Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Ni kweli mkuu kuna kifua kikali hata mamito wangu kilimtesa almost 3 months mpaka tuka check TB lakini tukajagundua ni alergy, tulitumia dawa ya vidonge kwa siku 10 now she is ok.
Dawa gani au aliandikiwa wapi??
Nina mwezi wa tatu siponi mafua hadi nikaitafuta VCT matokeo zaidi.
Dawa nimemeza na Machungwa nimekula wee hata 20 kwa siku.
Nielekeze
 
tofauti na masswala ya kidni unayoshabikia, kwa hili huwa nakukubali, veryy good
= ebola

Yaani hata ebola unashindwa kuelewa kuwa ni L badala ya R?

Hivi hizi shule huwa mnaenda kujifunza ujinga?
 
mimi ni shuhuda na 1, kikohizi imenisumbua toka mwezi wa 7 mpaka leo, namshukuru Mungu imepungua kwa kiasi
Wakuu.,kwa siku hizi za usoni nimegundua kuwa hapa DSM watu wengi wamekuwa wakikohoa kikogozi kikali sana.
Mtu mwingine aloona tatizo hili anaweza kutoa ushuhuda.
Watu wanaohusika na masuala ya afya watupe ushauri kujikinga.
 
Naona uko makini na spellings!. Hongera.. unabidii ya kuelimisha.

Hapana, si spellings, mimi sana sana hurekebisha R na L tu. Makosa mengine ya "spelling" huwa mara nyingi nayafungia macho.
 
Dawa gani au aliandikiwa wapi??
Nina mwezi wa tatu siponi mafua hadi nikaitafuta VCT matokeo zaidi.
Dawa nimemeza na Machungwa nimekula wee hata 20 kwa siku.
Nielekeze

rafiki kuhusu mafua dawa ni kitunguu swaumu! chukua punje kama sita kubwa kubwa(il hakikisha ni vile vya kienyeji sio breed) zisage halafu chukua maji kama vijiko vya chai vitatu au nne, changanya mchanganjiko huo halafu chukua pamba safi au chochote kisafi utakachoweza kutumia kuweka matone mawili katika kila tundu la pua zako! fanya hivyo kwa asubuhi mchana na kabla ya kulala! hutayaona mafua tena!
 
Mzizi mkavu ;kitunguu swaumu kina madhara gan?

Nini Madhara ya vitunguu swaumu?
jinsiulivyo.jpg


Ukiacha faida zake, vitunguu swaumu pia vina hasara na madhara mbalimbali kwa mtumiaji. Madhara hayo ni pamoja na;


  • Harufu mbaya mdomoni ambayo hutokana na kemikali ya AMS (allyl methyl sulfide). Harufu mbaya hii, hata hivyo, yaweza kupunguzwa kwa kunywa maziwa au kunywa maji mengi.
  • Kwa baadhi ya watumiaji, vinaweza kuwaletea mzio au mcharuko mwili (allergies au inflammatory reactions)
  • Kichefuchefu, Kutapika na kuharisha.
  • Huweza kusababisha hatari ya kuvuja damu, kwa sababu huzuia kazi ya seli sahani (platelets) zenye kusaidia kuganda kwa damu kushindwa kufanya kazi yake vizuri, na hususani kwa mama wajawazito, baada ya upasuaji au mara baada ya kujifungua.
  • Huingiliana katika utendaji kazi wake na dawa kadhaa kama vile warfarin, antiplatelets, saquinavir, dawa za shinikizo la damu kwa ujumla hasa calcium channel blockers, na antibiotiki za jamii ya quinolone kama vile ciproflaxacillin.
  • Aidha, vinaelezwa pia kuwa na madhara kwa wanyama jamii ya paka na mbwa.
 
Wakuu,

Nina siku tano mafua yananisumbua sana. Pua zinavuja kamasi kama bomba za DAWASCO masaa 24. Nimejaribu kwenda hospitali, nikapewa Piriton na PCM lakini hali bado ni tatanishi mpaka sasa.

Naomba anayejua dawa mbadala anijuze jamani, nateseka sana. Sina raha hadi nimeanza kukonda kwa hizo siku tano tu.

Msaada wa tiba tafadhali.
 
Tafuta asali safi...Saga tangawizi mbichi,mapoja vitunguu thoumu na pilipili manga(black pepper) kamua juice hii weka kwenye kikombe cha asali kunywa mara 3 kwa siku....Kama bado utakua nayo flue ni Pm na tutawasiliana zaidi....
 
duh mafua siku tano mbona nyingi ivo. Kawaida mafua ni siku tatu yanatakiwa kuisha
 
Kama unaweza chukua dodoki la asili lililokauka ( sijui jina lake kwa kiswahili, bali linafanana na matango likiwa bichi), choma kipande kidogo halafu nusa moshi unaotokana na dodoki hilo, mafua yatakoma mara moja. Taadhari kwani moshi ukiingia puani unauma kidogo.
 
Back
Top Bottom