Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Ushauri: Tiba ya kikohozi na mafua

Mimi nna mafua ila hutokea koon halafu ni mazito nitumie dawa ipi ya kiasili. Hospital yanapungua hali inakuwa pale pale
 
habr zenu wakuu ningependa kujua dawa ya mafua ni ipi maana yananisumbua sana na mazingira gani si favourable ili ku avoid haya mafua
 
Kumekuwako na mlipuko mkubwa wa magonjwa ya mfumo wa hewa na hasa kikohozi,mafindofindo(toncilitis) na mafua hasa katika kipindi hiki cha mvua fupi fupi zinazonyesha jijini Dar.Uchunguzi nilioufanya unaonyesha kuwa kila mara zinaponyesha mvua za ghafla jijini huwa kunatokea sana mlipuko wa magonjwa ya mfumo wa hewa muda mfupi baada ya mvua kunyesha.Hata hivyo mvua zilizonyesha hivi karibuni zimetia fora kwa kuacha watu wengi zaidi wakiugua kikohozi na mafua.Wadau wa afya nadhani umefika wakati inabidi serikali iandae utaratibu wa kuelimisha umma juu ya magonjwa ya milipuko yatokanayo na mabadiliko ya hali ya hewa ili kuondoa wasiwasi na sintofahamu zinazojitokeza na pia kuwasaidia wale watu wenye allergy na hali fulani ya hewa kujua cha kufanya inapotokea mabadiliko hayo.Kwa mfano katika nchi zilizoendelea utabiri wa hali ya hewa huonyesha hadi maeneo yenye pollen(unga fulani toka kwenye mimea)nyingi wakati wa spring hivyo watu wenye allergy hujiandaa na hata wengine kuhama miji hadi kipindi hicho kipite.Binafsi najiuliza sana,kwa nini mvua fupi fupi hapa Dar huleta kikohozi kibaya sana?Wataalam ni vema mkatuelimisha.
 
Umri wangu ni miaka 28. Ni mwanaume. Nasumbuliwa na Mafua tangu nikiwa mdogo mpaka sasa. Hali hii hujitokeza nyakati za usiku na asubuhi. Hii ni kila siku. Usiku nikilala nikishituka tu huanza chafya na kamasi.

Nimetumia dawa za hospitali na miti shamba na kufata masharti ila sijafanikiwa. Yananitesa sana, maana kupiga chafya kunatumia nguvu nyingi.

Pia nawakera watu ninaoshinda nao, ikiwemo mpenzi wangu wakati wa kulala.

Naomba msaada. Nipo Iringa sasa ila nimezaliwa Dar na kukulia Dar.
 
Pole mkuu. Kama ni mafua ya kawaida machungwa yangefaa kua dawa
 
Kuna uwezekano mkubwa ni ALLERGY. Unahitaji kudadisi kwa umakini ni kitu gani unatumia au unakutana nacho zaidi usiku uweze kuzuia,
eg. Matandiko ya Sufi, vumbi, mafuta au perfumes zipo wazi muda wote chumbani, mzunguko mdogo wa hewa chumbani, fungal dusts au nyumba yenye unyevu darini kutokana na kuvuja na mengine mengi etc. Jaribu kuboresha hayo na tatizo laweza kupungua au kwisha kabisa.
 
jihadhari sana na vumbi pia jitahd kuweka hasa mashuka kathka hali usafi sababu muda mwingi usiku pua zinakua zinavuta vumbi hasa wakati umelala hvyo jitahid kubadilisga mashuka japo kila baada ya cku 1 au 2.
 
Kuna uwezekano mkubwa ni ALLERGY. Unahitaji kudadisi kwa umakini ni kitu gani unatumia au unakutana nacho zaidi usiku uweze kuzuia,
eg. Matandiko ya Sufi, vumbi, mafuta au perfumes zipo wazi muda wote chumbani, mzunguko mdogo wa hewa chumbani, fungal dusts au nyumba yenye unyevu darini kutokana na kuvuja na mengine mengi etc. Jaribu kuboresha hayo na tatizo laweza kupungua au kwisha kabisa.

Je dawa ni nini?maana kuna mengine kwa mazingira yangu hayaepukiki.Anayejua miti shamba anisaidie.Allergy/mzio huwa na tiba?
 
Je dawa ni nini?maana kuna mengine kwa mazingira yangu hayaepukiki.Anayejua miti shamba anisaidie.Allergy/mzio huwa na tiba?

