na rasilimali za waislamu" hayatapelekwa kwenye mahakama hizi?
7: Je, mtu (mwislamu au asiye mwislamu) akiudhalilisha uislamu kwa namna yeyote ile, hatatangaziwa fatwa (hukumu) na mhakama hizi za kadhi?
8: je, huu sio mwanzo tu wa kuendelea kuingiza mambo ya kiislamu kwenye taifa la kisekula? Mfano; mlianza na uvaaji wa hijabu mashuleni na maofisini mkakubaliwa, mnaingiza mahakama ya kadhi..., mtaendelea Ijumaa nayo iwe siku ya mapumziko..., nafasi za serikalini ziwe nusu kwa nusu bila kujali sifa za nafasi husika..., Mwezi wa ramadhani watu wote wafunge... nk!
Ni nayo mengi ila kwa kuanzia ni hayo tu!