Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Kama huogopi uchungu, chukua vitungu swaumu leo asubuhi tafuna vipunje 7, mchana tafuna vipunje 7 kisha malizia jioni vivyo hivyo kesho utaamka salama kabisa.Pia unaweza kumega kipande cha tangawizi, weka mdomoni kisha mung'unya taratibu huku ukimeza mate yake kwani inasaidia.
 
Mafua (common cold) hayana tiba. Kilichopo ni dawa za kukupa nafuu tu ila kwa kawaida huwa yanaisha yenyewe tu ndani ya wiki au wiki mbili.

Vizuri ni kutambua ni dawa ipi au zipi zinazokupa nafuu zaidi na hilo huwezi kujua bila kujaribu dawa tofauti tofauti.
 
Wadau nnatafuta dawa ya ugonjwa huo kwani umekuwa ukisumbua kwa mdaa mrefu,,vipimo vya TB vinaonyesha hakuna maambikizi yanayosababisha TB,,naambiwa ni kikohozi cha kawaaida tu lakini hakitaki kupona,,naombeni ushauri wa tiba gani nitumie,,Asanteni!
 
Ahsante grand-mal ;; i iven cop ua notes ! Thanx a lot umeeleza vzr !
 
Mkuu grand-mal, samahan.. Waweza gusia garama za kipimo cha alergy? Na mm hua na matatizo ya mafua sana sana yan nikiuma inanibid nilale tu kwan hali huwa inakuwa mbaya sana, chakushangaza nikwamba kila ninapopona mafua lazima kifuate kikohozi ndio nakua nimepona kabisa. Nisaidie

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
ilibidi upate mchanganyiko wa moja ya antibiotics kama amplicox,amoxycilin,bromoxilin pamoja na syrup kama hiyo kofyln,zentus,mucolyn au phencod,ndio kitaweza kupona.
 
Umetusaidia kufahamu vema hii kitu.Ahsante mkuu grand-mal

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Tumia Flucamox caps 500mg kwa siku 7 uchanganye na dawa ambayo ni expectorant na mucolytic kama vile Broncophane syrup then tuangalie kama tatizo litaendelea au lah
 
Salam wadau!

Nina shemeji yangu ana tatizo la kikohozi kisichoisha, ni mwaka sasa, kilimuanza akiwa na mimba ya miezi miwili na mpk sasa mtoto ana miezi mitatu na wiki tatu.

Anatoa makohozi na imefika sehemu sauti imekuwa haitoki sawia.

Alicheki na TB but alikuwa ok!

Kuna watu walishauri akatwe kimeo but haijawa suluhisho kwani kwa sasa anakohoa mpk anatapika.

Na mwilini mwake ametokwa na vitu mithili ya "mapunye".

Katumia dawa za hospitali na mitishamba bila mafanikio.

JE TATIZO LAWEZA KUWA NINI??

Msaada wenu unahitajika wadau.

Natanguliza shukrani za dhati kwa ushauri utaotolewa.
 
MPE POLE MGONJWA MKUU.
>Kwa kikohozi: chukua Asali changanya na Majivu au Magadi mpe Mgonjwa arambe mara 3 kwa siku hadi atakapo pona.

>kwa tatizo lingine wasubirie wengne mkuu.
Ila ninauhakika kwa kikohozi atapona mapema sana.

{jaribu kupekua kwani kuna thread nyingi zinazohusu tatizo hili}
 
ajaribu kuchukua vipimo zaidi ili waangalie tatizo ni nini.nisikutishe lung cancer nayo,dalili zake ni kikohozi kisichopona,kupungua,sauti inabadilika,pumzi zinakuwa za shida.ila sometimes kifua huwa kinasumbua, na huchukua muda kupona.dada yangu anasumbuliwa na kifua miaka nenda miaka rudi,vipimo vyote amemaliza tatizo halijaonekana kbla hana watoto na sasa ana watoto 3.akianza kukohoa kujitengenezea dawa za kiswahili.asali na tangawizi
 
MPE POLE MGONJWA MKUU.
>Kwa kikohozi: chukua Asali changanya na Majivu au Magadi mpe Mgonjwa arambe mara 3 kwa siku hadi atakapo pona.

>kwa tatizo lingine wasubirie wengne mkuu.
Ila ninauhakika kwa kikohozi atapona mapema sana.

{jaribu kupekua kwani kuna thread nyingi zinazohusu tatizo hili}


Anatakiwa kuchanganya kwa kiwango gani mkuu?
 
Back
Top Bottom