Hiyo ni allergy, kama sio ya vitu na chakula, basi hali ya hewa ya sehemu unayoishi.
Nakuhakikishia iwapo utaenda mkoa mwingine, hutapata mafua.
Mimi nilikuaga naumwa kifua, nilitumia dawa za kila aina sikupona kwa miaka mingi, nilipobadili mazingira tu nilipona.

Embu jaribu kutumia dozi ya dawa ya clarinase 1x1.
 
Hiyo ni allergy, kama sio ya vitu na chakula, basi hali ya hewa ya sehemu unayoishi.
Nakuhakikishia iwapo utaenda mkoa mwingine, hutapata mafua.
Mimi nilikuaga naumwa kifua, nilitumia dawa za kila aina sikupona kwa miaka mingi, nilipobadili mazingira tu nilipona.

Embu jaribu kutumia dozi ya dawa ya clarinase 1x1.

Nitajaribu hiyo clarinase.Nimesoma kwenye mtandao sikumbuki jina kuna dawa inaitwa antihistamine hii hupunguza kitu kinaitwa histamine.Ni science ngumu kuielezea.wanasema kuna baadhi ya vyakula na vinywaji vina hii kitu kama vile pombe,wine na tea.kwa hiyo nikiviacha allergy itapungua.pia kusafisha chumba cha kulala,kufunga madirisha,kukaa mbali na mimea mida ya kuchavusha poleni.Mazoezi baada tu ya kuamka nisiache.

Kubwa na baya ninafanyia kiwanda cha maua na usindikaji wake huwa na vumbi jingi.Ajira siwezi kuacha nitafanyaje?
 
Kuna jamaa mahali ninafanyia kazi alikuwa na mara kwa mara anapata mafua siku moja akaenda kumuona prof. mmoja pale muhimbili ni pharmacist alipojieleza akabaini ni allerge akamwandika dawa ya kidonge inaitwa nazani ni CLARITINE kama sijakosea jamaa mara baada ya kutumia dose kapona kabisa na ile hali haipo tena
 
Pole. Kama walivyoandika wengine. tatizo lako inawezekana ni allegy tatizo hili huwa linasumbua sana mpaka kujua ni allegy ya kitu ganiili uepuke na upone na zipo allegy za aina nyingi sana . kwa vile umetibiwa sana na inaelekea kushindikana hospitali.

Ushauri wangu ni kwamba jaribu kufanya majaribio mwenyewe, soma vitabu au kwa enternet utaweza kupata majibu. Lakini ukipenda njoo kwetu Foreverliving products distributors tuna bidhaa vimewasaidi wengi wenye matatizo kama yako na mengine. Ukipenda nitafute +255 756 514 644/715 514 644.
 
Habari zenu, kuna dada anasumbuliwa kikohozi toka mwezi 2 mwaka jana hadi leo hajapona, alienda hospital akapima nakukutwa hana tatizo lolote akapewa dawa za kumsaidia dawa hizo hazikufanikiwa kumtibu.

Ametumia dawa nyingi sana zikiwemo vidonge na za chupa pia na na zakienyeji bila mafanikio.

Mwenye kujua tiba ya tatizo hili amsaidie.
 
habar zenu, kunadada anasumbuliwa kikohoz toka mwez 2 mwaka jana had leo hajapona, alienda hospital akapma nakukutwa hana tatzo lolo akapewa dawa za kumsaidia dawa hzo hazkufanikiwa kumtib, ame2mia dawa nying xna zikiwemo vdonge na za chupa pia na Nazakienyej bila mafanikio mwenye kujua tiba ya tatzo hli amsaidie

Dawa ya kıkohozı sugu



a) Kula punje 3 ya Vitunguu Saumu mara tatu kwa siku kwa muda wa siku 3 au siku 7.

b) Chukua kijiko cha chai cha kitunguu Saumu Changanya na Asali kijiko 1 kila baada masaa 4 kwa siku 3.
 

Attachments

  • 800px-Italian_garlic_PDO.jpg
    800px-Italian_garlic_PDO.jpg
    70.6 KB · Views: 152
Kuna dawa inatengenezwa kwa tangawizi, limao sijui na nini. Ni kiboko ya kikohozi.
 
Habari zenu wadau,

Mwenye kujua suluisho la tatizo la mafua yasiyoisha anisaidie, najua kuwa mafua ni virus disease ila kwangu mimi imekua too much, maana muda wote inabidi niwe na leso karibu, na yale makali sana hunishika kila baada ya wiki 3 mpaka nne na huwa yanadumu kwa siku 2 mpaka 3.
 
Back
Top Bottom