Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 43,037
- 34,741
MziziMkavu bado unazidi kuonyesha uwezo mdogo wa kufikiria na ujuzi wako mdogo kwa kuwa mtu wakumsilikiza Ilunga. ushauri fuatilia Tume ya kubadilisha sheria ya profesa Ibrahim Juma (Bingwa wa sharia law) ambayo pia ilisema serekali haiwezi kuanzisha mahakama ya kadhi. Huwezi kuwa na sheria tofauti kwa makudi tofauti ukawa na nchi moja. Ndio maana na sema na sisi wamasai tutadai na dini zetu zisitambulike ili tukiiba ng'ombe iwe halali kwasababu ndio Dini yetu inasema Ngomezetu dunia ni zetu wamasai na watu wengine wenye Ng'ombe wanatutunzia tu. Wakristo nao hawatambui talaka na kama mume na mke wakiachana haitambuliki kisheria wakati waislam mna talaka sijui tatu. Mahakama ya kadhi ni sawa na ubaguzi wa afrika ya kusini ulioweka sheria tofauti kwa wazungu na sheria kwa waafrika.
Hata raisi wennu zaifu alisema hapa (https://www.youtube.com/watch?v=Pk_ZyYwdIpE) ila tatizo CCM wanataka kubaki madarakani na wako tayari kufanya lolote iliwabaki madarakani ndio wanaleta siasa za makama ya kadhi. Hata Kenya mahakama ya kadhi iliingizwa kisiasa tu ila kama kweli unaangalia uwasa wa wananchi wote katika sheria huwezi kukubali mahakama ya kadhi. Waisilamu wenyewe bado hata amukubaliani jinsi ya kuziendesha maana wengine wanasema wanawake hwaruhusiwi kuwa kadhi wakati wangine wanakata kwa kisingizio cha Kadhi mwanamke hawezi kufungisha ndoa akiwa mwezini (https://www.youtube.com/watch?v=Ux_gaR4NxKY). Sasa kweli serekali inatakiwa kuingia kwenye mjadala wa ndoa sio halali kwasababu kadhi aliyefungisha ndoa alikuwa mwezini.
Je unaujua umuhimu wa mahakama ya Kadhi?
Last edited by a moderator: